Katiba Mpya isiyoitoa CCM ni kama kijarida tu

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,185
103,690
Kwa uchache sana ili nisiwachoshe.

1. CCM ni chama cha hovyo, hakizingatii Katiba ya nchi wala sheria. Mambo yanafanywa kwa utashi zaidi. Utasikia Rais katoa bilioni 2. Inatia uchungu sana.

2. CCM ni chama cha hovyo hata mambo yaliyopo kwenye katiba hii mtumba hawataki kuzingatia. Mtu anapiga marufuku shughuli za siasa zilizopo kikatiba. Halafu mamlama husika inasema tukae kujadili. Unajadili nini.

3. CCM ni chama cha hovyo kilichoshindwa kuwaletea watu maendeleo. Wanafikiria zaidi kutawala kuliko kuwaletea watu maendeleo. Leo unasikia 2025 tunaenda na Samia. Hovyo kabisa.

Kwa hiyo kama katiba haitakiondoa chama hiki cha hovyo basi hiyo katiba haina maana. Hiyo katiba itakuwa sawa na kijarida tu.

Mtakuwa na katiba nzuri, sheria nzuri lakini jamaa hawataifata wana katiba zao vichwani.

Asalam Aleikum
 
Kinachohitajika angalau ni Tume Huru ya Uchaguzi, kama katiba mpya imeshindikana!!

Hata wapinzani wakiingia kwa wingi bungeni wataweza kucontrol serikali isipitishe mambo ya hovyo na ya kukandamiza wananchi, tofauti na sasa hv kila kitu ndiyo mzeee
 
Ccm itatoka tu hata bila katiba mpya.
Watz waanaikataa KILA siku.
 
Kinachohitajika angalau ni Tume Huru ya Uchaguzi, kama katiba mpya imeshindikana!!

Hata wapinzani wakiingia kwa wingi bungeni wataweza kucontrol serikali isipitishe mambo ya hovyo na ya kukandamiza wananchi, tofauti na sasa hv kila kitu ndiyo mzeee
2025 upinzani utaingiza viti vingi sana bungeni
 
Back
Top Bottom