Katendwa lakini roho inamuuma sana kuachana nae

Enny

JF-Expert Member
May 26, 2009
962
130
Kuna topic nilileta hapa kwamba kuna dada, boyfriend wake alichukua kadi yake ya gari na kwenda kuchukulia mkopo wa riba huko mitaani. na alipogundua wanataka kuchukua gari aligombana sana na boyfriend wake huyo. Lakini ili kuepusha gari isichukuliwe ilibidi amwambie huyo bwana anatafute wateja kwa hali na mali ili auze kipande cha shamba nje kidogo ya jiji. kweli bwana alichakarika huku na huku akapata mteja na mteja huyo akatoa nusu ya hela ambayo ilitosha kukomboa gari. Sasa hela iliyobaki akaahidi kulipa mwezi wa kumi na moja. lakini cha kusikitisha yule bwana kaenda kuchukua hela na kaingiza kwenye biashara zake zingine bila kumwambia huyo dada. Dada baada ya kungundua kawaka sana mpaka kampeleka jamaa polisi. Na anaona uwezekano wa kuwa pamoja haupo tena kwani amemkosea mara mbili katika kipindi kifupi ila kwa jinsi ninavyomuaona bado roho yake inamuuma sana kuvunja uhusiano.
Mimi na dada yake tumejaribu kumsihi apige moyo konde amsahau kabisa, aanze ukurasa mpya. Lakini kuna rafiki yake mpenzi anamshauri amsamehe tu huyo bwana anaweza kujirekebisha kwani ameomba msamaha kupitia kwake.

Naomba mawazo yenu hapa katika kumfariji huyu dada.
 
mwanamke anapokuwa kichwa cha familia kwa kuwa na maono zaidi ya maisha na mwanammme ukashindwa kuplay part basi mwanamme unakuwa janga la familia

anyway amsamehe kwa sababu mungu anasema samehe 7x70=490
 
Kuna topic nilileta hapa kwamba kuna dada, boyfriend wake alichukua kadi yake ya gari na kwenda kuchukulia mkopo wa riba huko mitaani. na alipogundua wanataka kuchukua gari aligombana sana na boyfriend wake huyo. Lakini ili kuepusha gari isichukuliwe ilibidi amwambie huyo bwana anatafute wateja kwa hali na mali ili auze kipande cha shamba nje kidogo ya jiji. kweli bwana alichakarika huku na huku akapata mteja na mteja huyo akatoa nusu ya hela ambayo ilitosha kukomboa gari. Sasa hela iliyobaki akaahidi kulipa mwezi wa kumi na moja. lakini cha kusikitisha yule bwana kaenda kuchukua hela na kaingiza kwenye biashara zake zingine bila kumwambia huyo dada. Dada baada ya kungundua kawaka sana mpaka kampeleka jamaa polisi. Na anaona uwezekano wa kuwa pamoja haupo tena kwani amemkosea mara mbili katika kipindi kifupi ila kwa jinsi ninavyomuaona bado roho yake inamuuma sana kuvunja uhusiano.
Mimi na dada yake tumejaribu kumsihi apige moyo konde amsahau kabisa, aanze ukurasa mpya. Lakini kuna rafiki yake mpenzi anamshauri amsamehe tu huyo bwana anaweza kujirekebisha kwani ameomba msamaha kupitia kwake.

Naomba mawazo yenu hapa katika kumfariji huyu dada.

Kwenye purple endelea kumsihi.

Hapo chini, mwambie yeye si wa kwanza kutendwa na mwanaume anayempenda na hatakuwa wa mwisho. In as much as it hurts, lakini with time (hata kama ni 5 yrs) atapona. She is a woman, and a woman is known for surving!
 
Huyo bi dada anasubiri siku atakayouzwa yeye ndio ashtuke au?
Yaan mpaka hapo hajaona tu kuwa huyo mwanaume ni TAPELI...
Wanawake acheni mapenzi ya bluetooth, shirikisheni na ubongo kwenye kupenda sio kila mara mtumie MOYO...
 
Kuna topic nilileta hapa kwamba kuna dada, boyfriend wake alichukua kadi yake ya gari na kwenda kuchukulia mkopo wa riba huko mitaani. na alipogundua wanataka kuchukua gari aligombana sana na boyfriend wake huyo. Lakini ili kuepusha gari isichukuliwe ilibidi amwambie huyo bwana anatafute wateja kwa hali na mali ili auze kipande cha shamba nje kidogo ya jiji. kweli bwana alichakarika huku na huku akapata mteja na mteja huyo akatoa nusu ya hela ambayo ilitosha kukomboa gari. Sasa hela iliyobaki akaahidi kulipa mwezi wa kumi na moja. lakini cha kusikitisha yule bwana kaenda kuchukua hela na kaingiza kwenye biashara zake zingine bila kumwambia huyo dada. Dada baada ya kungundua kawaka sana mpaka kampeleka jamaa polisi. Na anaona uwezekano wa kuwa pamoja haupo tena kwani amemkosea mara mbili katika kipindi kifupi ila kwa jinsi ninavyomuaona bado roho yake inamuuma sana kuvunja uhusiano.
Mimi na dada yake tumejaribu kumsihi apige moyo konde amsahau kabisa, aanze ukurasa mpya. Lakini kuna rafiki yake mpenzi anamshauri amsamehe tu huyo bwana anaweza kujirekebisha kwani ameomba msamaha kupitia kwake.

Naomba mawazo yenu hapa katika kumfariji huyu dada.

Ni vyema mwanaume akawa anajishughulisha kutafuta pesa hata kama mkewe au mpenziwe ana uwezo hata wa kutunza familia bila msaada wa mwanaume. Mwanaume asiyejishughulisha anakuwa kama 'mwanaume kama binti' kama alivyoimba Lady Jee Dee!

Lakini kujishughulisha kwa kuchukua vitu vya mpenzio na kuingiza kwenye biashara bila kutoa taarifa kwa mhusika, hilo ni tatizo kamili, ni wizi sawa na wizi mwingine wowote! Kama alifanya kosa la kwanza, likataka kugharimu gari kuuzwa, na ndani ya muda mfupi kashindwa kujifunza akafanya janga lingine, basi ujue hilo ni sikio la kufa, ipo siku anaweza kufanya jambo baya zaidi hata kuuza nyumba.

Nia yake ya kujishughulisha ni nzuri lakini tabia yake ya kuiba na kutokumshirikisha mpenzi wake ni mbaya sana na inaweza kuleta madhara makubwa.

Ni bora lawama kuliko fedheha, kama kuna uwezekano wa KUMFUTA akilini, nampa go ahead. Anachosha bwana! Sijui wenzangu nivea, gfsonwin, FP, Kongosho, The Rocky, snowhite wanasemaje kuhusu hili?
 
kimsingi enny huyu bwana ni tapeli, ama mcheza kamari na kwa maisha ya hapa mjini ni bora uolewe na mwizi kuliko tapeli ma mcheza kamari.

amwache na kisha atafute maisha yake so far mbona atampata tu wa kumfaa?? bf asikupelekeshe kwenye haya maisha.
 
my kaka HorsePower heshima yako mkuu jana usiku mbona mlikuwa mnapiga sana kelele na wifi ?nikaja pale dirishanai kusikiliza kelele nikaambulia aibu maana ni kelele zilizojaa furaha kumbe hazikuwa keleel ni bashaha lol niliumbuka shikamoo kaka yangu asante sana kwakunihusisha!!!
katika maisha yangu nafurahi san maana najihisi ni moja ya mwanamke ambaye huwa sifikirii kesho huwa nawaza miaka kumi ijayo mbele na moyo waangu nimeufunga speed gavana kabisa kiasi kwamba hauna ruhusa yakusaidiana na akili yangu kamwe najua unanielewa vizuri .nanukuu akiliyangu:nilishawahi fanya maamuzi ambayo jamii ilinipigia magoti wazee na watu weny heshi ma zao ila akili yangu iliona mbali kuliko wao ndio sababu naishi leo la sivyo mimi na wewe hata tusingekaa tujuane kaka yangu katika maamuzi yangu yale yalikuwa yakiume sana sio ya kike na hakuna aliyewaza how can i move on so kila aliyetoka pale alijisemea tuone atakuja kwa magoti hee atakaaaweze maisha yenyewe yalivyomagumu? kila mtu akasubiri downfall of my empire but they 4get niliwaambia (iam the empire on which sun never set)walicheka kwa dharau sana.hii tu ni kwa sababu niliweka mbali akili na ubongo kujadili siwezi sema nimesuceed sababu i have long a run to go.jitambue thamani yako
back to topic huyo dada ni mjinga sana ameshindwa kuchukua experience na matukio muhimu akachanganya akaamua shauri yake wanaume wa type hiyo huishia kufa maskini n ukicheza anakuua maskini tena mbaya mno aachane naye kabisa huwa wanaitwa mamas boy.mwogope mwanamme ambaye anaridhika na mwanamke kulisha familia yeye anasoma novel mwogope sana na asilimia 99.5 anakutumia tu na kukushikilia asianguke lakini hamna mapenzi ya dhati ,sasa basi mwambie we makini kama hataki kufa maskini.
 
Last edited by a moderator:
huyu jamaa inaonekana kichwa maji na girl friend wake anaakili kuli yeye aachane naye huyo mjinga mjinga atamuletea kesi kubwa zaidi ya hiyo
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom