Katiba Mpya ya Kenya imeshindwa kutatua mambo muhimu

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,315
45,624
Ikiwa ni miaka 13 tangu Kenya iwe na katiba mpya bado katiba hiyo inaonekana kushindwa kutatua mambo ya msingi, haya ni baadhi

1. Ufisadi na Rushwa
Kenya bado inaendela kuwa mojawapo ya mataifa yenye kiwango kikubwa cha ufisadi barani Africa. Pesa za umma zinaibwa kwa kiwango cha juu sana. Katiba yao mpya haijaleta utofauti wowote katika suala hili.

2.Ukabila
Tatizo la ukabila bado ni sugu Kenya. Kura katika uchaguzi bado zinapigwa kwa mrengo wa makabila, ajira katika baadhi ya kaunti zinatolewa kwa ukabila, pia ajira za serikali kuu awamu zinatolewa kwa ukabila ambapo nafasi nyingi muhimu zinachukuliwa na watu kabila la Ruto, mfano katika wizara ya nishati ya Kenya nafasi zote za juu wamepewa Wakalenjini.

3.Udini
Kwa sasa nchini Kenya hakuna msitari kati ya dini, siasa na uongozi. Siasa zinafanyika katika makanisa na misikiti na pia dini hasa ya Ukristo imegeuza ofisi za serikali hasa Ikulu kuwa jukwaa lake la mahuburi na ibada.
 
Katiba inahitaji raia waadilifu kuisimamia na kuilinda. Hata hivyo, kuwa na katiba nzuri ni jambo moja na kuilinda isivunjwe ni jingine. Sasa, siyo sawa na haikubaliki kutumia kutokuwepo la pili kupinga la kwanza.

Ni waovu (wanaonufaika na katiba mbovu) au wajinga wanaopinga katiba mpya.
 
Katiba inahitaji raia waadilifu kuisimamia na kuilinda.
Hata hivyo, kuwa na katiba nzuri ni jambo moja na kuilinda isivunjwe ni jingine. Sasa, siyo sawa na haikubaliki kutumia kutokuwepo la pili kupinga la kwanza. Ni waovu (wanaonufaika na katiba mbovu) au wajinga wanaopinga katiba mpya.
Watu waadilifu ndilo jambo la muhimu zaidi, pia katiba nzuri ni muhimu sana na iliyopo inaweza kuboreshwa kufanywa nzuri zaidi.
 
Sawa, ila katiba mpya iko pale pale. Hututaki kuiga mtu
Tunapaswa kutazama na kujifunza kwa hao wanaosifiwa kuwa na katiba nzuri ili kutorudia makosa na kutopoteza muda.
 
Kuna majitu hayakuelewi.
Comparison analysis studies.

Unapo analyse kitu scientifically lazima uwe na vigezo vya kuangalia ili ulinganishe. Vingnevyo ni kutaka watu wenye upteo mkubwa wajadili vijihoja ambavyo mwisho wa siku ni viroja!

Hapa tunajadili masuala/ issues siyo vihoja. Tanzania ni Kenya?
 
Comparison analysis studies
Unapo analyse kitu scientifically lazima uwe na vigezo vya kuangalia ili ulinganishe. Vingnevyo ni kutaka watu wenye upteo mkubwa wajadili vijihoja ambavyo mwisho wa siku ni viroja!
Hapa tunajadili masuala/ issues siyo vihoja ! Tanzania ni Kenya?
Huna lolote uelewalo wewe.
 
Ikiwa ni miaka 13 tangu Kenya iwe na katiba mpya bado katiba hiyo inaonekana kushindwa kutatua mambo ya msingi, haya ni baadhi...
Binafsi sijui kama ni katiba ndiyo" imeshindwa"; lakini ninalojua isingekuwa katiba hiyo kuwepo Kenya, sasa hivi nchi hiyo ingekuwa na hali tofauti sana.

Kuna mambo muhimu zaidi yaliyoepushwa na uwepo wa Katiba hiyo nchini humo.

Kwa hiyo usisahauupande huo wa pili.
 
Katiba inahitaji raia waadilifu kuisimamia na kuilinda.
Hata hivyo, kuwa na katiba nzuri ni jambo moja na kuilinda isivunjwe ni jingine. Sasa, siyo sawa na haikubaliki kutumia kutokuwepo la pili kupinga la kwanza. Ni waovu (wanaonufaika na katiba mbovu) au wajinga wanaopinga katiba mpya.
Nitaongezea umuhimu wa kuwepo kwa viongozi wenye nia ya kujenga utaifa wao.

Hayo maswala ya "ukabila" kwa mfano, kama viongozi ndio wangekuwa mstari wa mbele kuyakataa na kusisitiza utaifa wa nchi yao, ukabila usingekuwa na nguvu. Badala yake sasa, viongozi hao hao ndio wanaozidi kuuchochea ukabila wenyewe.

Wananchi kuwa waadilifu kunatokana na kuwepo kwa haki kwa wote bila kujali tofauti zao za kikabila wala kidini. Uadilifu unajengeka juu ya haki na usawa kwa raia wote.

Kwa hiyo, nafasi ya uongozi wa nchi ni muhimu sana katika kujenga uadilifu wa wananchi, na kujiona kuwa wamoja kama taifa.
 
Ikiwa ni miaka 13 tangu Kenya iwe na katiba mpya bado katiba hiyo inaonekana kushindwa kutatua mambo ya msingi, haya ni baadhi....
Muhimu katika katiba ya JMT ni kutupatia kiongozi aliyechaguluwa kwa ridhaa ya Watanzania wenyewe. Kuwasimamia hao viongozi tuliowachagua wenyewe hiyo ni secondary.

Kwa hiyo tunahitaji katiba itakayotupatia tume huru ya kuwachagua viongozi wetu wenyewe! From there uadilifu wa viongozi tutausimamia wenyewe hata kwa kuwatandika bakora!
 
Back
Top Bottom