Kunguru Mjanja
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 2,012
- 2,000
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 20, Ibara ndogo ya Kwanza inasema
“Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria za nchi, kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo.”
Kwa maana hiyo Ibara hii ya Katiba inawapa uhuru wananchi kukusanyika kwa Amani, bila kuvunja sheria wala kutukana mtu au watu.
Lakini uhuru huu wa kukusanyika kwa amani unafinywa hapa nchini, hususani baada ya kuwepo kwa sheria kali kama vile inayowataka watu kuchukua kibali Polisi saa 48 kabla ya kukusanyika. Wakati huo huo Polisi hawa kupitia sheria ya polisi ya mwaka 2002 (The Police Force and Auxiliary Services Act 200) inawapa Polisi uwezo wa kukataa makusanyiko hayo.
Sheria hii imeonekana kufanya kazi mara kwa mara ambapo watu wananyimwa uhuru wao wa kukusanyika kwa amani.
Je, nini kifanyike ili watu wawe na uwezo wa kukusanyika kwa amani nakutoa maoni yao bila kumkwaza wala kumtukana mtu yeyote wakati tunasubiri kubadili Katiba yetu?
“Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria za nchi, kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo.”
Kwa maana hiyo Ibara hii ya Katiba inawapa uhuru wananchi kukusanyika kwa Amani, bila kuvunja sheria wala kutukana mtu au watu.
Lakini uhuru huu wa kukusanyika kwa amani unafinywa hapa nchini, hususani baada ya kuwepo kwa sheria kali kama vile inayowataka watu kuchukua kibali Polisi saa 48 kabla ya kukusanyika. Wakati huo huo Polisi hawa kupitia sheria ya polisi ya mwaka 2002 (The Police Force and Auxiliary Services Act 200) inawapa Polisi uwezo wa kukataa makusanyiko hayo.
Sheria hii imeonekana kufanya kazi mara kwa mara ambapo watu wananyimwa uhuru wao wa kukusanyika kwa amani.
Je, nini kifanyike ili watu wawe na uwezo wa kukusanyika kwa amani nakutoa maoni yao bila kumkwaza wala kumtukana mtu yeyote wakati tunasubiri kubadili Katiba yetu?