Kati ya Spika Ndugai, Balile na Gavana Luoga nani mkweli kuhusu deni la taifa?

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,215
3,587
Kuna mkanganyiko mkubwa nchini katika utoaji taarifa za deni la taifa. Kuna usemi kuwa miluzi mingi huchanganya mwelekeo wa Mbwa.

Ndugai ni Spika, Balile ni Mwandishi wa Habari za Uchunguzi, Luoga ni Gavana, sasa nani ana taarifa sahihi za kutufanya tumuamini?

Ndugai amesema deni la taifa ni 70 tr, Balile (Gazeti la Jamhuri October 26, 2021) alisema ni 78 tr, Luoga anasema liko 27.9% halijafikia hata nusu ya kiwango cha kukopa.

Lipumba naye huenda akaibuka na takwimu zake, Mbatia naye anajifua kufanya uchunguzi ili aje Ki-NCCR, Tundu naye ataibuka kivyake. Baghosha!

Kwa mkanganyiko huu kama hauna sababu za kisiasa basi huenda mtu akatamani enzi ya Magufuli ya kudhibiti utoaji takwimu, kwa sababu kama nchi, tunatia aibu duniani, tunajipaka matope wenyewe, tunaonekana hatuna mifumo mizuri ya kitakwimu, utoaji taarifa nyeti, wala kumbukumbu sahihi za deni la taifa.

Hivi unawezaje kumlipa mdeni wako kama hujui kiasi sahihi anachokudai?

Magufuli alisema kazi ya urais ni ngumu, Nyerere alisema Ikulu ni mzigo, JK alisema Ikulu ni sawa na kulalia kitanda chenye kunguni wengi.

Kwa upande wa Ndugai, nadhani kauli yake imethibitisha kwamba ameamua kufanyakazi ya Msemaji Rasmi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (simjui ni nani).


Msome Balile hapa:
Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78 | JamiiForums


Msome Ndugai hapa:
Rais Samia 'ampiga' Spika Ndugai | JamiiForums


Gavana yeye alitoa ufafanuzi wake jana Jumatano Disemba 29, 2021 kwenye kipindi cha Power Breakfast kinachoendeshwa na Redio ya Clouds FM. (nimetafuta clip nimeikosa).

1640855100447.png


1640855257444.png


1640855419280.png

Taswira zote kwa hisani ya google.
 
Kwa upeo wako mdogo unadhani kwanini mwenye dhamana amepokwa majukumu yake wakajitokeza wenye dhamana wengi?
Hajapokwa

Mavuvuzela wanadandia agenda

Ni kama wewe ulivyoleta ujinga hapa unataka clarifications while the system in protocols zake za kutoa taarifa

Man up dogo
 
Hajapokwa

Mavuvuzela wanadandia agenda

Ni kama wewe ulivyoleta ujinga hapa unataka clarifications while the system in protocols zake za kutoa taarifa

Man up dogo
Mkuu wa system aliyeondoka alituambia miradi tunajenga kwa pesa zetu za ndani wenyewe kumbe uongo mtupu.
 
Hajapokwa

Mavuvuzela wanadandia agenda

Ni kama wewe ulivyoleta ujinga hapa unataka clarifications while the system in protocols zake za kutoa taarifa

Man up dogo
Hiyo system imeflop kama ubongo wako ulivyoflop usijuwe kwamba "No question is stupid but the answer"
 
Wote wapo sahihi katokana na takwimu walivyoziweka. Mmoja amongelea deni la ndani na nje combined 78tr. Mwingine kazungumzia deni la nje tu 70+tr. Na mwingine kazungumzia denied la nje kwa kulinganisha na pato la taifa (GDP).
 
Tunataka Noah zetu! Walisikika wanyonge baada ya mwenyekiti wa ukoo kuuliza Kama Kuna mtu anamdai marehemu!
 
Kwani ukikopa benki milioni 10 inakua yako au ya benki?
Jaribu kukopa hizo milioni 10 weka kibanda chako dhamana halafu usizilipe, ukifanya hivyo uje kutuletea majibu kama zilikuwa zako au za benki.
 
Nchi inaongozwa na makundi ya wahalifu, kila kundi lina kikundi Chao cha watu waongo, wana propaganda, wanajaza matumbo yao
Navyoona Nchi yote imeshauzwa, maeneo yote yenye maliasili na utajiri CCM wamesha ya uza kwa Mabepari. Nchi inendeshwa kwa makusanyo ya kodi ndogo ndogo pamoja na TOZO ili kulipa mishahara, posho na gharama za kuwatunza watawala. Shuguli za maendeleo kama ujenzi wa madarasa, vyoo na zahanati tunaenda kukopa au tusubiri wafadhili.
 
Balile alikuwa yupo sahihi lakinj deni la nje sio trillion 78, Bali hiyo ni jumla na ya Deni la ndani.
Na pia Sasa hivi Deni ni trillion 82
Pia Magufuli aliacha Deni likiwa trillion 71
Source ya Balile ni wapi?

Na kwnn watanzania tunang'ang'ana na mada hiihii?

Raisi ameshafunga mjadala wa deni la taifa kwamba ni LAZIMA serikali ikope kumalizia miradi yote iliyoanzishwa ili iishe haraka bila kuumiza wananchi..

Rais anasema; mikopo hiyo inahimilika na italipwa kdgkdgo hadi miaka 20.

Hata deni lifike trilion 200 poa tu, as far as nitaona:
mgawo wa umeme umekuwa historia,
huku Reli ya umeme imeanza, pembeni mabarabara ya njia nane, maji safi kila kijiji...Hii ni mifano tu.

Kwani hata huko nyuma wakati deni la taifa lilipokuwa under 50 trilion..tulifaidi nini kikubwa cha kuonekana..

Sanasana tuliambiwa deni limefika kiasi hiki, saa nyngne bila kuona chochote kama kumbukumbu.
 
Bottomline is tunadaiwa tena fedha nyingi pasipo na sababu za msingi.

Kama tusingekuwa na Rasilimali ingekua sahihi ,

Tunakopa ili kufurahisha taasisi za mabeberu ambayo hayataki tuwe na uwezo wa kujitegemea.
 
Jaribu kukopa hizo milioni 10 weka kibanda chako dhamana halafu usizilipe, ukifanya hivyo uje kutuletea majibu kama zilikuwa zako au za benki.
Usipolipa lazima wakunyooshe

But pale unapokopa zinakua zako for the period ya loan and you pay Kwa systematic agreement
 
Bottomline is tunadaiwa tena fedha nyingi pasipo na sababu za msingi.

Kama tusingekuwa na Rasilimali ingekua sahihi ,

Tunakopa ili kufurahisha taasisi za mabeberu ambayo hayataki tuwe na uwezo wa kujitegemea.
Nini suluhisho?

Nini kifanyike?

Ova
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom