msumeno
JF-Expert Member
- Aug 3, 2009
- 2,827
- 1,729
Habari wakuu?. Hope tunajiandaa vema na sikukuu ya pasaka pia hongereni kwa mapumziko mareeeefu!.
OK nirudi kwenye kitu kilichonileta hapa kwenu nyie wadau na wataalam wa fani mbalimbali mliopo humu ndo maana hakuna kinachoshindikana ndani ya Jamiiforums. Naombeeni kujuzwa kati ya songea na Singida ni mkoa upi mzuri kwa mtu anaetaka kuishi na kujishuhurisha na UFUGAJI na KILIMO!?.
Hapa tutaangalia na gharama za maisha na huduma za kijamii pia.
KUMBUKA nipo tayar kuishi hata kijijini sana ili mradi nifanikishe lengo langu la kutoka kiuchumi kupitia ufugaji hasa wa UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI .
Asanteni sana na poleni kwa kuwatoa kwenye mada zetu za siasa
Mkuu Kilimo Singida hapana, mvua za kule shida, while Songea inaweza kua nzuri kwa vyote though ni mbali na soko ( DAR) ila kama mshabiki wa Yanga Singida sio pazuri sana ( last point ni jok)