figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,890
Mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali imesababisha madhara makubwa ikiwa ni pamoja na kujeruhi watu Saba na kubomoa nyumba 59 katika kijiji cha KIBAONI na ILALA – NGULU mkoani KATAVI.
Mkuu wa Wilaya ya MLELE, RACHIEL KASANDA amethibitisha kubomoka na kuezuliwa paa kwa nyumba hizo na kuwatahadharisha wakazi wa wilaya ya MLELE kuwa makini na mvua zinazoendelea kunyesha.
Mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Kakuni amesema shule hiyo imeathiriwa na Mvua hizo.