Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,422
- 911,172
Rasimu za katiba ya kenya zilizokuwa zikijulikana kama "Boma" na "Wako" ya mwaka 2005 zilikuwa wazi ya kuwa ushoga hapana lakini hii katiba mpya hiyo Ibara iliondolewa na hivyo kuhalalisha ushoga............
Kwenye rasimu ya "Boma" Ibara ya 41(3) na kwenye "Wako" Ibara ya 42(3) ushoga ulikuwa wazi kabisa umepigwa marufuku.
Baada ya katiba mpya kuondolewa Ibara inayokataza ushoga zipo ibara nyingine kwenye katiba hiyo ambazo zinalinda ushoga bila kuutaja moja kwa moja............Ibara 27(4) inakataza ubaguzi wa aina wowote ule hata ule wa "sex" na wala siyo jinsia tu kwa maana ya "gender" Hii imetafsiriwa na magwiji wa sheria huko Kenya ya kuwa "sex" inajumuisha ushoga........
Ibara 20(3) ya katiba mpya inatoa mamlaka kwa mahakama kutoa matamko ya kulinda haki za wanyonge ambao wamekuwa wakidhulumia haki zao. Hivyo kama kuna utata wowote ule mashoga Kenya wanaweza kwenda mahakamani ili kuziweka bayana haki ambazo walipewa na katiba mpya. Kwao itakuwa ni rahisi sana kuzitetea kwa sababu watakachokifanya ni kuiomba mahakama kutoa tamko kuwa haki za mashoga zinalindwa na katiba na kama waasisi wa katiba mpya wangelikuwa hawataki kuzilinda wangelifanya hivyo na kwa uwazi kabisa kama ilivyokuwa kwenye rasimu za "Boma" na "Wako"..........Hii ni hoja ya shoka na siyo rahisi kuitengua........
Mara mahakama itakapotoa tamko tajwa basi kuwanyanyapaa au kuwabughudhi mashoga waweza kujikuta unafikishwa mahakamani chini ya Ibara ya 20(3) na matamko hayo ya kimahakama kuwa na nguvu sawasawa na sheria zozote zilizotungwa na Bunge lao........
Ibara 19(3) imeweka wazi ya kuwa haki za uraia zilizomo kwenye katiba pia inajumuisha haki nyinginezo zozote zile ambazo hazikutajwa bayana kwenye katiba hiyo na kutoa mwanya mwingine wa kisheria kwa mashoga kupasua anga bila zengwe lolote lile.......
Wapo ambao watasema hivi ni kwa nini basi waasisi wa katiba mpya walizilinda haki za mashoga kimya kimya na kwa nini hawakuweka ulinzi huo wazi kabisa kuondoa utata unaoweza kujitokeza kisheria?
Maoni yangu ni kuwa kutokana na mashinikizo ya waumini wa madhehebu mbalimbali kuwa na mapingamizi makali dhidi ya ushoga waliona hili suala walichimbie ulaini wa kimya kimya tu..................lakini ndani ya katiba ya Kenya lolote ambalo katiba haijalikataza laweza kuundiwa sheria na kuwa rukhsa kishera.......Go Kenyan gays and lesbians an be our drag queens and kings.........Best wishes in you newfound freedoms but I do not know whether you deserve them.............
Kwenye rasimu ya "Boma" Ibara ya 41(3) na kwenye "Wako" Ibara ya 42(3) ushoga ulikuwa wazi kabisa umepigwa marufuku.
Baada ya katiba mpya kuondolewa Ibara inayokataza ushoga zipo ibara nyingine kwenye katiba hiyo ambazo zinalinda ushoga bila kuutaja moja kwa moja............Ibara 27(4) inakataza ubaguzi wa aina wowote ule hata ule wa "sex" na wala siyo jinsia tu kwa maana ya "gender" Hii imetafsiriwa na magwiji wa sheria huko Kenya ya kuwa "sex" inajumuisha ushoga........
Ibara 20(3) ya katiba mpya inatoa mamlaka kwa mahakama kutoa matamko ya kulinda haki za wanyonge ambao wamekuwa wakidhulumia haki zao. Hivyo kama kuna utata wowote ule mashoga Kenya wanaweza kwenda mahakamani ili kuziweka bayana haki ambazo walipewa na katiba mpya. Kwao itakuwa ni rahisi sana kuzitetea kwa sababu watakachokifanya ni kuiomba mahakama kutoa tamko kuwa haki za mashoga zinalindwa na katiba na kama waasisi wa katiba mpya wangelikuwa hawataki kuzilinda wangelifanya hivyo na kwa uwazi kabisa kama ilivyokuwa kwenye rasimu za "Boma" na "Wako"..........Hii ni hoja ya shoka na siyo rahisi kuitengua........
Mara mahakama itakapotoa tamko tajwa basi kuwanyanyapaa au kuwabughudhi mashoga waweza kujikuta unafikishwa mahakamani chini ya Ibara ya 20(3) na matamko hayo ya kimahakama kuwa na nguvu sawasawa na sheria zozote zilizotungwa na Bunge lao........
Ibara 19(3) imeweka wazi ya kuwa haki za uraia zilizomo kwenye katiba pia inajumuisha haki nyinginezo zozote zile ambazo hazikutajwa bayana kwenye katiba hiyo na kutoa mwanya mwingine wa kisheria kwa mashoga kupasua anga bila zengwe lolote lile.......
Wapo ambao watasema hivi ni kwa nini basi waasisi wa katiba mpya walizilinda haki za mashoga kimya kimya na kwa nini hawakuweka ulinzi huo wazi kabisa kuondoa utata unaoweza kujitokeza kisheria?
Maoni yangu ni kuwa kutokana na mashinikizo ya waumini wa madhehebu mbalimbali kuwa na mapingamizi makali dhidi ya ushoga waliona hili suala walichimbie ulaini wa kimya kimya tu..................lakini ndani ya katiba ya Kenya lolote ambalo katiba haijalikataza laweza kuundiwa sheria na kuwa rukhsa kishera.......Go Kenyan gays and lesbians an be our drag queens and kings.........Best wishes in you newfound freedoms but I do not know whether you deserve them.............