Katiba inasemaje: Rais akifukuzwa uanachama na chama chake?

Tanzania Mpya

JF-Expert Member
Apr 11, 2012
253
144
Wah, sijui kama katiba inaelekeza kuhusu hoja hii... Mbunge akifukuzwa na chama chake ataendelea na ubunge wake. Je, Rais itakuwaje? Mliopitia rasimu, vipi kuna maelekezo yoyote? Na je akihama chama wakati yupo madarakani?

Naomba ufafanuzi wakuu. Na kama haisemi chochote, je kuna haja ya kufafanua masuala haya?
 
Nakumbuka, kama sikosei, Rais wa Malawi alianzisha chama chake akiwa Rais na kuendelea, wakati aliupata urais kwa kupitia chama kingine.

Wenye kujua zaidi, pls wachangie nielimike.
 
Kwenu wadau na wanaojua katiba ya nchi yetu na kanuni zake pamoja na katiba za vyama vyetu vya siasa.

Kinachokwenda kutokea nchini mwetu ni uwezekano wa kuwa na Rais pamoja na makamu ambao si viongozi kwa maana ya wenyeviti au makamu wa vyama husika bali ni wanachama tu.

Sasa iwapo katika hali zao za uanachama ikatokea hawakwenda au kutekeleza yale ambayo Katiba za vyama vyao zinawaelekeza kufanya au kusimamia ilani ya uchaguzi na kupelekea kuvuliwa uanachama.

Je, ukomo wa urais wao ndio unaishia hapo au nini kinafuata? Swali hili nalitoa kwenye sababu ambazo Ubunge wa mtu unaweza kukoma.

Vyama vingi vimeweka wazi bila kusahau sheria ya Bunge kwamba iwapo mbunge yeyote yule akivuliwa uanachama katika chama basi nafasi yake ya ubunge nayo inakoma mara vinginevyo abakie kuwa mbunge wa mahakama kama ilivyokuwa kwa Mh. ZZK.

Naomba mwenye mawazo chanya ili watanzania tujue tunapofanya maamuzi nini tukitarajie! Kama tukishachagua ndio imetoka hatuwezi kumshikisha adabu bali yeye ni juu ya yote katika yote au chama kimeshika mpini na rais aliye mwanachama yuko kwenye makali! Akileta za kuleta, ANAKATWA! Nawasilisha!
 
Wale majaji aliowateuwa na kuwapa mamlaka ndo watakao toa hukumu ya kesi yake ya kuvuliwa uanachama. Sasa jiulize wataamua nini kwa aliyewapa nyadhifa hizo
 
Kutokana na uelewa wangu mdogo kwenye mambo ya sheria!nafaham nchi inaendeshwa kwa mujibu sheria na katiba!

Kukiuka ilan ambayo baadae unakuwa dira ya miaka mitano ambayo inathibitishwa na bunge ni kuvunja sheria za nch hivyi suala hili haliwi la chama linakuwa la bunge ambapo chama chenye hyo rais kinaweza kumchongea kwa wabunge wake ili wapige kura ya kutokuwa na imani na serkal kama chama hicho nancho kimemchukia!

Then baada takwa la kisheria la bunge kutokuwa na iman na serikal kinachofuata ni kuvunja bunge na automatic rais anapoteza madaraka! Hivyo process za chama kumvua uanachama zinaanzia hapo! Ref issue ya thabo mbeki na anc.

nasisitiza gii ni kwa uelewa wangu
 
Wale majaji aliowateuwa na kuwapa mamlaka ndo watakao toa hukumu ya kesi yake ya kuvuliwa uanachama. Sasa jiulize wataamua nini kwa aliyewapa nyadhifa hizo

Assume hao majaji wameteuliwa na rais mwingine aliyetangulia let's JK na anayeingia ni huyo EL au Magufuli then rais mteule akavunja kaiba ya chama na kuvuliwa uanachama. Unadhani Majaji bado watakuwa na nguvu ya kuendelea ku-favour ikiwa ni haki bin haki?
 
Katiba ya nchi inasema rais, makamu wa rais, waziri mkuu na wabunge lazima wawe wanachama wa chama fulani.
Endapo watafukuzwa uanachama ni kwamba wanaachia ngazi.
 
Kutokana na uelewa wangu mdogo kwenye mambo ya sheria!nafaham nchi inaendeshwa kwa mujibu sheria na katiba! Kukiuka ilan ambayo baadae unakuwa dira ya miaka mitano ambayo inathibitishwa na bunge ni kuvunja sheria za nch hivyi suala hili haliwi la chama linakuwa la bunge ambapo chama chenye hyo rais kinaweza kumchongea kwa wabunge wake ili wapige kura ya kutokuwa na imani na serkal kama chama hicho nancho kimemchukia! Then baada takwa la kisheria la bunge kutokuwa na iman na serikal kinachofuata ni kuvunja bunge na automatic rais anapoteza madaraka! Hivyo process za chama kumvua uanachama zinaanzia hapo! Ref issue ya thabo mbeki na anc
nasisitiza gii ni kwa uelewa wangu

Najua ndio kwamba Bunge linaweza piga kura ya kutokuwa na imani na Rais. Hii haijalishi huyo Rais anatoka chama gani. Na kosa hapa lazima liwe aidha matumizi mabaya ya ofisi au tuhuma nzito za kikatiba ya nchi na si chama. Lakini turudi kwenye vyama, Kwani Rais akishateuliwa anakuwa juu ya chama? Au chama ndio kina mamlaka juu ya Rais kama ilivyo kwa wabunge wa vyama? Maana Rais mteule amepewa tiketi na chama chake sasa kama amevunja katiba ya chama na kutemwa kwa nini urais nao usikome kama wabunge?
 
Katiba ya nchi inasema rais, makamu wa rais, waziri mkuu na wabunge lazima wawe wanachama wa chama fulani.
Endapo watafukuzwa uanachama ni kwamba wanaachia ngazi.

Asante Bavaria kwa jibu lako kwa hiyo unataka kusema ikitokea EL au Magufuli akileta za kuleta kwenye chama, anaweza kupigwa chini chamani na kibarua kikaota nyasi au sio?
 
Last edited by a moderator:
Ndugu yangu! Nafurah na mijadala kama hii maana najifunza na pengine nafundisha na wenzangu! Rais ni mkuu wa nchi,amiri jesh mkuu wa majesh ya ulinz na usalama! Anapochaguliwa ule umiliki wa chama nadhan unakufa ndio maana ccm wanamfanya awe mwenyekiti ili pamoja na kupokea favour uoka serikalin panakuwa na kakitisho ka wale mausalama ya protokali! Lkn pia rais ni taasisi sio mtu mmoja aliechaguliwa! Upo utaratibu wa kisheria wa kuunda serikal ya mpito ambayo itaongozwa na makam wa rais,jaji mkuu,waziri mkuu au spika wa bunge kutuvusha kwenda kwenye uchaguz
Najua ndio kwamba Bunge linaweza piga kura ya kutokuwa na imani na Rais. Hii haijalishi huyo Rais anatoka chama gani. Na kosa hapa lazima liwe aidha matumizi mabaya ya ofisi au tuhuma nzito za kikatiba ya nchi na si chama. Lakini turudi kwenye vyama, Kwani Rais akishateuliwa anakuwa juu ya chama? Au chama ndio kina mamlaka juu ya Rais kama ilivyo kwa wabunge wa vyama? Maana Rais mteule amepewa tiketi na chama chake sasa kama amevunja katiba ya chama na kutemwa kwa nini urais nao usikome kama wabunge?
 
Mods naomba hii iwe sticky kutokana na tanzania sasa inaelekea huko mtoa mada kama alivyoleta! Au ipelekwe GT maana tunaenda pata rais na makamu wake ambao ni wanachama wa kawaida kabisa kutoka UKAWA! Ambao mpaka sasa wanakuwa ni waalikwa kwenye vikao kama cc na baraza kuu
 
Asante Bavaria kwa jibu lako kwa hiyo unataka kusema ikitokea EL au Magufuli akileta za kuleta kwenye chama, anaweza kupigwa chini chamani na kibarua kikaota nyasi au sio?

Ndio kabisa, ndio maana CCM wanataka mwenyekiti wa chama awe rais kuogopa kuzidiwa nguvu.
 
Katiba ya nchi inasema rais, makamu wa rais, waziri mkuu na wabunge lazima wawe wanachama wa chama fulani.
Endapo watafukuzwa uanachama ni kwamba wanaachia ngazi.

Katiba haiko very clear. Haisema akifukuzwa uanachama anapoteza urais bali inasema "kiti cha Rais kitakuwa wazi endapo Rais atapoteza sifa za kushika nafasi madaraka ya kuchaguliwa". Ingesema "madaraka ya kuchaguliwa kuwa rais" ingekuwa clear. Kwa sababu kuwa rais lazima uwe mwanachama na upendekezwe nafasi ya urais na chama. Kwa mtazamo wangu naona kesi ya namna hii itakapotokea itabadi jopo la majaji litoe tafsiri hiyo "madaraka ya kuchaguliwa" ina maanisha nini hasa. Naweza kuwa nimekosea. Naomba wanasheria watujuze zaidi.
 
Wale majaji aliowateuwa na kuwapa mamlaka ndo watakao toa hukumu ya kesi yake ya kuvuliwa uanachama. Sasa jiulize wataamua nini kwa aliyewapa nyadhifa hizo
Ndio maana tumesema majaji sasa watapata ajira kwa kuomba kazi kama wa Kenya,habari ya uteuzi mwisho ili wawe huru.
 
Katiba ya nchi inasema rais, makamu wa rais, waziri mkuu na wabunge lazima wawe wanachama wa chama fulani.
Endapo watafukuzwa uanachama ni kwamba wanaachia ngazi.

Tupatie kifungu gani tukajisomee.
 
WanaJF,

Naomba kupata Elimu ya kisheria kwa kunisaidia vifungu vya katiba ya JMT. Leo Mtaani kwetu kumetokea mjadala baadhi wanasema ikitokea CCM wakamnyang'anya uanachama Rais Magufuli atakuwa amepoteza urais na hivyo kuitishwa uchaguzi mwingine, kwa kuwa ili ugombee urais sharti uwe mwanachama wa chama fulani hivo akishafutwa na chama chake amepoteza sifa za kua rais.

Wengine wanasema CCM ikimfuta uanachama, anayo kinga ya kikatiba na sheria za nchi ambazo, vinazungumza rais atakaa madarakani kwa kipindi cha miaka 5, na ikitokea kuugua kichaa au ugonjwa hatari sana kutojiweza, akivunja katiba kwa kutumia vibaya madaraka yake au akifariki uchaguzi mwingine waweza kuitishwa kikatiba.

Kundi hili likasisitiza kuwa kwa makosa ya kutumia vibaya madaraka yake, au kufutwa uanachama na chama chake atabakia kuwa rais mpaka Hoja ya kutaka kumuondoa madarakani ipelekwe bungeni na theluthi mbili au zaidi ya wabunge ikubali hoja hiyo ya kuondolewa madarakani na si eti ilimradi tu Magufuli anawakaba CCM eti wanaweza kupoteza urais wake kirahisi namna hiyo.

Ni kweli hakuna sheria ya mgombea binafsi lakini pia sheria ya kuwa kugombea ni sharti upitie chama cha siasa ipo lakini ni njia tu sasa ameshafika hivo haina nguvu tena yeye ni rais wa JMT analindwa na KATIBA YA JMT hao CCM hawana ubavu.

Naomba kuwasilisha.
 
WanaJF,

Naomba kupata Elimu ya kisheria kwa kunisaidia vifungu vya katiba ya JMT. Leo Mtaani kwetu kumetokea mjadala baadhi wanasema ikitokea CCM wakamnyang'anya uanachama Rais Magufuli atakuwa amepoteza urais na hivyo kuitishwa uchaguzi mwingine, kwa kuwa ili ugombee urais sharti uwe mwanachama wa chama fulani hivo akishafutwa na chama chake amepoteza sifa za kua rais. Wengine wanasema CCM ikimfuta uanachama, anayo kinga ya kikatiba na sheria za nchi ambazo, vinazungumza rais atakaa madarakani kwa kipindi cha miaka 5, na ikitokea kuugua kichaa au ugonjwa hatari sana kutojiweza, akivunja katiba kwa kutumia vibaya madaraka yake au akifariki uchaguzi mwingine waweza kuitishwa kikatiba.

Kundi hili likasisitiza kuwa kwa makosa ya kutumia vibaya madaraka yake, au kufutwa uanachama na chama chake atabakia kuwa rais mpaka Hoja ya kutaka kumuondoa madarakani ipelekwe bungeni na theluthi mbili au zaidi ya wabunge ikubali hoja hiyo ya kuondolewa madarakani na si eti ilimradi tu Magufuli anawakaba CCM eti wanaweza kupoteza urais wake kirahisi namna hiyo. Ni kweli hakuna sheria ya mgombea binafsi lakini pia sheria ya kuwa kugombea ni sharti upitie chama cha siasa ipo lakini ni njia tu sasa ameshafika hivo haina nguvu tena yeye ni rais wa JMT analindwa na KATIBA YA JMT hao CCM hawana ubavu.

Naomba kuwasilisha.

Kwa nini wamfute uanachama?hao walokua wanasema hayo hawajitambui na yamkini walikua wamepombeka,ccm kundi la watu wengi sana,na wapo ambao wana uchungu na nchi na sisi wananchi tulivyo na ugumu wa maisha,sasa walioshindwa kuongoza kama anavyoongoza JPM hawawezi shangaa na hawawezi mfuta huyo mtu uanachama kwa sababu siyo ccm wote ni watovu wa nidhamu,wapo watakaomtetea kwa utendaji wake,wenye kutenda ktk haki,kwa hyo kuwaza kua kuna siku Rais watamfuta uanachama ni kujifikirisha tu kusiko na majibu ya wakifikiliacho!
 
Mafisadi wote ndani ya ccm watamfuata fisadi mwenzao aliyekatwa.

salamu za kwa mzee wa pumzi hafifu aka Kingungue
 
Vikao vya CCM wiki ijayo vina agenda gani.? Kwanza tujuze.?
Magufuli ni mmoja wa wahudhuriaji.?
 
Back
Top Bottom