Kati ya mfungwa wa kisiasa na aliyepigwa risasi nani ni mzalendo zaidi kumfanya apate nafasi ya kugombea Urais

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,671
40,912
Chama Cha Demokrasia na Mandeleo kipo kwenye wakati mgumu sana wa kumpata mgombea wa kiti cha urais kwa uchaguzi wa mwaka 2020.

Ugumu wa upatikanaji wa mgombea unakuja kutokana na sifa mbali mbali walizonazo makada wake.

Ingawa mgombea wa nafasi hiyo bwana Lowasa bado ana nafasi hiyo ila ushindani umeongezeka kwake.

Mwenyekiti wa chama hicho Bwn. Freeman Mbowe ambaye kwa sasa anafahamika kama mfungwa wa kisiasa anazidi kuchanja mbuga katika kupaliilia nafasi hiyo adimu kabisa na ya kihistoria.

Mwanasheria mkuu wa Chama Bwn. Lisu naye hayuko nyuma kwani ameongeza umaarufu maradufu baada ya kuvamiwa na kupata shambulizi la risasi, jambo ambalo limemfanya afanye matibabu nje ya nchi , ambako kwa hivi sasa anafanya ziara ulaya na marekani akinadi tukio lake la kupigwa risasi.

Kwa kuangalia sifa hizo kemkem ambazo kwa macho ya wanachama na wafurukutwa na chadema ni uzalendo wa kutukuka, nakosa majibu ni nani kati yao atakayebeba mikoba ya kukiwakilisha chama.
 
huyo mahabusu wa kisiasa hawezi kugombea urais kazi yake kubwa ni kufanya biashara ya kuona nani ana dau kubwa la kumpatia ili umkabidhi mikoba ya ugombea.
 
huyo mahabusu wa kisiasa hawezi kugombea urais kazi yake kubwa ni kufanya biashara ya kuona nani ana dau kubwa la kumpatia ili umkabidhi mikoba ya ugombea.
Alishawahi kufanya hivyo;

Sio vibaya akijaribu tena kipindi hiki ambacho umaarufu umeongezeka maradufu.
 
Chadema ni taasisi ya uma ; Unless bado ile hulka kuwa ni mali binafsi ya familia bado mnayo.

Vile vile linapokuja swala la ugombea wa Urais lazima tuwafahamu wahusika vyema kwani wanataka kuwa viongozi wetu.
Chadema huwa hawaeleweki sasa kwa taarifa yako, wengi tulitarajia 2015 mgombea angekuwa Slaa, yakatokea maajabu akawa Lowasa........!!!!!!!!

Sasa usishangae 2020 asitokee hata mmoja kati ya uliowataja hapo juu, akawa labda kwa Mfano Bw. Membe...!!! Hawa Watu ni shida.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chadema huwa hawaeleweki sasa kwa taarifa yako, wengi tulitarajia 2015 mgombea angekuwa Slaa, yakatokea maajabu akawa Lowasa........!!!!!!!!

Sasa usishangae 2020 asitokee hata mmoja kati ya uliowataja hapo juu, akawa labda kwa Mfano Bw. Membe...!!! Hawa Watu ni shida.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wala usijeshangaa utakaposikia ni Nyalandu..
 
Chadema ni taasisi ya uma ; Unless bado ile hulka kuwa ni mali binafsi ya familia bado mnayo.

Vile vile linapokuja swala la ugombea wa Urais lazima tuwafahamu wahusika vyema kwani wanataka kuwa viongozi wetu.
Wewe ni kada wa CCM,hilo liache kwa wanachama wa CDM!Subiri atakayepatikana ndio kugombea urais ndio umchambue,kwa sasa mpaka hapo atakapopatikana ni mambo ya wana CDM wenyewe so shut up!
 
Alishawahi kufanya hivyo;

Sio vibaya akijaribu tena kipindi hiki ambacho umaarufu umeongezeka maradufu.
Alishawahi kufanya hivyo;

Sio vibaya akijaribu tena kipindi hiki ambacho umaarufu umeongezeka maradufu.
ni kweli alishafanya hivyo ila kwa sasa anaona kufanya biashara ya kulinganisha dau za wagombea ndio inalipa zaidi kuliko umakini wa mtu.
 
Chama Cha Demokrasia na Mandeleo kipo kwenye wakati mgumu sana wa kumpata mgombea wa kiti cha urais kwa uchaguzi wa mwaka 2020.

Ugumu wa upatikanaji wa mgombea unakuja kutokana na sifa mbali mbali walizonazo makada wake.

Ingawa mgombea wa nafasi hiyo bwana Lowasa bado ana nafasi hiyo ila ushindani umeongezeka kwake.

Mwenyekiti wa chama hicho Bwn. Freeman Mbowe ambaye kwa sasa anafahamika kama mfungwa wa kisiasa anazidi kuchanja mbuga katika kupaliilia nafasi hiyo adimu kabisa na ya kihistoria.

Mwanasheria mkuu wa Chama Bwn. Lisu naye hayuko nyuma kwani ameongeza umaarufu maradufu baada ya kuvamiwa na kupata shambulizi la risasi, jambo ambalo limemfanya afanye matibabu nje ya nchi , ambako kwa hivi sasa anafanya ziara ulaya na marekani akinadi tukio lake la kupigwa risasi.

Kwa kuangalia sifa hizo kemkem ambazo kwa macho ya wanachama na wafurukutwa na chadema ni uzalendo wa kutukuka, nakosa majibu ni nani kati yao atakayebeba mikoba ya kukiwakilisha chama.
Suala sio kupigwa risasi bali ni kwa nini apigwe risasi? Suala sio kugombea mara ya kwanza bali nini unajiandaa kulifanyina taifa hili. Suala sio kufungwa bali ni kwanini ufungwe! Hizo ni nia tu na wengine wanashauriwa wajitokeze. Zaidi ya wagombea 40 walichukua form kutoka kijani, lakini ni mmoja tu alipata urais.
 
Suala sio kupigwa risasi bali ni kwa nini apigwe risasi? Suala sio kugombea mara ya kwanza bali nini unajiandaa kulifanyina taifa hili. Suala sio kufungwa bali ni kwanini ufungwe! Hizo ni nia tu na wengine wanashauriwa wajitokeze. Zaidi ya wagombea 40 walichukua form kutoka kijani, lakini ni mmoja tu alipata urais.
Kwa bahati mbaya mpaka sasa sifa kuu za watajwa ni matukio yaliyowakuta. Unadhani hiyo ni sifa pekee ya kuwapatia hiyo nafasi?
 
Kwa bahati mbaya mpaka sasa sifa kuu za watajwa ni matukio yaliyowakuta. Unadhani hiyo ni sifa pekee ya kuwapatia hiyo nafasi?
Kimsingi unachosema ni kweli, kuwa rais kunahitaji sifa za ziada lakini historia ya marais wetu mbona inafanana? Rais Mbenajmin William Mkapa alikuwa Mbuge kwa vipindi kadhaa, akawa waziri kwa vipindi kadhaa na hatimaye akawa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznaia, tena kwa vipindi vyote viwili. Kwa kumbukumbu tulizonzo alifanya mengi mazuri na mabaya yapo. Rais JMK alikuwa mbunge kwa vipindi kadhaa na waziri wa wizara mbali mbali. Kuna mambo mazuri ameyafanya akiwa rais na kuna ujinga aliufanya kwa kipindi chake cha miaka 10 ya urais wa JMT. Mheshimiwa, JPM amekuwa mwalimu wa sekondary na unajua sifa za kuwa Mwalimu, Mkemia wa jinenari ya mafuta ya pamba, akawa mbunge kwa vipindi kadhaa na waziri wa wizara mbali mbali na sasa Rais wa zamu.

Katika kundi la wagombea tunao tunao wataja kutoka kwenye kundi la upinzani, yaani Mhe. Mbowe, Mhe. Lowasa na Mheshimiwa Tundu Lissu, unaona wanasifa gani pungufu ukilinganisha na hao marais waliotangulia? Nawaona hawa wanaweza kuwa bora labda kuliko hao wengine waliokwisha kuwa marais. Kwa mfano, Mheshimiwa Tundu Lissu ni mwanasheria mbobezi hadi amekuwa Rais wa wanasheria Tanzania, Mbunge kwa vipindi zaidi ya kimoja na mwanaharakati wa kutegemewa katika kutetea rasmali za nchi hii hasa madini.

Mhe. Lowasa, amekuwa wa mbunge kwa zaidi ya vipindi viwili, amekwa waziri wa wizara zaidi ya moja na Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa zaidi ya mika 2.5, mgombe urais aliyepata zaidi ya kura millioni 6 ukulinganisha na kura 8 millioni za rais aliyeko madarakani.

Mhe. Mbowe ni mbunge kwa zaidi ya vipndi viwili, Msemaji wa Kambi rasmi ya upinzani bungeni, mgombea urais aliyeshindwa na kumpongeza rais aliyeshinda na hadi kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwake. Anaongoza chama kilichokuwa kidogo sana nchi hii hadi kuwa chama tishio cha upinzani . Kwa maelezo hayo, sio siri ni kiongozi mwenye ushawishi mkubwa na wenye maono.

Naomba unieleweshe upungufu wao uko wapi kama sio kasumba na hopja zinazotawaaliwa na hisia kuliko hali halisi?
 
Back
Top Bottom