Kati ya Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi, Wakili Kibatala anasimama na ACT Wazalendo

Now, this is certainly a calm response from you that can be discussed rationaly.

Siwezi kamwe kuwatetea wapinzani kwamba hawafanyi/hawajawahi kufanya makosa, kuna sehemu mbalimbali wamefanya makosa, pengine hata mengine yanayotokana na kukosa uzoefu.
Lakini kuwalaumu kwa kushindwa kwao kwa mfano kutetea viti vyao vya ubunge katika uchaguzi mkuu kama ule uliofanyika 2020, hapo ni kuwaonea kuliko wazi kabisa.

Wapinzani wamefanyiwa bugdha, nyingi tu, hata za kuwanyima haki ya kufanya siasa, haya nayo walaumiwe wao kutoweza kutumia wale wabunge wachache waliokuwa nao bungeni kuongeza wingi wao? Huko bungeni kwenyewe, chini ya uongozi wa Ndugai na huyu binti sasa anayekalia kiti cha spika, hukuwahi kuona jinsi walivyokuwa wakitendewa humo ndani?

Hao wabunge waliokuwa wakinunuliwa kutoka upinzani, nako tuseme ni upinzani ulioshindwa kuwasimamia wabunge wake?

All in all, haya yote tunayoyasema hapa ni mfano mzuri unaoonyesha kwamba hata hiyo "Tume Huru" kwa muujiza ingetokea kuwepo, mfumo unaoendeshwa na CCM usingeruhusu hiyo tume ifanye kazi inavyotakiwa.

Kwa hiyo, jibu si kuwepo kwa "Tume Huru" kutakakoongeza wabunge upande wa upinzani, halafu wabunge hao ndio wasimamie kutengeneza Katiba Mpya.
Na kwa kweli nasita hata kusema kuwa uwepo wa Katiba Mpya 'per se' ndiko kutakakoondoa mfumo mbovu unaoilinda CCM kuendelea kuvuruga nchi.
Nadhani jibu la haya yote lipo kwa wananchi kuamua ku-overhaul the entire system. Kuung'oa kabisa mfumo huu mbovu na miziz yake yote, halafu tutengeneze Katiba Mpya, na matokeo yake yawe kupatikana kwa Tume Huru ya uchaguzi.
Ni wananchi pekee, ndio wenye uwezo huo, lakini wawe na elimu ya kutosha katika eneo hili, na pawepo na uongozi thabiti wa kuwaongoza kuikamilisha shughuli hii muhimu sana kwa taifa letu wakati huu.

CCM hataki kabisa mabadiliko haya, na katika kukataa huko, tunaona wanavyohangaika na hizi mbinu mpya za kuwalaghai watu, ikiwa ni pamoja na baadhi ya viongozi wa upinzani.
Hapo naona badala ya kusema "nadhani" jibu la haya yote lipo kwa wananchi kuondoa the entire political system waweke mfumo wao, ungetakiwa kuandika "naamini"

Hiyo ndio solution itakayoondoa kutoaminiana kulikojaa kwenye vichwa vya wanasiasa, wakiachwa peke yao waitafute Katiba Mpya kwa kuteua wajumbe wa bunge la Katiba tutakuwa tunadanganyana.

Hiyo move itakufa kama ilivyokufa ile ya mwanzo, political interest zitawateka matokeo yake wasahau mahitaji ya wananchi waangalie mahitaji ya vyama vyao hasa kushika madaraka (Urais, ubunge nk)

Hivyo kwa maoni yangu, suala la Katiba Mpya ni lazima waachiwe wananchi, wateuliwe viongozi wengine (wajumbe) na wananchi kutoka makundi mbalimbali ambao hawatakuwa na vinasaba na chama chochote cha siasa ili kuondoa dhana ya kutoaminiana.

Lakini tukianza tena CCM walete wajumbe wao, upinzani nao wapeleke wajumbe wao, halafu ipigwe kura ya kumchagua spika mwanasiasa ambae wajumbe wengi wa chama chake watampa kura, hapo tutakuwa tunafeli kila siku, hiyo Katiba Mpya haitakaa ipatikane.
 
Mkuu, wewe unakwenda mbele zaidi kabla ya kuangalia nyuma kuna nini.

Hiyo "majority in parliament" hao wapinzani wataipataje, kwa hiyo tume unayofikiria itakuwa huru? Hiyo tume huru itatoka wapi? Mungu ataidondosha Tanzania ianze kufanya kazi ikiwa huru kabisa ili wapinzani wapate "majority in parliament"?

Eleza kwanza hiyo "Tume Huru" itatoka wapi, halafu mengine yatafuata.
Na ili maelezo yako yawe kamilifu, usisahau hiyo "Tume Huru" itakuwaje huru katika mazingira yasiyokuwa rafiki kwake. Kwa mfano, polisi wakitaka kufanya yao wakati wa uchaguzi, tume itafanya nini na uhuru wake. Huo ni mfano mmoja tu ninaokupa, ipo mingi mingine inayoweza kukwamisha huo uhuru unaodhani itakuwa nao.
Kwanza nikubailiane na wewe, Tume huru kwangu ni zao la Katiba nguvu ya Tume huru should be drawn from the Katiba yenyewe. Kama tume haiwezi kuizuia Police wasiingilie uchaguzi na kulazimishwa na katiba uchaguzi kuwa fair then hakuna kitu hapo. Mimi ni muumini wa katiba kwanza ili yasijirudie ya Zanzibar eti tume huru kwa kuwaingiza wapinzani ndani yake na Mwenyekiti wake kumpa uhuru wa kufuta uchaguzi hata bila kushirikisha Tume yenyewe.
 
Shida ya wapinzani ni kukosa utashi wa kubaini na kusahihisha strategic mistakes zao. Wanapenda witch-hunting zaidi. Madai ya kupokwa ushindi ndiyo chorus wanayoipenda, lakini ukweli ni kwamba wanafanya makosa mengi ya kimkakati. Imekuwa kawaida yao kusema wamepokwa ushindi kila wanaposhindwa uchaguzi na kusema haki imetendeka pale wanaposhinda. Hiyo ambivalence ni uwendawazimu tu, kwasababu kuna empirical evidence ya repeated successes kwenye majimbo ambayo upinzani walikuwa na mikakati mizuri.

Kitu ambacho wapinzani walipaswa kukifanya tangu mwanzo ni kuvifanya viti vya ubunge na uwakilishi kuwa their first priority and to replicate their success stories. Wanapoteza resources nyingi na energy kubwa kupigania Ikulu badala ya kupigania vyombo ambavyo ndivyo vina uwezo wa kusawazisha uwanja wa mapambano. Fikiria, kwa mfano, resources na energy wanazotumia presidential candidates wanaodhaminiwa na vyama ambavyo havijawahi hata kuwa na kiti kimoja tu kwenye Bunge. Are those resources and energy put to good use? Wanataka kwenda Ikulu wakawe dictators au ili iweje labda?

‘Tume Huru’ ni sehemu ndogo sana ya mabadiliko ya Katiba yanayohitajika and it’s a more realistic goal, under the current political environment. So, long story short, if you think ‘Tume Huru’ is out of reach, juhudi zozote za kupigania Katiba mpya ni uwendawazimu!
Swali kwako ungekuwa mpinzani ungefanya nini hasa? Katiba ndio hiyo, usilaumu bila kuangalia hali halisi. Wapinzania sidhani kama ni wa ajinga wanajaribu kunavigate kwenye nchi yenye katiba isiyo ya wananchi. Ni nani kati ya serikali iliyoko madarakani yenye katiba yenye kuweza kuzalisha madikteta na wapinzani ambao hawajapata madaraka? Wapinzania wanataka mabadiliko ya katiba itakayoondoa udikteta kwa kumpunguzia Rias madaraka wewe unawalauma wapinzania hata hujielewi huna mashiko kabisa.
 
Hoja hapo juu ina dalili za divide and Rule, Kibatala ni mtazamo wake unaweza usiwe wa chama chake na sii kosa wala halina madhara kwa chama chake kwani wanafuata taratibu zilizopo ndani ya chama chao. Iwapo litashinda basi tutegemee chama chao kubadili mwelekeo. Ila the way you put it ina dalili ya kuwachonganisha yeye na chama chake. Natumaini utashindwa.
 
EeenHeeee!
Naona kila mtu anatwanga kivyake hapa. Mjadala hauwezi kwenda hivyo.

Mtu unaambiwa mfumo hauwezi kuruhusu wapinzani kupata huo wingi wa wabunge, halafu jibu linakuwa "kama kuna foulplay kwenye baadhi ya majimbo, hiyo si justification ya kukataa matokeo", sasa unataka wapate wabunge wengi kivipi?

Halafu unasema "Kujaribu kupandikiza kwenye jamii utamaduni wa umma kutafuta mabadiliko kwa njia za shari ni kujichimbia kaburi". Hivi unajuwa ni nani anayetumia njia za shari kubaki madarakani, huyu ataachaje madaraka kama halazimishwi na njia hizo hizo anazotumia yeye?

Nadhani nimefikia mwisho wa mjadala huu, maanake naona hakuna jipya tutakalojadili, angalao kuepusha hizo shari unazozizungumzia hapa.

Lakini sina hakika kama kweli uliyoandika hapa ndiyo hasa unayoyaamini. Nimejaribu kujikumbusha juu ya michango yako mbalimbali humu jukwaani, lakini sijaona msimamo unaoendana na mawazo haya. Labda uwe umeyaokota juzi ndani ya serikali ya mama.

Imenilazimu pia nitazame kwa makini 'Avatar' unayotumia hapa. Nimeshindwa kujuwa hasa unasimamia wapi katika hatma ya nchi yetu.

Kweli afadhali tuishie hapa kwasababu huu mjadala hauna tija. Tatizo wewe unajaribu kugeuza hisia kuwa facts. Kauli kwamba mfumo hauwezi kuruhusu wapinzani kupata majority ya viti vya Bunge ni hisia isiyokuwa na hata chembe ya uhalisia. How can that be accomplished? Matokeo ya uchaguzi wa wabunge hayatangazwi centrally; yanatangazwa kwenye level ya jimbo. Kitu pekee ambacho kinaweza kufanya hii hisia yako kuwa na mashiko ni ushahidi wa specific names za majimbo ambayo ndiyo yametengwa kwa ajili ya vyama vya upinzani (na kwa idadi yake hayawezi kuwapa wapinzani control ya Bunge). Kama unao huo ushahidi, ulete hapa.

Usidhani hakuna wanasiasa wenye uchu wa madaraka kiasi cha hata kutaka kutumia vibaya nguvu ya umma. Ukishapandikiza huo utamaduni wa shari, kila mwanasiasa anayeshindwa kufikia malengo yake anao uwezo wa kuamsha shari ya umma. Unfortunately, hiyo shari itambeba kwa muda tu, kwasababu wapo wanasiasa wengine ambao nao baadaye wataamsha shari nyingine. Obviously, that’s a destabilizing strategy that cannot be in the best interest of a nation. Ndiyo maana nikasema ni kujichimbia kaburi.

Hii sio mara yangu ya kwanza kuzungumza juu ya strategic mistakes za vyama vyetu vya upinzani. Kila nilipofanya hivyo, nimesema priorities za hivi vyama vyetu zimekuwa upside down tangu mwanzo!
 
Swali kwako ungekuwa mpinzani ungefanya nini hasa? Katiba ndio hiyo, usilaumu bila kuangalia hali halisi. Wapinzania sidhani kama ni wa ajinga wanajaribu kunavigate kwenye nchi yenye katiba isiyo ya wananchi. Ni nani kati ya serikali iliyoko madarakani yenye katiba yenye kuweza kuzalisha madikteta na wapinzani ambao hawajapata madaraka? Wapinzania wanataka mabadiliko ya katiba itakayoondoa udikteta kwa kumpunguzia Rias madaraka wewe unawalauma wapinzania hata hujielewi huna mashiko kabisa.

Kama ungekuwa umesoma na kuelewa nilichoandika, usingeandika ulichoandika. Katiba mpya haipatikani kwa kutoa matamko tu!
 
Kweli afadhali tuishie hapa kwasababu huu mjadala hauna tija. Tatizo wewe unajaribu kugeuza hisia kuwa facts. Kauli kwamba mfumo hauwezi kuruhusu wapinzani kupata majority ya viti vya Bunge ni hisia isiyokuwa na hata chembe ya uhalisia. How can that be accomplished? Matokeo ya uchaguzi wa wabunge hayatangazwi centrally; yanatangazwa kwenye level ya jimbo. Kitu pekee ambacho kinaweza kufanya hii hisia yako kuwa na mashiko ni ushahidi wa specific names za majimbo ambayo ndiyo yametengwa kwa ajili ya vyama vya upinzani (na kwa idadi yake hayawezi kuwapa wapinzani control ya Bunge). Kama unao huo ushahidi, ulete hapa.

Usidhani hakuna wanasiasa wenye uchu wa madaraka kiasi cha hata kutaka kutumia vibaya nguvu ya umma. Ukishapandikiza huo utamaduni wa shari, kila mwanasiasa anayeshindwa kufikia malengo yake anao uwezo wa kuamsha shari ya umma. Unfortunately, hiyo shari itambeba kwa muda tu, kwasababu wapo wanasiasa wengine ambao nao baadaye wataamsha shari nyingine. Obviously, that’s a destabilizing strategy that cannot be in the best interest of a nation. Ndiyo maana nikasema ni kujichimbia kaburi.

Hii sio mara yangu ya kwanza kuzungumza juu ya strategic mistakes za vyama vyetu vya upinzani. Kila nilipofanya hivyo, nimesema priorities za hivi vyama vyetu zimekuwa upside down tangu mwanzo!
"...kugeuza hisia kuwa fact"? Unafanya nikudharau moja kwa moja. Wewe una akili gani za kutoona uchafu woote uliowazi na kuuita 'hisia'?
Uchaguzi mkuu 2020 kuchafuka ni 'hisia' kwako? Vyama vya upinzani kuzuiwa kufanya siasa, ni 'hisia' kwako? Polisi kunyanyasa watu kwa sababu za kisiasa, ni 'hisia' kwako?

Rudi nyuma usome unayoandika katika mada hii tangu nilipoanza kuruhusu tujadili, kama kweli utaona kuna 'objectivity' yoyote katika yote uliyoandika.

Nilishawahi jibishana nawe kwa kirefu huko siku za nyuma katika mijadala mingine, staili yako ni ile ile, haibadiliki, ni kama unaupungufu katika 'thought process yako' unapoandika chochote humu.

"Pulchra Animo"- whatever that means, but certainly has a certain ring to it that describes you appropriately.

Can't waste any further time on useless exchanges with you.
 
"...kugeuza hisia kuwa fact"? Unafanya nikudharau moja kwa moja. Wewe una akili gani za kutoona uchafu woote uliowazi na kuuita 'hisia'?
Uchaguzi mkuu 2020 kuchafuka ni 'hisia' kwako? Vyama vya upinzani kuzuiwa kufanya siasa, ni 'hisia' kwako? Polisi kunyanyasa watu kwa sababu za kisiasa, ni 'hisia' kwako?

Rudi nyuma usome unayoandika katika mada hii tangu nilipoanza kuruhusu tujadili, kama kweli utaona kuna 'objectivity' yoyote katika yote uliyoandika.

Nilishawahi jibishana nawe kwa kirefu huko siku za nyuma katika mijadala mingine, staili yako ni ile ile, haibadiliki, ni kama unaupungufu katika 'thought process yako' unapoandika chochote humu.

"Pulchra Animo"- whatever that means, but certainly has a certain ring to it that describes you appropriately.

Can't waste any further time on useless exchanges with you.

Una changamoto kubwa kwenye eneo la comprehension ya kile kilichoandikwa. Ultimately, that’s what causes you to ask questions or bring up issues that have nothing to do with what one has said.

Kujadiliana na wewe ni kama kutwanga maji kwenye kinu!
 
Katiba mpya is a long term project

It is a long term project to FISADIS who want to continue to loot the country!! The KATIBA issue would have been resolved during KIKWETE"S tenure if only he did not sabotage the process to safeguard his personal interests!! He is still at it again by trying to influence Samia and the ruling party to sabotage the people's ardent wish to have their KATIBA!
 
Una changamoto kubwa kwenye eneo la comprehension ya kile kilichoandikwa. Ultimately, that’s what causes you to ask questions or bring up issues that have nothing to do with what one has said.

Kujadiliana na wewe ni kama kutwanga maji kwenye kinu!
Sawa.
 
Kama ungekuwa umesoma na kuelewa nilichoandika, usingeandika ulichoandika. Katiba mpya haipatikani kwa kutoa matamko tu!
Ndugu tamko nililotoa hapo lipi hapo? bado narudia huna locus ndio wale wale wanakula matunda ya katiba iliyopo.
 
Ndugu tamko nililotoa hapo lipi hapo? bado narudia huna locus ndio wale wale wanakula matunda ya katiba iliyopo.

Hivi wapinzani wakisema, “tunataka Katiba mpya” ni kitu gani kama sio tamko?

Kama Katiba iliyopo ina matunda, mgao wangu mimi na familia yangu hauna tofauti na wa mwingine yeyote!
 
Kwa sasa Kuna mjadala wa kipi kianze Kati ya katiba ya wananchi na Tume huru ya Uchaguzi.

Mvutano mkubwa unaonekana katika vyama viwili vya ACT Wazalendo na Chadema.

ACT Wazalendo wanataka ianze Tume huru ya Uchaguzi katika kuiendea katiba mpya na Chadema wanataka katiba mpya kwenye kuiendea Tume huru.

Mawazo yao yamewaingiza katika uadui mkubwa huku upande wa ACT Wazalendo ukijenga hoja ya kwanini ni muhimu kuanza na Tume huru na Chadema wakiwangooshea vidole na kuwatukana wakati mwingine kuwa wanatumiwa na serikali kuihujumu

Katika hatua hii Kuna makundi ya watu wenye ushawishi wametoa maoni yao.

Miongoni mwao ni Maria Sarungi kupitia bunge la Space anayetaka katiba mpya kwa kuungana na Chadema

Lakini wote hao hawasemi wataifikia vipi katiba mpya kutoka katika kura za wananchi hadi tume ya Sasa yenye jukumu la kuhesabu kura za maoni zitakazopigwa.

Kwa upande wa ACT Wazalendo,mawazo yao yanaungwa mkono na wanasheria nguli wa Chadema, Peter Kibatala na Tundu Lissu kuwa ni muhimu kuanza na Tume huru kabla ya Katiba mpya huku wakielezea sababu zao.

Kibatala amesema katika moja ya mahojiano na Clouds Tv kuwa sheria ya mabadiliko ya katiba ya Jaji warioba inataja tume ya uchaguzi ya Taifa NEC na ZEC kuwa ndiyo watakaosimamia kura za maoni kwenye kuipata katiba mpya.

Anasema hiyo tume isipokuwa huru hata wananchi asilimia 98 wakiwa wamepigwa kura ya kuidhinisha katiba mpya tume hizo zinaweza kupindisha ukweli na wananchi wakapoteza haki zao.

Pia Tundu Lissu kwa mlango wa Nyuma amesema mchakato wa Katiba uanze na ikiwa itafikia Uchaguzi wa 2024-25 katiba ikiwa haijaakamilika basi iundwe Tume huru,itakayosimamia Uchaguzi huo.

Kauli yake hii ambayo kwa namna moja ama nyingine imebeba tahadhari zote za kuzuia ukosolewaji ndani ya chama inaashiria wazi tamanio lake ni kuanza na Tume huru kabla ya Katiba mpya.

Kwa hiyo utaona mitazamo ya ACT Wazalendo na hao wanasheria nguli kwa pamoja kwao muhimu ni TUME huru Kwanza kabla ya Katiba.

Na Kibatala amekuwa muwazi zaidi katika hili tofauti na Lissu,anayesema chaguo lake kwa kuzunguka
Mbona hata wewe uandishi wako unaonekana unatumika na ACT na ccm. Hilo waachieni wenye agenda zao ndo wanajua uzito wake.
 
Back
Top Bottom