Katiba Ijayo: Utumishi wa Umma

Emc2

JF-Expert Member
Sep 26, 2011
16,808
16,834
Nimeipenda sana. Kuna baadhi ya vipengele vimenikosha zaidi.

Hebu cheki:

15.-(1) Zawadi au kitu chochote kitakachotolewa kwa
mtumishi wa umma katika shughuli za kiserikali ni zawadi kwa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na itawasilishwa kwa Katibu
Mkuu Kiongozi kupitia kwa Katibu Mkuu wa Wizara au taasisi ya
Serikali inayohusika, akiainisha:
(a) aina ya zawadi;
(b) thamani ya zawadi;
(c) sababu ya kupewa zawadi; na
(d) mtu au mamlaka iliyotoa zawadi hiyo.
(2) Mtumishi wa Umma -
(a) hatafungua au kuendesha akaunti ya benki nje ya
Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kwa namna
ambayo sheria za nchi zinaruhusu; na
(b) hataomba au kupokea mkopo au faida yoyote kwa
namna au mazingira ambayo yanashusha hadhi au
heshima ya mtumishi wa umma.




16.-(1) Kiongozi wa Umma atalazimika kutangaza, ndani ya
siku thelathini baada ya kupata uongozi na baada ya kuacha uongozi,
mali na thamani zake na madeni yake katika Tume ya Maadili na
Uwajibikaji.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), Kiongozi
wa Umma atalazimika kutangaza mali zake na madeni:
(a) yake binafsi;
(b) ya mwenza wake wa ndoa; na
(c) watoto wake walio chini ya umri wa miaka kumi na nane,
mara moja kila mwaka, au kadri itakavyoamuliwa na sheria.



shughuli yoyote ambayo ana maslahi nayo yeye binafsi, mwenza
wake, mtoto wake, jamaa yake, rafiki au mtu yeyote wake wa karibu.
(2) Kiongozi wa umma hatozungumzia kitu chochote katika
Baraza la Mawaziri, Bunge, kamati au chombo kingine chochote
rasmi ambacho ana maslahi nacho ya moja kwa moja au vinginevyo,
isipokuwa tu kama atatoa taarifa ya mgongano huo wa maslahi katika
vyombo hivyo.
(3) Itakuwa ni marufuku kwa Kiongozi yeyote wa Umma,
kushiriki kuongeza au kwa namna yoyote ile, kuboresha maslahi
yanayohusu wadhifa alionao, na endapo atashiriki, basi masharti hayo
mapya yataanza kutumika kwa Kiongozi atakayekuja baada ya yeye
kuondoka au kumaliza muda wa kukaa madarakani.
(4) Bunge litatunga sheria itakayosimamia, pamoja na mambo
mengine, masuala ya:
(a) ngazi au orodha ya Viongozi wa Umma, wanaopaswa
kutangaza mali zao;
(b) utaratibu wa utwaaji wa mali za Viongozi wa Umma
zilizopatikana kwa njia za ukiukaji wa sheria;
(c) utaratibu wa kumwajibisha Kiongozi wa Umma aliyeenda
kinyume na maadili na Miiko ya Uongozi;
(d) uanzishaji wa mitaala inayohusu maadili na uraia,
mashuleni na vyuoni; na
(e) uanzishaji wa mitaala inayohusu Katiba mashuleni na
vyuoni.
(5) Kiongozi wa Umma hataruhusiwa kushika nyadhifa mbili
au zaidi au kutumikia Mihimili ya Dola zaidi ya mmoja kwa wakati
mmoja.
 
Nimeipenda sana. Kuna baadhi ya vipengele vimenikosha zaidi.

Hebu cheki:

15.-(1) Zawadi au kitu chochote kitakachotolewa kwa
mtumishi wa umma katika shughuli za kiserikali ni zawadi kwa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na itawasilishwa kwa Katibu
Mkuu Kiongozi kupitia kwa Katibu Mkuu wa Wizara au taasisi ya
Serikali inayohusika, akiainisha:
(a) aina ya zawadi;
(b) thamani ya zawadi;
(c) sababu ya kupewa zawadi; na
(d) mtu au mamlaka iliyotoa zawadi hiyo.
(2) Mtumishi wa Umma -
(a) hatafungua au kuendesha akaunti ya benki nje ya
Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kwa namna
ambayo sheria za nchi zinaruhusu; na
(b) hataomba au kupokea mkopo au faida yoyote kwa
namna au mazingira ambayo yanashusha hadhi au
heshima ya mtumishi wa umma.




16.-(1) Kiongozi wa Umma atalazimika kutangaza, ndani ya
siku thelathini baada ya kupata uongozi na baada ya kuacha uongozi,
mali na thamani zake na madeni yake katika Tume ya Maadili na
Uwajibikaji.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), Kiongozi
wa Umma atalazimika kutangaza mali zake na madeni:
(a) yake binafsi;
(b) ya mwenza wake wa ndoa; na
(c) watoto wake walio chini ya umri wa miaka kumi na nane,
mara moja kila mwaka, au kadri itakavyoamuliwa na sheria.



shughuli yoyote ambayo ana maslahi nayo yeye binafsi, mwenza
wake, mtoto wake, jamaa yake, rafiki au mtu yeyote wake wa karibu.
(2) Kiongozi wa umma hatozungumzia kitu chochote katika
Baraza la Mawaziri, Bunge, kamati au chombo kingine chochote
rasmi ambacho ana maslahi nacho ya moja kwa moja au vinginevyo,
isipokuwa tu kama atatoa taarifa ya mgongano huo wa maslahi katika
vyombo hivyo.
(3) Itakuwa ni marufuku kwa Kiongozi yeyote wa Umma,
kushiriki kuongeza au kwa namna yoyote ile, kuboresha maslahi
yanayohusu wadhifa alionao, na endapo atashiriki, basi masharti hayo
mapya yataanza kutumika kwa Kiongozi atakayekuja baada ya yeye
kuondoka au kumaliza muda wa kukaa madarakani.
(4) Bunge litatunga sheria itakayosimamia, pamoja na mambo
mengine, masuala ya:
(a) ngazi au orodha ya Viongozi wa Umma, wanaopaswa
kutangaza mali zao;
(b) utaratibu wa utwaaji wa mali za Viongozi wa Umma
zilizopatikana kwa njia za ukiukaji wa sheria;
(c) utaratibu wa kumwajibisha Kiongozi wa Umma aliyeenda
kinyume na maadili na Miiko ya Uongozi;
(d) uanzishaji wa mitaala inayohusu maadili na uraia,
mashuleni na vyuoni; na
(e) uanzishaji wa mitaala inayohusu Katiba mashuleni na
vyuoni.
(5) Kiongozi wa Umma hataruhusiwa kushika nyadhifa mbili
au zaidi au kutumikia Mihimili ya Dola zaidi ya mmoja kwa wakati
mmoja.

Mbona kipengele cha 5 kinazungumzia madaraka kwenye mihimili ya dola tu? Wangeongeza na kwenye mashirika na taasisi za umma. Naomba uangalie vizuri labda umemisquote.
 
Back
Top Bottom