KATIBA Mpya haitamruhusu Profesa Ibrahim Haruna Lipumba kugombea urais, CUF mwafa

Chief Isike

JF-Expert Member
Jan 17, 2010
445
462
Wenzangu wanabodi, hususan wale waliberali, turudini kwenye ile hoja nyingine, maana mntaka kutumia 'kombora' la uliberali kama exit ya zile tuhuma nyeti zinazowakabili CUF na hasa mwenyekiti wenu na mgombea urais wa maisha, Profesa Ibrahim Haruna Lipumba, kuwa;

1. Ni washirika wakubwa wa CCM kiasi mlijitoa mhanga, mkaligawanya taifa kwa misingi ya udini, ili CCM inusurike kuondoka madarakani iendelee kutawala.

2. Profesa Lipumba ni kati ya viongozi wa siasa wanaopaswa kuogopwa kama ukoma hapa nchini kutokana na kuwa na malengo ya kuwagawa Watanzania (wanaopendana kama ndugu) katika misingi ya imani za dini, hasa uislamu na ukristo. Inaonekana hata hatambui haki za watu wenye imani za dini zingine tofauti na hizo mbili na wapagani.

Ni mtu hatari sana huyu!

Lakini katika hali inayoonesha au kudhihirisha kumkoma nyani gidari...Tume ya Katiba Mpya, kupitia rasimu yake ya juzi, imepigilia msumari, hasa katika ibara ya 75(h)...

Ibara hiyo inayozungumzia sifa za mtu kuwa rais inasema;

Mtu atakuwa na sifa ya kuchaguliwa kushika nafasi ya kushika madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano, ikiwa;

(h) Sera ZAKE au sera za CHAMA CHAKE, si za mrengo wa kuligawa taifa kwa misingi ya ukabila, udini, rangi au jinsia.


Wandugu wangu, hapo kwenye herufi kubwa msisitizo ni wa kwangu. Lakini hapa CUF ambao siku za hivi karibuni wameskikika wakililia 'utamu' wa kuwa mojawapo ya vyama vya upinzani, wakati keki yao walishaila baada ya kuamua kuungana na CCM kisirisiri kwenye uchaguzi mkuu kama alivyotoboa Profesa Lipumba kwenye ule mkanda wake wa udini na wakaungana na CCM kwanza sirini, kisha hadharani huko Zanzibar, hawachomoki.

Hadi tunavyozungumza hapa, si CUF wala Profesa Lipumba waliotoa hoja za maana juu ya ule mkanda wa video unaomuonesha Prof mzima akifanya kazi ambayo hata mtoto wa chekechea, akisimuliwa atasema 'hakuna maana ya kwenda shule, kama elimu haijamsaidia hata huyu profesa...kuwagawa watu...kwa udini'.

Atashindwa nini kutugawa kwa ushia, sunni, ukabila, kisha maeneo!

Tunashukuru watu wa tume, katika eneo hili, hakuna Mtanzania mpenda nchi yake, atapingana nanyi hapo. Ingawa kunasikika minong'oni kuwa Profesa na watu wake watakataa, maana ndiyo uchochoro wanaotaka tena kuutumia kuibakisha CCM madarakani, maana wao kama wao, hawawezi kushinda. Wanajua.

Watanzania wote, bila kujali tofauti zetu zingine tuiunge mkono hii ibara hasa hicho kipengele.

Wote wataanguka anguko moja, maana wako pamoja.
 
Salute Chief!

Mimi kwangu ni maajabu kusikia kuwa Haruna Lipumba ni profesa hasa wa kusoma shuleni na baadaye chuoni. Kipindi cha mwanzo nilidhani ni class moja na Prof. Maji Marefu

Mwana Mtoka Pabaya

Tena mtu kama huyo akiachwa kuendelea kuwa kiongozi hata huko aliko atatufanya sote 'waenda pabaya' zaidi ya wewe 'Mtoka Pabaya', utaenda pabaya zaidi.

Hata kama hawakusoma darasa moja, lakini kwa fikra zile, kwa kweli huenda Prof. Maji Marefu anaweza kuwa afadhali kwa sababu yeye hatujawahi kumsikia akitoa hoja hatari kama zile za Prof. Ibrahim Haruna Lipumba.

Hatari kabisa.
 
hata akigombea ni nani atakayempa huo urais.

Kama hujui siasa za bongo zinavyokwenda nibora ukafyata mkia. Leohii ukimwambia mtu wa pwani na kusini kwa ujumla kuhusu CDM atakujibu "hao ni makafili na siwapi kurayangu" alkadhalika kwa wakaskazini hamuwezi ungamkono harakati zozote zifanywazo na CUF.
 
mkia upi lakini.
Kama hujui siasa za bongo zinavyokwenda nibora ukafyata mkia. Leohii ukimwambia mtu wa pwani na kusini kwa ujumla kuhusu CDM atakujibu "hao ni makafili na siwapi kurayangu" alkadhalika kwa wakaskazini hamuwezi ungamkono harakati zozote zifanywazo na CUF.
 
Vp familia yake imempa baraka ya kugombea tena?

Dallai Lama

Kwa hoja zile kwenye mkanda wa video, hata watu makini wa familia yake si kwamba hawatamuunga mkono, bali watalazimika kumkimbia na kumwogopa kama ukoma. Maana ni mtu mfilisi wa hoja na masuala na agenda kwa ajili ya watu wote. Huyu ni rahisi sana kutumika na kununulika.

Kama CCM tu wameweza kumtumia na kumnunua kwa kiwango hicho...yaaaaaaaani kumbe haya madhira tunayopata ya CCM kuendelea kubakia madarakani ikinyonya hadi tone la mwisho la Watanzania, kumbe CUF wameshiriki na Prof wao anakiri kabisa.

Jamani jamani jamani....
 
Kama hujui siasa za bongo zinavyokwenda nibora ukafyata mkia. Leohii ukimwambia mtu wa pwani na kusini kwa ujumla kuhusu CDM atakujibu "hao ni makafili na siwapi kurayangu" alkadhalika kwa wakaskazini hamuwezi ungamkono harakati zozote zifanywazo na CUF.

Kitoabu

Hoja iliyopo ni hawa jamaa au huyo jamaa kuwa hatari kwa kueneza udini, badala ya siasa. Tena kwa kuibeba CCM na mkuu wao anakiri kabisa kuwa wao na CCM ni damu damu. Maana yake hapo ni kwamba wako kinyume na Watanzania. Nani Mtanzania makini anataka chama mamluki kinachotumiwa na CCM kuendeleza mambo yale yale. Labda wewe! Watanzania makini wanataka upinzani makini ili CCM iondoke madarakani.

Vyama vyote vikifanya siasa safi vitapata mashabiki, wafuasi na wanachama kila mahali. Au unataka kuibua lingine tena la ukabila na ukanda, baada ya kuona hili la udini, limesanuka. Waislamu wajanja na makini wamelikataa.

Naona nawe unazo fikra kama za Profesa, vipi wamoja nini au ndiyo yale mambo ya "Wastara hazumbuki, wa mbili havai moja".

Jamani tunashukuru rasimu ya katiba katika kipengele hicho imetuokoa taifa zima...maana ule mkanda ni hatari

Mods mnaweza kutusaidia kuuweka tena hapa...hatari ile du!
 
CHADEMA na Sera yao ya Majimbo tena ambayo wameanza kuitekeleza kwa kuzindua kanda watachomoka?
 
lipumba has disappointed me alot,maji yashamwagika,siasa kwake imeshaingia doa,aende u-dom akashike chaki...period.
 
mkuu, hiyo katiba mpya ni mwiba kwa watu wengi sana hasa CUF na CHADEMA kwani vyote vina mwelekeo wa kidini. mbaya zaidi kwa chadema ni kuwa sera yao ya majimbo ambayo waliwadanganya watanzania kuwa ni kuharakisha maendeleo, imebainika kuwa itachochea uasi, itawagawa watu kwa misingi ya dini na ukabila. tume imekataa kata kata na kwa hali hiyo, chadema inabidi wajitathmini upya
 
Kwani Slaa mpaka sasa hivi ni padri? kwani Rasimu inasemaje kuhusu hilo

mkuu, mtu akiwa padri haiwezi kufutika. kwani upadre hutunukiwa baada ya kufikia kiwango fulani cha elimu ya dini ya kikiristo. uaskofu ndo hukoma lakini hapo pa upadre ni vigumu. kwa kuwa dr slaa ni padre, ni wazi kuwa akichaguliwa kuwamrais wa nchi basi atafanya kazi yake kwa kuipendelea dini yake. hivyo lipumba na dr slaa wote hawatufai
 
CHADEMA na Sera yao ya Majimbo tena ambayo wameanza kuitekeleza kwa kuzindua kanda watachomoka?

Vipi ile sera CCM ambao wako pamoja na CUF, ile ya kugawanya wilaya kwa makabila ni nzuri eeeeh! Ndiyo maana mko pamoja, eti Wilaya ya Iramba (Wanyiramba), Wilaya ya Ukerewe (Wakerewe) Wilaya ya....malizia ziko kibao tu. Mnawagawa watu kwa makabila yao.

Sasa sera ya hao jamaa wa chadema unaowaponda mfano, Kanda yao ya Kaskazini inajumuisha mikoa ya Manyara, Tanga, Kilimanjaro na Arusha, hebu tuambie yote hiyo ni kabila na dini moja.

Usiwe mfuasi tu wa profesa kuibeba CCM kwenye uchaguzi kwa misingi ya dini. Yaani watu wanatumia dini kuabudu, kwenda peponi, ninyi kwa fikra za akina Profesa Lipumba mnaitumia kuibeba CCM.

Aisee kizazi hiki na vijavyo vitawalaani. Hata Mwenyezi Mungu hawezi kukubali.
 
Wapo wa kumpa kura, ndiyo maana wana hamu sana wajue wapo wangapi nchini, hawa jamaa hawapo organized kabisa hivi wanashindwa vipi kujijua wapo wangapi?

'Via Mobile'
nyie mnaojijua mbona hamsemi mko wangapi? mna tofauti gani na wale wasiojijua?
 
Vipi ile sera CCM ambao wako pamoja na CUF, ile ya kugawanya wilaya kwa makabila ni nzuri eeeeh! Ndiyo maana mko pamoja, eti Wilaya ya Iramba (Wanyiramba), Wilaya ya Ukerewe (Wakerewe) Wilaya ya....malizia ziko kibao tu. Mnawagawa watu kwa makabila yao.

Sasa sera ya hao jamaa wa chadema unaowaponda mfano, Kanda yao ya Kaskazini inajumuisha mikoa ya Manyara, Tanga, Kilimanjaro na Arusha, hebu tuambie yote hiyo ni kabila na dini moja.

Usiwe mfuasi tu wa profesa kuibeba CCM kwenye uchaguzi kwa misingi ya dini. Yaani watu wanatumia dini kuabudu, kwenda peponi, ninyi kwa fikra za akina Profesa Lipumba mnaitumia kuibeba CCM.

Aisee kizazi hiki na vijavyo vitawalaani. Hata Mwenyezi Mungu hawezi kukubali.
subutu? eti tanga ipo kanda ya kaskazini. tanga haipo huko. chadema wamegawa kanda zao kwa misingi ya udini zaidi
 

Similar Discussions

7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom