Kati ya Tajiri na Maskini ni nani mwenye stress nyingi?

Mwanga Lutila

JF-Expert Member
Nov 10, 2016
3,804
12,239
Kila mtu ana msongo wa mawazo ila kunakuzidiana, Sasa kati ya mwenye mimali(tajiri like Dangote, Mo, ) na Asiye Mali (Maskini like Mimi hapa) ni na mwenye wingi wa stres?
 
Kila mtu ana msongo wa mawazo ila kunakuzidiana, Sasa kati ya mwenye mimali(tajiri like Dangote, Mo, ) na Asiye Mali (Maskini like Mimi hapa) ni na mwenye wingi wa stres?
Mkuu Kwa kiwango cha ulinganifu ulichokiweka kati yako na hao ma bilionea napata stres kukupa jibu sahihi.
 
Stress itakuja kutegemea na tatizo stress za Mo zitakuja pale atakapogungiwa leseni yake yake ya kufanya biashara au kupata tatizo lolote baya kwrnye biashara ( Mungu amuhifadhi) ila stress zako ww zitkuja ushajenga banda lako la kujifichia mvua na jua kwa shida na kukopa na madeni kibao halfu linakuja bordoza linavunja then unaambiwa hulipwi hapa kunajengwa barabara
 
Maskini hana cha kupoteza ila ana vya kutafuta... akikosa stress huanzia hapo...

Tajiri anavyovyakupoteza kwa hiyo inabidi atafute zaidi ili asipoteze... stress huanzia hapo...


cc: mahondaw
 
Stress huletwa na majukumu kama madeni na matatizo kama maradhi.

Unaweza kukuta Mtu ni masikini lakini Hana majukumu makubwa.

Hivyo hakuna anayemshinda mwenzake
 
Wewe ni tajiri au maskini?? Jitambue kwanza ww ndio uje na hizi stori
 
Kila mtu ana msongo wa mawazo ila kunakuzidiana, Sasa kati ya mwenye mimali(tajiri like Dangote, Mo, ) na Asiye Mali (Maskini like Mimi hapa) ni na mwenye wingi wa stres?
Maskini wengi wana shida tu, stress mara chache, matajiri karibu wote wana stress karibu muda wote.
 
Labda ujiulize kwanza kilio ndani ya v8,range au benzi na kilio kwenye daladala kipi ni kilio nafuu.brother asikudanganye mtu,ni bora Mara Mia kuwa na stress ukiwa Tajiri kuliko umasikini. amini amini nakuambia umasikini sio kitu kizuri.
 
wote wanaweza kuwa na stress ila tajiri ana wigo mpana wakuziondoa hizo stress , mfano kwenda vacation paris,
au akiingia cassino strss zishaisha hapo
 
Umasikini sio mzuri aisee. Stress za maskini ni kubwa kuliko za tajiri. Tajiri hata pesa zikipungua anaweza kupata mtu wa kumkopesha akijua ana weledi wa kuzalisha amrudishie. Wewe maskini nani atakuamini akukopeshe ilhali hata baiskeli huna?

Hata Biblia Takatifu inasema:- Maskini huchukiwa hata na jirani yake; Bali tajiri ana rafiki wengi. (Mithali 14:20)
 
mwenye stress ni yule mwenye stress haijalishi tajiri au masikini


nielewe nikuelewe
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom