Money Penny
JF-Expert Member
- Jun 20, 2016
- 15,913
- 14,797
Jana nilikuwa airport napata huduma, katika kusubiria huduma kukawa na malumbano Kati ya binti mmoja na Mzee mmoja
Mzee: akawa anamtania Huyo binti kuwa amuoe wawe wapenzi, atampatia Mapenzi ya Raha, kupetipeti aachane na vijana, vijana NI stress, amkubali atamlea binti kama Yai, tena Mimi NI MTU wa Tanga
Binti: woi, we Mzee ujana ule na Nani, uzee umalizie na Mimi? Usiniletee gundu la maisha, Kwanza mume WA mtu Mimi simtaki
Mzee: Mimi naruhusiwa kuoa wake wengi, kwahiyo usiwe na wasiwasi
Binti: Mzee naomba nikuombe Radhi kabla ya haya nayotaka kusema, mimi siwezi oleww na mzee wala kuteleza na Mzee. Bora niolewe na Kijana mwenzangu tupambane na maisha na akili yangu ichangamke kuliko kupetiwapetiwa Kila siku na Mzee niwe kama kamasi, nimefungiwa ndani kama paka la kiarabu naishia kuwa zuzu
Mzee: vijana wanasumbua binti nikubali Mimi Mzee sikusumbui na hautofanya kazi, wanawake NI mapambo sio kuchakarika kama vichaa
Binti: Bora nisumbuliwe na Kijana akili isimame kuliko Mzee kunifanya ndondocha WA kukaa ndani kisa Raha, KAZI nitafanya sana ndio furaha yangu
Nikuulize mdau WA JF, je Kati ya penzi la Mzee na Kijana lini linanoga zaidi? Hili ni swali la wote wanaume na wanawake
Mzee: akawa anamtania Huyo binti kuwa amuoe wawe wapenzi, atampatia Mapenzi ya Raha, kupetipeti aachane na vijana, vijana NI stress, amkubali atamlea binti kama Yai, tena Mimi NI MTU wa Tanga
Binti: woi, we Mzee ujana ule na Nani, uzee umalizie na Mimi? Usiniletee gundu la maisha, Kwanza mume WA mtu Mimi simtaki
Mzee: Mimi naruhusiwa kuoa wake wengi, kwahiyo usiwe na wasiwasi
Binti: Mzee naomba nikuombe Radhi kabla ya haya nayotaka kusema, mimi siwezi oleww na mzee wala kuteleza na Mzee. Bora niolewe na Kijana mwenzangu tupambane na maisha na akili yangu ichangamke kuliko kupetiwapetiwa Kila siku na Mzee niwe kama kamasi, nimefungiwa ndani kama paka la kiarabu naishia kuwa zuzu
Mzee: vijana wanasumbua binti nikubali Mimi Mzee sikusumbui na hautofanya kazi, wanawake NI mapambo sio kuchakarika kama vichaa
Binti: Bora nisumbuliwe na Kijana akili isimame kuliko Mzee kunifanya ndondocha WA kukaa ndani kisa Raha, KAZI nitafanya sana ndio furaha yangu
Nikuulize mdau WA JF, je Kati ya penzi la Mzee na Kijana lini linanoga zaidi? Hili ni swali la wote wanaume na wanawake