Kati ya Songea na Singida ni mkoa upi mzuri kwa mtu anaetaka kuishi na kujishuhurisha na ufugaji na kilimo?

Habari wakuu?. Hope tunajiandaa vema na sikukuu ya pasaka pia hongereni kwa mapumziko mareeeefu!.

OK nirudi kwenye kitu kilichonileta hapa kwenu nyie wadau na wataalam wa fani mbalimbali mliopo humu ndo maana hakuna kinachoshindikana ndani ya Jamiiforums. Naombeeni kujuzwa kati ya songea na Singida ni mkoa upi mzuri kwa mtu anaetaka kuishi na kujishuhurisha na UFUGAJI na KILIMO!?.

Hapa tutaangalia na gharama za maisha na huduma za kijamii pia.
KUMBUKA nipo tayar kuishi hata kijijini sana ili mradi nifanikishe lengo langu la kutoka kiuchumi kupitia ufugaji hasa wa UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI .

Asanteni sana na poleni kwa kuwatoa kwenye mada zetu za siasa

Mkuu Kilimo Singida hapana, mvua za kule shida, while Songea inaweza kua nzuri kwa vyote though ni mbali na soko ( DAR) ila kama mshabiki wa Yanga Singida sio pazuri sana ( last point ni jok)
 
Samahani Mkuu nimezaliwa Dar japo huko Mtwara ni Nyumbani kwa upande wa ' Bidashi ' wangu ( Mum ) pamoja na Lindi ila sijawahi ' Kukanyaga ' kabisa Mtwara isipokuwa Lindi hasa ' Nachingwea ' niliwahi kwenda mwaka 1988 kama siyo 1989. Mkoa ambao nimeenda na naenda sana ni wa Mara ( Musoma ) ambako ndiko ' Mshua ' wangu ( Dingi ) anatokea. Na naenda sana Mara ( Musoma ) kwasababu ya Samaki wengi na naogopa kwenda Mtwara kwakuwa Panya ni wengi halafu wametukuka. Narudia tena kukuomba usipoteze kabisa muda wako kwenda sijui Ruvuma au Singida huko hakuna Kitu halafu Watu wa huko ni ' Washamba / Mambwigira ' sana.
duuuh unapotosha watu boss... Hivi mtwara kuna nini
 
Mara mia uende singida coz iko jirani na miji mikubwa ya soko kama Dar Arusha,mwanza na Dom,,pili ni transit,,Ruvuma hata ulime au ufuge hakuna soko,dar iko mbali,pili miundombinu ya barabara na umeme ni shida ,mwisho iko kanda ya kilimo hakuna mzunguko wa pesa,
Last hata ukilinganisha maendeleo na ukuaji wa miji hii Singida iko mbele ya Dar
Ruvuma mbona panafikika kiurahisi kila siku Fuso zinapishana usiku na barabara ni nzuri kabisa tena nadhani wao kwa upande wa miundombinu walianza kitambo kuw na lami hivyo hata issue ya usafirishaji wa bidhaa wapo vizuri (FUSO kila siku usiku zinapishana)
 
Mkuu Kilimo Singida hapana, mvua za kule shida, while Songea inaweza kua nzuri kwa vyote though ni mbali na soko ( DAR) ila kama mshabiki wa Yanga Singida sio pazuri sana ( last point ni jok)
Njoo na alizeti kama upo Singida mkuu najua utapata lifta
 
Hauni kwamba sehemu ambayo kuku wapatikana kwa bei juu ndyo ina opportunity kubwa katika ufugaji wa wa kuku... ??! Kafugie kuku songea utapiga mpunga
Ndugu yangu nilichogundua humu watu wengi wanaongea kwa kutumia uzoefu wa kwenye keyboard. Ukimuuliza kwanini unashauri akafugie Singida sjuwi atakujibu kule wafugaji wa kuku wa kienyeji ni wengi, then wakiwa wengi wewe ina faida gani kwako?!
 
Singida ni jangwa, hakunafursa yoyote, am nimesahaukitu Ukitaka kuliwazwa kisawasa nenda singida. wanawake wa kisingida apana mchezo Tanga inasubiria.
 
Asante sana mkuu,umenipa kitu kipya hivyo kama hutojar naomba unisaidie haya kwa mkoa wa Mtwara!
1. Wilaya ipi nzur kwa UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI. Unaweza kushaur hata kijiji kipi nianzie kwenda kuangalia
2. Kijiji hicho hali ya usafir mpaka mjin ipoje?

Asante
mkuu kwenye mtwara naunga mkono hasa ukizingatia una taka kufuga kuku..mkoa wa mtwara wilaya ya masasi biashara ya kuku wa kienyeji na mayai yake ni dili sana mkuu.kuna kipindi kuku anafika 30 elfu mmoja..mayai ya kienyeji ni buku moja yakishuka sana ni 700
OK ni vizuri pia...
 
  • Thanks
Reactions: rr3
Samahani Mkuu nimezaliwa Dar japo huko Mtwara ni Nyumbani kwa upande wa ' Bidashi ' wangu ( Mum ) pamoja na Lindi ila sijawahi ' Kukanyaga ' kabisa Mtwara isipokuwa Lindi hasa ' Nachingwea ' niliwahi kwenda mwaka 1988 kama siyo 1989. Mkoa ambao nimeenda na naenda sana ni wa Mara ( Musoma ) ambako ndiko ' Mshua ' wangu ( Dingi ) anatokea. Na naenda sana Mara ( Musoma ) kwasababu ya Samaki wengi na naogopa kwenda Mtwara kwakuwa Panya ni wengi halafu wametukuka. Narudia tena kukuomba usipoteze kabisa muda wako kwenda sijui Ruvuma au Singida huko hakuna Kitu halafu Watu wa huko ni ' Washamba / Mambwigira ' sana.
usiongee kishabiki ukawapotosha watu wasiojua jografia ya MUSOMA. Kwanza upatikanaji wa ardhi utaipata wapi? ardhi kule kama Kilimanjaro na Kagera ambapo inamilikiwa kiukoo kuuza ni marufuku. La pili kuna usalama gani? utalima gunia mbili tu za maindi MKURYA (baba zako wadogo) wanakuja usiku kukucharanga na mapanga mwili mzima au kukutifuatifua na bunduki wanabeba kila kitu mpaka panya. Musoma hapafaiiiiii!!! kwa uwekezaji wenyeji wa kule wakifanikiwa kuiba mgodini huko hawawekezi kwao wanakwenda kujenga Mwanza sembuse mgeni!!! ma woya!!!!???
 
Lazima ujue aina ya mazao unayotaka kuwekeza na pia ujue aina ya mifugo pia.
Hali ya hewa mfano ukame.
Hali ya chakula kwa ujumla,usiende kufanya uwekezaji mikoa ambayo gharama za chakula ziko juu sahau kutoka.
Usafiri na usafirishaji gharama zake.
Masoko kwa ujumla.
Japo mikoa yote sijaishi naona ungeenda ruvuma huko kuna previlage.
Singida kwa ufugaji na kilimo ni afadhari maana kuna uhakika wa kuuza unachokizalisha usafiri ni wa uhakika tofauti na Ruvuma ambako mtu anavuna gunia 50 za mahindi na anaendelea kuwa masikini asiyejiweza.
 
Asante sana mkuu!. Watoto wazur hapana boss nazisaka kwanza pesa
Singida ni pazuri na kuna usafiri wa uhakika nenda manyoni au itigi kuna fursa nyingi kilimo cha Alzeti, choroko, Ufuta Dengu mahindi Ngano Soya niwewe kuamua.
 
usiongee kishabiki ukawapotosha watu wasiojua jografia ya MUSOMA. Kwanza upatikanaji wa ardhi utaipata wapi? ardhi kule kama Kilimanjaro na Kagera ambapo inamilikiwa kiukoo kuuza ni marufuku. La pili kuna usalama gani? utalima gunia mbili tu za maindi MKURYA (baba zako wadogo) wanakuja usiku kukucharanga na mapanga mwili mzima au kukutifuatifua na bunduki wanabeba kila kitu mpaka panya. Musoma hapafaiiiiii!!! kwa uwekezaji wenyeji wa kule wakifanikiwa kuiba mgodini huko hawawekezi kwao wanakwenda kujenga Mwanza sembuse mgeni!!! ma woya!!!!???
Bora hata Mtwara huko Msoma hakufai kabisa mijamaa mikatili sana
 
Ruvuma mbona panafikika kiurahisi kila siku Fuso zinapishana usiku na barabara ni nzuri kabisa tena nadhani wao kwa upande wa miundombinu walianza kitambo kuw na lami hivyo hata issue ya usafirishaji wa bidhaa wapo vizuri (FUSO kila siku usiku zinapishana)


Samahani Mkuu nimezaliwa Dar japo huko Mtwara ni Nyumbani kwa upande wa ' Bidashi ' wangu ( Mum ) pamoja na Lindi ila sijawahi ' Kukanyaga ' kabisa Mtwara isipokuwa Lindi hasa ' Nachingwea ' niliwahi kwenda mwaka 1988 kama siyo 1989. Mkoa ambao nimeenda na naenda sana ni wa Mara ( Musoma ) ambako ndiko ' Mshua ' wangu ( Dingi ) anatokea. Na naenda sana Mara ( Musoma ) kwasababu ya Samaki wengi na naogopa kwenda Mtwara kwakuwa Panya ni wengi halafu wametukuka. Narudia tena kukuomba usipoteze kabisa muda wako kwenda sijui Ruvuma au Singida huko hakuna Kitu halafu Watu wa huko ni ' Washamba / Mambwigira ' sana.
Hahahahaa, safi mkuu. Mara ya kwanza kabisa kwenda mkoa wa ruvuma aliniita jamaa yangu mmoja Mkinga (very successfull) wa kutokea njombe kwa sababu ya kazi moja maalum, nilipofika nikakutana na wazee wengine wawili ambao nafahamiana nao vizuri sana kupitia kwa mzee wangu, wote waliwahi kufanya kazi na mzee wangu huko serikalini na walikuwa kama family friends (angalizo; sijawahi kufanya kazi serikalini, wala kazi ya kuajiriwa popote), hao wote siyo kwao mkuo huo...lakini wamezamia. Kukatisha story ni kwamba, baada ya kumaliza tu project ile ilonipeleka nilijikuta nina ekari zaidi ya miambili za mashamba, yule jamaa akawa ananitania "tayaaari", kila mara ananiambia "tayariii", nikikutana na wazee wangu nao "tayaariii". Nikuibie siri, sehem yoyote ambayo watu wamelala fofofo kuna oportunities nyingi sana kwa wajanja, sehem zooote zenye migogoro wajanja ndiyo hupatia pesa. Ingia kariakoo, wakinga wooote wamechukua mitaji huko unakosema watu wasiende. Haya ni mawazo tu mkuu, huenda yasikufae sana wewe waofisini, lakini washambani kama mimi yatamfaa.
 
Hauni kwamba sehemu ambayo kuku wapatikana kwa bei juu ndyo ina opportunity kubwa katika ufugaji wa wa kuku... ??! Kafugie kuku songea utapiga mpunga
Sio lazima uzalishie sokoni, anaweza akazalishia Singida akauza Zanzibar.
Nakuunga mkono kwa hoja ya kufugia Ruvuma kwa sababu ya upatikanaji wa chakula cha mifugo yake.
 
Ruvuma mbona panafikika kiurahisi kila siku Fuso zinapishana usiku na barabara ni nzuri kabisa tena nadhani wao kwa upande wa miundombinu walianza kitambo kuw na lami hivyo hata issue ya usafirishaji wa bidhaa wapo vizuri (FUSO kila siku usiku zinapishana)
Mwambie ahamie kama ni dili
 
Hakuna soko lakitu gani mkuu? Na kwanini production cost iko juu?
Unaongea kimakaratasi zaidi au wewe ni mkulima?
Uhakika wa soko la mazao kati ya dar na songea wapi ni uhakika?
Mkulima au mfugaji wa morogoro au singida wakienda kuuza zao aina moja nani atakuwa kwenye disadvantage zaidi?
 
Nipo naelekea songea,then lindi mpaka mtwara na ntapitia morogoro kurudi mbeya. Nina wilaya na vijiji ambavyo wadau wameshauri nikajionee fursa huko
Utatuwekea hapa matokeo yake mkuu na sisi tujisomee!
 
Watu wengi wanajibu kwa kuisikia hiyo mikoa lakini si kwa kufanya utafiti wa ulichokiuliza!

Jibu langu, ingia Ruvuma: sababu
Mvua za kutosha
Ardhi ya kutosha bei karibu na bure.
Chakula cha mifugo kama Pumba na mashudu bei chini, hivi sasa pumba unapata kwa 1000tshs debe.
Maji yanapatikana kwa urahisi
Usafiri upo wa ndani na nje ya mkoa hivi sasa barabara ya kuunganisha mtwara ipo tayari hivyo uhakika wa soko kwani mtwara na hata Lindi zinategea chakula toka Ruvuma..changamoto zingine ni kawaida.
 
Habari wakuu?. Hope tunajiandaa vema na sikukuu ya pasaka pia hongereni kwa mapumziko mareeeefu!.

OK nirudi kwenye kitu kilichonileta hapa kwenu nyie wadau na wataalam wa fani mbalimbali mliopo humu ndo maana hakuna kinachoshindikana ndani ya Jamiiforums. Naombeeni kujuzwa kati ya songea na Singida ni mkoa upi mzuri kwa mtu anaetaka kuishi na kujishuhurisha na UFUGAJI na KILIMO!?.

Hapa tutaangalia na gharama za maisha na huduma za kijamii pia.
KUMBUKA nipo tayar kuishi hata kijijini sana ili mradi nifanikishe lengo langu la kutoka kiuchumi kupitia ufugaji hasa wa UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI .

Asanteni sana na poleni kwa kuwatoa kwenye mada zetu za siasa
watu wengi hapa wanashauri kiushabiki na kila mmoja anavutia kwao, wa singida atakuambia njoo huku na wa ruvuma vilevile. fanya analysisi tu vizuri mkuu,mi naamini si Ruvuma wala singida popote unatoboa ila dhamira yako ndio itakayokuongoza. Tanzania hii popote utakapoenda kuna matajiri wanaoheshimika na kuna majumba mazuri tu.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom