Katiba mpya: Muundo wa bunge

mshaurimkuu

Member
Jan 23, 2011
57
30
Ndugu Watanzania na wote wenye mapenzi mema kwa nchi yetu; Salaam.

Kutokana na matatizo mbalimbali ya bunge letu hasa haya yafuatayo:-

(i) Asilimia kubwa ya wabunge kujiona kuwa ni wamiliki wa majimbo wanayoyawakilisha ikishadidiwa na mfumo wa hovyo uliopo ambapo ni rahisi watu kupita kwa rushwa.

(ii) Asilimia kubwa ya wabunge kukimbilia Bungeni si kwa ajili ya uwakilishi wa dhati bali kufuata mishahara na posho nono.

(iii) Asilimia kubwa ya wabunge kutoonekana/kutoishi katika majimbo/maeneo yao ya uwakilishi.

(iv) Uwezekano wa kuwakilishwa na mbunge ambaye mchango wake si mzuri - kusinzia tu bungeni kwa MIAKA MITANO.

Kutokana na hilo, nashauri Katiba ijayo iwe hivi:-

(i) Kusiwe na nafasi ya kugombea kwenye uchaguzi inayojulikana kama Mbunge.

(ii) Badala yake kuwe na MADIWANI tu.

(iii) Madiwani wa jimbo husika wawe pia ndio wabunge wa jimbo hilo.

(iv) Diwani atawakilisha Jimbo Bungeni kwa kipindi cha mwaka mmoja tu kwa mzunguko yaani, kwa mfano kama jimbo lina kata labda saba, kila Bunge jipya linapoanza, Majina ya Kata yapangwe ki-alfabeti.

(v) Diwani wa kata ya kwanza (au ya mwisho kadiri itakavyoonekana inafaa) atawakilisha Jimbo Bungeni kwa mwaka wa kwanza. Utaratibu mwingine mzuri pia wa kupanga Kata ipi ianze uwakilishi unaweza kutumika (kama kupanga majina ya Madiwani ki-alfabeti, kuchagua jina kwa mfumo wa nasibu, n.k.).

(vi) Mwaka wa pili, atafuata diwani wa kata ya pili, hivyo hivyo hadi kata tano za kwanza ziishe.

(vi) Uchaguzi mkuu utakaofuata; wataanza madiwani wa zile kata ambazo hazikuwakilisha jimbo msimu uliopita hadi ziishe halafu tunaanza tena mwanzo - KITU KAMA MDUARA HIVI.

MANUFAA YA MFUMO HUU:

(i) Utaongeza ushirikishwaji zaidi wa wananchi kwani kila kata itawakilisha jimbo badala ya ilivyo sasa ambapo inawezekana mbunge mmoja kutoka eneo moja tu kuwakilisha jimbo kwa hata miaka 30!

(ii) Matumizi mazuri ya rasilimali: Hakutakuwa tena na kitu kinachoitwa gari la mbunge kama mtu binafsi bali gari la mbunge kama ofisi; mwaka ukiisha, gari linakabidhiwa kwa mwakilishi anayefuata.

(iii) Kuwa karibu zaidi na wananchi: Kusema ukweli wabunge wengi wa sasa hawaishi majimboni lakini madiwani wengi wanaishi huko hivyo wanajua vizuri sana shida na matatizo ya maeneo yao kuliko mbunge kwa mfumo wa sasa.

(iv) Mgawanyo mzuri zaidi wa mapato/keki ya taifa: Badala ya wachache kugawana kidogo kilichopo, angalau wigo unaweza kupanuliwa wakapata wengi yaani MARA TANO ZAIDI.

VIKWAZO:

Najua "wasomi" na viongozi wetu wengi wamekariri mambo ya wenzetu huko duniani na kudhani ndio amri au unabii kutoka kwa Mungu ambayo hakuna awezaye kuyabadili. Huwa nachukia sana unapomsikia mtu fulani mkubwa akisema "... tumerithi mfumo wa Westminster na ndio unaoutumika kuendesha Bunge letu". HIVI HATUWEZI KUWA NA KITU CHETU WENYEWE? Kwanini wenzetu wasiige kwetu badala ya sisi ndio wa kuiga tu? Hebu tujaribu mfumo wetu wenyewe maana hii ya wenzetu inatuletea tu matatizo.

Tafadhali jibu kwa hoja.

Naomba kuwasilisha hoja.
 
So interesting!!! Kwa namna nyingine namna ya kuwapata wabunge (madiwani) 5 wawakilishi ni kupiga kura kuchanguaNA miongoni Mwao baada ya uchanguzi ili kuepuka mduara wa milele kila uchanguzi ambao unajenga complexities za muda mrefu kadri mfumo unapozidi endelea na pengine kata mpya kuanzishwa. Kuliweka kuwa practical SIFA ya diwani lazima zipanuliwe (academically) ili kuwezesha kuwa na wawakilishi wanaoweza kuwa na uelewa wa mambo ya kuongoza muhimili wa utungaji sheria, kutoa mwongozo mwema kwa serikali katika bajeti ya mapato na matumizi ya fedha. Aidha, WAZIRI kwa mfumo huo, asiwe mbunge au "DIWANI" kwa mujibu wa dondoo hili. Kuwe na wizara chache sanana kadri iwezekananyo, possibly 20 only NA ZITAMKWE KWENYE KATIBA. DIWANI (mbunge) akifa, chama kilichokuwa na jimbo kiweke mwanachama wake mwingine hadi uchaguzi utakapofuata. HII NI BANA MATUMIZI KIBOKO, NA FEDHA NYINGI ZA SERIKALI ZITAELEKEZWA KWENYE MAENDELEO YA NCHI. Mimi pia ni muumuni wa mambo mapya ya kivyetu, it is so interesting to have some thing of our own context that may shed a new light for others to come and study for...
 
Ndugu Nsimba;

Hakuna suala la kupiga tena kura miongoni mwao, inaweza kuleta rushwa/ufisadi ambao hatutaki kuisikia. Iko hivi:

Diwani akishachaguliwa, automatically ni mbunge, anasubiri mwaka wake wa kuliwakilisha jimbo ufike kutegemea kata yake/jina lake ni la ngapi kwenye mtiririko (alphabetical order). Endapo jimbo lina kata tano (na hivyo madiwani 5), utaona kila kata ina nafasi ya kuliwakilisha jimbo bungeni katika kipindi cha uhai wa Bunge (miaka 5) kwa sababu Diwani anawakilisha kwa mwaka mmoja tu unaofuata jimbo linawakilishwa na kata inayofuata.

Endapo kata ni pungufu ya tano, utaona kuna uwezekano wa ile kata iliyoanza kuliwakilisha jimbo kurudia. Baadaya ya uchaguzi mwingine, zitaanza zile kata ambazo zimewakilisha mara moja tu.

Endapo kata ni zaidi ya tano, utaona baadhi ya kata hazitapata nafasi katika ule mzunguko wa kwanza; hizi ndizo zitakazoanza uwakilishi Bunge linalofuata.

KUMBUKA: Hapa sizungumzii watu, nazungumzia Kata ambazo hudumu milele lakini watu (madiwaji kwa nafsi zao) huja na kupita.

Kwamba ili liwe "practical" bado siamini kwamba madiwani wetu ni mbumbumbu kwamba lazima wawe na sifa za juu sana kielimu. Ndugu yangu, katika suala la uwakilishi kinachotakiwa ni UZALENDO tu na si vinginevyo - hivi huoni wanaotusumbua sana nchi hii ni wasomi mahiri ambao wamegeuka badala ya kuwa na tabaka la wanyonge wamejitumbukiza kwenye ufisadi usiomithilika? Hata hivo kama profesa akiamua kwenda kugombe udiwani mimi sina tatizo na hilo - tuepuke kuweka majitu bungeni kwa muda mrefu (miaka 5) badala ya kuwa msaada yanageuka kuwa mizigo na kero.


Nakubaliana na wewe (na hata ndivyo wananchi wengi wanavyotaka) kwamba waziri asiwe diwani (na hivyo mbunge). Hakuna mduara a milele hapa, miaka mitano ikiisha ni uchaguzi kama kawaida halafu kata husika katika jimbo zinajipanga tena (hata kama kuna mpya iliyoongezwa) ni nani aanze kuliwakilisha jimbo kwa mwaka wa kwanza, vivyo hivyo wa pili, tatu, n.k hadi uchaguzi mkuu mwingine.

Pia faida nyingine ya mfumo huu ambayo sikuitaja awali ni kwamba tofauti na ilivyo sasa ambapo pesa zinatumika kwenye chaguzi ndogo pindi mbunge anapokosa sifa za kuwa mbunge, kwa mfumo unaopendekezwa hapa uchaguzi mdogo ni wa diwani tu ambao hauna gharama kubwa.

Hebu tuachane na kasumba za ku-copy kila kitu kutoka magharibi, hata mfumo wa kuendesha nchi yetu wenyewe? Kama wazee wetu kina Kimweri, Mkwawa, Isike, na watemi wengine wa nyakati hizo waliweza, kizazi hiki kinachojidai kimeendelea kinashindwa nini? Kama kusoma ni kunakili kila kitu, heri kutokusoma.

Nawasilisha.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom