Kalunguine
JF-Expert Member
- Jul 27, 2010
- 2,543
- 134
Kwa kuangalia mwenendo wa siasa katika nchi yetu, hakuna uhakika kama wanasiasa katika nchi yetu wanajadiliwa kwa usawa. Je kuna usawa? Kama upo ni kwa namna gani upo? Na kama haupo ni kwa nini na kitu gani kifanyike kurekebisha hali hii. Naomba suala hili lijadiliwe bila upendeleo yaani bila kuegemea upande mmoja. Mjadala uzingatie katiba, sera na sheria za sasa katika nchi yetu au nini kifanyike katika kurekebisha katiba, sera na sheria za nchi katika kuleta usawa na kwa manufaa ya wananchi wote. Nawasilisha.