Katiba mpya: Mapendekezo yangu kuhusu uchaguzi wa Rais wa Muungano wa Tanzania

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
waungwana baada ya muamko wa kutaka katiba mpya mm nilikua na mapendekezo haya yafuatayo katika ucahguzi wa kumchagua Rais wa Jamhuri yetu ya muungano.


kwanza ningependa kuona kuwa Rais wa Jamhuri yetu anatoka upande mmoja wa muungano mara moja na inayofuata atoke upande mwengine (nnakusudia nchi zilizounda muungano sio tuache tu mtu yeyote kutoka upande wowote awanie hii huenda ikazaa malalamiko ambayo kwa chini chini yapo kuwa upande mmoja wa muungano unatawaliwa na upande mmoja unatawala).

Pointi ya pili ni kuhusu kura ambazo zinamuweka Rais madarakani, ningependekeza Rais wa Jamhuri wa muungano lazima ashinde kwa zaidi asilimia hamsini kwa kura za Kila upande wa jamhuri na sio kuzihesabu kura zote na kushinda zaidi ya hamsini asilimia


nnakusudia kusema kwa vile zanzibar kuna wapiga kura wachache huenda ikatokea Rais wa jamhuri akawa hatakiwi upande mmoja wa muungano lakini upande wa pili wakamchagua na ukienda kwenye majumuisho akashinda kwa zaidi ya asilimia hamsini na kuwa Rais, kitu ambacho kinaleta malalamiko kuwa Rais huyo hawezi kuwa wa muungano bali rais wa upande mmoja tu wa muungano

nnapenda kuwasilisha mapendekezo yangu haya kwenu waungwana tuyajadili
 
bwana masauni mm sina haki kuzungumza haya hapa na watanzania wenzangu juu ya haya ?
wewe si ndo ulikuwa mstali wa mbele kumpinga Dr. Slaa wakati akieleza kwamba akiingia ikulu ataanzisha mchakato wa katiba mpya. Leo unajifanya unatoa mapendekezo ya katiba mpya. Sasa unataka tuchangie nini? Siku ya ukombozi itakapo fika wewe, malaria sugu tutawashitaki kwa usaliti.
 
keep reminding them that JF members are watching! We know what everybody stands for and we can not be hooked by people who keep changing positions!!! huyu anataka kujenga dhana kuwa ni lazima rais atoke CCM kama wanavyoimba kila siku
 
ccm ndio walioanza mbio hizi za katiba mpya na wameunda kamati nyingi tu kwa hilo
 
ccm ndio walioanza mbio hizi za katiba mpya na wameunda kamati nyingi tu kwa hilo

Pamoja na kuunda hizo kamati/tume, je walifanyia kazi mapendekezo ya kamati hizo? Tume ya Nyalali ilifanya kazi almost 20 yrs ago, mpaka leo serikali ya CCM haikutekeleza mapendekezo ya Tume hiyo. Tume ya Jaji Kisanga ilipendekeza swala la katiba mpya, ikaambiwa imevuka mipaka ya majukumu yake, kwamba ilienda beyond terms of reference or scope ya mambo ambayo walipewa kufanyia kazi.

How many times mawaziri wa sheria na ofisi ya rais wamekuwa wakitamka kwamba Katiba iliyopo inakidhi mahitaji ya watanzania na wala hakuna haja ya kuibadilisha? Labda nikutajie wachache, ni pamoja na Marmo, Chikawe, Nagu, na huyu wa sasa Celina Kombani.

Ni bora uwe mkweli kwamba joto la mwamko wa madai ya Katiba limekuwa kubwa na CCM/serikali ya CCM haina ubavu wa kuendelea kulivumilia. Hoja kwamba CCM ndio waanzilishi wa madai ya Katiba ni uongo. Kama wangekuwa na nia ya kuandaa Katiba Mpya wangefanya hivyo siku nyingi sana maana wao ndio wana serikali na ndio wana zaidi ya theluthi mbili ya wabunge mjengoni, walishindwa nini kubadilisha katiba miaka yote hiyo tangu 1990?
 
Pamoja na kuunda hizo kamati/tume, je walifanyia kazi mapendekezo ya kamati hizo? Tume ya Nyalali ilifanya kazi almost 20 yrs ago, mpaka leo serikali ya CCM haikutekeleza mapendekezo ya Tume hiyo. Tume ya Jaji Kisanga ilipendekeza swala la katiba mpya, ikaambiwa imevuka mipaka ya majukumu yake, kwamba ilienda beyond terms of reference or scope ya mambo ambayo walipewa kufanyia kazi.

How many times mawaziri wa sheria na ofisi ya rais wamekuwa wakitamka kwamba Katiba iliyopo inakidhi mahitaji ya watanzania na wala hakuna haja ya kuibadilisha? Labda nikutajie wachache, ni pamoja na Marmo, Chikawe, Nagu, na huyu wa sasa Celina Kombani.

Ni bora uwe mkweli kwamba joto la mwamko wa madai ya Katiba limekuwa kubwa na CCM/serikali ya CCM haina ubavu wa kuendelea kulivumilia. Hoja kwamba CCM ndio waanzilishi wa madai ya Katiba ni uongo. Kama wangekuwa na nia ya kuandaa Katiba Mpya wangefanya hivyo siku nyingi sana maana wao ndio wana serikali na ndio wana zaidi ya theluthi mbili ya wabunge mjengoni, walishindwa nini kubadilisha katiba miaka yote hiyo tangu 1990?
Asante sana nadhani umemjibu vizuri sana
 
waungwana baada ya muamko wa kutaka katiba mpya mm nilikua na mapendekezo haya yafuatayo katika ucahguzi wa kumchagua Rais wa Jamhuri yetu ya muungano.


kwanza ningependa kuona kuwa Rais wa Jamhuri yetu anatoka upande mmoja wa muungano mara moja na inayofuata atoke upande mwengine (nnakusudia nchi zilizounda muungano sio tuache tu mtu yeyote kutoka upande wowote awanie hii huenda ikazaa malalamiko ambayo kwa chini chini yapo kuwa upande mmoja wa muungano unatawaliwa na upande mmoja unatawala).

Pointi ya pili ni kuhusu kura ambazo zinamuweka Rais madarakani, ningependekeza Rais wa Jamhuri wa muungano lazima ashinde kwa zaidi asilimia hamsini kwa kura za Kila upande wa jamhuri na sio kuzihesabu kura zote na kushinda zaidi ya hamsini asilimia


nnakusudia kusema kwa vile zanzibar kuna wapiga kura wachache huenda ikatokea Rais wa jamhuri akawa hatakiwi upande mmoja wa muungano lakini upande wa pili wakamchagua na ukienda kwenye majumuisho akashinda kwa zaidi ya asilimia hamsini na kuwa Rais, kitu ambacho kinaleta malalamiko kuwa Rais huyo hawezi kuwa wa muungano bali rais wa upande mmoja tu wa muungano

nnapenda kuwasilisha mapendekezo yangu haya kwenu waungwana tuyajadili

Fikra ulizonazo NI BUTU na zinatoka katika mfumo wa chama kimoja.... alafu WEWE NI KILAZA HUFIKIRII...

TAFAKARI HAPA
Kama CHAMA CHENU MPAKA kikawa kimefanya muundo huo... alafu UDP au NCCR au CHADEMA wao wamemchagua mtu wa bara ... alafu akashinda... ikiwa raisi aliyetangulia alikuwa ni wa bara, alkafu CHAMA CHENU MPAKA kikawa kimeamua kumueka mtu wa Visiwani alafu akashindwa na chama kingine cha upinzani, kilichoweka mgombea wa bara huoni bara wataendelea kutawala?? Vivyo hivyo hata kwa chama cha upinzania???

Huu nni mfumo wa vyama vingi, mnapoingia katika uchaguzi TAMBUA kuwa hakuna anayejua nani anashinda (hiyo ndo fikra ya awali) ila kwa kuwa una fikra za ki CCM, mnaona mtaendelea kutawala tuuuuuuuuuu, kwa hiyo mtakuwa mnajibadilishia bara----visiwani---bara---visiwani.

Weka akilini MFUMO huo hauwezekani kwa siasa ya vyama vingi.

ONDOA FIKRA HIYO KICHWANI MWAKO
 
waungwana baada ya muamko wa kutaka katiba mpya mm nilikua na mapendekezo haya yafuatayo katika ucahguzi wa kumchagua Rais wa Jamhuri yetu ya muungano.


kwanza ningependa kuona kuwa Rais wa Jamhuri yetu anatoka upande mmoja wa muungano mara moja na inayofuata atoke upande mwengine (nnakusudia nchi zilizounda muungano sio tuache tu mtu yeyote kutoka upande wowote awanie hii huenda ikazaa malalamiko ambayo kwa chini chini yapo kuwa upande mmoja wa muungano unatawaliwa na upande mmoja unatawala).

Pointi ya pili ni kuhusu kura ambazo zinamuweka Rais madarakani, ningependekeza Rais wa Jamhuri wa muungano lazima ashinde kwa zaidi asilimia hamsini kwa kura za Kila upande wa jamhuri na sio kuzihesabu kura zote na kushinda zaidi ya hamsini asilimia


nnakusudia kusema kwa vile zanzibar kuna wapiga kura wachache huenda ikatokea Rais wa jamhuri akawa hatakiwi upande mmoja wa muungano lakini upande wa pili wakamchagua na ukienda kwenye majumuisho akashinda kwa zaidi ya asilimia hamsini na kuwa Rais, kitu ambacho kinaleta malalamiko kuwa Rais huyo hawezi kuwa wa muungano bali rais wa upande mmoja tu wa muungano

nnapenda kuwasilisha mapendekezo yangu haya kwenu waungwana tuyajadili

Baadaye tutabomoa muungano wenyewe kwa sababu mtu mmoja anaweza kufanya kampeni upande mmoja tu wa muungano umchague yeye na mwingine kufanya kampeni upande mwingine! Kisha baadaye tutadai mikoani nako Rais afikishe 50%, asipofikisha basi hajachaguliwa kihalali! Hoja zako ni za kiubaguzi Mtu wa Pwani!
 
Back
Top Bottom