Katiba ifanyiwe marekebisho, marais wastaafu waruhusiwe kugombea tena

kitalembwa

JF-Expert Member
Jul 12, 2014
2,859
7,123
Wana bodi salaam,

Katiba yetu sio Msahafu/Biblia, nikiwa na maana muda wowote inaweza fanyiwa marekebisho pale inapohitajika kwa maslahi ya taifa yenye tija. Hili tumekuwa tukiliona likitokea kwani kufikia sasa katiba yetu imeshafanyiwa marekebisho mara kadhaa, pia nadhani hili linaweza kuendelea.

Naam, ninaona kuna haja ya kurekebisha katiba yetu, ili maraisi wastaafu waruhusiwe kugombea tena nafasi hiyo, pale watakapohisi wanaweza kufanya hivo, baada ya wao kujitosa kwenye kinyang'anyiro sisi wananchi ndio tutawapima kama tunaweza kuwaamini na kuwapa tena mamlaka ya kuliongoza taifa letu ama la.

Kwa hapa kwetu tunao maraisi wastaafu watatu ambao ni Mzee Mwinyi A.H, Mzee Mkapa B.W, na Mzee Kikwete J.K. kwa uhalisia Mzee Mwinyi amezeeka kwa umri wake (miaka 90 na kuendelea), lakini kwa hawa wawili bado nguvu zipo, zaidi kwa JK bado anaonekana anaweza kabisa kuongoza zipo.

Hakika ingependeza tena tungemuona JK kwenye harakati za kuwania tena hii nafasi, sio kwamba ni mkamilifu sana au kwenye uongozi wake hakuwa na dosari, ila dosari za awamu ya tano zimezidi kuvuka mipaka.
Enzi za JK;

-Wafanyakazi waliboreshewa maslahi, walipanda madaraja kwa wakati na kupata stahiki zao

-Demokrasia ilikuwepo ya kweli, hivi kwa ungozi huu wa JPM , kina slaa wangepata mwanya wa kuandaa mkutano wa kisiasa nchi nzima, sijui mambo ya kushukuru wanachi kwa kuwapigia kura ? mambo ya list of shame mnazi mmoja ? wangekaripiwa kwa makatazo, na wangeishia kuswekwa jela kwa kesi za uchochezi, lakini JK hakuwa anahaingaika nao, anawaacha wanatoa ya moyoni maisha yanaendelea.

-Mishahara ilikuwa inatoka kwa wakati, longolongo hazikuwepo

-Ajira zilikuwepo, japo hapa naomba nikiri kwamba aliweza kuajiri kwa kiasi chache kulingana na uhitaji na bajeti. Nikiri tatizo la ajira limekuwa sugu hata huko nchi za watu japo tatizo sio kubwa kama nchi za ulimwengu wa tatu mfano Tanzania. Hata USA, England, Germany na kwingineko hili tatizo lipo lakini huwezi kulinganisha na bongo.

-Uhuru wa habari ulikuwepo.

-Alijitahidi kujenga mahusiano mazuri na wapinzani, kuwaita kukaa nao pamoja na kujadili baadhi ya mambo yenye maslahi kwa nchi. Mara ngapi kina ZZK, Mbowe, Slaa, Lipumba wameenda ikulu na kunywa chai na mheshimiwa JK huku wakijadili mambo ya taifa letu ? vipi kwa huyu wa sasa ?

-Walau uchumi ulikuwa wastani, mambo yalikuwa yanaenda sio kama sasa, pesa ilikuwepo kwenye mzunguko. kwa kipindi hiki mambo yamebadilika sana.

-Miradi ya maendeleo ilikuwepo na ilifanyika vizuri kabisa, mifano mnayo.

Kwa kifupi hayo niliyoorodhesha hapo na mengine mengi ni baadhi ya mazuri ya JK, nchi ilikuwa na usawa, kila mtu alikula kwa namna yake, haki za binadamu zilizingatiwa n.k

Kwa nini katiba isirekebishwe hiki kipengele cha wastaafu waruhusiwe kugombea tena kikawekwa? hakika JK akijitosa tena atashinda kwa kishindo kikubwa sana.

Huyu mzee wetu ni mwanasiasa haswa, master mind, anajua afanye nini kwa wakati gani, hakurupuki na anapokea ushauri, kwa kifupi yupo smart sana na maamuzi anayoyafanya.
 
Hakika ingependeza tena tungemuona JK kwenye harakati za kuwania tena hii nafasi, sio kwamba ni mkamilifu sana au kwenye uongozi wake hakuwa na dosari, ila dosari za awamu ya tano zimezidi kuvuka mipaka.
Enzi za JK;
upload_2018-3-14_12-20-2.png
upload_2018-3-14_12-20-38.png
 
Mawazo ya aliyekufa hayo! Unatamani kuongozwa na Mkapa na Kikwete ili walete jambo gani? Anapoambaiwa imetosha maana yake siyo kwamba amezeeka, NO! Tafsiri yake ni kwamba hana jipya kichwani!

Wewe unamtamani MKapa kwa lipi? Kikwete kwa lipi? Ushoga na urafiki uishie nje ya mfumo wa serikali, bhana!
 
Mawazo ya aliyekufa hayo! Unatamani kuongozwa na Mkapa na Kikwete ili walete jambo gani? Anapoambaiwa imetosha maana yake siyo kwamba amezeeka, NO! Tafsiri yake ni kwamba hana jipya kichwani!

Wewe unamtamani MKapa kwa lipi? Kikwete kwa lipi? Ushoga na urafiki uishie nje ya mfumo wa serikali, bhana!
huyo unaedhani yupo ama anafaa ana masilahi gani kwako kama raia na taifa kwa ujumla ? uchumi unaserereka tu kila siku, kazi kupika data, imeishia kuwa serikali ya matamko, mabank yanafunga kwa kushindwa kujiendesha, uhuru wa maoni kuminywa, demokrasia ya maandishi lakini kivitendo sio, watu kutekwa, kuuwawa, kupigwa risasi ndicho unachokitaka ?
what a shame.
 
huyo unaedhani yupo ama anafaa ana masilahi gani kwako kama raia na taifa kwa ujumla ? uchumi unaserereka tu kila siku, kazi kupika data, imeishia kuwa serikali ya matamko, mabank yanafunga kwa kushindwa kujiendesha, uhuru wa maoni kuminywa, demokrasia ya maandishi lakini kivitendo sio, watu kutekwa, kuuwawa, kupigwa risasi ndicho unachokitaka ?
what a shame.
Mwenzako anaweka jiwe LA msingi UJENZI wa SGR we umekaa humu kumponda ,piga kazi jpm wenye roho kubwa wajinyonge
 
Wana bodi salaam,

Katiba yetu sio Msahafu/Biblia, nikiwa na maana muda wowote inaweza fanyiwa marekebisho pale inapohitajika kwa maslahi ya taifa yenye tija. Hili tumekuwa tukiliona likitokea kwani kufikia sasa katiba yetu imeshafanyiwa marekebisho mara kadhaa, pia nadhani hili linaweza kuendelea.

Naam, ninaona kuna haja ya kurekebisha katiba yetu, ili maraisi wastaafu waruhusiwe kugombea tena nafasi hiyo, pale watakapohisi wanaweza kufanya hivo, baada ya wao kujitosa kwenye kinyang'anyiro sisi wananchi ndio tutawapima kama tunaweza kuwaamini na kuwapa tena mamlaka ya kuliongoza taifa letu ama la.

Kwa hapa kwetu tunao maraisi wastaafu watatu ambao ni Mzee Mwinyi A.H, Mzee Mkapa B.W, na Mzee Kikwete J.K. kwa uhalisia Mzee Mwinyi amezeeka kwa umri wake (miaka 90 na kuendelea), lakini kwa hawa wawili bado nguvu zipo, zaidi kwa JK bado anaonekana anaweza kabisa kuongoza zipo.

Hakika ingependeza tena tungemuona JK kwenye harakati za kuwania tena hii nafasi, sio kwamba ni mkamilifu sana au kwenye uongozi wake hakuwa na dosari, ila dosari za awamu ya tano zimezidi kuvuka mipaka.
Enzi za JK;

-Wafanyakazi waliboreshewa maslahi, walipanda madaraja kwa wakati na kupata stahiki zao

-Demokrasia ilikuwepo ya kweli, hivi kwa ungozi huu wa JPM , kina slaa wangepata mwanya wa kuandaa mkutano wa kisiasa nchi nzima, sijui mambo ya kushukuru wanachi kwa kuwapigia kura ? mambo ya list of shame mnazi mmoja ? wangekaripiwa kwa makatazo, na wangeishia kuswekwa jela kwa kesi za uchochezi, lakini JK hakuwa anahaingaika nao, anawaacha wanatoa ya moyoni maisha yanaendelea.

-Mishahara ilikuwa inatoka kwa wakati, longolongo hazikuwepo

-Ajira zilikuwepo, japo hapa naomba nikiri kwamba aliweza kuajiri kwa kiasi chache kulingana na uhitaji na bajeti. Nikiri tatizo la ajira limekuwa sugu hata huko nchi za watu japo tatizo sio kubwa kama nchi za ulimwengu wa tatu mfano Tanzania. Hata USA, England, Germany na kwingineko hili tatizo lipo lakini huwezi kulinganisha na bongo.

-Uhuru wa habari ulikuwepo.

-Alijitahidi kujenga mahusiano mazuri na wapinzani, kuwaita kukaa nao pamoja na kujadili baadhi ya mambo yenye maslahi kwa nchi. Mara ngapi kina ZZK, Mbowe, Slaa, Lipumba wameenda ikulu na kunywa chai na mheshimiwa JK huku wakijadili mambo ya taifa letu ? vipi kwa huyu wa sasa ?

-Walau uchumi ulikuwa wastani, mambo yalikuwa yanaenda sio kama sasa, pesa ilikuwepo kwenye mzunguko. kwa kipindi hiki mambo yamebadilika sana.

-Miradi ya maendeleo ilikuwepo na ilifanyika vizuri kabisa, mifano mnayo.

Kwa kifupi hayo niliyoorodhesha hapo na mengine mengi ni baadhi ya mazuri ya JK, nchi ilikuwa na usawa, kila mtu alikula kwa namna yake, haki za binadamu zilizingatiwa n.k

Kwa nini katiba isirekebishwe hiki kipengele cha wastaafu waruhusiwe kugombea tena kikawekwa? hakika JK akijitosa tena atashinda kwa kishindo kikubwa sana.

Huyu mzee wetu ni mwanasiasa haswa, master mind, anajua afanye nini kwa wakati gani, hakurupuki na anapokea ushauri, kwa kifupi yupo smart sana na maamuzi anayoyafanya.
Akili za akina Abdul Nondo izi
 
Mtu akimaliza muda wake "aachwe apumzike" huku akilea wajukuu zake na akila pension yake taratibu. Ni matusi kuhisi kwamba katika kundi la watanzania watu wazima zaidi ya million 25, hakuna mtu bora zaidi ya Rais aliyepita.
 
Kwa sasa unamuona JPM kama hafai. Muda ukifika akaachia mwingine, utaona heri ya JPM. Kwani enzi za Kikwete, si wengi tu walikuwa wanamponda, ila siku hizi kawa kama malaika asiye na doa.
 
Ukiona Rais akingia madarakani akawa anapendwa na kusifiwa kwa mapambio, hujuwe huyo sio Rais wa maamuzi magumu.
 
Ila sisi watanzania NI WANAFKI.....naamini tunaweza kushika namba moja DUNIANI
Yaani. Bora wamuache Mzee apumzike tu. Alikuwa na madhaifu yake lakini hata kwa Yale mazuri aliyofanya alidhihakiwa. Hata huyu kipindi chake kitapita.
 
Kwani hatupo tunaoweza kuongoza hii nchi hadi ulete maraisi wastaafu? tatizo lako kuna 'kitu umekichoka' sasa una -compare na waliopita ILA bado tupo hazina kubwa sana ya watu wenye weledi, hekima na busara ktk kuongoza ondoa wasiwasi.
 
Back
Top Bottom