Katibu Mkuu ashinda kwenye banda la Tanzania akiuza utalii London

M

MegaPyne

Guest
Katibu Mkuu wa wizara ya Utalii Tanzania Bibi Blandina Nyoni juzi alikesha katika banda la Tanzania akiuza utalii na kutoa huduma kwa watu mbalimbali waliofika katika banda hilo kwa kuwafahamisha mikakati ya Serikali ya awamu ya nne kwenye sekta ya utalii.


Katibu Mkuu alikuwa akiyafanya hayo katika mkutano wa siku tatu ulianza jumatatu wa soko la wasafiri duniani ‘World Travel Market’ uliofanyika katika Excel pembeni kidogo ya jiji la London.


Akionekana kama mama mwenye nyumba anayewakaribisha wageni, Mama Blandina aliuvua wadhifa wake na kuanza kututangaza utalii wa Tanzania na kuwafahamisha wale wanaotaka kukeza katika sekta hiyo faida za kufanya hivyo.


Pia alitumia nafasi hiyo kuzungumza na washiriki karibu na makala wote wanaouza utalii wa Tanzania kujua matatizo yao na kuwaeleza bayana mikakati ya Serikali ya awamu ya nne katika kupanua soko la utalii.


Akizungumza katika mahijiano maalum na jarida la Jambo Tanzania linalosambazwa katika ofisi za balozi za Tanzania huku Ulaya, Bibi Nyoni alisema mkutano huo umewafundisha mambo mengi washiriki waliotoka Tanzania, kwanza waliweza kukutana na watu kutoka nchi nyingine ambao wameendelea zaidi katika kuutangaza Utalii, na hivyo waliweza kujifunza baadhi ya mbinu ambazo zinaweza kusaidia kuutanganza zaidi utalii wa Tanzania.


“ Wanaofanya kazi kwenye sekta ya Utalii Tanzania kujionea ukubwa wa soko la utalii na kupata nafasi ya kutangaza vivutio na huduma zilizopo kwa makampuni ya Utalii ya dunia yanayotaka kutuma watalii Tanzania” alisema Bibi Blandina.
Akiuzungumzia matatizo mbalimbali yaliyojitokeza huko nyuma katika sekta ya utalii, Bibi Blandina alisema ni miundo mbinu ikiwa ni pamoja na hoteli na huduma zinazotolewa kwenye mbuga za utalii na kudai kuwa serikali ya Tanzania imeona hali hiyo, na sasa inafanya juhudi za kuboresha miundo mbinu ya kwenye mbuga za wanyama, na tayari mahoteli yanajengwa na barabara zinaendelea kujengwa.


Akizungumzia suala la usalama wa watalii na mali zao , Bibi Nyoni alisema wizara ya Utalii ya Tanzania kwa kushirikiana na idara nyingine za serikali, wameanzsiha utaratibu wa kuwa na kikosi cha pamoja usalama kinachoshirikisha askari wa Jeshi la Polisi na askari wanaolinda wanyamapori ambayo kazi yao kubwa ni kukomesha vitendo vya uhalifu dhidi ya watalii na ujangili kwenye mbuga za wanyama .


“Kweli uhalifu katika mbuga za wanyama umepungua kabisa , lakini juhudi zinaendelea ili kufanya usalama uwe mkubwa zaidi na kusiwe na malalamiko kama hayo yanatokea kani ndivyo vitu vinavyoweza kushusha soko la utalii la Tanzanua, hili tumelitilia mkazo mkubwa,” alisema.


Akizungumzia mafanikio ya ziara za Rais Kikwete huku Ulaya na Marekani, Bibi Blandina alisema kweli zimewasafishia njia, kwani hata wao sasa hawapati tabu sana katika kufanya hiyo kazi kwa nchi hizo kwani katika nusu ya hutuba zake zilikuwa zinalenga kwenye utalii na wawekezaji.


“Mheshimiwa Rais kuwa bega kwa bega kutangaza utalii huku Ulaya na Marekani umetujengea hamasa kubwa sisi watendaji na kweli faida yake Watanzania waiona si muda mrefu,hata wananachi nao watanufaika na hizo hutuba zake” alisema.


Katibu Mkuu huyo wa Wizara alisema wananchi si watanufaika na pesa za kodi za utalii, bali pia wanapokuja kwa wingi na kwenda kwenye maneneo yao, wananzci wataweza kuuza vito vyao kama vile shanga, vinyago na vitu vingine, hivyo ni mwananchi nae ananufaika.


Alisema Wizara yake ipo katika mkakati mkubwa kuasnza kujitangaza huku ulaya baada ya kumaliza kule Marekani na China na kusema kuwa kwa mwaka wa fedha wa mwakani wanatarajia kuongeza bajeti kuona uwezekano a kujitangaza zaidi.


Mbali na Bi Blandina viongozi wengine waliambana nae ni Waziri wa Utalii, Biashara na Uwekezaji wa Zanzibar Bi Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti wa bodi ya Utalii Tanzania, ,Bw. Daniel Yona,Waziri wa Mkurugenzi wa hifadhi za Taifa, Bw. Gerald Bigurube, Mkurugenzi wa Utalii wa TANAPA, Bw. Allan Kijazi, Kaimu Mkurugenzi wa Ngorongor Bw. B.Mrunya,
 
huyu mama ni mchapakazi katika makatibu wa kuu wa kikwete ndiyo aliye anzisha TRA yupo makini sana
 
wewe unafikiri huku angemletea nani nyodo? Nyodo zao hao huwa zinaishia wakipanda ndege. Wewe hushangai hata boss alikuwa anachekelea kuitwa good boy na wazungu. Lakini huyu dadako ngoja umkute huku home ndio utajua yeye ni nani?

Hamna kipya kabisa katika hili, wala sio news ya kupachika hapa. Na wale sio yeye, kwa nini hushangai watu huku wanaweza kubeba mabksi, wakaosha sufuria hadi wakateguka mikono, wakati nyumbani hata kufundisha shule ya sekondari wanaona so?
 
wewe unafikiri huku angemletea nani nyodo? Nyodo zao hao huwa zinaishia wakipanda ndege. Wewe hushangai hata boss alikuwa anachekelea kuitwa good boy na wazungu. Lakini huyu dadako ngoja umkute huku home ndio utajua yeye ni nani?

Hamna kipya kabisa katika hili, wala sio news ya kupachika hapa. Na wale sio yeye, kwa nini hushangai watu huku wanaweza kubeba mabksi, wakaosha sufuria hadi wakateguka mikono, wakati nyumbani hata kufundisha shule ya sekondari wanaona so?

Kitila mkuu hayo uliyosema mimi nakubaliana na wewe kwa asiliamia 100. Mimi mwenyewe nakubali huyu mama ni mchapakazi lakini pia huyo mama ni anayodo sana. Uliza watu wanaofanya kazi kwa Accountant General au Hazina watakuambia huyo mama alikuwa kama Mungu mtu. Huwezi kuongea na yule mama nakwaambia anajeuri sema tuu wakija huku ugaibuni wanakuwa wapole tuu sasa kwani watamringia nani?

Yule mama sio msafi kama watu wanavyodhani. Tenda nyingi za computer alizokuwa anawapa wahindi zote zilikuwa za Kinyemela tafuteni watu wa pale ofisini kwake alipokuwa Hazina ndio utajua mambo yake.
 
JAMANII HIYO SIYO KAZI YAKE KATIBU MKUU KUKAA KWENYE MABANDA,AMEIKIMBIA KAZI YAKE YA UTENDAJI HUSUSAN ILE YA KUKUSANYA BILLION 33 ZA NYONGEZA KWENYE UWINDISHAJI WA KITALII.AMBAPO MATAJIRI WENYEKUMILIKI VITALUU WAMEKATAA KULIPA ADA MPYA AMBAPO DEADLINE YAKE ILIKUA TAREHE 30/09/2007 NA BADO WANAPEWA LESENI.hii NI KAZI YAKE LAKINI ANAIKACHAA KWANINI!!!!! jiulize
 
wewe unafikiri huku angemletea nani nyodo? Nyodo zao hao huwa zinaishia wakipanda ndege. Wewe hushangai hata boss alikuwa anachekelea kuitwa good boy na wazungu. Lakini huyu dadako ngoja umkute huku home ndio utajua yeye ni nani?

Hamna kipya kabisa katika hili, wala sio news ya kupachika hapa. Na wale sio yeye, kwa nini hushangai watu huku wanaweza kubeba mabksi, wakaosha sufuria hadi wakateguka mikono, wakati nyumbani hata kufundisha shule ya sekondari wanaona so?


Kitila, kuna 5 kubwa mkuu...hii imetulia.
 
wewe unafikiri huku angemletea nani nyodo? Nyodo zao hao huwa zinaishia wakipanda ndege. Wewe hushangai hata boss alikuwa anachekelea kuitwa good boy na wazungu. Lakini huyu dadako ngoja umkute huku home ndio utajua yeye ni nani?

Hamna kipya kabisa katika hili, wala sio news ya kupachika hapa. Na wale sio yeye, kwa nini hushangai watu huku wanaweza kubeba mabksi, wakaosha sufuria hadi wakateguka mikono, wakati nyumbani hata kufundisha shule ya sekondari wanaona so?

Give the devil its dues.Jamani,kwani angeamua kwenda zake kufanya shopping na kuwaacha wababishaji flani kwenye banda,angeshindwa?Au kama angeamua kufunga kabisa banda na kutokomea mtaani,nani angemuhoji?Au angefanya hivyo angefukuzwa kazi?Kama Karamagi alifanya alofanya na hadi leo anapeta,Severe alifanya alofanya na hadi leo anapeta,then huyu mwanamama kwanini aogope "kufanya kile kinachowaleta huku ng'ambo" (shopping,more shopping,and even more shopping),nk

Suala hapa sio kama angemletea nani nyodo,ila ni namna alivyojituma.Nakumbuka Bwana Kitila uliwahi kuanzisha mada kwamba TUSIWE WA KULAUMU TU bali tuchambue na maeneo mengine yenye maslahi kwa Taifa.So far,you cant substantiate kuwa huyo mwanamama alijituma kwa vile tu "hapa hakuna wa kumeletea nyodo" na sio dhana kwamba ni mchapakazi.

As to kubeba maboksi na sufuria,nadhani hiyo ni misguided overgeneralization.Kuna wenzetu hapa wanafundisha shule (ulizia career service ya chuo kuhusu nia ya ku-gain teaching experience),kuna wenzetu wanaendesha biashara zao zinazowawezesha kuendesha maisha yao bila kubeba maboksi,na tupo akina sie ambao tunawatengenezea digrii hawa watu....hawa hawaoshi sufuria.Tell you what,kama huna uwezo na akili ya kupata kazi,utaishia kuosha sufuria,BBC,ulinzi,etc.Inferiority complex kwamba kazi pekee kwa wageni ni kuosha masufuria na kubeba maboksi ndio zinazopelekea ndugu zetu wengi wanapokuja hapa kuogopa ku-apply kazi za maana wakidhani kuwa kazi za wageni ndo hizo tu...

Na kudai kuwa "hapa hakuna jipya na hii sio news ya kupachika hapa"....be fair!Who sets the bar as to what to or not to be posted here?Tuheshimu ichango ya wengine.Hivi unaweza kutusaidia kutupatia mfano wa wa hiv karibuni wa kiongozi yeyote alohanagaika kuitangaza nchi namna alivyofanya huyo mama?If not,then it's news coz here "the woman bit a dog",which is always news in a journalistic speak.
 
wewe unafikiri huku angemletea nani nyodo? Nyodo zao hao huwa zinaishia wakipanda ndege. Wewe hushangai hata boss alikuwa anachekelea kuitwa good boy na wazungu. Lakini huyu dadako ngoja umkute huku home ndio utajua yeye ni nani?

Hamna kipya kabisa katika hili, wala sio news ya kupachika hapa. Na wale sio yeye, kwa nini hushangai watu huku wanaweza kubeba mabksi, wakaosha sufuria hadi wakateguka mikono, wakati nyumbani hata kufundisha shule ya sekondari wanaona so?

nimecheka sana hapo !
 
jamani mwacheni aunt yangu....ni mchapakazi hodari tangu alipokuwa lecturer Mzumbe!
 
Hii ni kali,hebu tuone wataishia wapi.Sasa sijui alikumbuka kuwasisitizia Wazungu kwamba Mlima Kilimanjaro upo Tanzania na wala si Kenya,na kwamba Mbuga ya Serengeti pia iko tanzania n na si Kenya kama wanavyojua.Kama kafanya hayo,then nampongeza.Hata kitendo cha kuuvua ukatibu wa wizara na kuwa mhudumu wa watalii,walau kwa siku moja si kazi ndogo.Nampongeza sana,mfano mzuri.Keep it up Blandina.
 
wewe unafikiri huku angemletea nani nyodo? Nyodo zao hao huwa zinaishia wakipanda ndege. Wewe hushangai hata boss alikuwa anachekelea kuitwa good boy na wazungu. Lakini huyu dadako ngoja umkute huku home ndio utajua yeye ni nani?

Hamna kipya kabisa katika hili, wala sio news ya kupachika hapa. Na wale sio yeye, kwa nini hushangai watu huku wanaweza kubeba mabksi, wakaosha sufuria hadi wakateguka mikono, wakati nyumbani hata kufundisha shule ya sekondari wanaona so?

kwi kwi kwi kwi Mkubwa sijakuelewa vizuri ina mana huyu mama pia alikwenda kunyanyu box?nifahamishe vizuri
 
Akiuzungumzia matatizo mbalimbali yaliyojitokeza huko nyuma katika sekta ya utalii, Bibi Blandina alisema ni miundo mbinu ikiwa ni pamoja na hoteli na huduma zinazotolewa kwenye mbuga za utalii na kudai kuwa serikali ya Tanzania imeona hali hiyo, na sasa inafanya juhudi za kuboresha miundo mbinu ya kwenye mbuga za wanyama, na tayari mahoteli yanajengwa na barabara zinaendelea kujengwa.

Mimi hii ndiyo inayonitisha! Athari ya hayo mahoteli na barabara kwa mazingira ya mbuga zetu iameangaliwa? Nilivyosikia ni kuwa wana mazingira wamepinga ujenzi huu kwa vile utaathiri wanyama ambao hao watalii ndiyo wanawafuata. Badala ya kupanua wigo la vivutio kwa kuwekeza kwenye mbuga ambazo hazitembelewi kwa wingi( Saadani, Ruaha n.k) tunakazania Serengeti, Manyara, Mlima Kilimanjaro na kadhalika. Hapo wanyama watakapopotea na theluji kwenye mlima huo tunaojivunia tutawaambia nini kizazi kinachotufuate? Kuwa tulikuwa na bata anayetaga mayai ya dhahabu lakini kwa uroho wetu tulimchinga?
 
.....kituko cha mwaka!
Hivi haw amakatibu wakuu wana "job description???? Au wanabahatisha tu kazi zao.
Katibu Mkuu....kwenye banda la Utalii? Na Mkurugenzi wa Utalii na watu wake wanafanya nini? Mind you hii Wizara sio ya Utalii peke yake in pia Maliasili etc sasa KM ndio amekuwa implementer? Na kwa kwenye trade fair ni kisehemu kiduchu katika kuinua huu utalii. Trade fair zenyewe ziko kibao atahudhuria ngapi?? Yeye si anatakiwa awe msimamizi sasa kwenda kukaa mlangoni kama mama mwenye nyumba ndio kusimamia??
Atafunga ofisi?? To be honest hii shughuli ingeweza hata kuwa sub contracted kwa wataalam wa PR....
We have a long way to go!!!mmmh
 
.....kituko cha mwaka!
Hivi haw amakatibu wakuu wana "job description???? Au wanabahatisha tu kazi zao.
Katibu Mkuu....kwenye banda la Utalii? Na Mkurugenzi wa Utalii na watu wake wanafanya nini? Mind you hii Wizara sio ya Utalii peke yake in pia Maliasili etc sasa KM ndio amekuwa implementer? Na kwa kwenye trade fair ni kisehemu kiduchu katika kuinua huu utalii. Trade fair zenyewe ziko kibao atahudhuria ngapi?? Yeye si anatakiwa awe msimamizi sasa kwenda kukaa mlangoni kama mama mwenye nyumba ndio kusimamia??
Atafunga ofisi?? To be honest hii shughuli ingeweza hata kuwa sub contracted kwa wataalam wa PR....
We have a long way to go!!!mmmh

...mama lao kuna ubaya gani na anachofanya hapo? hebu tuache kuwa critical kwa kila kitu,anachofanya ndio nia kubwa iliyowapeleka huko London
 
Kuwepo kwa KM katika shughuli kama hii pengine ndiyo kuonyesha uongozi wa vitendo. Hilo, ingawa sioni umuhimu wake halinitii wasiwasi kama matamshi aliyoyatoa kuhusu ujenzi wa hoteli na infrastructure nyingine kwenye mbuga zetu. Ni mwaka jana tuu serikali ilisitisha ujenzi wa Hoteli ya Bilia ambayo ingemilikiwa na kampuni ya Albawardy Investments kutoka Dubai ( ndiye mmiliki wa Hoteli Kempiski ya Dar es Salaam) baada ya wana mazingira kutahadharisha kuhusu madhara yatakayotokea kwa wanyama wetu wahamiaji. Waliendelea kutoa mifano ya mbuga za jirani wtu wa Kenya zilivyoathirika kutokana na maendelezi kama haya! Na mwaka huu wameendelea kusema hayo hayo lakini inaelekea viongozi wetu wameziba masikio. Hao watalii tunaojaribu kuwavutia sasa hivi wanakimbilia Botswana, Afrika ya kusini ambako bado wanalinda mbuga zao. Ni mtalii gani wa maana anayependa kuja kusongamana na watalii wengine lukuki kumshangalia tembo mmoja kama inavyotokea kwa jirani zetu. Sifa ya mbuga zetu ni kwamba zilikuwa bado kama asili na sio mfano wa "zoo"! Soma link hii uone hao tunaotaka kuwavutia wanavyotushangaa. Au pengine tunategemea watalii kutoka Dubai na China?

http://news.independent.co.uk/world/africa/article2898435.ece
Naungana na Mama Lao katika kusisitiza kuwa hii wizara si ya utalii tuu. Ni lazima vile vyote vilimo katika wizara hii viangaliwe kwa kuzingatia "sustainability" na sio short term returns.
Tutachekwa!
 
.....kituko cha mwaka!
Hivi haw amakatibu wakuu wana "job description???? Au wanabahatisha tu kazi zao.

Koba ni sawa na kumkuta CEO wa VODACOM AU CELTEL ameamua afanye kazi ya kuuza VOCHA peke yake. As simple as that! Kituko cha mwaka.[U[/U]
 
Back
Top Bottom