Katiba mpya Tanzania

Mroojr

Member
Nov 15, 2010
65
8
Kidogo kidogo kumeanza kuzuka mjadala na hoja za kutengenezwa katiba mpya Tanzania. Mjadala huu na hoja hii ianzishwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani na kujaribu kushawishi wananchi kuunga mkono hoja hii. Lakini mimi najiuliza kitu kimoja kichwani kwangu. Asilimia 90 kama sio 95 ya watanzania hatuijui kwanza katiba iliyopo. Hatuyajui kabisa yale yaliyomo ktk katiba iliyopo yanayotakiwa kuondolewa au kufanyiwa marekebisho. Tutakachounga mkono ktk katiba hii mpya ni kipi ikiwa yazamani yenyewe hatuijui! Mimi ninachoshauri mimi ni kwamba hao wanaotushawishi kuunga mkono katiba mpya wasilifanyie haraka hili waandae semina mbalimbali na warsha nyingi kuwaelisha wananchi kipi kimepitwa na wakati,kipi kiondolewe na kipi kirekebishwe ktk katiba ya zamani ndio itakuwa rahisi kwetu kuunga mkono au lah. Huo uharaka wao wa kudai katiba mpya utatutia mashaka kuwa pengine itakuwa kwa maslahi yao. Hapa nimewasemea watanzania walio wengi.
 
Wazamivu watatatuwakilisha!!elimu ya uraia yenyewe haijawafikia wananchi!wengine hawajui nini vyama vingi!!hivyo walio na huelewa wakatiba hii wanatosha kutuwakilisha!!kwakuwa kutakuwepo maoni watu watatoa maoni kama una kumbuka white paper ndo itakavyo kuwa!
 
Wewe umewasilisha mawazo yako,na si ya watanzania waliowengi bana.
Hivi unataka kuniambia watu wote[pamoja na wewe] wanaokwenda misikitini na
makanisani kwenda kumuabudu muumba wetu, Je hao watu wote wanajua Bible na
kuran vinaongeanini kuhusu dini zao? Hapo ulipo hujui hata kitabu cha dini yako hata
misitari 2 na haujasema kuwa JAMANI TUSIENDE KWENYE NYUMBA ZA IBADA MPAKA
mashekhe na wachungaji watuelimishe maandiko yote ndani ya vitabu vya mungu!
au kwako wewe katiba ni muhimu kuliko mungu? Acha usanii wako hapa. Watanzania
tuliowengi tunahitaji katiba mpya haraka iwezekanavyo.
 
Kidogo kidogo kumeanza kuzuka mjadala na hoja za kutengenezwa katiba mpya Tanzania. Mjadala huu na hoja hii ianzishwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani na kujaribu kushawishi wananchi kuunga mkono hoja hii. Lakini mimi najiuliza kitu kimoja kichwani kwangu. Asilimia 90 kama sio 95 ya watanzania hatuijui kwanza katiba iliyopo. Hatuyajui kabisa yale yaliyomo ktk katiba iliyopo yanayotakiwa kuondolewa au kufanyiwa marekebisho. Tutakachounga mkono ktk katiba hii mpya ni kipi ikiwa yazamani yenyewe hatuijui! Mimi ninachoshauri mimi ni kwamba hao wanaotushawishi kuunga mkono katiba mpya wasilifanyie haraka hili waandae semina mbalimbali na warsha nyingi kuwaelisha wananchi kipi kimepitwa na wakati,kipi kiondolewe na kipi kirekebishwe ktk katiba ya zamani ndio itakuwa rahisi kwetu kuunga mkono au lah. Huo uharaka wao wa kudai katiba mpya utatutia mashaka kuwa pengine itakuwa kwa maslahi yao. Hapa nimewasemea watanzania walio wengi.

Soma hoja za Tume ya Nyarari aliyoiunda Mkapa!
 
Wewe acha unafiki kwani umeingia lini jamvini hivi hujui kuna mambo mengi yanatakiwa kubadilika? Hujui kama kuna haki ya mgombea binafis imefinywa, je hujui uchakachuaji wa tume ya uchaguzi, je hujui kama watawala wako juu ya sheria?, je hujui kama principal of separation of pewers haipo tanzania? Mbunge anakuwa waziri, nini kazi ya mkuu wa wilaya wakati mkurugenzi yupo?, kwanini pccb, cag wawajibike kwa rais?, je hujui rais anao uwezo wa kuteua hata baraza la watu 200?, je hujui yote hayo??? Acha uzandiki soma ripoti ya nyalali utaelewa una point kuwae,emisha watanzania wengine lakini sio wewe ambae upo jamvini au umetumwa kama ni hivyo basi wewe sio great thinker, tafuta soft copy ipo humu jamvini ya katiba usome utaelewa.
 
wewe acha unafiki kwani umeingia lini jamvini hivi hujui kuna mambo mengi yanatakiwa kubadilika? Hujui kama kuna haki ya mgombea binafis imefinywa, je hujui uchakachuaji wa tume ya uchaguzi, je hujui kama watawala wako juu ya sheria?, je hujui kama principal of separation of pewers haipo tanzania? Mbunge anakuwa waziri, nini kazi ya mkuu wa wilaya wakati mkurugenzi yupo?, kwanini pccb, cag wawajibike kwa rais?, je hujui rais anao uwezo wa kuteua hata baraza la watu 200?, je hujui yote hayo??? Acha uzandiki soma ripoti ya nyalali utaelewa una point kuwae,emisha watanzania wengine lakini sio wewe ambae upo jamvini au umetumwa kama ni hivyo basi wewe sio great thinker, tafuta soft copy ipo humu jamvini ya katiba usome utaelewa.
nchi hii inavilaza wengi ndugu yangu unaweza kuzimia kwa huruma hiyo mijitu huwa tunaiacha kama ilivyo1
 
Muda muafaka ukifika hata iweje lazima mabadiliko yawepo. It high time katiba mpya inahitajika ili kuleta ukombozi kisiasa, kijamii na kiuchumi katika nchi hii.
 
Wewe acha unafiki kwani umeingia lini jamvini hivi hujui kuna mambo mengi yanatakiwa kubadilika? Hujui kama kuna haki ya mgombea binafis imefinywa, je hujui uchakachuaji wa tume ya uchaguzi, je hujui kama watawala wako juu ya sheria?, je hujui kama principal of separation of pewers haipo tanzania? Mbunge anakuwa waziri, nini kazi ya mkuu wa wilaya wakati mkurugenzi yupo?, kwanini pccb, cag wawajibike kwa rais?, je hujui rais anao uwezo wa kuteua hata baraza la watu 200?, je hujui yote hayo??? Acha uzandiki soma ripoti ya nyalali utaelewa una point kuwae,emisha watanzania wengine lakini sio wewe ambae upo jamvini au umetumwa kama ni hivyo basi wewe sio great thinker, tafuta soft copy ipo humu jamvini ya katiba usome utaelewa.

Unaweza tuwekea ripoti ya tume ya nyalali mkuu? Au kwa mwenye nayo pleaseeeeeeeeeeee soft copy aturushie
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom