Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Wanabodi, nimeona niwawekee kauli ya M/Kiti wa Chadema, Mhe. Freeman Mbowe akihojiwa na BBC jana jioni kuhusu mazungumzo ya Chadema na rais Jakaya Kikwete.
Ili kuwasaidia wasioweza kuifungua haya mahojiano, nitawawekea transcription ya alichoongea neno kwa neno.
Hear for yourself from Horses Mouth!.
Pasco
Update 1. Transcript:
Transcript
Charles Hillary : " ...Rais wa nchi hiyo Jakaya Kikwete kuendelea kuineemesha katiba hiyo ili kukidhi mahitaji ya kujenga kuaminiana na muafaka wa kitaifa. Makubaliano hayo yamefanyika baada ya chama cha Chadema ambacho wabunge wake walisusia hatua ya kusomwa na kupitishwa kwa muswada wa juu ya kuundwa katiba mpya nchini humo, kuomba kukutana na rais Kikwete.
Eric David Nampesya, amezungumza na mwenyekiti wa chama cha Chadema, Freeman Mbowe, kwanza anaeleza kilichoafikiwa kwenye mazungumzo hayo"
Mhe. Mbowe: "Cha msingi kuliko vyote, ni kwamba ni vyema kila mmoja wetu na kila Mtanzania akatambua kwamba, hoja ya kubadilisha ama kuandika upya katiba yetu ni ho
ja ambayo ni ya mchakato, siyo jambo ambalo linamalizika kwa siku moja, kwa maana hiyo tumekubalianan kimsingi kwamba, iko haja ya kufanya mashauriano mara kwa mara na wadau mbalimbali, sio Chadema peke yake, wako wadau wengi katika taifa hili ambao wanapenda kuona mabadiliko haya ya katiba, yanatujenga kama taifa na hayatugawi kama taifa, kwa hiyo tumekubaliana kimsingi kwamba, ipo haja ya kuendelea kufanya vikao vya mashauriano tumemuomba rais pia aendelee kufa mashauriano na wadau wengine ndani ya vyama vya siasa, nje ya vyama vya siasa ili kuendelea zaidi kupata muafaka wa kitaifa
Eric David Nampesya: " Lakini hoja yenu ya msingi ilikuwa ni kupinga jinsi mchakato ule mzima ulivyoendesha ambapo muswada ulisomwa kwa mara ya pili, nyinyi mkipinga kutaka usomwe kwa mara ya kwanza, inamaana sasa mmeridhia kilichotokea katika bunge mjini Dodoma?.
Mhe. Freeman Mbowe: "Hapana, hapana, hatujaridhia kilichofanyika Dodoma, bado tumelalamika kuwa muswada ule ni mbovu, na bado tumeiachia serikali tuone itafanya nini katika kuurekebisha muswada huo, na tunajua wako wadau wengine wengi ambao nao wana mawazo yao, tunaimani kwamba serikali, kwa kauli aliyoitoa rais, pengine nae atawapa fursa ya kuwasikiliza malalamiko yao, kisha pengine serikali ilete sasa marekebisho ya ya ya sheria, ili kuwezesha kuingiza hoja mbalimbali ama kupunguza mambo mbalimbali yaliyokuwa yana lalamikiwa".
Eric David Nampesya: Awali mlisema kwamba kama rais asingekutana na ninyi mngepeleka kilio chenu kwa wananchi hali inayotafsiriwa kwamba ni kuhamasisha maandamano nchi nzima, kwa maana hii, baada ya rais kukutana na ninyi, sasa mnafuta mpango wenu huo?.
Mhe. Freeman Mbowe: "Ehe ee niseme tuu kwambaa..., tumezungumza tuu kwa kina kwa kweli, tumezungumza kwa kina, naa na serikali imeonyesha nia kutaka kufanya marekebisho ya msingi katika katiba hii, na kwa maana hiyo, tutaitegemea serikali kuchukua hatua za haraka, katika kikao kijacho cha bunge, tufanye baadhi ya mabadiliko ambayo yatapelekea kuleta mshikamano na maridhiano. Kwa maana hiyo, hatutakuwa na maandamano ya kupinga katiba katika hatua ya sasa, mpaka tungojee serikali ifanye mabadiliko ya msingi"
Transcript inaendelea...
Ili kuwasaidia wasioweza kuifungua haya mahojiano, nitawawekea transcription ya alichoongea neno kwa neno.
Hear for yourself from Horses Mouth!.
Pasco
Update 1. Transcript:
Transcript
Charles Hillary : " ...Rais wa nchi hiyo Jakaya Kikwete kuendelea kuineemesha katiba hiyo ili kukidhi mahitaji ya kujenga kuaminiana na muafaka wa kitaifa. Makubaliano hayo yamefanyika baada ya chama cha Chadema ambacho wabunge wake walisusia hatua ya kusomwa na kupitishwa kwa muswada wa juu ya kuundwa katiba mpya nchini humo, kuomba kukutana na rais Kikwete.
Eric David Nampesya, amezungumza na mwenyekiti wa chama cha Chadema, Freeman Mbowe, kwanza anaeleza kilichoafikiwa kwenye mazungumzo hayo"
Mhe. Mbowe: "Cha msingi kuliko vyote, ni kwamba ni vyema kila mmoja wetu na kila Mtanzania akatambua kwamba, hoja ya kubadilisha ama kuandika upya katiba yetu ni ho
ja ambayo ni ya mchakato, siyo jambo ambalo linamalizika kwa siku moja, kwa maana hiyo tumekubalianan kimsingi kwamba, iko haja ya kufanya mashauriano mara kwa mara na wadau mbalimbali, sio Chadema peke yake, wako wadau wengi katika taifa hili ambao wanapenda kuona mabadiliko haya ya katiba, yanatujenga kama taifa na hayatugawi kama taifa, kwa hiyo tumekubaliana kimsingi kwamba, ipo haja ya kuendelea kufanya vikao vya mashauriano tumemuomba rais pia aendelee kufa mashauriano na wadau wengine ndani ya vyama vya siasa, nje ya vyama vya siasa ili kuendelea zaidi kupata muafaka wa kitaifa
Eric David Nampesya: " Lakini hoja yenu ya msingi ilikuwa ni kupinga jinsi mchakato ule mzima ulivyoendesha ambapo muswada ulisomwa kwa mara ya pili, nyinyi mkipinga kutaka usomwe kwa mara ya kwanza, inamaana sasa mmeridhia kilichotokea katika bunge mjini Dodoma?.
Mhe. Freeman Mbowe: "Hapana, hapana, hatujaridhia kilichofanyika Dodoma, bado tumelalamika kuwa muswada ule ni mbovu, na bado tumeiachia serikali tuone itafanya nini katika kuurekebisha muswada huo, na tunajua wako wadau wengine wengi ambao nao wana mawazo yao, tunaimani kwamba serikali, kwa kauli aliyoitoa rais, pengine nae atawapa fursa ya kuwasikiliza malalamiko yao, kisha pengine serikali ilete sasa marekebisho ya ya ya sheria, ili kuwezesha kuingiza hoja mbalimbali ama kupunguza mambo mbalimbali yaliyokuwa yana lalamikiwa".
Eric David Nampesya: Awali mlisema kwamba kama rais asingekutana na ninyi mngepeleka kilio chenu kwa wananchi hali inayotafsiriwa kwamba ni kuhamasisha maandamano nchi nzima, kwa maana hii, baada ya rais kukutana na ninyi, sasa mnafuta mpango wenu huo?.
Mhe. Freeman Mbowe: "Ehe ee niseme tuu kwambaa..., tumezungumza tuu kwa kina kwa kweli, tumezungumza kwa kina, naa na serikali imeonyesha nia kutaka kufanya marekebisho ya msingi katika katiba hii, na kwa maana hiyo, tutaitegemea serikali kuchukua hatua za haraka, katika kikao kijacho cha bunge, tufanye baadhi ya mabadiliko ambayo yatapelekea kuleta mshikamano na maridhiano. Kwa maana hiyo, hatutakuwa na maandamano ya kupinga katiba katika hatua ya sasa, mpaka tungojee serikali ifanye mabadiliko ya msingi"
Transcript inaendelea...