Katiba Mpya: JK anaogopa yai la Muungano kumpasukia mikononi??

The Khoisan

JF-Expert Member
Jun 5, 2007
15,383
12,969
Ni takiribani miezi minne tangu Rais atuahidi katiba mpya. Kwa jinsi kimya kilivyo inaelekea mwaka utaisha hatujasikia kitu.

Zanzibar washaanza kujipanga namna ya kuchangia kwenye katiba kupitia Zanzibar legal society, chama cha waandishi wa habari n.k.

Kwa jinsi upepo ulivyo inaelekea Wazanzibar hawako tayari kuwa na muungano wa design ya 1964. Kama watafanikiwa kwa hilo kuna kila dalili za Tanganyika kurudi......!!

Je JK ansoma upepo wa siasa za Tanzania ...............ili yai la Muungano lisimpasukie mikonono au?

Kuna wakati watu waliandika humu kuwa JK kasema hatakubali CCM au Muungano vifie mikononi mwake.

Anyway, swali ni kwamba je mchakato wa katiba utaanza lini?? Au ndiyo SUBIRA YAVUTA HERI???
 
tatizo watu na waandishi masikio loliondo, wamesahau mambo mengine ya msingi hasa katiba
 
Mimi naogopa hizi habari za Loliondo zisije zikawa zimepikwa ili kuwafanya wananchi wa concentrate kwa mambo ya kikombe waachane na Dowans pamoja na Katiba. Tuwe macho
 
Ni takiribani miezi minne tangu Rais atuahidi katiba mpya. Kwa jinsi kimya kilivyo inaelekea mwaka utaisha hatujasikia kitu.

Zanzibar washaanza kujipanga namna ya kuchangia kwenye katiba kupitia Zanzibar legal society, chama cha waandishi wa habari n.k.

Kwa jinsi upepo ulivyo inaelekea Wazanzibar hawako tayari kuwa na muungano wa design ya 1964. Kama watafanikiwa kwa hilo kuna kila dalili za Tanganyika kurudi......!!

Je JK ansoma upepo wa siasa za Tanzania ...............ili yai la Muungano lisimpasukie mikonono au?

Kuna wakati watu waliandika humu kuwa JK kasema hatakubali CCM au Muungano vifie mikononi mwake.

Anyway, swali ni kwamba je mchakato wa katiba utaanza lini?? Au ndiyo SUBIRA YAVUTA HERI???
Mkuu.
Kwa maoni yangu huwezi kuzungumzia Katiba mpya ya Muungano bila ya kuzungumzia Muungano wenyewe.

Kama Watanzania tuko makini basi tungeanza na mjadala wa Muungano na Muundo wake na uendeshaji wake kwanza kwa sababu Katiba ya Muungano inatakiwa isisuguane na Katiba za nchi wanachama wa Muungano.

Kwa usiri mkubwa uliougubika muungano leo nchi moja mwanachama wa Muungano haonekani na katiba yake pia imepotezwa. Jambo la lazima limejitokeza, kuiandika upya Katiba ya Muungano. Wako wapi wawakilishi halali wa nchi mbili za Muungano wa Tanzania(Tanganyika na Zanzibar). mambo ni mkorogo tu, hata mkorogo ule wa "mchina" una afadhali.

Inawezekana kabisa Muungano ni jinamizi linaloisumbua serikali ya Muungano kwa sababu hapo nyuma wamejinyakulia mamlaka kienyeji bila ya majadiliano kama yale yaliyofanyika wakati wa kuunda Muungano wenyewe.

Kwa hiyo, Nionavyo mimi ni kuwa Zaznibar wanafanya jambo zuri sana kujitayarisha kama wananchi wa upande mmoja wa Muungano ili waweze kuchangia kile wanachokitaka kiwemo katika katiba ya Muungano.

Ingekuwa jambo la busara pia wananchi wa Tanganyika(Tanzania bara) pia kujitayarisha kama wananchi wa upande mwengine wa Muungano ili tuweze kuchangia kile ambacho tunakitaka kiwemo ndani ya Katiba mpya ya Muungano.

Lakini la muhimu zaidi pia tujitayarishe kuifufua katiba ya Tanganyika ili iwepo sambamba na Katiba ya Muungano na katiba ya Zanzibar. Kuna mambo ya Tanganyika(Tanzania bara) yaongozwe na katiba yake. Kuna Mambo ya Muungano yaongozwe kwa Katiba yake na Zanzibar wanayo katiba yao inayoongoza mambo ya Zanzibar.Hizi ni mamlaka tatu tofauti.

Kwa kutaka kwetu na kupenda kwetu njia za mkato ndio zinatuletea ugumu usio wa lazima. na kufanya uwepo Muungano usieleweka. na iwepo nchi ya kiini macho na mazingaombwe.
 
my great worry/doubt ni ikiwa kweli mh presidaa alivosema anaanzisha mchakato wa katiba mpya ili tunaposherekea miaka 50 ya uhuru december tuwe na kitu kipya (katiba) alikuwa anamaanisha real au ilikuwa tu ni kutuliza upepo uliokuwa mkali sana kipindi kile. sioni any developments and days are rushing. pengine tatizo la mtu asiekuwa serious with what he/she always speaks.
 
Tatizo la JK ni kuogopa kufanya maamuzi magumu, na hili litamgharimu sana. Pia kumbukeni katibu wa bunge alisema hoja binafsi ya Mnyika imetupiliwa mbali kwa sababu hakuna kifungu katika katiba ya sasa kinachoruhusu katiba ya sasa kujadiliwa kwa kubadilishwa! kwa hivyo si Bunge si serikali wala mahakama vyenye uwezo wa kubadilika au kujadili kubadilishwa kwa katiba! Huu ni upuuzi mkubwa. Lazima kuwa na Bunge la Katiba siyo hili la akina Makinda na mabosi wake mafisadi ambalo litakuwa na nguvu kisheria kujadili au kubadili katiba
 
Mkuu.
Kwa maoni yangu huwezi kuzungumzia Katiba mpya ya Muungano bila ya kuzungumzia Muungano wenyewe.

Kama Watanzania tuko makini basi tungeanza na mjadala wa Muungano na Muundo wake na uendeshaji wake kwanza kwa sababu Katiba ya Muungano inatakiwa isisuguane na Katiba za nchi wanachama wa Muungano.

Kwa usiri mkubwa uliougubika muungano leo nchi moja mwanachama wa Muungano haonekani na katiba yake pia imepotezwa. Jambo la lazima limejitokeza, kuiandika upya Katiba ya Muungano. Wako wapi wawakilishi halali wa nchi mbili za Muungano wa Tanzania(Tanganyika na Zanzibar). mambo ni mkorogo tu, hata mkorogo ule wa "mchina" una afadhali.

Inawezekana kabisa Muungano ni jinamizi linaloisumbua serikali ya Muungano kwa sababu hapo nyuma wamejinyakulia mamlaka kienyeji bila ya majadiliano kama yale yaliyofanyika wakati wa kuunda Muungano wenyewe.

Kwa hiyo, Nionavyo mimi ni kuwa Zaznibar wanafanya jambo zuri sana kujitayarisha kama wananchi wa upande mmoja wa Muungano ili waweze kuchangia kile wanachokitaka kiwemo katika katiba ya Muungano.

Ingekuwa jambo la busara pia wananchi wa Tanganyika(Tanzania bara) pia kujitayarisha kama wananchi wa upande mwengine wa Muungano ili tuweze kuchangia kile ambacho tunakitaka kiwemo ndani ya Katiba mpya ya Muungano.

Lakini la muhimu zaidi pia tujitayarishe kuifufua katiba ya Tanganyika ili iwepo sambamba na Katiba ya Muungano na katiba ya Zanzibar. Kuna mambo ya Tanganyika(Tanzania bara) yaongozwe na katiba yake. Kuna Mambo ya Muungano yaongozwe kwa Katiba yake na Zanzibar wanayo katiba yao inayoongoza mambo ya Zanzibar.Hizi ni mamlaka tatu tofauti.

Kwa kutaka kwetu na kupenda kwetu njia za mkato ndio zinatuletea ugumu usio wa lazima. na kufanya uwepo Muungano usieleweka. na iwepo nchi ya kiini macho na mazingaombwe.

Nakubaliana nawe, ila hiyo katiba ya kwetu Tanganyika ipoo ama walishaichakachulia mbali kama siyo kufilisi kabisa?
 
Asanteni wachangiyaji wa mada hii. Kwa ufupi, muungano ilikuwa ni kiini macho. Kulingana na sisi wazanzibari tumegundua kuwa hakuna muungano kisheria. Jambo lilioko ni utawala wakimabavu dhidi ya wazanzibari. Nahisi, Bw. J.K. haogopi muungano kuvunjika. Kitu kinacho mtia wasiwasi ni namna ya kuwaeleza watanganyika jinsi Raisi Nyerere alivo boronga mambo. Kwetu sisi, Nyerere hajawa "biggie" sababu tunamchukulia kama kiongozi alietuhujumu. VP Jk amlaumu Nyerere?. Hilo ndio suala la kujibiwa. Kama muungano utaendelea, basi, utaendela ki mabavu. Public Opinion z'bar ni kuwa 90% hawautaki muungano. Huu ndio uhakika wa wazanzibari. Kama uhalali wa muungano haupo, tunajadili katiba ya muungano ya nini?.
 
Back
Top Bottom