Katiba Mpya: Kulikoni Makamanda na ndugu Wananchi Kusita Sita?

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,817
35,827
Tukubali kuziweka siasa pembeni. Kama ilivyo kwa mwenda kuoga, tukubali kuyavulia maji nguo, tuukabili ukweli usiosemeka:

1. Ridhaa ya kuongoza nchi hupatikana kutoka kwa wananchi.
2. Haiwezekani popote kuwa ridhaa hiyo ikatolewa kwa mtu ambaye agenda zake hakuna kuheshimu usawa, uhuru wala haki.
3. Wapo walioingia madarakani pasipokuwa na ridhaa za wananchi wao. Wakitumia mitutu ya bunduki, wizi, ghiliba na hata hadaa.

Kutegemeana na walivyoingia madarakani nchi moja hufanana na nyingine au hata kutofautiana wazi wazi.

A: Tanzania, Burundi, Rwanda, Uganda, Zimbabwe zina kufanana kwingi kwenye nyanja nyingi za kiutawala. Kwenye nchi hizi mihimili ya utawala haiko huru na kote upo mmoja uliojichimbia zaidi.

Matokeo yake, harakati za wazi za watu wasiojulikana, tuhuma za ugaidi kwa wapinzani, malalamiko ya kuminywa demokrasia, na vyote vya namna hiyo, huko ndiyo kwao.

Katika nchi hizi watu kupotea, kutekwa na kuuwawa vidole vikielekezewa dola ndiyo maisha yenyewe.

Kama tunavyo waulizia kina Moses Lijenje, kwenye nchi za kwenye kundi hili nako ni hivyo hivyo.

Waliingia bila ridhaa ya wananchi hawataondoka kwa maamuzi ya wananchi.

Alisema Museveni kwa nyundo kama quarter pin ya baiskeli aliingia na ndivyo atakavyotoka.

B:. Kenya, Malawi, Zambia, Afrika Kusini; mihimili yaani serikali, bunge na mahakama iko huru na kila mmoja unatekeleza wajibu wake kwa mujibu wa katiba.

Haipo mivutano ya dola na wapinzani. Hazipo harakati za wasiojulikana na maisha yanasonga kwa amani pasipo na matumizi ya nguvu kuwanyamazisha wenye mawazo tofauti kisiasa.

IMG_20211026_221742_205.jpg


Hawa waliingia kwa ridhaa za wananchi, watatoka kwa maamuzi wananchi.

Hatustahili kuwa katika kundi lenye viongozi wasiokuwa chaguo letu.

Hatustahili kuwa kwenye kundi ambalo leo wako kwenye kujipangia nafasi za uongozi 2025 bila ridhaa zetu.

Tunauhuru wa kuchagua hali hii kuendelea au kukataa.

Uamuzi ni wetu.
 
Una mawazo mazuri ila tatizo unataka nguvu itumike jambo ambalo ni kinyume na demokrasia unayoihubiri. Leo ww ukiingia madaraka kwa mtutu wa bunduki au maandamano yupo atakayekuja na kukuambia kuwa naww hujufuata misingi ya demokrasia kuiningia madarakani kwa nguvu ya box la kura.

Ona Libya, Ethiopia, Sudan, Tunisia wamefaidika nini na mapinduzi waliyoyafanya. Je majeraha yao yameshatibika. Ndugu pambana tuijenge nchi yetu. Hayo mengine achana nayo... yatakukuta bure halafu familia yako ndo ihangaike. Mwanasiasa hutetea tumbo lake siku zote.

Ona Kenya, wana tume huru sijui mihili yao yote mitatu iko huru lakini mikoa zaidi ya 17 (kama nimekosea nirekebishe) imetangaza NJAA kuwa janga la kitaifa. Katiba imewasaidia nini kuepukana na njaa...??? Jacob Zuma ametuhumiwa kuiba pesa ngapi kwenye nchi yake, katiba mpya imesaidia nini?

Leo hii mtu anaweza kudhani ya kuwa KATIBA ndo kila kitu lakini pasipk kuwa na weledi wa wale wanaitekeleza katiba ni kazi bure. Ndugu cha kufanya pambama usomeshe, uchumi ukue, uishi maisha ya furaha wewe na kizazi chako.

Mwisho, US wana KATIBA nzuri sana but still kuna masikini wa kutupwa. So usiweke matarajio makuubwa kuwa KATIBA ndo suluhisho la kila kitu.

FANYA KAZI, KIJANA JITUME... Muda ukienda umeenda hutoweza kusingizia katiba kama ukilala njaa wewe na familia yako.

Eeh MUNGU TWAKUOMBA UENDELEE KUTUJALIA AMANI.
 
Hizi nchi zinahitaji Mapinduzi niamini Mkuu hawa viongozi wa Afrika Demokrasia hawaijui kabisa

Kwa usahihi Museveni alisema:

Kwa nyundo kama quarter pin ya baiskeli aliingia na kutoka itakuwa hivyo hivyo kwa nyundo kama quarter pin atatoka - si vinginevyo.

Nakubaliana nawe:

Hawakuingia kwa ridhaa za wananchi hawatatoka kwa maamuzi ya wananchi.
 
Una mawazo mazuri ila tatizo unataka nguvu itumike jambo ambalo ni kinyume na demokrasia unayoihubiri. Leo ww ukiingia madaraka kwa mtutu wa bunduki au maandamano yupo atakayekuja na kukuambia kuwa naww hujufuata misingi ya demokrasia kuiningia madarakani kwa nguvu ya box la kura.

Ona Libya, Ethiopia, Sudan, Tunisia wamefaidika nini na mapinduzi waliyoyafanya. Je majeraha yao yameshatibika. Ndugu pambana tuijenge nchi yetu. Hayo mengine achana nayo... yatakukuta bure halafu familia yako ndo ihangaike. Mwanasiasa hutetea tumbo lake siku zote.

Ona Kenya, wana tume huru sijui mihili yao yote mitatu iko huru lakini mikoa zaidi ya 17 (kama nimekosea nirekebishe) imetangaza NJAA kuwa janga la kitaifa. Katiba imewasaidia nini kuepukana na njaa...??? Jacob Zuma ametuhumiwa kuiba pesa ngapi kwenye nchi yake, katiba mpya imesaidia nini?

Leo hii mtu anaweza kudhani ya kuwa KATIBA ndo kila kitu lakini pasipk kuwa na weledi wa wale wanaitekeleza katiba ni kazi bure. Ndugu cha kufanya pambama usomeshe, uchumi ukue, uishi maisha ya furaha wewe na kizazi chako.

Mwisho, US wana KATIBA nzuri sana but still kuna masikini wa kutupwa. So usiweke matarajio makuubwa kuwa KATIBA ndo suluhisho la kila kitu.

FANYA KAZI, KIJANA JITUME... Muda ukienda umeenda hutoweza kusingizia katiba kama ukilala njaa wewe na familia yako.

Eeh MUNGU TWAKUOMBA UENDELEE KUTUJALIA AMANI.

Umejichanganya sana:

1. Nimeandika wazi kuingia bila ridhaa ya wananchi iwe kwa mtutu, ghiliba, hadaa, wizi na vya namna hiyo hakukubaliki.
2. Nimeonyesha pia kupata ridhaa bila kuwakikishia wananchi uhuru, usawa na haki zao haiwezekani.

Unasoma wapi kuwa ninataka nguvu itumike?

Vipi bandiko hili limekugusa?

Kwamba mmeingia bila ridhaa ya watu ni kuwa mmengia kama Museveni kwa quarter pin tu.

Ndiyo maana hamtaridhia katiba mpya hata kama ndiyo mahitaji yetu.

Si kuwa yote uliyoyaandika msingi wake ni uzi huu hapa chini?

Tuwatambue Wanaopotosha Ajenda kuhusu Katiba Mpya

Mengine ya kutishana kama watu wazima hayalipi.

Hata Nyerere na akina Mandela walitishiwa hivyo hivyo tena na watu waliokuwa kuwa wanufaika kama wewe.
 
Umejichanganya sana:

1. Nimeenda wazi kuingia bila ridhaa ya wananchi iwe kwa mtutu, ghiliba, hadaa, wizi na vya namna hiyo hakukubaliki.
2. Nimeonyesha pia kupata ridhaa bila kuwakikishia wananchi uhuru, usawa na haki zao haiwezekani.

Unasoma wapi kuwa ninataka nguvu itumike?

Vipi bandiko hili limekugusa?

Kwamba mmeingia bila ridhaa ya watu ni kuwa mmengia kama Museveni kwa quarter pin tu.

Ndiyo maana hamtaridhia katiba mpya hata kama ndiyo mahitaji yetu.

Si kuwa yote uliyoyaandika msingi wake ni uzi huu hapa chini?

Tuwatambue Wanaopotosha Ajenda kuhusu Katiba Mpya

Mengine ya kutishana kama watu wazima hayalipi.

Hata Nyerere na akina Mandela ealitishiwa hivyo hivyo tena watu waliokuwa kuwa wanufaika kama wewe.
Mimi ni nani katika nchi hii hata niseme nina mamlaka ya kuridhia katiba mpya ama lah. Nilikuwa nakupa tu ushauri. Maana hata tuwe na sheria au katiba nzuri kiasi gani bado maovu hayatoweza kuisha. Katiba bora ni kiongozi bora. Ona Zambia, pigeni kura acheni porojo mitandaoni.

Labda nikupe mfano mzuri. Kipindi kile wakati mchakato wa katiba mpya unaanza mambo yalienda vizuri sana. Lakini baadae ikatokea sintofahamu tukaisikia kuwa kuna rasimu ya warioba og na ambayo imebadilishwa mambo mengi hali iliyopelekea mchakato ule kuvurugika. Maana yangu ni hii, watu waliendekeza maslahi binafsi zaidi kuliko ya Taifa, na kwa mantiki hiyo walipoona vitu vyao havitakiwi basi, maelewano yakapotea.

Lakini katiba hii ndo imetulea kwa miongo mingi kwa amani, mshikamano ma upendo mpaka leo. Ingekuwa ni katiba mbaya basi inawezekana leo hii tungekuwa matatizoni. Tuvumiliane mpaka pale wenye kuona muda unafaa wataamua. Hata Rais Mstaafu Nd. Kikwete alianzisha mchakato akiwa anamalizia muda wake... hakuna anayetaka jumba bovu limwangukie yeye.

Nikipokuambia somesha maaana yangu ni kuhakikisha vijana na mabinti wengi wanapata eleimu ambayo baabdae itawakomboa kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Tunza familia yako, na Mungu atakubariki.
 
Mimi ni nani katika nchi hii hata niseme nina mamlaka ya kuridhia katiba mpya ama lah. Nilikuwa nakupa tu ushauri. Maana hata tuwe na sheria au katiba nzuri kiasi gani bado maovu hayatoweza kuisha. Katiba bora ni kiongozi bora. Ona Zambia, pigeni kura acheni porojo mitandaoni.

Labda nikupe mfano mzuri. Kipindi kile wakati mchakato wa katiba mpya unaanza mambo yalienda vizuri sana. Lakini baadae ikatokea sintofahamu tukaisikia kuwa kuna rasimu ya warioba og na ambayo imebadilishwa mambo mengi hali iliyopelekea mchakato ule kuvurugika. Maana yangu ni hii, watu waliendekeza maslahi binafsi zaidi kuliko ya Taifa, na kwa mantiki hiyo walipoona vitu vyao havitakiwi basi, maelewano yakapotea.

Lakini katiba hii ndo imetulea kwa miongo mingi kwa amani, mshikamano ma upendo mpaka leo. Ingekuwa ni katiba mbaya basi inawezekana leo hii tungekuwa matatizoni. Tuvumiliane mpaka pale wenye kuona muda unafaa wataamua. Hata Rais Mstaafu Nd. Kikwete alianzisha mchakato akiwa anamalizia muda wake... hakuna anayetaka jumba bovu limwangukie yeye.

Nikipokuambia somesha maaana yangu ni kuhakikisha vijana na mabinti wengi wanapata eleimu ambayo baabdae itawakomboa kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Tunza familia yako, na Mungu atakubariki.

Sina hakika kama ulipata nafasi ya kuusoma uzi niliokuwa nimeambatanisha. Hata hivyo nisiache kuweka vijisehemu vyake hapa:

IMG_20211101_224337_761.jpg


Mbaya zaidi ni kuwa katiba mpya ni muhimu na dharura sana kwa Sekta zote isipokuwa kwa walio wanufaika kweri kweri wa katiba iliyopo:

Katiba Mpya ni muhimu kwa Sekta Zote

Kulikoni wewe huoni umuhimu? Kwani wewe ni sekta gani?

Nime ku-zoom:

IMG_20211101_225113_693.jpg


Naona ukakasi mwingi zaidi kwako.
 
Hizi nchi zinahitaji Mapinduzi niamini Mkuu hawa viongozi wa Afrika Demokrasia hawaijui kabisa
Katika hayo makundi ondoa TZ. Wakati hizo nchi zina mtawala mmoja, TZ imekuwa ikibadilisha watawala kila baada ya miaka minne. That is a huge difference!
 
Katika hayo makundi ondoa TZ. Wakati hizo nchi zina mtawala mmoja, TZ imekuwa ikibadilisha watawala kila baada ya miaka minne. That is a huge difference!

Hapana Tanzania inabidi iwe hapo kwa sababu chama kile kile kimeendelea kuwepo madarakani. That is a huge resemblance!
 
Katika hayo makundi ondoa TZ. Wakati hizo nchi zina mtawala mmoja, TZ imekuwa ikibadilisha watawala kila baada ya miaka minne. That is a huge difference!
Tatizo sio kukabidhiana madaraka kwa uchaguzi hio sio inshu kabisa..but pia kwenye hizo chaguz nahisi kuna kitu kimekua kikitoea unakifahamu yan ccm had wabibi ni wezi tu daaa
 
Tatizo sio kukabidhiana madaraka kwa uchaguzi hio sio inshu kabisa..but pia kwenye hizo chaguz nahisi kio kitu kimekua kikitoea unakifahamu yan ccm had wabibi ni wezi tu daaa

Nchi zote hizo kwenye list Tanzania, Rwanda, Burundi, Uganda, Zimbabwe wanafanana sawia. Wote ni wezi wa kutupwa kwenye sanduku la kura.

Kwamba Nkurunziza au Mugabe walitoka? Mizizi yao yaani core systems zilibakia pale pale.

Hadi pale tutakapo kuwa na total overhaul ya core system na kusimika mpya yenye kutambua haki, uhuru, usawa na demokrasia hakuna kitakacho songa hapa:

"Hakutakuwa na katiba mpya, utawala wa sheria, wala mihimili iliyo huru."

Wamachinga leo wameonyesha njia. Hiyo ndiyo iliyo njia pekee ya kufikishwa ujumbe kwa wenye uthubutu wa kujiita mawe au hata quarter pin.
 
Nchi zote hizo kwenye list Tanzania, Rwanda, Burundi, Uganda, Zimbabwe wanafanana sawia. Wote ni wezi wa kutupwa kwenye sanduku la kura.

Kwamba Nkurunziza au Mugabe walitoka? Mizizi yao yaani core systems zilibakia pale pale.

Hadi pale tutakapo kuwa na total overhaul ya core system na kumsimika mpya yenye kutambua haki, uhuru, usawa na demokrasia hakuna kitakachosonga hapa hapa:

"Hakutakuwa na katiba mpya, utawala wa sheria, wala mihimili iliyo huru."

Wamachinga leo wameonyesha njia. Hiyo ndiyo iliyo njia pekee ya kufikishwa ujumbe kwa wenye uthubutu wa kujiita mawe au hata quarter pin.
Nchi za Afrika Viongozi wana Tamaa sana sa wanavyofahamu kua wakitoka madarakani kuna watu waliwatendea ubaya watalipiza so wanahakikisha either wanaiba kura waendelee kubaki au wanabadili katiba kabisa au kingine wanaweka viongozi kutoka kwenye hizo Chain zao ili waendelee kulindwa coz hata Mihimili yetu ipoipo tu ka MOUNT-MERU imelala lala tu haifanyi kazi kwa uhuru.

And Mi nilivyoona ile ya wamachinga hadi nikasema hawa huenda ndio watanzania kweli sisi wengine huenda sio watanzania tumeletwa kutoka jangwani tukatupiwa hapa.
 
Nchi za Afrika Viongozi wana Tamaa sana sa wanavyofahamu kua wakitoka madarakani kuna watu waliwatendea ubaya watalipiza so wanahakikisha either wanaiba kura waendelee kubaki au wanabadili katiba kabisa au kingine wanaweka viongozi kutoka kwenye hizo Chain zao ili waendelee kulindwa coz hata Mihimili yetu ipoipo tu ka MOUNT-MERU imelala lala tu haifanyi kazi kwa uhuru.

And Mi nilivyoona ile ya wamachinga hadi nikasema hawa huenda ndio watanzania kweli sisi wengine huenda sio watanzania tumeletwa kutoka jangwani tukatupiwa hapa.

Mkuu ninakubaliana nawe ila niongezee, si kuogopa kulipiziwa visasi peke yake bali madaraka ni matamu mno.

Bila kuwa na katiba madhubuti roho za binadamu madarakani ni heri za wanyama.

Kumbuka Samia alivyoingia madarakani. Kumbuka ulinzi wake ulivyokuwa. Angalia ulivyo leo.

Samia alipoingia akiongelea kuitibu nchi na majeraha ya awamu ya tano. Msikilize leo kama anayakumbuka hayo.

Leo Samia 2021 anataka kujimilikisha post 2025 tayari. Kuhakikisha hilo hataki tume huru ya uchaguzi.

Jiwe alipoingia hali kadhalika ilikuwa hivyo hivyo. Alipoingia hakutaka kutoka. Jiwe alikuja na mpya zaidi kuwa bila yeye miradi ya kimkakati kama alivyo iita yeye ingekoma.

Jiwe alishaandaa mazingira ya mitano tena baada ya 2025.

Museveni aliingia 1987 akitanabaisha tatizo kuu Afrika ilikuwa ni kwa viongozi ni ku overstay madarakani. Ilikuwa akae vipindi viwili na katiba yake ikawa na age limit kwa rais madarakani. Leo anaendelea na age limit kaondoa kwenye katiba.

Kagame aliingia literally 1994 limits za vipindi viwili zikawa manipulated na sasa ndiyo kabisa kajaa tele officially hadi 2034.

Nkurunziza ilikuwa je hadi kupelekea kupinduliwa na kupelekea kurejeshwa madarakani kwa nguvu na JK?

Vivyo hivyo kwa Robert Mugabe. Mugabe alikuwa hatoki madarakani hadi jeshi kuamua kumtoa.
 
Sina hakika kama ulipata nafasi ya kuusoma uzi niliokuwa nimeambatanisha. Hata hivyo nisiache kuweka vijisehemu vyake hapa:

View attachment 1995113

Mbaya zaidi ni kuwa katiba mpya ni muhimu na dharura sana kwa Sekta zote isipokuwa kwa walio wanufaika kweri kweri wa katiba iliyopo:

Katiba Mpya ni muhimu kwa Sekta Zote

Kulikoni wewe huoni umuhimu? Kwani wewe ni sekta gani?

Nime ku-zoom:

View attachment 1995127

Naona ukakasi mwingi zaidi kwako.
You are making a great mistake. Screenshot ya profile yangu ima tatizo gani kwani. Acheni kuwa na kasumba za mbaya zakuwajudge watu. Mimi kujiunga hiyo mwaka jana kuna shida gani. Labda ngoja nkuueleze kitu. Jamii forum nimeitumia for more than 6 years kama guest tu. I doubt uwezo wako wa kufkr...
 
Una mawazo mazuri ila tatizo unataka nguvu itumike jambo ambalo ni kinyume na demokrasia unayoihubiri. Leo ww ukiingia madaraka kwa mtutu wa bunduki au maandamano yupo atakayekuja na kukuambia kuwa naww hujufuata misingi ya demokrasia kuiningia madarakani kwa nguvu ya box la kura.

Ona Libya, Ethiopia, Sudan, Tunisia wamefaidika nini na mapinduzi waliyoyafanya. Je majeraha yao yameshatibika. Ndugu pambana tuijenge nchi yetu. Hayo mengine achana nayo... yatakukuta bure halafu familia yako ndo ihangaike. Mwanasiasa hutetea tumbo lake siku zote.

Ona Kenya, wana tume huru sijui mihili yao yote mitatu iko huru lakini mikoa zaidi ya 17 (kama nimekosea nirekebishe) imetangaza NJAA kuwa janga la kitaifa. Katiba imewasaidia nini kuepukana na njaa...??? Jacob Zuma ametuhumiwa kuiba pesa ngapi kwenye nchi yake, katiba mpya imesaidia nini?

Leo hii mtu anaweza kudhani ya kuwa KATIBA ndo kila kitu lakini pasipk kuwa na weledi wa wale wanaitekeleza katiba ni kazi bure. Ndugu cha kufanya pambama usomeshe, uchumi ukue, uishi maisha ya furaha wewe na kizazi chako.

Mwisho, US wana KATIBA nzuri sana but still kuna masikini wa kutupwa. So usiweke matarajio makuubwa kuwa KATIBA ndo suluhisho la kila kitu.

FANYA KAZI, KIJANA JITUME... Muda ukienda umeenda hutoweza kusingizia katiba kama ukilala njaa wewe na familia yako.

Eeh MUNGU TWAKUOMBA UENDELEE KUTUJALIA AMANI.
iyo amani unayohubiri ukiwa na njaa/umasikini inasaidia nini?
 
Mkuu ninakubaliana nawe ila niongezee, si kuogopa kulipiziwa visasi peke yake bali madaraka ni matamu mno.

Bila kuwa na katiba madhubuti roho za binadamu madarakani ni heri za wanyama.

Kumbuka Samia alivyoingia madarakani. Kumbuka ulinzi wake ulivyokuwa. Angalia ulivyo leo.

Samia alipoingia akiongelea kuitibu nchi na majeraha ya awamu ya tano. Msikilize leo kama anayakumbuka hayo.

Leo Samia 2021 anataka kujimilikisha post 2025 tayari. Kuhakikisha hilo hataki tume huru ya uchaguzi.

Jiwe alipoingia hali kadhalika ilikuwa hivyo hivyo. Alipoingia hakutaka kutoka. Jiwe alikuja na mpya zaidi kuwa bila yeye miradi ya kimkakati kama alivyo iita yeye ingekoma.

Jiwe alishaandaa mazingira ya mitano tena baada ya 2025.

Museveni aliingia 1987 akitanabaisha tatizo kuu Afrika ilikuwa ni kwa viongozi ni ku overstay madarakani. Ilikuwa akae vipindi viwili na katiba yake ikawa na age limit kwa rais madarakani. Leo anaendelea na age limit kaondoa kwenye katiba.

Kagame aliingia literally 1994 limits za vipindi viwili zikawa manipulated na sasa ndiyo kabisa kajaa tele officially hadi 2034.

Nkurunziza ilikuwa je hadi kupelekea kupinduliwa na kupelekea kurejeshwa madarakani kwa nguvu na JK?

Vivyo hivyo kwa Robert Mugabe. Mugabe alikuwa hatoki madarakani hadi jeshi kuamua
Unaposema katiba madhubuti umaanisha nini? Ikiwa hao walio madarakani wanauwezo wa kumanupulate hiyo katiba? Kinachotakiwa Tanzania 🇹🇿 ni viongozi wazalendo, watakaoipenda nchi kwa dhati. Mambo mengine ni story. Hata hivyo sio kwamba sitaki hii ya sasa isibadilishwe but nnichotaka kujua hiyo itakayoletwa itaweza kukidhi mahitaji ya sasa na miongo kadhaa ijayo?

Mwisho si vyema kufikiri kuwa katiba mpya ndo itakuwa suluhisho la kila kitu. Pambaneni katika box la kura mkishinda mbadili katiba vile mtakavyo. Nchi nyingi upinzani umeshinda bila hata vurugu, mfano mzuri, Zambia. Box la kura ndo jambo la msingi.

#boxlakuraKATIBAYANGU
 
katiba mpya sio hitaji la wananchi kwa sasa,bali wanasiasa.kama hutaki shauri yako.

katiba mpya inayopigiwa kelele na wanasiasa hao baadhi imejikita katika jambo kuu moja tu,nalo ni uchaguzi.
kama ujuavyo vyeo vya kisiasa ni mara zote inakuwa ni ajira kwa mwanasiasa zaidi ya kutanguliza utumishi kwanza.

hili la katiba wacha mwenye umuhimu nalo ahangaike nalo,wengine wako busy wanahangaikia maisha yao binafsi.
 
Una mawazo mazuri ila tatizo unataka nguvu itumike jambo ambalo ni kinyume na demokrasia unayoihubiri. Leo ww ukiingia madaraka kwa mtutu wa bunduki au maandamano yupo atakayekuja na kukuambia kuwa naww hujufuata misingi ya demokrasia kuiningia madarakani kwa nguvu ya box la kura.

Ona Libya, Ethiopia, Sudan, Tunisia wamefaidika nini na mapinduzi waliyoyafanya. Je majeraha yao yameshatibika. Ndugu pambana tuijenge nchi yetu. Hayo mengine achana nayo... yatakukuta bure halafu familia yako ndo ihangaike. Mwanasiasa hutetea tumbo lake siku zote.

Ona Kenya, wana tume huru sijui mihili yao yote mitatu iko huru lakini mikoa zaidi ya 17 (kama nimekosea nirekebishe) imetangaza NJAA kuwa janga la kitaifa. Katiba imewasaidia nini kuepukana na njaa...??? Jacob Zuma ametuhumiwa kuiba pesa ngapi kwenye nchi yake, katiba mpya imesaidia nini?

Leo hii mtu anaweza kudhani ya kuwa KATIBA ndo kila kitu lakini pasipk kuwa na weledi wa wale wanaitekeleza katiba ni kazi bure. Ndugu cha kufanya pambama usomeshe, uchumi ukue, uishi maisha ya furaha wewe na kizazi chako.

Mwisho, US wana KATIBA nzuri sana but still kuna masikini wa kutupwa. So usiweke matarajio makuubwa kuwa KATIBA ndo suluhisho la kila kitu.

FANYA KAZI, KIJANA JITUME... Muda ukienda umeenda hutoweza kusingizia katiba kama ukilala njaa wewe na familia yako.

Eeh MUNGU TWAKUOMBA UENDELEE KUTUJALIA AMANI.
😍
 
Back
Top Bottom