Katiba iliyopo ikifumuliwa

South

JF-Expert Member
Jan 11, 2016
3,514
5,137
Habari wakuu natumai juma pili ilikua tulivu kwenu. Turudi kwenye maada, kama tujuavyo katiba yetu hii tuliyoachiwa na mkoloni ilivyo na madudu hasa kwa kumpa nguvu kubwa raisi. Pia kumpa kinga ya kutoshitakiwa endapo atakua kamaliza madaraka yake hata kama alifanya makosa.
Ikitokea tukafanikiwa kuifumua na kuirekebisha upya hasa kwa kuondoa kile kipengele cha kinga ya kutoshitakiwa, je tutakua na marais wastaafu wafungwa au tutasahau yaliyopita? Maana hakuna rais atakaye salimika kwani wote ni watuhumiwa kwa madudu waliyoyafanya zama zao japo hiyo kinga yao ndo inayo block kushitakiwa kwao.
 
Habari wakuu natumai juma pili ilikua tulivu kwenu. Turudi kwenye maada, kama tujuavyo katiba yetu hii tuliyoachiwa na mkoloni ilivyo na madudu hasa kwa kumpa nguvu kubwa raisi. Pia kumpa kinga ya kutoshitakiwa endapo atakua kamaliza madaraka yake hata kama alifanya makosa.
Ikitokea tukafanikiwa kuifumua na kuirekebisha upya hasa kwa kuondoa kile kipengele cha kinga ya kutoshitakiwa, je tutakua na marais wastaafu wafungwa au tutasahau yaliyopita? Maana hakuna rais atakaye salimika kwani wote ni watuhumiwa kwa madudu waliyoyafanya zama zao japo hiyo kinga yao ndo inayo block kushitakiwa kwao.


Mimi mpaka leo sijaelewa yale maoni ya wananchi kwenye katiba mpya yalienda wapi na huo mchakato sijui uliishia wapi?? au ndio ile katiba pendekezwa?
 
Mimi mpaka leo sijaelewa yale maoni ya wananchi kwenye katiba mpya yalienda wapi na huo mchakato sijui uliishia wapi?? au ndio ile katiba pendekezwa?
Yapo kwenye kabati maana huyu aliyepo alisema ktk ahadi zake hakukua na maswala ya katiba mpya
 
Magufuli siku nitamuelewa anaposema anawapigania wanyonge ni pale atakapo amua kuliacha bunge liwe huru na haki sawa kwa wote.

Akishafanya hivyo arudi kwa wabunge aombe swala la katiba mpya lirudiwe tena, baada ya hapo aende mbali kuvunja mikataba yote ya kinyonyaji huku katiba ikimpa nguvu na kiburi kuwa Watanzania hata kama sio wote tupo nyuma yake...

Haya yote sijui kama yatatokea kwa huyu Magufuli anayeona kuwa mpinzani ni laana kwa nchi hii kwa kauli zake kama za Moshi eti amewasamehe watu kisa kuchagua upinzani ama wabunge ambao wangeenda kumsalimia Lema gerezani basi ni dhambi ama Bulembo sijui amkanye bintiye kisa anatembea sijui na Mpinzani atatoa siri zao.

Vinginevyo tuendelee kupiga tantalila tu tusubirie miaka mingine mitano ya kuliwa resources za nchi yetu.
 
Magufuli siku nitamuelewa anaposema anawapigania wanyonge ni pale atakapo amua kuliacha bunge liwe huru na haki sawa kwa wote.

Akishafanya hivyo arudi kwa wabunge aombe swala la katiba mpya lirudiwe tena, baada ya hapo aende mbali kuvunja mikataba yote ya kinyonyaji huku katiba ikimpa nguvu na kiburi kuwa Watanzania hata kama sio wote tupo nyuma yake...

Haya yote sijui kama yatatokea kwa huyu Magufuli anayeona kuwa mpinzani ni laana kwa nchi hii kwa kauli zake kama za Moshi eti amewasamehe watu kisa kuchagua upinzani ama wabunge ambao wangeenda kumsalimia Lema gerezani basi ni dhambi ama Bulembo sijui amkanye bintiye kisa anatembea sijui na Mpinzani atatoa siri zao.

Vinginevyo tuendelee kupiga tantalila tu tusubirie miaka mingine mitano ya kuliwa resources za nchi yetu.
Ni ngumu kwa yeye kuligusia swala la katiba mpya hasa ukizingatia yeye mwenyewe amekua mstari wa mbele kutoisimamia
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom