Katiba Mpya na Tume Huru siyo Mkombozi katika suala zima la kuwa na Siasa za Ushindani

DaudiAiko

JF-Expert Member
Dec 2, 2012
302
274
Wanabodi,

Mfumo wa vyama vingi ulianzishwa Tanzania kwa madhumuni ya kuruhusu vyama mbadala kushiriki katika kila chaguzi na kuenzi suala zima la demokrasia kwa kuwa wezesha wananchi kuchagua viongozi wao baada ya kusikiliza na kuelewa sera tofauti tofauti.

Demokrasia zilizo komaa huwezesha mabadiliko mazuri ya kila awamu ya uongozi. Mabadiliko haya ya uongozi yanatakiwa yafanyike vizuri hata katika vipindi ambavyo chama tawala kinashindwa uchaguzi wa urais na hivyo kutakiwa kuruhusu chama cha upinzani kushika wadhifa mkubwa wa uongozi kuliko yote. Lakini je mifumo iliyopo ina uwezo wa kuruhusu mabadiliko haya?

Katika uongozi, aliye katika nafasi ya juu hutegemea sana walio katika nafasi za chini kutekeleza wadhifa wao. Kwasababu hiyo rais yeyote hawezi kufanya kazi yake vizuri bila vyombo mbalimbali vya usalama.

Vyombo hivi ni kama idara ya usalama wa taifa, polisi, jeshi la wananchi bila kusahau watumishi wa umma katika sekta tofauti tofauti serikalini kama vile ofisi ya rais, ofisi ya makamu wa rais, ofisi ya waziri mkuu, ikulu, bunge na wizara zote kwa ujumla.

Swali zito ambalo wote tunatakiwa kujiuliza ni kama waliopo kwenye vyombo hivi wanaweza kuheshimu maamuzi yoyote yanayoweza kufanywa na wananchi na kumpokea mgombea yeyote wa chama chochote madarakani.

Katika demokrasia ya ukweli na demokrasia iliyo komaa, vyombo hivi vyote vinatakiwa kuweza kushirikiana na chama chochote cha siasa na kwasababu hiyo, kuna umuhimu wa kuwa "Neutral" na kusisitiza utanzania kwanza.

Jambo ambalo sisi wananchi hatu fahamu ni kama wahusika wa vyombo hivi wana pendelea zaidi chama tawala kuendelea kubaki madarakani. Kama hii ni kweli, basi kuna "Forces" nyingi sana zinazo hakikisha kwamba chama tawala kina endelea kubaki madarakani na demokrasia yetu siyo ya kweli.

Nawasihi wana JF wenzangu waendelee kutafakari haya yote. Labda tume huru ya uchaguzi na katiba mpya havina uhusiano mkubwa katika suala zima la kuwa na siasa zenye ushindani.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
 
Wanabodi,

Mfumo wa vyama vingi ulianzishwa Tanzania kwa madhumuni ya kuruhusu vyama mbadala kushiriki katika kila chaguzi na kuenzi suala zima la demokrasia kwa kuwa wezesha wananchi kuchagua viongozi wao baada ya kusikiliza na kuelewa sera tofauti tofauti.

Demokrasia zilizo komaa huwezesha mabadiliko mazuri ya kila awamu ya uongozi. Mabadiliko haya ya uongozi yanatakiwa yafanyike vizuri hata katika vipindi ambavyo chama tawala kinashindwa uchaguzi wa urais na hivyo kutakiwa kuruhusu chama cha upinzani kushika wadhifa mkubwa wa uongozi kuliko yote. Lakini je mifumo iliyopo ina uwezo wa kuruhusu mabadiliko haya?

Katika uongozi, aliye katika nafasi ya juu hutegemea sana walio katika nafasi za chini kutekeleza wadhifa wao. Kwasababu hiyo rais yeyote hawezi kufanya kazi yake vizuri bila vyombo mbalimbali vya usalama.

Vyombo hivi ni kama idara ya usalama wa taifa, polisi, jeshi la wananchi bila kusahau watumishi wa umma katika sekta tofauti tofauti serikalini kama vile ofisi ya rais, ofisi ya makamu wa rais, ofisi ya waziri mkuu, ikulu, bunge na wizara zote kwa ujumla.

Swali zito ambalo wote tunatakiwa kujiuliza ni kama waliopo kwenye vyombo hivi wanaweza kuheshimu maamuzi yoyote yanayoweza kufanywa na wananchi na kumpokea mgombea yeyote wa chama chochote madarakani.

Katika demokrasia ya ukweli na demokrasia iliyo komaa, vyombo hivi vyote vinatakiwa kuweza kushirikiana na chama chochote cha siasa na kwasababu hiyo, kuna umuhimu wa kuwa "Neutral" na kusisitiza utanzania kwanza.

Jambo ambalo sisi wananchi hatu fahamu ni kama wahusika wa vyombo hivi wana pendelea zaidi chama tawala kuendelea kubaki madarakani. Kama hii ni kweli, basi kuna "Forces" nyingi sana zinazo hakikisha kwamba chama tawala kina endelea kubaki madarakani na demokrasia yetu siyo ya kweli.

Nawasihi wana JF wenzangu waendelee kutafakari haya yote. Labda tume huru ya uchaguzi na katiba mpya havina uhusiano mkubwa katika suala zima la kuwa na siasa zenye ushindani.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Hujui kitu unabwabwaja tu.
Unao muda wa kupoteza, na ni haki yako kufanya hivyo. Au pengine hii ndiyo kazi mahsusi inayokupa fursa ya kwenda chooni, baada ya kutupiwa visenti kadhaa!

Watu kama nyinyi hamtofautiani sana na yale makaratasi myololo yaliypo kule msalani. Mnatumiwa tu na kutupwa humo humo baada ya kufanya kazi chafu.

Hovyo kabisa!
 
Wanabodi,

Mfumo wa vyama vingi ulianzishwa Tanzania kwa madhumuni ya kuruhusu vyama mbadala kushiriki katika kila chaguzi na kuenzi suala zima la demokrasia kwa kuwa wezesha wananchi kuchagua viongozi wao baada ya kusikiliza na kuelewa sera tofauti tofauti.

Demokrasia zilizo komaa huwezesha mabadiliko mazuri ya kila awamu ya uongozi. Mabadiliko haya ya uongozi yanatakiwa yafanyike vizuri hata katika vipindi ambavyo chama tawala kinashindwa uchaguzi wa urais na hivyo kutakiwa kuruhusu chama cha upinzani kushika wadhifa mkubwa wa uongozi kuliko yote. Lakini je mifumo iliyopo ina uwezo wa kuruhusu mabadiliko haya?

Katika uongozi, aliye katika nafasi ya juu hutegemea sana walio katika nafasi za chini kutekeleza wadhifa wao. Kwasababu hiyo rais yeyote hawezi kufanya kazi yake vizuri bila vyombo mbalimbali vya usalama.

Vyombo hivi ni kama idara ya usalama wa taifa, polisi, jeshi la wananchi bila kusahau watumishi wa umma katika sekta tofauti tofauti serikalini kama vile ofisi ya rais, ofisi ya makamu wa rais, ofisi ya waziri mkuu, ikulu, bunge na wizara zote kwa ujumla.

Swali zito ambalo wote tunatakiwa kujiuliza ni kama waliopo kwenye vyombo hivi wanaweza kuheshimu maamuzi yoyote yanayoweza kufanywa na wananchi na kumpokea mgombea yeyote wa chama chochote madarakani.

Katika demokrasia ya ukweli na demokrasia iliyo komaa, vyombo hivi vyote vinatakiwa kuweza kushirikiana na chama chochote cha siasa na kwasababu hiyo, kuna umuhimu wa kuwa "Neutral" na kusisitiza utanzania kwanza.

Jambo ambalo sisi wananchi hatu fahamu ni kama wahusika wa vyombo hivi wana pendelea zaidi chama tawala kuendelea kubaki madarakani. Kama hii ni kweli, basi kuna "Forces" nyingi sana zinazo hakikisha kwamba chama tawala kina endelea kubaki madarakani na demokrasia yetu siyo ya kweli.

Nawasihi wana JF wenzangu waendelee kutafakari haya yote. Labda tume huru ya uchaguzi na katiba mpya havina uhusiano mkubwa katika suala zima la kuwa na siasa zenye ushindani.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
AKILI NDOGO MPO WENGI SANA
Nani alikudanganya kuwa KATIBA MPYA ni kwa ajili ya USHINDANI?Acheni kuandika Upuuzi na kupotosha Watu.
 
Hujui kitu unabwabwaja tu.
Unao muda wa kupoteza, na ni haki yako kufanya hivyo. Au pengine hii ndiyo kazi mahsusi inayokupa fursa ya kwenda chooni, baada ya kutupiwa visenti kadhaa!

Watu kama nyinyi hamtofautiani sana na yale makaratasi myololo yaliypo kule msalani. Mnatumiwa tu na kutupwa humo humo baada ya kufanya kazi chafu.

Hovyo kabisa!
Mtu mwenye akili siku zote anajibu hoja kwa hoja na sio hoja kwa majungu. Kichefuchefu chako kilicho kufanya utapike kwenye uzi huu pamoja na uwezo wako mfinyu wa kufikiria kuna thibitisha kwamba kweli wewe ni boya. Hebu tafuta kitu cha maana cha kufanya
 
AKILI NDOGO MPO WENGI SANA
Nani alikudanganya kuwa KATIBA MPYA ni kwa ajili ya USHINDANI?Acheni kuandika Upuuzi na kupotosha Watu.
Kweli kuna vipofu wengi sana JF. Katiba mpya na tume huru ni vitu vya ziada kama mifumo iliyopo ina ruhusu uendeshaji mzuri wa serikali kwa chama chochote cha siasa. Chukua spana, fungua boneti tuone kuna nini
 
Hata ukienda kumuona daktari hospitali ukiwa mgonjwa sio uhakika wa kwamba utapona lakini huwezi kuacha kwenda hospitali ukiwa mgonjwa eti sababu huna uhakika kama utapona.
 

Katiba mpya haiwezi kuwa suluhisho kama bado watanzania wana tabia za kichawa na kujikombakomba.

Leo hii tuna taasisi huru kikatiba, lakini viongozi wa hizo taasisi wanaulinda huo uhuru?

Tunahitaji kwanza watu huru ndipo tuanze kusumbuka na katiba mpya.

Nafikiri wote mliona vile Prof. Assad alivyopambana kulinda uhuru wa taasisi aliyokuwa akiiongoza 'mazuzu' walivyomuandama na hata kumtoa kihuni. Tunahitaji watu huru kuanzia pale juu kwenye ofisi kuu.
 
Wanabodi,

Mfumo wa vyama vingi ulianzishwa Tanzania kwa madhumuni ya kuruhusu vyama mbadala kushiriki katika kila chaguzi na kuenzi suala zima la demokrasia kwa kuwa wezesha wananchi kuchagua viongozi wao baada ya kusikiliza na kuelewa sera tofauti tofauti.

Demokrasia zilizo komaa huwezesha mabadiliko mazuri ya kila awamu ya uongozi. Mabadiliko haya ya uongozi yanatakiwa yafanyike vizuri hata katika vipindi ambavyo chama tawala kinashindwa uchaguzi wa urais na hivyo kutakiwa kuruhusu chama cha upinzani kushika wadhifa mkubwa wa uongozi kuliko yote. Lakini je mifumo iliyopo ina uwezo wa kuruhusu mabadiliko haya?

Katika uongozi, aliye katika nafasi ya juu hutegemea sana walio katika nafasi za chini kutekeleza wadhifa wao. Kwasababu hiyo rais yeyote hawezi kufanya kazi yake vizuri bila vyombo mbalimbali vya usalama.

Vyombo hivi ni kama idara ya usalama wa taifa, polisi, jeshi la wananchi bila kusahau watumishi wa umma katika sekta tofauti tofauti serikalini kama vile ofisi ya rais, ofisi ya makamu wa rais, ofisi ya waziri mkuu, ikulu, bunge na wizara zote kwa ujumla.

Swali zito ambalo wote tunatakiwa kujiuliza ni kama waliopo kwenye vyombo hivi wanaweza kuheshimu maamuzi yoyote yanayoweza kufanywa na wananchi na kumpokea mgombea yeyote wa chama chochote madarakani.

Katika demokrasia ya ukweli na demokrasia iliyo komaa, vyombo hivi vyote vinatakiwa kuweza kushirikiana na chama chochote cha siasa na kwasababu hiyo, kuna umuhimu wa kuwa "Neutral" na kusisitiza utanzania kwanza.

Jambo ambalo sisi wananchi hatu fahamu ni kama wahusika wa vyombo hivi wana pendelea zaidi chama tawala kuendelea kubaki madarakani. Kama hii ni kweli, basi kuna "Forces" nyingi sana zinazo hakikisha kwamba chama tawala kina endelea kubaki madarakani na demokrasia yetu siyo ya kweli.

Nawasihi wana JF wenzangu waendelee kutafakari haya yote. Labda tume huru ya uchaguzi na katiba mpya havina uhusiano mkubwa katika suala zima la kuwa na siasa zenye ushindani.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Kichwa cha habari kimekuangusha ,unaweza kuwa Ulikua na maana nzuri. Angalia wanavyokushambulia Great Thinkers humu.
 

Katiba mpya haiwezi kuwa suluhisho kama bado watanzania wana tabia za kichawa na kujikombakomba.

Leo hii tuna taasisi huru kikatiba, lakini viongozi wa hizo taasisi wanaulinda huo uhuru?

Tunahitaji kwanza watu huru ndipo tuanze kusumbuka na katiba mpya.

Nafikiri wote mliona vile Prof. Assad alivyopambana kulinda uhuru wa taasisi aliyokuwa akiiongoza 'mazuzu' walivyomuandama na hata kumtoa kihuni. Tunahitaji watu huru kuanzia pale juu kwenye ofisi kuu.
Katiba ndiyo msingi wa watu kuwa huru. Kumbuka uhuru hutafutwa, sasa kama Katiba imenyonga watu kutafuta uhuru wao je watu watakuaje huru?
 
Hata ukienda kumuona daktari hospitali ukiwa mgonjwa sio uhakika wa kwamba utapona lakini huwezi kuacha kwenda hospitali ukiwa mgonjwa eti sababu huna uhakika kama utapona.
Ni kweli
 

Katiba mpya haiwezi kuwa suluhisho kama bado watanzania wana tabia za kichawa na kujikombakomba.

Leo hii tuna taasisi huru kikatiba, lakini viongozi wa hizo taasisi wanaulinda huo uhuru?

Tunahitaji kwanza watu huru ndipo tuanze kusumbuka na katiba mpya.

Nafikiri wote mliona vile Prof. Assad alivyopambana kulinda uhuru wa taasisi aliyokuwa akiiongoza 'mazuzu' walivyomuandama na hata kumtoa kihuni. Tunahitaji watu huru kuanzia pale juu kwenye ofisi kuu.
Kama ni kweli kwamba taasisi zote za kiusalama zote zina wana CCM basi hata ije katiba ipi, siasa zetu zitazidi kuwa za chama kimoja
 
Wanabodi,

Mfumo wa vyama vingi ulianzishwa Tanzania kwa madhumuni ya kuruhusu vyama mbadala kushiriki katika kila chaguzi na kuenzi suala zima la demokrasia kwa kuwa wezesha wananchi kuchagua viongozi wao baada ya kusikiliza na kuelewa sera tofauti tofauti.

Demokrasia zilizo komaa huwezesha mabadiliko mazuri ya kila awamu ya uongozi. Mabadiliko haya ya uongozi yanatakiwa yafanyike vizuri hata katika vipindi ambavyo chama tawala kinashindwa uchaguzi wa urais na hivyo kutakiwa kuruhusu chama cha upinzani kushika wadhifa mkubwa wa uongozi kuliko yote. Lakini je mifumo iliyopo ina uwezo wa kuruhusu mabadiliko haya?

Katika uongozi, aliye katika nafasi ya juu hutegemea sana walio katika nafasi za chini kutekeleza wadhifa wao. Kwasababu hiyo rais yeyote hawezi kufanya kazi yake vizuri bila vyombo mbalimbali vya usalama.

Vyombo hivi ni kama idara ya usalama wa taifa, polisi, jeshi la wananchi bila kusahau watumishi wa umma katika sekta tofauti tofauti serikalini kama vile ofisi ya rais, ofisi ya makamu wa rais, ofisi ya waziri mkuu, ikulu, bunge na wizara zote kwa ujumla.

Swali zito ambalo wote tunatakiwa kujiuliza ni kama waliopo kwenye vyombo hivi wanaweza kuheshimu maamuzi yoyote yanayoweza kufanywa na wananchi na kumpokea mgombea yeyote wa chama chochote madarakani.

Katika demokrasia ya ukweli na demokrasia iliyo komaa, vyombo hivi vyote vinatakiwa kuweza kushirikiana na chama chochote cha siasa na kwasababu hiyo, kuna umuhimu wa kuwa "Neutral" na kusisitiza utanzania kwanza.

Jambo ambalo sisi wananchi hatu fahamu ni kama wahusika wa vyombo hivi wana pendelea zaidi chama tawala kuendelea kubaki madarakani. Kama hii ni kweli, basi kuna "Forces" nyingi sana zinazo hakikisha kwamba chama tawala kina endelea kubaki madarakani na demokrasia yetu siyo ya kweli.

Nawasihi wana JF wenzangu waendelee kutafakari haya yote. Labda tume huru ya uchaguzi na katiba mpya havina uhusiano mkubwa katika suala zima la kuwa na siasa zenye ushindani.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
KINACHOHIYAJIKA !!

WATU IMARA ,Hawa watapatikana kwa wachache waliopo Sasa kuendelea kuwaelimisha na kuhamasisha bila kuchoka walio wengi umuhimu na manufaaa ya kuwa na Katiba mpya itakayoendana na maisha ya Sasa ya jamii,,

Watu imara hao wakiwa wengi nnawameshajua nn Cha kufanya Sasa ndio kwa wingi wao na nguvu Yao ,wataaamua Sasa tutengeneze KATIBA MPYA , inayoendana na maisha ya Sasa ya jamii yetu ,,

Humo ndani ya KATIBA MPYA ndipo patazaa Sasa , STRONG INSTITUTIONS zitakazokuwa kwenye idara mbali mbali Katika nchi yetu
Polisi
Magerezaa
Jeshi
Elimu
Afya
Biashara
,,
Sasa Kama umeshatengeneza katiba mpya inayotakiwa na wananchi na hao wananchi wanaamua na wameweka mipaka na kila kitu Cha uongozi ,

Hapo ndipo ushindani wa kisiasa by free and fair utakuwepo

##Tunachojua ,kitupi tu ###,

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Katiba na tume huru ndio njia sahihi ya kuwadhibiti wavaa mashati ya kijani waliokithiri kwa wizi wa kura,huwezi kumdhibiti kibaka wakati hakuna sheria inayokupa nguvu ya kumdhibiti.
 
KINACHOHIYAJIKA !!

WATU IMARA ,Hawa watapatikana kwa wachache waliopo Sasa kuendelea kuwaelimisha na kuhamasisha bila kuchoka walio wengi umuhimu na manufaaa ya kuwa na Katiba mpya itakayoendana na maisha ya Sasa ya jamii,,

Watu imara hao wakiwa wengi nnawameshajua nn Cha kufanya Sasa ndio kwa wingi wao na nguvu Yao ,wataaamua Sasa tutengeneze KATIBA MPYA , inayoendana na maisha ya Sasa ya jamii yetu ,,

Humo ndani ya KATIBA MPYA ndipo patazaa Sasa , STRONG INSTITUTIONS zitakazokuwa kwenye idara mbali mbali Katika nchi yetu
Polisi
Magerezaa
Jeshi
Elimu
Afya
Biashara
,,
Sasa Kama umeshatengeneza katiba mpya inayotakiwa na wananchi na hao wananchi wanaamua na wameweka mipaka na kila kitu Cha uongozi ,

Hapo ndipo ushindani wa kisiasa by free and fair utakuwepo

##Tunachojua ,kitupi tu ###,

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Kweli kabisa. Hizi strong institutions zinatakiwa ziwe na wawakilishi kutoka vyama vyote vya siasa. Vile vile tunatakiwa kuwa na kanuni inayotoa maelezo kuhusu cha kufanya endapo chama cha upinzani kina ingia madarakani. Leo hii mpinzani akishinda uchaguzi wa urais, institutions zilizopo hazi mruhusu kuendesha serikali
 
Kama ni kweli kwamba taasisi zote za kiusalama zote zina wana CCM basi hata ije katiba ipi, siasa zetu zitazidi kuwa za chama kimoja
Utaitunza hii mkuu, hata tukipata katiba mpya leo hii haitosaidia kitu.

Tuna mifano mingi sana ambayo inatuonyesha kwamba katiba mpya kwa wananchi hawa labda kama nia ni kuongeza ukubwa wa serikali, basi itawasaidia wanasiasa.

Juzi hapo, Spike aliikosoa na kuishauri serikali juu ya kukopa, nini kilifuata? Nakukumbusha kwamba Spika ni mkuu wa mhimili mmoja wa serikali wenye kazi ya kuisimamia na kuishauri serikali. Hii ndio kazi yake kikatiba.

Juzi tena mbunge Bashiru alifanya kazi yake ya kibunge, uliona vile 'mazuzu' walivyo ruka nae ajiuzulu?

Sasa tafakari kama kuna katiba mpya inayoweza kuponya 'mazuzu' kama hao.
 
Back
Top Bottom