Katibu Kata CCM afariki baada ya kupoteza Mitaa

Zyansiku

Member
Jul 27, 2009
49
10
Katika hali ya kushitua! katibu kata wa CCM kata Mbugani wilaya ya Tabora Mjini, Bwana Kasimu Idrisa amefarika Dunia dakika chache zilizopita baada ya kupokea barua ya kusimamishwa uongozi uliosababishwa na yeye kupoteza mitaa mingi kama kiongozi. Kata ya Mbugani yenye jumla ya mitaa 11 katika uchaguzi wa mitaa uliomalizika siku chache zilizopita CCM walipata mitaa 5 CUF 5 na UDP 1. kwa matokeo hayo katibu wa CCM mkoa wa Tabora alimsimamisha uongozi katibu kata huyo hasa baada ya kupewa taarifa zisizo rasmi na Diwani wa kata ambaye pia ni katibu wa siasa na uenezi wa CCM Mkoa wa Tabora Bwana Kapama, habari ninazoendelea kuzipata ni kuwa mahusiano ya Mh Diwani kapama na katibu kata hayakuwa mazuri hivyo baada ya matokeo hayo Diwani alimshitaki katibu kata wake CCM mkoa kuwa ndiye aliyesababisha kupotea kwa mitaa mingi hali ilisababisha katibu kata huyo kupewa barua ya kusimamishwa jana na leo asubuhi kuugua ghafla na kupelekwa Hospitali ya Kalunde ambapo amefariki Dunia.
 
Naam! ni kweli yametokea, inasikitisha sana kifo cha ghafla ambacho kwa kweli Diwani kapama anastahili kubeba lawama zote mbaya zaidi aliyefariki alikuwa hamuungi mkono Mh kapama katika maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao
RIP Idrisa
 
Duh ushabiki huu wa kisiasa umepitiliza sasa dah alijua cheo kitapotea?
 
Duh ushabiki huu wa kisiasa umepitiliza sasa dah alijua cheo kitapotea?

nani aliyejua kwamba cheo kitapotea?

by the way, siasa za namna hii ndo zinasababisha wizi, hujuma na uhuni dhidi ya upinzani ktk chaguzi. Kiongozi anajua atafukuzwa kazi hivyo anatumia mbinu zote chafu kuhakikisha wanashinda.

siasa za kitoto hizi. Lakini hatuwezi kusema moja kwa moja kuwa kifo kimesababisha na hili, mpaka ripoti ya daktari.
 
Kitendawili........
Asiyekubali kushindwa si mshindani.....

Ni nani huyo......................?
 
Marehemu ulale pema peponi!
Atakuwa alitishwa kwamba akipoteza mtaa naye amekwisha, hivyo presha ikamzidia!
Umafia wa CCM wa kuteka mitaa kiubabe una madhara sana!
 
Back
Top Bottom