Kikwete eteue Constitutional Review Commission
DAR ES SALAAM, November 21, 2010
Ili kuiokoa Tanzania na political crisis au impasse/stalemate kama iliyotokea
Zanzibar, Rais Kikwete anapaswa kukubali matakwa ya wananchi ya kuwepo katiba
mpya.
Hii inatokana na ukweli kuwa Katiba iliyopo ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ya
mwaka 1977 ni batili.
Katiba iliyopo ni batili kwa sababu 3 kuu:
1. Ilitungwa kwa kukiukwa kwa mchakato unaokubalika kimataifa wa kutengeneza
katiba ambao unataka uwepo mkutano wa kitaifa wa katiba ambapo makundi yote ya
jamii yatakuwa yamewakilishwa, eg wanawake, vijana, wazee, viongozi wa dini,
viongozi wa siasa, wasomi, wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara, n.k.
2. Katiba iliandikwa mwaka 1977 wakati Tanzania iko katika mfumo wa chama kimoja
cha siasa na kikundi cha watu wachache wasiozidi watano ambao walikuwa ni makada
wa CCM.
3. Miaka 33 tangu katiba ilipoandikwa, imewekwa viraka visivyopungua 14
(marekebisho ya katiba). Katiba iliyo kamili huwa haibadilishwi mara kwa mara. Hii
ni ishara kuwa katiba iliyopo ni batili na haijazingatia mabadiliko makubwa
yaliyotokea Tanzania, ikiwemo kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi 1992.
Kama Kikwete anataka kuacha legacy ili akumbukwe kwa mema, basi iwe ni hii ya kuleta
katiba mpya.
Kuanzia, Kikwete anashauriwa aunde Tume ya Kupitia Upya Katiba (Constitutional
Review Commission) ambayo ipewe miezi 6 kukamilisha kazi yake na kukabidhi ripoti
kwa serikali ifikapo Mei 31, 2011. Kuna majaji wengi waadilifu kama Robert Kissanga wanaweza kuongoza tume hii.
Kwenye Bunge la Bajeti ya July-September 2011, upelekwe Bungeni muswada wa the
National Constitutional Conference (NCC) Bill of 2011.
Bunge likishapitisha muswada huu kuwa sheria, serikali inaunda rasmi the National
Constitutional Conference (mkutano mkuu wa kitaifa wa katiba).
Hii National Constitutional Conference ipewe kazi ya kukamilisha katiba mpya na
kupitishwa kwake na Bunge kabla ya kuisha kwa mwaka 2013.
Hii ina maana kuwa itabaki miaka 2 ambayo serikali, vyama vya siasa, NGOs na
taasisi nyingine zitakuwa na muda wa kutoa elimu kwa jamii ili Watanzania waielewe
katiba mpya kabla ya uchaguzi wa 2015.
Katiba ya watu (a people's constitution) ndiyo suluhisho pekee la haki, maendeleo,
amani na utulivu ya kudumu Tanzania.
* Kenya wamepata katiba mpya baada ya damu nyingi za raia kumwagika. Tusifike
huko. Tuige mfano wa majirani zetu Zambia ambao wameanzisha mchakato wa katiba
mpya kwa amani na utulivu.
Tembelea: About the NCC - National Constitutional Conference, Zambia