Katiba: Tanganyika Irudi Kwanza Ndipo Rasimu ya Katiba Ifuate

Unapenda Muundo Gani wa Muungano


  • Total voters
    210
Kwa muelekeo huu, niwaombe tume ya katiba wachukulie zoezi lao kama project ili waweze kujipanga vizuri. naona kiza huko mbeleni.
 
Ni kweli asilimia kubwa hatuijui Tanganyika na hatukuiona,naunga mkono wazo la kufanyia mabadiliko makubwa sana muundo wa Muungano wa sasa ili twende sawa na kupunguza kelele zisizo na maana kwa kila upande na kusawazisha mawazo mgando!
 
Ni kweli asilimia kubwa hatuijui Tanganyika na hatukuiona,naunga mkono wazo la kufanyia mabadiliko makubwa sana muundo wa Muungano wa sasa ili twende sawa na kupunguza kelele zisizo na maana kwa kila upande na kusawazisha mawazo mgando!

Wafungue macho na masiki0, vile vile waone na wasikie. Hiki ni kilio cha mustakabali wa taifa letu
 
Yaani bado wapo tuu? Aaargh, wataondoka lini hawa wapemba, mie kuna duka nalitamani pale kariakoo

"yaonesha una chuki binafsi na roho mbaya, ila kwa kweli siyo kama inatushughulisha saana, sisi wavivu/hatujasoma na tumeishia elimu ya madrassa, bado unataka chetu bila kukitolea jasho?! ama kweli!!"

 
Ni kweli mie siwapendi


Tatizo moja nililogundua toka kwa ndugu zenu kutoka tanganyika ni ile kujiona wamesoma sana lakin hawajatambua kuwa KUSOMA SI MALI KAMA HUJAELIMIKA.
Wanahitaji darsa kubwa sana la kuwaelimisha na sio kumalizo vyumba vyote vya madarasa kwa kukariri na kujiita msomi.

Msomi mzuri ni yule aliyeelimika
 
Tatizo moja nililogundua toka kwa ndugu zenu kutoka tanganyika ni ile kujiona wamesoma sana lakin hawajatambua kuwa KUSOMA SI MALI KAMA HUJAELIMIKA.
Wanahitaji darsa kubwa sana la kuwaelimisha na sio kumalizo vyumba vyote vya madarasa kwa kukariri na kujiita msomi.

Msomi mzuri ni yule aliyeelimika
Mbona wazenji ni watu wakarimu sana. Sisi watanganyika nafikiri tuna matatizo, tunawachokoza sana. Aina ya muungano sio uadui
 
Mwambieni Mh. Tundu Lissu apeleke mswada wa kuvunja muungano bungeni tutafanya kampeni kabambe tuhakikishe amepata 2/3 ya wabunge wa zanzibar.
 
Mwambieni Mh. Tundu Lissu apeleke mswada wa kuvunja muungano bungeni tutafanya kampeni kabambe tuhakikishe amepata 2/3 ya wabunge wa zanzibar.
Hana nguvu kama mwanasheria wa SMZ na BLW. Umemsikia alivyoboronga kuhusu hoja za Lissu! hakuna lolote la maana au la kisheria alilojibu. Mwansheria ambaye ndugu yangu Baru baru kasema amesoma ametia aibu. Kama ule ndio usomi anaoupigia upata Baru baru basi ipo kazi.

Baru baru unajua hakuna mtu aliyezaliwa na dharau, dharau anaitengeneza mtu mwenyewe. Ukisikia hoja za UAMSHO na za Mwanasheria wa BLW, utahitaji miaka 99 kunishawishi kuwa kuna usomi pale. Hata kwa bahati mbaya. Ukinihitaji ni kuthibitishie nipo radhi

Falconer, anayeonewa ni nani? aliyeanzisha vurugu za moto na petrol ni nani? Anayedai kuwa ni koloni ni nani? Kelele zote za UAMSHO, BLW na Mwanasheria wa SMZ na BLW hakuna hata mmoja aliyesimama na kusema analeta hoja ya kuvunja muungano. Hakuna! Hakuna!

Baru baru na wenzake wote wamejikita katika
serikali 3
mkataba
mahusiano

Na leo tumesikia kituko cha mwanasheria wa Unguja, tunataka muungano kama wa SWISS. Kwik kwi mbavu zangu jamani

The bottom line ni kuwa Zanzibar iende zake hata kesho! ndiyo maana tuna uthubutu wa kusema LET ZNZ GO!
 
Nguruvi3 Mimi sio mwanasheria, lakini nimesoma maoni ya huyo mwanasheria nikacheka sana sana. Vituko hivi, hebu wekeni CV yake, tusije tukamwonea bure.

Ila pita paragraph ya kwanza, imenichanagnya kidogo.
 
Last edited by a moderator:
Najua kwamba pamoja na kwamba napenda serikali moja, wazenji hawatakubali, basi iwe serikali tatu. Na suala hili lirudishwe bungeni ili hadidu za rejea za tume zirekebishwe. Hii itawezasha upatikanaji wa rasimu ya katiba ya Tanganyika pia.

Muungano wa serikali tatu ni njia pekee ya kuimarisha muungano na vilevile ni njia yakuvutia nchi zingine kuona faida ya muungano. Tusiwe wanafiki, hakuna nchi inayotamani muundo wa sasa maana unalalamikiwa na watu wote hata viongozi wenyewe (wakiwa pembeni). Mchakato wa sasa umejaa hadaa. Wanchi waulizwe kwanza wanataka muungano wa serikali ngapi. Ninavyoamini mimi wananchi wengi kwa asilimia kubwa, wanataka serikali tatu. Asilimia inayofuatia kwa ile ya serikali tatu ni wale ambao hawataki muungano kabisa. Wanaotaka serikali mbili ni wachache sana hasa viongozi tu na wale wanaofaidi muungano huu kwa ufisadi. Hivyo ninawaomba wabunge wasome hisia za watu wasiendeleze matakwa ya serikali katika hili. Wabunge waazimie na kubadilisha sheria ya mchakato ili kuwepo na umuhimu wa kupiga kura ya maoni kuhusu muungano wananchi wautao kwanza. Kama ni serikali tatu, basi mchakato wa kutenegeneza katiba ya kila nchi ifanyike kwanza ikifuatiwa na mchakato wa katiba ya muungano. Hii ndio sawa yake. Kama serikali haitasikia hili, mimi ninadhani wananchi (WaTanganyika) wanapoenda kwenye mikutano ya maoni, wasichangie mengine zaidi ya kutaka Tanganyika izaliwe na tuunde katiba yake ndipo tuanze kujadili namna ya kuungana. Kwa maneno mengine muungano uvunjwe kwanza ili tuifufue Tanganyika. Baada ya hapo tujadili muungano tuutao. Mimi kama mimi na familia yangu tumesimamia hili. Je wewe?
 
Mi nina options mbili.
Serikali moja au hakuna muungano. Vote yangu ikaeje?
 
Muungano wa serikali tatu ni njia pekee ya kuimarisha muungano na vilevile ni njia yakuvutia nchi zingine kuona faida ya muungano. Tusiwe wanafiki, hakuna nchi inayotamani muundo wa sasa maana unalalamikiwa na watu wote hata viongozi wenyewe (wakiwa pembeni). Mchakato wa sasa umejaa hadaa. Wanchi waulizwe kwanza wanataka muungano wa serikali ngapi. Ninavyoamini mimi wananchi wengi kwa asilimia kubwa, wanataka serikali tatu. Asilimia inayofuatia kwa ile ya serikali tatu ni wale ambao hawataki muungano kabisa. Wanaotaka serikali mbili ni wachache sana hasa viongozi tu na wale wanaofaidi muungano huu kwa ufisadi. Hivyo ninawaomba wabunge wasome hisia za watu wasiendeleze matakwa ya serikali katika hili. Wabunge waazimie na kubadilisha sheria ya mchakato ili kuwepo na umuhimu wa kupiga kura ya maoni kuhusu muungano wananchi wautao kwanza. Kama ni serikali tatu, basi mchakato wa kutenegeneza katiba ya kila nchi ifanyike kwanza ikifuatiwa na mchakato wa katiba ya muungano. Hii ndio sawa yake. Kama serikali haitasikia hili, mimi ninadhani wananchi (WaTanganyika) wanapoenda kwenye mikutano ya maoni, wasichangie mengine zaidi ya kutaka Tanganyika izaliwe na tuunde katiba yake ndipo tuanze kujadili namna ya kuungana. Kwa maneno mengine muungano uvunjwe kwanza ili tuifufue Tanganyika. Baada ya hapo tujadili muungano tuutao. Mimi kama mimi na familia yangu tumesimamia hili. Je wewe?

Watu kama nyinyi, hakika ni thinkers. Nimekusoma na reputation yangu juu.
 
Analyse kwanza faida ya muungano wa serikali tatu ueleweke kwani kwa sasa bado hatujui tukiwa na aina hiyo utasaidiaje katika kukuza uchumi wa nchi zaidi ya kuongeza gharama za kuendesha serikali na mwananchi wa kawaida ndiye atakayezidi kuumia kura yangu kwa sasa kama ni muungano ni wa serikali moja ili kupunguza gharama za uendeshaji .From what I think kwa sasa tungejadili kwa hoja zenye mashiko namna ya kwaconvince wazenji wakafiki muungano wa serikali moja.That`s is my opinion
 
Analyse kwanza faida ya muungano wa serikali tatu ueleweke kwani kwa sasa bado hatujui tukiwa na aina hiyo utasaidiaje katika kukuza uchumi wa nchi zaidi ya kuongeza gharama za kuendesha serikali na mwananchi wa kawaida ndiye atakayezidi kuumia kura yangu kwa sasa kama ni muungano ni wa serikali moja ili kupunguza gharama za uendeshaji .From what I think kwa sasa tungejadili kwa hoja zenye mashiko namna ya kwaconvince wazenji wakafiki muungano wa serikali moja.That`s is my opinion

Nakubakiana na wewe kwa msingi, kwamba serikali moja, ni cheap. but cheap may be expensive.
Raisi atabaki mmoja Wa Tanzania
Raisi wa zanzibar mmoja, na makamo moja
Raisi wa tanganyika mmoja

Baraza la mawaziri litabaki kama lilivyo, yaani wa muungano watakwenda muungano, wa bara ambao wanaitwa wa muungano, watabaki bara, na zanzibar

Mawaziri wakuu watakuwa wawili au watatu (Sasa wako wawili), Kwanza tunaweza kuondoa hii nafasi.

Baraza la mawaziri lipunguzwe

Bunge:
Zanzibar: Baraza la wawakilishi Litakuwa bunge la zanzibar (Jimbo litakuwa na mbunge tu hakuna haja ya kuwa na wawakilishi wawili

Tanganyika: Majimbo yaridi kiwilaya, hawa wabunge wengi sana, kama kuna haja ya kuongeza majimbo basi na wilaya ziongezwe, sio kutengenezeana majimbo.

Wabunge wawe wenyeviti wa wiliaya, Hatutakuwa na haja ya wakuu wa wilaya (Nafasi kibao zitafutika). Kumbuka kuna DAS na Mkurugenzi upande wa serikali.

Nkadhalika,

Jamhuri ya muungano, iwe na wabunge wachache sana, ikiwezekana wawe wa mikoa, na hawa pia wanaweza kuwa wakuu wa mikoa.

Sasa hapa inabidi tufanye hesabu kama kweli kutakuwa na ongezeko la gharama.

Kupanga ni kuchagua,
Lakini ndugu yangu we kazana kuwahamasisha hao jamaa kuhusu serikali moja. mimi nimeshindwa.
 
Tatizo moja nililogundua toka kwa ndugu zenu kutoka tanganyika ni ile kujiona wamesoma sana lakin hawajatambua kuwa KUSOMA SI MALI KAMA HUJAELIMIKA.
Wanahitaji darsa kubwa sana la kuwaelimisha na sio kumalizo vyumba vyote vya madarasa kwa kukariri na kujiita msomi.

Msomi mzuri ni yule aliyeelimika
Kweli dokta Barubaru.
Sigara ya kuokota haindoshi hamu
 
Back
Top Bottom