KATANGA: Je, ni tamaa ya hazina dhidi ya Uzalendo?

zitto junior

JF-Expert Member
Oct 7, 2013
19,005
28,627
Habari za mchana wana JF, hivi Karibuni nimekuwa nafuatilia kwa ukaribu historia ya siasa za maziwa makuu ila nikagundua kitu fulani kilichonishangaza kidogo nikaona nilete mjadala kwa great thinkers tujadili pamoja.
images (8).jpg

Utangulizi
Kama tunavyofahamu DRC ni nchi iliyojaaliwa kuwa na maliasili ya kila aina kuanzia Gesi mpaka madini, ardhi nzuri, mvua za kutosha na mito/maziwa ya kutosha. Lakini changamoto kubwa imekua migogoro isiyoisha ama isiyo na nia ya kumalizwa sababu ya maslahi fulani wanayovuna kwenye utajiri wa nchi hii.

Hapo nyuma kidogo nimewahi kuleta uzi kuhusu 2nd congo war na jinsi majeshi ya Kitutsi yaani Banyamulenge, Rwanda,UG na Burundi walivyoiteka mashariki ya Congo na kujaribu kumpindua Rais Laurent Desire Kabila August 1998 kupitia operation kitona huko Kinshasa ambayo awali ilifeli kutokana na kuingia vitani kwa majeshi na ufadhili wa Zimbabwe na Angola pale kinshasa.

Nilipata maoni mengi sana kuonyesha Rwanda ilikua inatumika na wazungu, ama Rwanda iliingia kupora mali za DRC na maoni ya upande huo lakini tukisoma zaidi leo tutaangalia upande wa pili wa shilingi. Je majeshi yaliyoingia upande wa Kabilw yaliongozwa na tamaa ya hazina ama uzalendo?

KATANGA
images (2).jpg

Hili ni jimbo lililopo kusini mwa DRC na kiufupi tu ndio eneo lenye utajiri mkubwa sana wa madini DRC na liliwahi kuchangia 80% ya bajeti ya serikali ya DRC kila mwaka. Inazalisha madini kma dhahabu,almasi,shaba,fedha,cobalt,platinum,nickel n.k. Wakati vita inaanza mwaka 1998, DRC ilikua inazalisha Almasi yenye thamani ya Tsh 1.2 Trillion kwa mwaka achilia mbali zilizokuwa zinatoroshwa kifisadi mipakani.

Katanga ina 34% ya hazina ya madini ya Cobalt duniani ambayo hutengenezea battery za simu &Laptop, Engine za ndege, mashine za kuchakata gesi n.k. pia 10% ya hazina ya shaba duniani ipo Katanga. Kwa utajiri huu makampuni mengi ya madini yalikua pale Lubumbashi kusafirisha madini dunia nzima, kiufupi walipaita ''Kitovu cha madini ya DRC''.

Baada ya kidogo kupata picha kuhusu eneo hili sasa turudi kwenye kisa cha 2nd Congo war ama ''Vita kuu ya dunia ya Africa'' sababu ilihusisha nchi 13 kwenye mapigano ambapo upande mmoja walikuwepo Burundi,UG na Rwanda dhidi ya DRC, Sudan,Chad,Angola,Zimbabwe, Namibia,Libya,CAR,Ethiopia, Eritrea n.k

Kwa summary tu majeshi ya Rwanda na washirika wao yalipovamia DRC ili kumtoa Kabila waliyemuweka madarakani takribani mwaka mmoja tu uliopita, yaliteka haraka majimbo yote ya mashariki na kaskazini kuanzia Kivu zote mbili, Province Oriental na Manyema hivyo walikua wanaelekea kuteka Jimbo la Katanga ili kupata nguvu ya kiuchumi ya kuwawezesha kuendesha vita, kuparalyse nguvu ya kabila, na kuwapa njia fupi zaidi ya kufika Kinshasa.

Kabla ya kufika lubumbashi ambapo ni makao makuu ya Katanga, mapigano makali yalizuka kwenye mji muhimu wa Kindu ambapo ndio geti la kuelekea kusini mwa DRC palipo na jimbo la Katanga. Baada ya mtanange mzito kwa siku kadhaa Majeshi ya washirika wa Rwanda yalifanikiwa kuuteka mji huu October 1998, hivyo safari rasmi ya kuteka Hazina ya congo ilikua imeanza rasmi.

images (4).jpg
 
ALLIANCE INAJENGWA
Kufuatia hofu ya Hazina ama Roho ya DRC kuishia mikononi mwa kagame, ilibidi Zimbabwe na Angola ziingilie kwa kumsaidia Kabila na serikali yake dhidi ya majeshi ya waasi na washirika wao wa Rwanda.
images (9).jpg

Ndege vita
Mpaka vita inaisha Zimbabwe na Angola zilitoa wanajeshi zaidi ya elfu 50. Kwa kufahamu askari wa wavamizi walikua wababe kwenye vita za ardhini, Mbinu mpya ilisukwa ambapo zimbabwe ilipeleka ndege vita za kutosha hku Angola ikipeleka Helicopter ili kuweza kupambana nao kutokea angani.

Hatimaye mbinu hii ilizaa matunda ambapo majeshi haya yaliweza zuia nguvu ya waasi kuiteka miji muhimu kma Mbujimayi na lubumbashi. Licha ya kwamba walikuja kuteka mji muhimu wa pweto uliopo mashariki ya Katanga ila majeshi ya zimbabwe yalisimama imara mpaka mwisho ambapo walisaini makubaliano ya amani.
Kiini cha uzi huu ni hili swali Je Zimbabwe na washirika wake walisukumwa na uzalendo ama ujasirialamali?

Zimbabwe
Kupitia vyanzo mbalimbali inasemekana kwenye 1st Congo war ile ya kumng'oa Mobutu, zimbabwe ilikua inaidai DRC $400 Million (Tsh 1 Trillioni ya sasa) kama gharama za kusaidia vita. Hivyo Mugabe aliogopa serikali ya Kabila ikipinduliwa atakosa malipo yake hayo mazito.

Sababu ya Pili ni kwamba Zimbabwe iliahidiwa kupewa migodi mikubwa huko Kasai, pia waliingia ubia na kampuni ya mabeberu ya ORYX ili watoe utaalamu wa uchimbaji na masoko, then wagawane faida Pasu kwa pasu. Kampuni Mama ya OSLEG ikaanzishwa!! Ukumbuke mkataba ulikua wa miaka 25 wa kuchimba kwenye migodi miwili mikubwa zaidi ya Almasi huko Katanga na kasai. Hivyo Zimbabwe iliweza kufaidika zaidi na vita hii kiuchumi kuliko hata wavamizi wa kutoka Afrika mashariki!!
images (7).jpg

Moja ya migodi huko Katanga

ANGOLA
1. Sababu ya kwanza ya kuingia kwenye vita ni hofu ya Kagame kushirikiana na UNITA ya Savimbi kuivamia Angola.
Ikumbukwe kwenye uzi wa Operation kitona nilieleza jinsi Savimbi alivyoshiriki kusaidia majeshi ya kagame kutoroka Angola kwa kuwapa ground cover kuingia nchini humo, hivyo kama Jimbo la Katanga lingeangukia mikononi mwa waasi basi Savimbi naye angepewa migodi na ukizingatia Jimbo hilo linapakana na Angola basi usalama wa nchi hiyo ungekuwa shakani.

2. Sababu ya pili, kama wenzao wa zimbabwe, nao walipewa migodi kadhaa huko Tshipaka ya kuchimba Almasi na dhahabu. Achilia mbali walipewa kitalu Huko pwani ya DRC kutafiti mafuta kwa sharti watagawana faida!! Kiufupi wanadiplomasia na majenerali wa Angola waligeuka wafanyabiashara wa kuuza madini ulimwenguni. Na ziliendesha mpaka bajeti za wizara za ulinzi kwa malipo ya kuilinda Katanga isiangukie mikononi mwa Kagame!!

Nimeweka nyaraka hapo chini unaweza zipitia kwa takwimu zote na pesa walizoingiza mpka vita inaisha kwa Pande zote mbili kuvuna madini ya DRC.

Ila kwa mtazamo wenu wana JF intelligence

1. Je walisukumwa na Uzalendo ama Ujasiriamali?
2. Nini hatma ya kuzuia ''Mwizi'' huku na wewe unaiba kitu kilekile?
3. Je hatma ya uzalendo Afrika ni upi kma wanaopinga uchafu nao wanaishia kufanya yaleyale?
4. Je Mugabe ni Pan Africanist kama alivyojinasibu?

Karibuni kwa mjadala
 
Pdf zinagoma ku upload ila google document zifuatazo.

1. Conflict of Interests or Interests in
Conflict? Diamonds & War in the DRC by Ingrid Samset.

2. The great African war - P. Rentyjens

3.Africa's world war By Gerard prunier
Unaweza kukisoma bure humu
Africa's world war : Congo, the Rwandan genocide, and the making of a continental catastrophe : Prunier, Gérard, author : Free Download, Borrow, and Streaming : Internet Archive

Article 1. War turns commercial

2. Congo’s hidden war

Pia ripoti juu ya Katanga
 

Attachments

  • katanga-the-congo-s-forgotten-crisis.pdf
    698.2 KB · Views: 59
Habari za mchana wana JF, hivi Karibuni nimekuwa nafuatilia kwa ukaribu historia ya siasa za maziwa makuu ila nikagundua kitu fulani kilichonishangaza kidogo nikaona nilete mjadala kwa great thinkers tujadili pamoja.
View attachment 1457372
Utangulizi
Kama tunavyofahamu DRC ni nchi iliyojaaliwa kuwa na maliasili ya kila aina kuanzia Gesi mpaka madini, ardhi nzuri, mvua za kutosha na mito/maziwa ya kutosha. Lakini changamoto kubwa imekua migogoro isiyoisha ama isiyo na nia ya kumalizwa sababu ya maslahi fulani wanayovuna kwenye utajiri wa nchi hii.

Hapo nyuma kidogo nimewahi kuleta uzi kuhusu 2nd congo war na jinsi majeshi ya Kitutsi yaani Banyamulenge, Rwanda,UG na Burundi walivyoiteka mashariki ya Congo na kujaribu kumpindua Rais Laurent Desire Kabila August 1998 kupitia operation kitona huko Kinshasa ambayo awali ilifeli kutokana na kuingia vitani kwa majeshi na ufadhili wa Zimbabwe na Angola pale kinshasa.

Nilipata maoni mengi sana kuonyesha Rwanda ilikua inatumika na wazungu, ama Rwanda iliingia kupora mali za DRC na maoni ya upande huo lakini tukisoma zaidi leo tutaangalia upande wa pili wa shilingi. Je majeshi yaliyoingia upande wa Kabilw yaliongozwa na tamaa ya hazina ama uzalendo?

KATANGA
View attachment 1457371
Hili ni jimbo lililopo kusini mwa DRC na kiufupi tu ndio eneo lenye utajiri mkubwa sana wa madini DRC na liliwahi kuchangia 80% ya bajeti ya serikali ya DRC kila mwaka. Inazalisha madini kma dhahabu,almasi,shaba,fedha,cobalt,platinum,nickel n.k. Wakati vita inaanza mwaka 1998, DRC ilikua inazalisha Almasi yenye thamani ya Tsh 1.2 Trillion kwa mwaka achilia mbali zilizokuwa zinatoroshwa kifisadi mipakani.

Katanga ina 34% ya hazina ya madini ya Cobalt duniani ambayo hutengenezea battery za simu &Laptop, Engine za ndege, mashine za kuchakata gesi n.k. pia 10% ya hazina ya shaba duniani ipo Katanga. Kwa utajiri huu makampuni mengi ya madini yalikua pale Lubumbashi kusafirisha madini dunia nzima, kiufupi walipaita ''Kitovu cha madini ya DRC''.

Baada ya kidogo kupata picha kuhusu eneo hili sasa turudi kwenye kisa cha 2nd Congo war ama ''Vita kuu ya dunia ya Africa'' sababu ilihusisha nchi 13 kwenye mapigano ambapo upande mmoja walikuwepo Burundi,UG na Rwanda dhidi ya DRC, Sudan,Chad,Angola,Zimbabwe, Namibia,Libya,CAR,Ethiopia, Eritrea n.k

Kwa summary tu majeshi ya Rwanda na washirika wao yalipovamia DRC ili kumtoa Kabila waliyemuweka madarakani takribani mwaka mmoja tu uliopita, yaliteka haraka majimbo yote ya mashariki na kaskazini kuanzia Kivu zote mbili, Province Oriental na Manyema hivyo walikua wanaelekea kuteka Jimbo la Katanga ili kupata nguvu ya kiuchumi ya kuwawezesha kuendesha vita, kuparalyse nguvu ya kabila, na kuwapa njia fupi zaidi ya kufika Kinshasa.

Kabla ya kufika lubumbashi ambapo ni makao makuu ya Katanga, mapigano makali yalizuka kwenye mji muhimu wa Kindu ambapo ndio geti la kuelekea kusini mwa DRC palipo na jimbo la Katanga. Baada ya mtanange mzito kwa siku kadhaa Majeshi ya washirika wa Rwanda yalifanikiwa kuuteka mji huu October 1998, hivyo safari rasmi ya kuteka Hazina ya congo ilikua imeanza rasmi.

View attachment 1457378

ZITTO Hii imekaajeniitumiwa na mtu


Waafrica siku zote tunajizika wenyewe zito na wenzake wapo Kama wale watu ambao wanamtaka dereva wa gari Aliebeba abiria ndani ya gari ambalo liko speed so wamemsimamisha dereva hajasimama so wanaona ili wampate Basi itabidi wajitaid gar ipate ajali bila kujal abilia waliomo ndan wao wanacho jali ni dereva atoke hayo mengine Sio inshu kwao Sasa leo sukari hamna sidhan Kama magufuli anakosa sukari yeye Ila wananch wa kawaida ndio wanao angaika OGOPA PROPAGANDA ACHA UPOTOSHAJI TETEA TANZANIA NYAMAZISHA MAADUI WETu
 
Angola wana interaction kubwa sana na DRC so uwepo wao naona kama umejengwa na misingi ya ujirani refer mikono ya Mobutu vita vya wenyewe kwa wenyewe Angola kati ya UNITA na MPLA : UNITA walikuwa bega kwa bega na Mobutu wakati Kabila akiwa anti Mobotu and also anti UNITA

And hence naweza Conclude kwamba Angola walimfuata mshirika wao kumsaidia , Mobutu alieondolewa madarakani alikuwa adui yao i.e serikali ya Angola chini ya MPLA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ZITTO Hii imekaajeniitumiwa na mtu


Waafrica siku zote tunajizika wenyewe zito na wenzake wapo Kama wale watu ambao wanamtaka dereva wa gari Aliebeba abiria ndani ya gari ambalo liko speed so wamemsimamisha dereva hajasimama so wanaona ili wampate Basi itabidi wajitaid gar ipate ajali bila kujal abilia waliomo ndan wao wanacho jali ni dereva atoke hayo mengine Sio inshu kwao Sasa leo sukari hamna sidhan Kama magufuli anakosa sukari yeye Ila wananch wa kawaida ndio wanao angaika OGOPA PROPAGANDA ACHA UPOTOSHAJI TETEA TANZANIA NYAMAZISHA MAADUI WETu
Mkuu hii hoja haihusiani na mada, nadhani ingefaa kama ikiwekwa jukwaa la siasa then huyo Zitto atakujibu.
 
Asante kwa makala nzuri mkuu, ni kweli kama ulivyoandika kwamba hayo mataifa ya Angola na Zimbabwe yalinufaika sana na vita huko Drc.

Ila tambua Drc kama mwanachama wa SADC ilikuwa na haki ya kuomba msaada maana ilivamiwa na nchi hasimu zisizo wanachama wa SADC hivyo Kabila na serikali yake walikuwa sahihi kuomba msaada wa kijeshi kutoka SADC.

Lakini mkuu lazima tukubali kuwa kama isingekua uingiliaji kijeshi wa hayo mataifa basi Drc ingepasuka vipande vipande na kuibuka "viji nchi" vinavyodhibitiwa na wapiganaji ambavyo vingegeuka maficho ya magaidi, magenge ya wahalifu ambao wangehatarisha usalama wa eneo lote la maziwa makuu.

Kwa mgawanyiko huo ambao ungetokea ina maana ile ndoto ya waasisi wa Africa ya kuiunganisha Africa ingekuwa imezikwa rasmi.

Pia lazima tukiri ukweli kwamba mali walizovuna Angola na Zimbabwe huko Drc ni kidogo sana tena sana ukilinganisha na gharama ambazo raia wa Drc wangelipa iwapo nchi yao ingeangukia mikononi mwa wale wavamizi.

Hayo ya uvunaji wa maliasili ya Drc yaliyofanyika naweza kuyaita ni gharama za vita (Costs of war) ambazo haziwezi kuepukika na Drc haikuwa na namna nyingine ya kulipa zaidi ya kutumia rasilimali zake.

Tunaweza kuhitimisha kwa kusema ni kweli ile Vita iliyanufaisha yale mataifa ila pia iliiokoa Drc kutoka mikononi mwa wavamizi waliojawa na visasi, chuki, ukabila (Utusi na Uhutu) ambao ni vigumu kutabiri wangelipeleka wapi lile taifa.

Hivyo Marehemu Mugabe na Rais mstaafu wa Angola( Dos Santos) walifanya kitendo cha kizalendo kuisaidia Drc, hayo ya kunufaika na rasilimali za Drc ni gharama za vita ambazo haziepukiki maana vita ni gharama (gharam ya uhai, fedha, silaha, chakula na mengine mengi).
 
ALLIANCE INAJENGWA
Kufuatia hofu ya Hazina ama Roho ya DRC kuishia mikononi mwa kagame, ilibidi Zimbabwe na Angola ziingilie kwa kumsaidia Kabila na serikali yake dhidi ya majeshi ya waasi na washirika wao wa Rwanda.
View attachment 1457388
Ndege vita
Mpaka vita inaisha Zimbabwe na Angola zilitoa wanajeshi zaidi ya elfu 50. Kwa kufahamu askari wa wavamizi walikua wababe kwenye vita za ardhini, Mbinu mpya ilisukwa ambapo zimbabwe ilipeleka ndege vita za kutosha hku Angola ikipeleka Helicopter ili kuweza kupambana nao kutokea angani.

Hatimaye mbinu hii ilizaa matunda ambapo majeshi haya yaliweza zuia nguvu ya waasi kuiteka miji muhimu kma Mbujimayi na lubumbashi. Licha ya kwamba walikuja kuteka mji muhimu wa pweto uliopo mashariki ya Katanga ila majeshi ya zimbabwe yalisimama imara mpaka mwisho ambapo walisaini makubaliano ya amani.
Kiini cha uzi huu ni hili swali Je Zimbabwe na washirika wake walisukumwa na uzalendo ama ujasirialamali?

Zimbabwe
Kupitia vyanzo mbalimbali inasemekana kwenye 1st Congo war ile ya kumng'oa Mobutu, zimbabwe ilikua inaidai DRC $400 Million (Tsh 1 Trillioni ya sasa) kama gharama za kusaidia vita. Hivyo Mugabe aliogopa serikali ya Kabila ikipinduliwa atakosa malipo yake hayo mazito.

Sababu ya Pili ni kwamba Zimbabwe iliahidiwa kupewa migodi mikubwa huko Kasai, pia waliingia ubia na kampuni ya mabeberu ya ORYX ili watoe utaalamu wa uchimbaji na masoko, then wagawane faida Pasu kwa pasu. Kampuni Mama ya OSLEG ikaanzishwa!! Ukumbuke mkataba ulikua wa miaka 25 wa kuchimba kwenye migodi miwili mikubwa zaidi ya Almasi huko Katanga na kasai. Hivyo Zimbabwe iliweza kufaidika zaidi na vita hii kiuchumi kuliko hata wavamizi wa kutoka Afrika mashariki!!
View attachment 1457377
Moja ya migodi huko Katanga

ANGOLA
1. Sababu ya kwanza ya kuingia kwenye vita ni hofu ya Kagame kushirikiana na UNITA ya Savimbi kuivamia Angola.
Ikumbukwe kwenye uzi wa Operation kitona nilieleza jinsi Savimbi alivyoshiriki kusaidia majeshi ya kagame kutoroka Angola kwa kuwapa ground cover kuingia nchini humo, hivyo kama Jimbo la Katanga lingeangukia mikononi mwa waasi basi Savimbi naye angepewa migodi na ukizingatia Jimbo hilo linapakana na Angola basi usalama wa nchi hiyo ungekuwa shakani.

2. Sababu ya pili, kama wenzao wa zimbabwe, nao walipewa migodi kadhaa huko Tshipaka ya kuchimba Almasi na dhahabu. Achilia mbali walipewa kitalu Huko pwani ya DRC kutafiti mafuta kwa sharti watagawana faida!! Kiufupi wanadiplomasia na majenerali wa Angola waligeuka wafanyabiashara wa kuuza madini ulimwenguni. Na ziliendesha mpaka bajeti za wizara za ulinzi kwa malipo ya kuilinda Katanga isiangukie mikononi mwa Kagame!!

Nimeweka nyaraka hapo chini unaweza zipitia kwa takwimu zote na pesa walizoingiza mpka vita inaisha kwa Pande zote mbili kuvuna madini ya DRC.

Ila kwa mtazamo wenu wana JF intelligence

1. Je walisukumwa na Uzalendo ama Ujasiriamali?
2. Nini hatma ya kuzuia ''Mwizi'' huku na wewe unaiba kitu kilekile?
3. Je hatma ya uzalendo Afrika ni upi kma wanaopinga uchafu nao wanaishia kufanya yaleyale?
4. Je Mugabe ni Pan Africanist kama alivyojinasibu?

Karibuni kwa mjadala
Nimeamua kulike tu kesho nitarudi
 
Scratch my back, I scratch your back.

Ndiyo mfumo wa maisha.
Ni kama biashara zingine mali kauli!

Eti kuna African Union?
Itoke wapi? wakati Mr Slim & co wana akili sawa na beberu...

Everyday is Saturday.......................... :cool:
 
Angola wana interaction kubwa sana na DRC so uwepo wao naona kama umejengwa na misingi ya ujirani refer mikono ya Mobutu vita vya wenyewe kwa wenyewe Angola kati ya UNITA na MPLA : UNITA walikuwa bega kwa bega na Mobutu wakati Kabila akiwa anti Mobotu and also anti UNITA

And hence naweza Conclude kwamba Angola walimfuata mshirika wao kumsaidia , Mobutu alieondolewa madarakani alikuwa adui yao i.e serikali ya Angola chini ya MPLA

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini mkuu siasa hazina adui wa kudumu sababu hata Kagame pia alipambana dhidi ya UNITA kwenye vita ya kumng'oa Mobutu je mbona bado walishirikiana na hao UNITA kwenye Hii vita ya pili? Kwanini Angola waogope Kagame akishinda ilihali vita ya kwanza hawakuogopa kuwa atawasaidia UNITA?

Ikumbukwe vita ya kwanza askari wapinzani wa serikali za Burundi na Rwanda yaani CNDD na FDLR walikua upande wa Mobutu na UNITA ila vita hii ya kumng'oa Kabila mbona bado Angola ilitoa mafunzo na silaha kwa hao Wahutu ili wapambane na majeshi ya kina kagame?

Je huoni ni kisingizio tu ili nao wavune rasilimali?
 
Hivyo Marehemu Mugabe na Rais mstaafu wa Angola( Dos Santos) walifanya kitendo cha kizalendo kuisaidia Drc, hayo ya kunufaika na rasilimali za Drc ni gharama za vita ambazo haziepukiki maana vita ni gharama (gharam ya uhai, fedha, silaha, chakula na mengine mengi).
Mkuu Nashukuru kwa nondo zako nimekuelewa sawia kabisa, ila kwa faida ya mjadala utusaidie yafuatayo.
1. Kama hoja ni kuogopa mpasuko wa DRC kma nchi itaangukia kwa Wavamizi ilikuwaje vita ya kumpindua Mobutu hawakuwa na hiyo hofu? Ina maana hofu ya vikundi vya waasi imekuja kipindi kabila anatolewa pekee na sio Mobutu?

2. Hoja ya kwamba ni gharama za vita, je kuna faida gani ya kuhofu wavamizi kunyonya mali ilihali na wewe ukienda ikomboa DRC unanyonya zile zile mali? Je hapo ni uzalendo au kuwahi tu fursa.

3. Lakini mkuu kuna ushahidi kwamba hata wakati wa Kabila magenge mengi ya uhalifu yalianzishwa na mengi yalipewa support na Kabila mwenyewe mfano Mai Mai ya Katanga kwa hoja kwamba ikitokea wavamizi basi wacheleweshwe na hao rebels. Ikiwa na maana makundi ya waasi yapo kimkakati kma buffer zone.

Tuwekane sawa
 
Mkuu Nashukuru kwa nondo zako nimekuelewa sawia kabisa, ila kwa faida ya mjadala utusaidie yafuatayo.
1. Kama hoja ni kuogopa mpasuko wa DRC kma nchi itaangukia kwa Wavamizi ilikuwaje vita ya kumpindua Mobutu hawakuwa na hiyo hofu? Ina maana hofu ya vikundi vya waasi imekuja kipindi kabila anatolewa pekee na sio Mobutu?

2. Hoja ya kwamba ni gharama za vita, je kuna faida gani ya kuhofu wavamizi kunyonya mali ilihali na wewe ukienda ikomboa DRC unanyonya zile zile mali? Je hapo ni uzalendo au kuwahi tu fursa.

3. Lakini mkuu kuna ushahidi kwamba hata wakati wa Kabila magenge mengi ya uhalifu yalianzishwa na mengi yalipewa support na Kabila mwenyewe mfano Mai Mai ya Katanga kwa hoja kwamba ikitokea wavamizi basi wacheleweshwe na hao rebels. Ikiwa na maana makundi ya waasi yapo kimkakati kma buffer zone.

Tuwekane sawa
Ile Vita ya kwanza ya kumpindua Mobutu iliwaleta pamoja mahasimu wa Mobutu na wafadhili wao.

Hata kundi la waasi la AFDL lilikuwa muungano wa makundi mengi kwa ajenda moja ya kumg'oa Mobutu, hata mataifa ya Rwanda, Angola, Uganda na Zimbabwe wote walikuwa na ajenda moja iliyowaunganisha yaani kumg'oa Mobutu.

Kwenye Vita vya pili, ule mpasuko uliotokea ulizalisha makundi mengi huko huku kila nchi ikihodhi makundi kadhaa kwa maslahi yake, jambo ambalo lingekuwa rahisi kuleta mpasuko wa nchi.

Rwanda ililidhibiti kundi la RCD ambalo lilishikilia maeneo makubwa huko mashariki hivyo ingekuwa rahisi kulimega hilo eneo.

Uganda iliunga mkono vikundi vya waasi vilivyodhibiti maeneo makubwa huko Ituri na baadhi ya maeneo ya Kisangani. Huu udhibiti ulichochea uhasama wa Wahema na Walendu maana Uganda iliwapendelea Wahema huko Ituri huku ikifumbia macho vitendo vya jina walivyofanyiwa Walendu, kama mgawanyiko ungetokea huenda hayo maeneo yangemegwa.

Hayo mataifa (Rwanda na Uganda) yalikuwa karibu sana kuipasua Drc kwa tamaa zao , japo pia sidhani kama wangeweza kuyadhibiti hayo maeneo sana sana usalama ungezidi kuzorota huko.

Hayo makundi yaliyoanzishwa na Kabila yalihusisha zaidi raia wa hayo maeneo kama njia ya kujilinda kutoka kwa majeshi vamizi ya nchi jirani, pia maadamu serikali haikuwa na uwezo wa kudhibiti kila eneo sababu ya ukubwa wa nchi,hiyo ilikuwa njia pekee ya kueneza udhibiti wa serikali kipindi hicho. Japo kwa sasa haya makundi yamegeuka mateso kwa raia wa huko ila lengo la kuanzishwa awali halikuwa hilo.
 
asante sana kwa hii makala fikirishi

lakini mkuu hivyo ndivyo ambavyo siasa ilivyo. Katika siasa hauwezi kuingiamakubaliano ya kutoa msaada kwa mtu au kikundicha watu ama taifa pasipo wewe na watu wako ama taifa lako kutonufaika na chochote.. hakunaga hiyo kitu
 
asante sana kwa hii makala fikirishi

lakini mkuu hivyo ndivyo ambavyo siasa ilivyo. Katika siasa hauwezi kuingiamakubaliano ya kutoa msaada kwa mtu au kikundicha watu ama taifa pasipo wewe na watu wako ama taifa lako kutonufaika na chochote.. hakunaga hiyo kitu
Mkuu za masiku, nmefurahi kukuona umetia timu.

Kwahyo mkuu ina maana tunawalaumu bure mabeberu kuweka maslahi ya nchi zao mbele kumbe hta sisi waafrika tupo kimaslahi zaidi kuliko uzalendo.

Kuna mahala nilisoma kuwa hta muaji ya kimbari Rwanda hakuna aliyeingilia moja kwa moja sababu hawakuona kuna rasilimali zozote za kunyonya!!
 
Mkuu za masiku, nmefurahi kukuona umetia timu.

Kwahyo mkuu ina maana tunawalaumu bure mabeberu kuweka maslahi ya nchi zao mbele kumbe hta sisi waafrika tupo kimaslahi zaidi kuliko uzalendo.

Kuna mahala nilisoma kuwa hta muaji ya kimbari Rwanda hakuna aliyeingilia moja kwa moja sababu hawakuona kuna rasilimali zozote za kunyonya!!
Mkuu wanacho kifanya mabeberu leo ndivyo haswaa siasa ilivyo na ndivyo inavyopaswa kuwa hata sisi leo ikitokea moja ya nchi zetu ikawa super power lazima itafanya kile ambacho wanafanya mabeberu. falsafa ya ulimwengu ilivyo inahitaji mtawala na mtawaliwa kwa namna moja ama nyingine hakuna mtawala ambaye huwa ana kubali kuona mataifa mengine ya kinyanyuka nakuwa kama yeye kwa sababu wote mkiwa na nguvu sawa nani atakaye mtawala mwenzie. nani atakaye weza kulitawala soko la dunia na kuwa mwenye sauti

mandela aliwahi kusema kwamba ubaya na wema wa che guevera unategemea na upande aliousimamia. ..nina maana kwamba yale wanayo tufanyia mabeberu kwao wao huitwa mashujaa kwakuwa wana simamia ama kuipigania nafasi waliyonayo isiweze kuwaponyoka na katika wakati huo huo wao kwetu ni maadui kwa sababu wana Tufanyia mbinu chafu na urasimu ili tusiweze kunyanyuka

hivi ndivyo maisha yalivyo mkuu
 
Back
Top Bottom