Elections 2010 Katiba inasema kiti cha Rais kipo wazi

Wakati na muda
wa kushika
madaraka ya
Rais
Sheria ya 1984
Na.15 ib.9
42.-(1) Rais mteule atashika madaraka ya Rais mapema
iwezekanavyo baada ya kutangazwa kwamba amechaguliwa
kuwa Rais, lakini kwa hali yoyote itabidi ashike madaraka kabla
ya kupita siku saba.
(2) Isipokuwa kama atajiuzulu au atafariki mapema zaidi mtu
aliyechaguliwa kuwa Rais, bila ya kuathiri masharti yaliyo katika
ibara ndogo ya (3), atashika kiti cha Rais kwa muda wa miaka
mitano tangu siku alipochaguliwa kuwa Rais.
(3) Mtu aliyechaguliwa kuwa Rais atashika kiti cha Rais hadi-
(a) siku ambapo mtu atakayemfuatia katika kushika kiti
hicho atakula kiapo cha Rais;
au
(b) siku ambapo atafariki dunia akiwa katika madaraka;
au
(c) siku atakapojiuzulu; au
(d) atakapoacha kushika kiti cha Rais kwa mujibu wa
masharti ya Katiba hii.


Au wanatumia kifungu hichi, kuwa rais aliyechaguliwa ataendelea kuwa rais hadi rais mpya atakapo apishwa
 
Wakati na muda
wa kushika
madaraka ya
Rais
Sheria ya 1984
Na.15 ib.9
42.-(1) Rais mteule atashika madaraka ya Rais mapema
iwezekanavyo baada ya kutangazwa kwamba amechaguliwa
kuwa Rais, lakini kwa hali yoyote itabidi ashike madaraka kabla
ya kupita siku saba.
(2) Isipokuwa kama atajiuzulu au atafariki mapema zaidi mtu
aliyechaguliwa kuwa Rais, bila ya kuathiri masharti yaliyo katika
ibara ndogo ya (3), atashika kiti cha Rais kwa muda wa miaka
mitano tangu siku alipochaguliwa kuwa Rais.
(3) Mtu aliyechaguliwa kuwa Rais atashika kiti cha Rais hadi-
(a) siku ambapo mtu atakayemfuatia katika kushika kiti
hicho atakula kiapo cha Rais;
au
(b) siku ambapo atafariki dunia akiwa katika madaraka;
au
(c) siku atakapojiuzulu; au
(d) atakapoacha kushika kiti cha Rais kwa mujibu wa
masharti ya Katiba hii.


Au wanatumia kifungu hichi, kuwa rais aliyechaguliwa ataendelea kuwa rais hadi rais mpya atakapo apishwa

Nafikiri hapo umeshamaliza, JK bado ni Rais hadi hapo mteule anayefuata (Dkt Slaa) atakayeapishwa!
 
Wadau nilikuwa napitia katiba katika tovuti ya taifa (www.tanzania.go.tz) nimekutana na hiki kipengele ambacho nimekuwa interested kujua zaidi:


38.-(1) Rais atachaguliwa na wananchi kwa mujibu wa
masharti ya Katiba hii na kwa mujibu wa sheria itakayoweka
masharti kuhusu uchaguzi wa Rais ambayo itatungwa na Bunge
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kwa kufuata masharti ya Katiba hii.
Sheria ya 1992
Na.20 ib.5
Sheria ya 1994
Na.34 ib.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Katiba hii, kiti cha
Rais kitakuwa ki wazi, na uchaguzi wa Rais utafanyika au nafasi
hiyo itajazwa vinginevyo kwa mujibu wa Katiba hii, kadri
itakavyokuwa, kila mara litokeapo lolote kati ya mambo
yafuatayo:-
(a) baada ya Bunge kuvunjwa;
(b) baada ya Rais kujiuzulu bila ya kulivunja Bunge
kwanza:
(c) baada ya Rais kupoteza sifa za kushika nafasi
madaraka ya kuchaguliwa;
(d) baada ya Rais kushtakiwa Bungeni kwa mujibu wa
Katiba hii, na kuondolewa katika madaraka;
(e) baada ya kuthibitishwa kwa mujibu wa masharti ya
ibara ya 37 ya Katiba hii kwamba Rais hawezi
kumudu kazi na shughuli zake;
(f) baada ya Rais kufariki.
(3) Kiti cha Rais hakitahesabiwa kuwa kiwazi kwa sababu tu
ya Bunge kupitisha hoja ya kutokuwa na imani kwa Waziri Mkuu.


Kwa sasa bunge lilishavunjwa, Kwanini JK bado anaitwa Rais wa JMT?!
Au kuna kipengele kingine kinachosema otherwise?!

Ibara ya 42 (3) (a) inapinga na kusema Rais aliyepo madarakani atamaliza muda wake mara tu yule mteule akiapishwa. Katiba yetu utafikiri ilitungwa na kurekebishwa na walevi!!
 
Back
Top Bottom