Mohamedi Mtoi
R I P
- Dec 11, 2010
- 3,321
- 6,328
Soma kwa makini na nanukuu (neno kwa neno) gazeti la Mwananchi toleo Na: 4741;
Jumanne, Juni 18 2013 ukurasa wa 4;
Majeruhi Mwengine Majeruhi mwingine, Abdallah Hilali (39) aliyelazwa katika Hospitali ya Arusha Lutheran Center amedai kuwa majeraha aliyopata miguuni yametokana na kupigwa risasi na Polisi na kudondekewa na vipande vya bomu.
Alisema alikuwa nyma ya jukwa kuu akimsikiliza Mbowe na alipomaliza kuhutubia alishuka jukwaani kukusanya sadaka, ndipo alipoona mfuko wa mweusi mdogo wa plasitiki ukipeperuka juu.Nilidhani ni upepo unapeperusha kitu, lakini ghafla nilisikia kishindo na nikamsikia mama mmoja akipiga kelele kuwa aliyerusha mfuko anakimbia, nilipogeuka nikajikuta nipo chini, alisema Hilali.
Alisema alipokuwa anaangalia aliona kijana mmoja amekaribia kumfikia aliyerusha bomu lakini ghafla akapigwa risasi na kuanguka chinina aliyekuwa nafuatia kwa nyuma naye akapigwa risasi akaona anaruka na kudondoka chini huku damu zikivuja.Likini mwisho wa yote kijana alirusha hilo fuko aliingia kwenye gari na kuondoka kwa kasi. Mimi nilikuwa chini, alisema Hilali ambeya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alipotembelea majeruhi Hospitalini hapo.
Mbowe: Tunawajua WatuhumiwaMbowe amedai kuwa wameagundua watu waliohusika na urushaji wa mabomu katika viwanja vya Soweto Juni 15, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu watatu na majeruhi 60.Akizungumza jana baada ya kutembelea majeruhi katika Hospitali ya Seliani, Mbowe alisema CHADEMA tayari imeajua wahusika wakuu wa mabomu hayo kwa ushahidi wa picha.
Alidai kuwa ni askari mmoja wa Kikosi cha Polisi wa Kuzuia Fujo (FFU).Alidai kuwa ushahidi huo unaonyesha kuwa wakati askari huyo akirusha bomu, alikuwa na kofia inayofanana na ile inayotumiwa na Polisi na mara baada ya kurusha bomu na risasi za mfululizo alikimbilia kwenye gari aina ya Land Cruiser na kusindikizwa na Polisi.Duniani hakuna siri yoyote ile. Tumeshafanikiwa kugundua chanzo kikubwa na ushahidi unaonyesha wahiskia ni polisi.
Ushahidi huu tutauweka hadharani na kila mwanadamu aweze kujionea kwa kuwa waliokufa hawana hatia yoyote na sisi tumechoka kil siku kuonewa na Polisi. Alisema
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.
Jumanne, Juni 18 2013 ukurasa wa 4;
Majeruhi Mwengine Majeruhi mwingine, Abdallah Hilali (39) aliyelazwa katika Hospitali ya Arusha Lutheran Center amedai kuwa majeraha aliyopata miguuni yametokana na kupigwa risasi na Polisi na kudondekewa na vipande vya bomu.
Alisema alikuwa nyma ya jukwa kuu akimsikiliza Mbowe na alipomaliza kuhutubia alishuka jukwaani kukusanya sadaka, ndipo alipoona mfuko wa mweusi mdogo wa plasitiki ukipeperuka juu.Nilidhani ni upepo unapeperusha kitu, lakini ghafla nilisikia kishindo na nikamsikia mama mmoja akipiga kelele kuwa aliyerusha mfuko anakimbia, nilipogeuka nikajikuta nipo chini, alisema Hilali.
Alisema alipokuwa anaangalia aliona kijana mmoja amekaribia kumfikia aliyerusha bomu lakini ghafla akapigwa risasi na kuanguka chinina aliyekuwa nafuatia kwa nyuma naye akapigwa risasi akaona anaruka na kudondoka chini huku damu zikivuja.Likini mwisho wa yote kijana alirusha hilo fuko aliingia kwenye gari na kuondoka kwa kasi. Mimi nilikuwa chini, alisema Hilali ambeya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alipotembelea majeruhi Hospitalini hapo.
Mbowe: Tunawajua WatuhumiwaMbowe amedai kuwa wameagundua watu waliohusika na urushaji wa mabomu katika viwanja vya Soweto Juni 15, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu watatu na majeruhi 60.Akizungumza jana baada ya kutembelea majeruhi katika Hospitali ya Seliani, Mbowe alisema CHADEMA tayari imeajua wahusika wakuu wa mabomu hayo kwa ushahidi wa picha.
Alidai kuwa ni askari mmoja wa Kikosi cha Polisi wa Kuzuia Fujo (FFU).Alidai kuwa ushahidi huo unaonyesha kuwa wakati askari huyo akirusha bomu, alikuwa na kofia inayofanana na ile inayotumiwa na Polisi na mara baada ya kurusha bomu na risasi za mfululizo alikimbilia kwenye gari aina ya Land Cruiser na kusindikizwa na Polisi.Duniani hakuna siri yoyote ile. Tumeshafanikiwa kugundua chanzo kikubwa na ushahidi unaonyesha wahiskia ni polisi.
Ushahidi huu tutauweka hadharani na kila mwanadamu aweze kujionea kwa kuwa waliokufa hawana hatia yoyote na sisi tumechoka kil siku kuonewa na Polisi. Alisema
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums.