Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,887
- 143,983
Ukifuatilia mijadala bungeni tangu kuanza kwa mchakato wa katiba mpya na huu mjadala unaoendelea sasa kuhusu muswada wa sheria ya kura ya maoni utagundua kuna mgawanyiko mkubwa kwa misingi ya itikadi za kisiasa.Ni jambo la kusikitisha kuwa mijadala ya wabunge juu ya jambo hili iko kisiasa zaidi badala ya kuwa ya kitaifa.
Ninachokiona hapa ni kuwa mgawanyiko huo hautaushia bungeni tu bali utahamia uraiani mara campain zitakapoaanza juu ya upigaji kura ya maoni kuhusu katiba mpya.Campain hizi zitakuwa ni zaidi ya zile za uchaguzi mkuu kwani kuna uwezekano mkubwa wa baadhi ya vyama vya siasa kuunganisha nguvu na hapa ndipo patakapokuwa msingi wa msuguano mkubwa na hatimae machafuko makubwa.
Wanasiasa ndani na nje ya bunge tambueni kuwa mkishindwa kuelewana juu ya jambo hili basi mjue kuwa "katiba mpya ni bomu linalosubiri kulipuka".Tena yawapasa kutambua kuwa hili ni bomu hatari kuliko hata lile la vijana kukosa ajira.
Ninachokiona hapa ni kuwa mgawanyiko huo hautaushia bungeni tu bali utahamia uraiani mara campain zitakapoaanza juu ya upigaji kura ya maoni kuhusu katiba mpya.Campain hizi zitakuwa ni zaidi ya zile za uchaguzi mkuu kwani kuna uwezekano mkubwa wa baadhi ya vyama vya siasa kuunganisha nguvu na hapa ndipo patakapokuwa msingi wa msuguano mkubwa na hatimae machafuko makubwa.
Wanasiasa ndani na nje ya bunge tambueni kuwa mkishindwa kuelewana juu ya jambo hili basi mjue kuwa "katiba mpya ni bomu linalosubiri kulipuka".Tena yawapasa kutambua kuwa hili ni bomu hatari kuliko hata lile la vijana kukosa ajira.