Maseto
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 944
- 545
Wakuu,
Nilikuwa Musoma hivi karibuni kwenye Msiba wa Mzee Fabian Samo aliyekuwa mwenyekiti wa TFF Mkoa wa Mara.Alikuwa mkwe wangu.Katika msiba huo nilibahatika kukutana na ndugu wa karibu sana na Mzee Mukama,Katibu Mkuu wa CCM.
Nilimuuliza ndugu huyo kwa nini Katibu Mkuu huyo ameshindwa kufanya maboresho katika chama,pamoja na kuwa na historia ya msimamo usiotetereka tangu alipokuwa Mkuu wa Chuo cha Kivukoni wakati huo (sasa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere),pia kuwa Afisa Mwandamizi TISS.Nilijibiwa kuwa Mukama alijitahidi sana kushauri na kuandaa mikakati ya kukifufua chama,lakini amekutana na vikwazo vigumu sana,hasa kutoka kwa Mwenyekiti wake ambaye amekuwa akisiliza kwa makini ushauri na kuonekana anakubaliana nao lakini amekuwa mzito mno kuugeuza katika matendo.
Kwa mfano, katika moja ya vikao vya NEC iliamuriwa kuwa wanachama wote,wakiwemo viongozi wa chama na serikali,wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajadiliwe ili wakuchuliwe hatua za kinidhamu katika vikao mbalimbali vya kamati za maaadili za chama kwa ngazi mbalimbali husika,kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa.Na mpango kazi pamoja na bajeti viliandaliwa.Utekelezaji wake umeshindikana hadi sasa kwa sababu ya uzito wa mwenyekiti.
Baada ya Mzee Mkama kujiridhisha kwamba hakuna la maana analoweza kufanya, akaamua kukaa kimya na "kula maisha".
Nilitegemea Mhe.Nape angekuwa mkweli na kutolea majibu juu ya haya badala ya kusema kuwa watawawajibisha mafisadi hao kwa kuwavizia wakati wa uchaguzi wa ndani ya chama.
Nilikuwa Musoma hivi karibuni kwenye Msiba wa Mzee Fabian Samo aliyekuwa mwenyekiti wa TFF Mkoa wa Mara.Alikuwa mkwe wangu.Katika msiba huo nilibahatika kukutana na ndugu wa karibu sana na Mzee Mukama,Katibu Mkuu wa CCM.
Nilimuuliza ndugu huyo kwa nini Katibu Mkuu huyo ameshindwa kufanya maboresho katika chama,pamoja na kuwa na historia ya msimamo usiotetereka tangu alipokuwa Mkuu wa Chuo cha Kivukoni wakati huo (sasa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere),pia kuwa Afisa Mwandamizi TISS.Nilijibiwa kuwa Mukama alijitahidi sana kushauri na kuandaa mikakati ya kukifufua chama,lakini amekutana na vikwazo vigumu sana,hasa kutoka kwa Mwenyekiti wake ambaye amekuwa akisiliza kwa makini ushauri na kuonekana anakubaliana nao lakini amekuwa mzito mno kuugeuza katika matendo.
Kwa mfano, katika moja ya vikao vya NEC iliamuriwa kuwa wanachama wote,wakiwemo viongozi wa chama na serikali,wanaotuhumiwa kwa ufisadi wajadiliwe ili wakuchuliwe hatua za kinidhamu katika vikao mbalimbali vya kamati za maaadili za chama kwa ngazi mbalimbali husika,kuanzia ngazi ya wilaya hadi taifa.Na mpango kazi pamoja na bajeti viliandaliwa.Utekelezaji wake umeshindikana hadi sasa kwa sababu ya uzito wa mwenyekiti.
Baada ya Mzee Mkama kujiridhisha kwamba hakuna la maana analoweza kufanya, akaamua kukaa kimya na "kula maisha".
Nilitegemea Mhe.Nape angekuwa mkweli na kutolea majibu juu ya haya badala ya kusema kuwa watawawajibisha mafisadi hao kwa kuwavizia wakati wa uchaguzi wa ndani ya chama.