Katazo la Rais Kusafiri Nje ya Nchi bila Vibali: Je, Halikiuki 'Separation of Powers'?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,571
Wanabodi,

Naomba kuanza na angalizo: Ukosoaji wowote, utaofanywa kwa kinachofanywa na serikali yetu, kama unatolewa in good faith, kwa nia ya kujenga na sio kubomoa, ukosoaji huu ukatoa ushauri wa the right thing to do, huitwa "constructive criticism" ambao ni ukosoaji mzuri, very healthy katika ujenzi wa taifa lolote la kidemokrasia linaloheshimu uhuru, haki na kufuata utawala wa sheria.

Serikali yoyote yenye nia ya dhati ujenzi wa taifa lake kwa kufuata misingi ya katiba nzuri na kuheshimu misingi ya haki binaadamu na utawala wa sheria!, inakuwa makini sana na hoja zozote zinazohusu katiba. Zikitokea kelele zozote zinazohusu ukiukwaji wa katiba au uminyaji wa demokrasia, serikali makini huzichukulia hoja hizi very serious, serikali yoyote inayopuuzia hoja za ukiukwaji wa haki zilizotolewa na katiba, then serikali hiyo ni ya ki imla, au ni ya kidikiteta!, na rais yoyote anayekiuka katiba aliyoapa kuilinda, huyo ni dikiteta.

Serikali nyingi za mataifa, zinazo heshimu katiba, na kufuata mfumo wa kidemokrasia na utawala wa sheria, zina mihimili mitatu ya dola ambayo ni Serikali, Bunge na Mahakama. Mihimili hii inatakiwa kuwa sawa kwa kufanya kazi kwa uhuru na kujitegemea bila kuingiliwa na Mhimili mwingine (independent) na wakati huo huo kila mhimili ukiwa ni mlinzi na mdhibiti wa mhimili mwenzake, (check and balance) ili mihimili mmoja usizidishe mamlaka yake na kuingilia mihimili mingine.

Kitendo cha rais wa nchi ambaye ni Mkuu wa mhimili mmoja wa dola, kutoa amri kwa mihimili mingine, ni kuingilia haki, uhuru na mamlaka za mihimili mingine, hivyo kukiuka ile kanuni ya "The Doctrine of Separation of Powers and Checks and Balances".

Nimehamasika Kuanzisha uzi huu, kufuatia mjadala wa amri ya rais Magufuli kuzuia safari za nje, kwa watumishi wa umma ambao pia imewakumba watumishi wa mhimili wa Bunge na watumishi wa muhimili wa Mahakama!.
kuna mihimili mitatu
1. bunge
2. mahakama
3. serikali

Pesa za kuendesha ShUGHULI zao zinatoka HAZINA .

Kuna wizara mahsusi zinazosimamia Mihimili hiyo. Unapojitahidi kutenganisha pia jitahidi kuhusianisha utafikia tamati nzuri
Mkuu Mahesabu hapa umeongea jambo la maana sana!, angalia nilivyowajibu hawa watu!.
Kwa ufahamu wako serekali ni nani????
Mtumishi wa watu na waserikali kunatofauti?
Ungesema ni kiongozi wa kisiasa hapo sawa!!
Mtumishi wa watu na waserikali kunatofauti?
Ungesema ni kiongozi wa kisiasa hapo sawa!!
kama sio mtumishi wa serikali mbona analipwa mshahara na serikali,,, we bwege kweli
najiuliza waziri mkuu au waziri ni mtumishi wa watu au?pia najiuliza mbunge wa kuteuliwa na rais ni mtumishi wa watu pia?halafu nikiangalia kwenye payroll ya serikali nauona mshahara wa mbunge...mfumo wetu unanichanginyi
Wabunge ni watumishi wa umma.
Zuio la Rais Magufuli linahusu watumishi wa umma.
sawa but analipwa na nani,
Sio kila anayelipwa na fedha za umma ni mtumishi wa serikali au mtumishi wa Umma, hata vyama vya siasa, watumishi wa vyama vya siasa, kikiwemo Chadema, wanalipwa kwa fedha za umma kupitia ruzuku, lakini hawa sio watumishi wa umma.

Rais wa nchi ni mkuu wa mhimili mmoja tuu wa dola ambao ni serikali, mkuu wa mhimili wa Bunge ni Spika na mkuu wa mhimili wa Mahakama ni Jaji Mkuu!. Kitendo cha rais wa nchi kutoa amri ya mihimili yote kuomba ruhusa ya kusafiri nje kwa watumishi wa bunge na mahakama bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi ni kuingilia uhuru ,haki na madaraka ya mihimili mingine ambayo rais hana mamlaka hayo, huku ni kwenda kinyume cha utawala bora!, ambako mimi nakuita ni sehemu tuu ya udikiteta wa Mhe. Rais John Pombe Joseph Magufuli!, kitendo cha watu wanaojua the principle of separation of powers, na checks and balance, hawakupaswa kulinyamazia hili!.

Rais wa nchi, Jaji Mkuu na Spika wa Bunge, ni watu wenye hadhi sawa as wakuu wa mihimili, lolote likitokea kwa rais, hao wanashika wadhifa wa urais kwa mujibu wa katiba, hivyo kitendo cha kumfanya Jaji Mkuu na Spika wa Bunge kuomba kibali cha kutimoza wajibu wao kwa Katibu Mkuu Kiongozi, sio tuu kinakiuka kanuni hii ya sepaations of powers, pekee, bali kinawadhalilisha, na kuwafanya washindwe kufanya checks na kumbalance rais anapovuka mipaka ya mamlaka yake!, kwa mwendo huu Magufuli anao anza nao, huko mbele nani atathubutu kumcheck au kumbalance?.

Kwa vile katazo la rais kuzuia safari za nje bila kibali, limetolewa kwa nia njema kabisa ili kuzuia safari za nje zisizo na tija na manufaa kwa taifa, ili kutunza hadhi na heshma ya mihimili ya dola, rais kama mkuu wa mhimili mmoja wa serikali, alipaswa kuwaita wale wakuu wa ile mihimili mingine, Spika na Jaji Mkuu, na kuwaelezea nia yake njema katika kuthibiti safari za ulaji, ili spika na yeye atoe amri kama hiyo kwa wabunge na watumishi wa bunge kuomba kibali kwa Spika kupitia kwa Katibu wa Bunge, na watumishi wa mahakama, kuomba kibali kwa Jaji Mkuu kupitia kwa Msajili wa Mahakama na ile amri ya rais iwahusu watumishi wa serikali kuu tuu na serikali za mitaa wakala na idara za serikali. Wabunge wapate vibali ofisi ya bunge na majaji na watumishi wa mahakama wapate vibali kwa Jaji Mkuu ili kuepusha kuingiliana majukumu kati ya mihimili hii!.

Watanzania tunapaswa kuwa waangalifu sana na hatua kama hizi na hili jambo sio la kulinyamazia hata kidogo, linabidi kukemewa kwa nguvu zote, kwa sababu madikiteta wengine wote duniani huanza hivi hivi kwa kulisupress Bunge, kisha atakuja kuisupress Mahakama, kisha ata supress the media na mitandao ya kijamii, na kumalizia na kuwa target individuals watakaonekana kuwa very vocal, or threat, kwa kuwatisha kama ilivyofanyika kwa Dr. Ulimboka, Kubenea na Kibanda, au msije kushanga, watu wakaja ku vanish into thin air, hata unywele usionekane!.

Kazi hii "doctrine of separation of powers", jukumu la mhimili wa serikali ni kuliwezesha bunge na mahakama kutimiza majukumu yake kwa kuipatia tuu pesa za uendeshaji na maendeleo, kwa mtindo wa "eyes on, hands off ", anachofanya rais Magufuli kwa mihimili hii ni "ayes on, hands on" kwa kutia mkono wake hadi jikoni, chumbani hadi kuchungulia uvunguni kwa wengine ambako huku ni kuuingilia.

Naomba kuwasilisha.

Heri ya Mwaka Mpya.
Paskali
 
Wanabodi,

Naomba kuanza na angalizo: Ukosoaji wowote, utaofanywa kwa kinachofanywa na serikali yetu, kama unatolewa in good faith, kwa nia ya kujenga na sio kubomoa, huu ni ukosoaji mzuri na ni very heathy kwa serikali yoyote yenye nia ya dhati ya kufuata katiba na kuheshimu utawala wa sheria!, kinyume cha hapo ni udikiteta!.

Kitendo cha Mkuu mmoja wa mihimili ya dola, kuingilia haki, uhuru na mamlaka za mihimili mingine, sio kukiuka ile kanuni ya Checks and Balances and The Separation of Powers?!.

Nimehamasika Kuanzisha uzi huu, kufuatia mjadala wa ami ya rais kuzuia safari za nje, pia imewakumba watumishi wa bunge na watumishi wa mahakama!.


Mkuu Mahesabu hapa umeongea jambo la maana sana!, angalia nilivyowajibu hawa watu!.







Sio kila anayelipwa na fedha za umma ni mtumishi wa serikali!, hata vyama, watumishi wote wa vyama vya siasa, kikiwemo Chadema, wanalipwa kwa fedha za umma kupitia ruzuku, hawa sio watumishi wa umma!.

Kuna kanuni za uendeshaji wa serikali zote dunia nzima, ambapo kuna mihimili mitatu, seikali bunge na mahakama!, rais wa nchi ni mkuu wa mhimili mmoja tuu wa serikali, mkuu wa bunge ni spika na mkuu wa mahakama ni Jaji Mkuu!. Kitendo cha rais wa nchi kutoa amri ya kutosafiri kwa watumishi wa bunge na mahakama bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi ni rais kuingilia uhuu na madaraka ya vyombo hivi, huku ni kwenda kinyume cha utawala bora!, mimi nakuita ni sehemu tuu ya udikiteta wa Mhe. Rais John Pombe Magufuli!, kitendo cha watu wanaojua the principle of separation of powers, hawakupaswa kulinyamazia hili!.

Kwa vile katazo la rais kuzui safari za nje bila kibali, limetolewa kwa nia njema ili kuzuia safari za nje zisizo na manufaa kwa taifa, rais alipaswa kuwaita Spika na Jaji Mkuu, ili spika na yeye atoe amri kama hiyo kwa wabunge na watumishi wa bunge kuomba kibali kwa Spika kupitia kwa Katibu wa Bunge, na watumishi wa mahakama, kuomba kibali kwa Jaji Mkuu kupitia kwa Msajili wa Mahakama ili ami ya rais iwahusu watumishi wa serikali tuu ikiwa ni seikali kuu na serikali za mitaa. Wabunge wapate vibali ofisi ya bunge na watumishi wa mahakama wapate vibali vya mahakama ili kuepusha kuingilia majukumu kati ya mihimili hii!.

Naomba kuwasilisha.

Heri ya Mwaka Mpya.
Pasco


WatanZania kwa wingi wetu tunautaka huwo Udikteta ili ututoe hapa, kama Raisi wa nchi mpaka leo hii hajasafiri ili kuokoa gharama hata kutoka tu nje ya Dar ukiondoa kwenda Dodoma mara moja kufungua Bunge, iweje Mbunge yeye asafiri kwa gharama zetu?
 
Mimi nimeshangaa kwamba hadi wabunge waombe ruksa?
na waseme safari zao zina manufaa gani kwa taifa?

ina maana hata safari binafsi now sio ruksa?

Ningependa kuwepo na utaratibu..na sio ruksa
mtu akitaka safari yake binafsi aambiwe utaratibu ukoje hasa kama hatumii pesa ya serikali
aufuate.....otherwise tupo China ya Mao.....
 
Mimi nimeshangaa kwamba hadi wabunge waombe ruksa?
na waseme safari zao zina manufaa gani kwa taifa?

ina maana hata safari binafsi now sio ruksa?

Ningependa kuwepo na utaratibu..na sio ruksa
mtu akitaka safari yake binafsi aambiwe utaratibu ukoje hasa kama hatumii pesa ya serikali
aufuate.....otherwise tupo China ya Mao.....


Kuomba ruhusa ni lazima kwa maana Mbunge kama Mfanyakazi mwingine analipwa na Serikali anapaswa kuwa ofisini na kuwahudumia wananchi, kama vile wafanyakazi wengine sasa kama anaondoka tu kwa utashi wake tuseme anasafiri na kwenda nje kwa miezi miwili kwa safari binafsi halafu mwisho wa mwezi analipwa mishahara kwa kazi gani?
 
Wanabodi,

Naomba kuanza na angalizo: Ukosoaji wowote, utaofanywa kwa kinachofanywa na serikali yetu, kama unatolewa in good faith, kwa nia ya kujenga na sio kubomoa, huu ni ukosoaji mzuri na ni very heathy kwa serikali yoyote yenye nia ya dhati ya kufuata katiba na kuheshimu utawala wa sheria!, kinyume cha hapo ni udikiteta!.

Kitendo cha Mkuu mmoja wa mihimili ya dola, kuingilia haki, uhuru na mamlaka za mihimili mingine, sio kukiuka ile kanuni ya Checks and Balances and The Separation of Powers?!.

Nimehamasika Kuanzisha uzi huu, kufuatia mjadala wa ami ya rais kuzuia safari za nje, pia imewakumba watumishi wa bunge na watumishi wa mahakama!.


Mkuu Mahesabu hapa umeongea jambo la maana sana!, angalia nilivyowajibu hawa watu!.







Sio kila anayelipwa na fedha za umma ni mtumishi wa serikali!, hata vyama, watumishi wote wa vyama vya siasa, kikiwemo Chadema, wanalipwa kwa fedha za umma kupitia ruzuku, hawa sio watumishi wa umma!.

Kuna kanuni za uendeshaji wa serikali zote dunia nzima, ambapo kuna mihimili mitatu, seikali bunge na mahakama!, rais wa nchi ni mkuu wa mhimili mmoja tuu wa serikali, mkuu wa bunge ni spika na mkuu wa mahakama ni Jaji Mkuu!. Kitendo cha rais wa nchi kutoa amri ya kutosafiri kwa watumishi wa bunge na mahakama bila kibali cha Katibu Mkuu Kiongozi ni rais kuingilia uhuu na madaraka ya vyombo hivi, huku ni kwenda kinyume cha utawala bora!, mimi nakuita ni sehemu tuu ya udikiteta wa Mhe. Rais John Pombe Magufuli!, kitendo cha watu wanaojua the principle of separation of powers, hawakupaswa kulinyamazia hili!.

Kwa vile katazo la rais kuzui safari za nje bila kibali, limetolewa kwa nia njema ili kuzuia safari za nje zisizo na manufaa kwa taifa, rais alipaswa kuwaita Spika na Jaji Mkuu, ili spika na yeye atoe amri kama hiyo kwa wabunge na watumishi wa bunge kuomba kibali kwa Spika kupitia kwa Katibu wa Bunge, na watumishi wa mahakama, kuomba kibali kwa Jaji Mkuu kupitia kwa Msajili wa Mahakama ili ami ya rais iwahusu watumishi wa serikali tuu ikiwa ni seikali kuu na serikali za mitaa. Wabunge wapate vibali ofisi ya bunge na watumishi wa mahakama wapate vibali vya mahakama ili kuepusha kuingilia majukumu kati ya mihimili hii!.

Naomba kuwasilisha.

Heri ya Mwaka Mpya.
Pasco
Msome hapa ndugu pandii
Kilichosababisha martha kuzuiwa ni kwamba alikuwa anatumia diplomatic passport kwa safari yake binafsi,hiyo paspot inalipiwa na serikali.sasa kama anataka kutumia hiyo paspot ni lazima apate kibali cha katibu wa bunge kutoka kwa katibu mkuu maana fedha inatoka hazina kulipia safari,lakini angetumia paspot binafsi asingezuiwa
Kama hujaelewa basi sawa.
 
Mimi nimeshangaa kwamba hadi wabunge waombe ruksa?
na waseme safari zao zina manufaa gani kwa taifa?

ina maana hata safari binafsi now sio ruksa?

Ningependa kuwepo na utaratibu..na sio ruksa
mtu akitaka safari yake binafsi aambiwe utaratibu ukoje hasa kama hatumii pesa ya serikali
aufuate.....otherwise tupo China ya Mao.....
Msome hapa pandii..........
Kilichosababisha martha kuzuiwa ni kwamba alikuwa anatumia diplomatic passport kwa safari yake binafsi,hiyo paspot inalipiwa na serikali.sasa kama anataka kutumia hiyo paspot ni lazima apate kibali cha katibu wa bunge kutoka kwa katibu mkuu maana fedha inatoka hazina kulipia safari,lakini angetumia paspot binafsi asingezuiwa
Ualimu shughuli aisee.................
 
Pasco.

Kabla ya kuanza kujenga hoja yako ulitakiwa kwanza upate ukweli kama Rais hajakaa na Spika na pia Jaji Mkuu ili kulijadili suala la safari za nje kwa watumishi wa umma.

Kumbuka tangazo lilikuwa specific. Halikusema watumishi wa serikali bali lilisema watumishi wa umma.

Rais ni taasisi na kwa maana hii, kabla hajafanya jambo lolote hupata ushauri wa kiutaratibu, kanuni, sheria, hekima na busara.
 
Kila anayetumia fedha ya umma (Kodi) ni mfanyakazi wa umma.Umma lazima ujue kinachompeleka huko nje ya nchi.Awe kiongozi wa Chama kinachotumia ruzuku ya kodi,mbunge,mfanyakazi wa serikali au mahakama.

Pia ni udhibiti wa matumizi holela ya pesa za kigeni.Hebu fikiria mbunge anaenda kubadilisha pesa za kigeni na kwenda shopping na mbunge mwenzie kwenda kufanya ufuska dubai hadi wanazalishana.Unaona thamani ya shilingi dhidi ya dola inashuka kisa kuna watu wanatumia dola kwenda nje kufanyana.Safari zisizo na tija lazima zidhibitiwe.
 
Rais angefanya kitu kimoja tu rahisi, kuwaamuru wote wenye diplomat passport wazirudishe kwanza na wakiwa na safari inayohitaji diplomat wapeleke maelezo, safar binafs wawaache ila waweke mfumo wa mahudhurio kuanzia bungen ili kudhibiti utoro, sasa mtu akikosekana eneo la kazi mpaka bungeni ni kukata mshahara tu mf. kwa siku moja kwa mbunge akikosekana bila tuhusa maalum iwe mil 1 tu nafikiri tutaheshimiana. Rais ashasema nendeni vijijin mkatatue kero za wananchi nyinyi mmekomaa kusafiri na kudhurura mijini tu wakat wananchi wanakufa huko vijijini.
Ikiwezekana tena kuwe na mfumo wa kuomba ruhusa kutoka jimboni kwako na lazima kuwe na saini kuanzia mia 2 zinazoruhusu wewe kusafiri nje kwa siku maalum, ole wako ughushi saini....
Suluhisho ni katiba mpya tu yenye meno makali kwa wajanjawajanja.
 
Last edited:
WatanZania kwa wingi wetu tunautaka huwo Udikteta ili ututoe hapa, kama Raisi wa nchi mpaka leo hii hajasafiri ili kuokoa gharama hata kutoka tu nje ya Dar ukiondoa kwenda Dodoma mara moja kufungua Bunge, iweje Mbunge yeye asafiri kwa gharama zetu?
Rais anaweza asisafiri kwenda nje kwa sababu zake Kama alivyokuwa Jomo Kenyata(1963-77). Hoja hapa ni kuwa kwa maelekezo yaliyotolewa, ni sawa kumzuia Mh Mbunge?
 
Kumbuka kutunzwa kuna masharti. Utunzwaji usio na masharti haupo duniani. USA inapotoa misaada kwa Tanzania jua kuna masharti yake yaliyofichama.

Tuache masuala ya Kiutawala wa serikali, tuangalie mfano rahisi wa familia.

Kama mtoto anaishi kwako kama mzazi, hata akiwa na fedha zake haiwezekani akaenda disco usiku bila kuomba ruhusa. Kama hataki anahamia kwake ili awe huru. Kwa mbunge kwa vile anapata angalau senti tano toka serikalini, hawezi kufanya atakalo kwa vile ni mhimili mwingine. Hata kama ni safari ya binafsi, bado mwisho wa mwezi anapokea mshahara. Kama anataka kuwa huru, anachukua likizo bila malipo.
 
Kwani hiyo mihimili mingine miwili iliyobakia hua inazalisha hela zake yenyewe? Hela si za serikali na ndiyo inayopaswa kuhakikisha kua matumizi yake ni sahihi kulingana hali na uwezo uliopo? Kuna haja gani ya kuendekeza safari za nje kwa pesa ya walipa kodi ambao wengi wao ni maskini?
 
WatanZania kwa wingi wetu tunautaka huwo Udikteta ili ututoe hapa, kama Raisi wa nchi mpaka leo hii hajasafiri ili kuokoa gharama hata kutoka tu nje ya Dar ukiondoa kwenda Dodoma mara moja kufungua Bunge, iweje Mbunge yeye asafiri kwa gharama zetu?

Taarifa zilizopo Hata huko ADDIS kwa mkutanoo wa AU January hii hatokwenda, atakwenda Makamu wa Rais na ujumbe mdogo.
 
Wanabodi,
....

Kuna kanuni za uendeshaji wa serikali zote dunia nzima, ambapo kuna mihimili mitatu, seikali bunge na mahakama!, rais wa nchi ni mkuu wa mhimili mmoja tuu wa serikali, mkuu wa bunge ni spika na mkuu wa mahakama ni Jaji Mkuu!.

....
Naomba kuwasilisha.

Heri ya Mwaka Mpya.
Pasco

Kwa mujibu wa katiba;
Rais atakuwa mkuu wa NCHI,
Kiongozi wa Serikali na
Amiri Jeshi Mkuu.

Tusisahau ukuu wa Rais kikatiba.
 
Udikteta wa Paul Kagame umeipatia Rwanda mafanikio yanayosifiwa na kila mnyarwanda, alianza na kusimika misingi ya udikteta kwanza, usitupe taka hapa na ukitupa utakamatwa na kufungwa, usifanye jambo fulani sasa ole wako ufanye lile lililokatazwa. Zinaweza kuwepo checks and balances na kila upande ukawa na haki ya kutimiza majukumu yake kikatiba lakini naamini katazo la rais lilielezewa kiufasaha sana bungeni pale alipoonyesha ni jinsi gani safari za nje zinavyochangia katika matumizi mengi yenye madhara ya moja kwa moja kwa masikini walio wengi. Naamini mleta uzi aliiona ile clip ya rais alipokwenda Muhimbili akakuta wagonjwa wengi tu wanalala chini na mashine muhimu zikiwa zimeharibika halafu eti zile za hospitali binafsi zinafanya kazi!, kwa uchungu sana akasema vifaa muhimu vya matibabu havifanyi kazi halafu watu wanasafiri kwenda Ulaya!!. Watu wanazitumia vibaya hizo checks and balances kwa kuzua safari za nje, wengine wanapeleka nyumba ndogo zao kwa sababu tu ya vyeo vyao!. Ni hii tabia ya kusafiri hovyo haijaanzia Tanzania, Nigeria ni mabingwa wa safari za nje ambazo hazina faida kwa Mnigeria maskini. Rais anashughulika na shida za watu wa chini kwa kuhakikisha kile kinachopatikana kinawapatia faida walio wengi na sio wasomi wachache wenye kuishi kwenye majiji makubwa. Ni maamuzi ya kizalendo na kishujaa kutoa agizo la watu kutosafiri bila ya kuwa na sababu za msingi. Tulizoea kula raha, tulizoea kula bata bila ya kuwafikiria walio wengi.
 
Back
Top Bottom