Katiba ya Warioba: Serikali ya mseto inanukia?

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,791
3,360
Habari kwenu wana JF. Nimeangalia kinachoendelea katika teuzi za karibuni kwa Mh. Prof. Kitila (Katibu Mkuu W/Maji) na jana Mh. Mghwira(RC. Kilimanjaro) na kunitia moyo fulani. Moyo wenyewe,ni matumaini ya maendeleo ya haraka zaidi,kwa wapinzani kushirikishwa moja kwa moja ktk kutenda na siyo kukosoa tu.

Ninaona dalili za Mapendekezo ya Katiba ya Warioba juu ya kuunda serikali ya pamoja yakinukia! Ukiangalia kwa undani,malengo makuu ya Vyama vyote yanafanana yaani "Kuwatumikia wananchi". Hivyo,kwa teuzi hizi mbili,naunga mkono,na ifike mahali iwe rasmi,serikali iundwe kutokana na vyama vyote.

Au wadau mnalionaje hili?
 
Wabongo bwana aliewaminisha kwamba act ni wapinzani ni nani,just branch tu,sasa watu wanateua washirikawao mnasema upinzani,au dhana ya upinzani hamuielewi vizuri,kama kweli ni mkweli ,achanganye na chadema au cuf ya maalim hapo 2020wenye akili watamwelewa
 
Habari kwenu wana JF. Nimeangalia kinachoendelea katika teuzi za karibuni kwa Mh. Prof. Kitila (Katibu Mkuu W/Maji) na jana Mh. Mghwira(RC. Kilimanjaro) na kunitia moyo fulani. Moyo wenyewe,ni matumaini ya maendeleo ya haraka zaidi,kwa wapinzani kushirikishwa moja kwa moja ktk kutenda na siyo kukosoa tu. Ninaona dalili za Mapendekezo ya Katiba ya Warioba juu ya kuunda serikali ya pamoja yakinukia! Ukiangalia kwa undani,malengo makuu ya Vyama vyote yanafanana yaani "Kuwatumikia wananchi". Hivyo,kwa teuzi hizi mbili,naunga mkono,na ifike mahali iwe rasmi,serikali iundwe kutokana na vyama vyote. Au wadau mnalionaje hili?

Hizo teuzi zote zimetoka ACT, na ACT hakijawahi kuwa chama cha Upinzani Tanzania, kilikuwa chama cha kuipinga CHADEMA kama kilivyo CCM tu
 
Hii haiwezi kuwa ya mseto kwa sababu ama wateuliwa wanajivua uanachama baada ya kuteuliwa; au walikuwa wanachama wa siri wa chama kinachowateua. Mwisho wa siku hii ni serikali inayoundwa na chama kimoja - si mseto. Labda dimension ya muungano ndiyo inazua maswali mengi maana Zanzibar ni kama imesahaulika kabisaaaa
 
Habari kwenu wana JF. Nimeangalia kinachoendelea katika teuzi za karibuni kwa Mh. Prof. Kitila (Katibu Mkuu W/Maji) na jana Mh. Mghwira(RC. Kilimanjaro) na kunitia moyo fulani. Moyo wenyewe,ni matumaini ya maendeleo ya haraka zaidi,kwa wapinzani kushirikishwa moja kwa moja ktk kutenda na siyo kukosoa tu. Ninaona dalili za Mapendekezo ya Katiba ya Warioba juu ya kuunda serikali ya pamoja yakinukia! Ukiangalia kwa undani,malengo makuu ya Vyama vyote yanafanana yaani "Kuwatumikia wananchi". Hivyo,kwa teuzi hizi mbili,naunga mkono,na ifike mahali iwe rasmi,serikali iundwe kutokana na vyama vyote. Au wadau mnalionaje hili?
Wala usitiwe moyo kabisa. Rais Magufuli hajateua wapinzani, kama alivyoahidi kule Zanzibar. Hao wanaoteuliwa wala siyo wapinzani. kwa hiyo hakuna cha mseto wala nini.
 
Wala usitiwe moyo kabisa. Rais Magufuli hajateua wapinzani, kama alivyoahidi kule Zanzibar. Hao wanaoteuliwa wala siyo wapinzani. kwa hiyo hakuna cha mseto wala nini.
Labda ndiko anaelekea! ACT siyo chama dola! Ni kati ya vyama vya upinzani hapa nchini. Na,ningependa wanaoteuliwa kutoka upinzani,wasibadili vyama harakaharaka. Na pia ateue vyama vingine,tujenge utaifa kama Kenya, Afrika ya Kusini n.k. Tuendelee kumshauri kwa nia njema.
 
Tayari ACT-Wazalendo wameshatoa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji. Ni Prof. Kitila Mkumbo. Tena,ACT-Wazalendo wametoa Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,tena Mwenyekiti wa chama hicho,Anna Mghwira.

Hakuna lugha nyingine zaidi ya kusema kuwa sasa tuna Serikali ya Mseto ya CCM na ACT-Wazalendo. Ni wazi kuwa wanaCCM wenye uwezo wa kushika nafasi hizo hawakuwepo.CCM tumeishiwa,kwa mujibu wa Mwenyekiti

Kwanini Mhe. Rais ameichagua ACT-Wazalendo kuunda nao Serikali ya Mseto? Kwanini wasiwe watani wetu wa jadi CHADEMA au UKAWA kwa ujumla? Nawasikitikia waliojipanga mstari ndani ya CCM kusubiri uteuzi. Makada wamechanganyikiwa na kuishiwa. Ilani ya CCM sasa inapaswa kurekebishwa!

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Kumbuka jamaa alituumiwa na zitto ile kipindi yuko wizara ya ujenzi na sasa hivi vinaitwa chuki na visasi.


Swissme
 
Hakuna Serikali ya Tanzania huo ni uteuzi tu Rais kwa nafasi zake za uteuzi kwa watanzania anaoona wanafaa kumsaidia kufanya nao kazi.

Serikali za mseto huo Sina sheria na taratibu zake kabisa zilizowekwa na Rais aliyepo madarakani anapaswa kuzifuatwa.
 
Back
Top Bottom