Katiba mpya bila utekelezaji ni kazi bure

MKEHA

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
713
1,136
Kumekuwa na movement na msukumo kutoka makundi mbali mbali ya kutetea haki za nimadamu, NGO na vyama vya siasa hasahasa vya upinzani kutaka katiba mpya. Ni jambo zuri sana japo kwa upande wa CCM hainekani kuwa ni ajenda wala kioaumbele chao.

Lakini kama tunavyojua nchi hii haijawahi kuwa na upungufu wa mipango mizuri,sera nzuri na sheria nzuri kiasi chake. Tatizo huwa ni implementation yake.

Nani asijejua kuwa Katiba yetu imetoa Uhuru wa kutoa maoni, kujiunga na vyama vya siasa, kujumuika pakoja, kuandamana kama kuna jambo mahsusi. Je yote haya huwa tunayakazania kwenye maisha yetu ya kila siku?

Katiba yetu japo ina mapungufu lakini imeweka bayana majukumu ya mihimili yetu ya dola kwa maana ya wajibu wa kila muhilimi yaani Serikali, Bunge na Mahakama. Lakini bado kama nchi na raia bado tumelala sana na hatujui wapi wajibu wetu kwa vyombo hivyo unaanzia wapi na kuishia wapi.

Wasomi wachache ndio wanaoweza kuona mapungufu ya katiba yetu.
Hivyo Nina wasiwasi sana tunaweza kuwa na katiba mpya nzuri sana lakini watekelezaji wake na utekelezaji wa katiba hiyo usionueshe tofauti ya katiba ya zamani na mpya.

Ni matumaini yangu kuwa kuna haja kwanza ta kuelimisha umma na vyama vyote kuwa na agenda hiyo ili kazi iwe nyepesi sana lakini pia utekelezaji wake uwe mwepesi kwa kila mtekelezaji wa katiba hiyo kwa nafasi zao
 
Tatizo la Katiba iliyopo kiutekelezaji ni madaraka makubwa aliyonayo rais. Unakuta katiba inatekelezwa kwa utashi wa rais aliyeko madarakani. Ndio maana tunataka madaraka ya rais yapunguzwe,na nguvu hizo zihamie kwenye taasisi.
 
Ndio maana wanataka katiba mpya ambayo itapunguza mamlaka ya Rais
 
Tatizo la Katiba iliyopo kiutekelezaji ni madaraka makubwa aliyonayo rais. Unakuta katiba inatekelezwa kwa utashi wa rais aliyeko madarakani. Ndio maana tunataka madaraka ya rais yapunguzwe,na nguvu hizo zihamie kwenye taasisi.
Hizo taasi nazo zinàongozwa na binadamu wenye utashi wao pia
 
Hizo taasi nazo zinàongozwa na binadamu wenye utashi wao pia

Uko sahihi kabisa, lakini nguvu zinapokuwa kwenye taasisi kutakuwa na check and balancies ambazo zitapunguza wote kuongozwa na utashi wa mtu mmoja.
 
Uko sahihi kabisa, lakini nguvu zinapokuwa kwenye taasisi kutakuwa na check and balancies ambazo zitapunguza wote kuongozwa na utashi wa mtu mmoja.
Bunge lipo kwa kazi hiyo ya Check and balance tena kikatiba. Je wanafanya hivyo effectively pamoja na kuwa na gutts zote kwa mujibu wa katiba?
 
Bunge lipo kwa kazi hiyo ya Check and balance tena kikatiba. Je wanafanya hivyo effectively pamoja na kuwa na gutts zote kwa mujibu wa katiba?

Narudia tena, kwa katiba hii rais ndio muamuzi wa kila kitu, hakuna cha bunge wala mahakama. Mfano mrahisi ni jinsi hiko bunge lilivyopatikana safari hii, ni kwa maagizo ya rais na wala sio kwa kura za wananchi. Huko mahakamani Jaji Mkuu ni mteule wa rais, hivyo mihimili yote hiyo miwili inategemea hisani ya rais.
 
Bunge lipo kwa kazi hiyo ya Check and balance tena kikatiba. Je wanafanya hivyo effectively pamoja na kuwa na gutts zote kwa mujibu wa katiba?

Hukusikia mhimili mmoja unamizizi mirefu zaidi ya mingine.

Wafukuze bungeni niwashughulikie huku nje

Job akatekeleza alivotumwa, kawafukuza

Nje wakashughulikiwa.

Unaongelea bunge gani?
 
Ukiona katiba inaweza kuvunjwa na anayeivunja hiyo katiba haimsulubishi basi hiyo siyo katiba ni kijarida tu.

Katiba huwa ina wivu, huwa inajilinda, huwa ina meno makali yanayo ng'ata.

Kwahiyo usitutishe.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom