Kwa sababu ya ugumu wa maisha uliopo mtaani kwa sasa, kuna hatari kubwa ya watu kutengeneza taarifa za uongo au "kuwasingizia" maadui zao wa kibiashara au kisiasa ili tu wapate hiyo Shilingi milioni kadhaa.
Ndio maana mimi nasisitiza kuwa taarifa lazima zithibitike kuwa za kweli badala ya kuwa propaganda za kisiasa.
Umesema kweli kabisa mkuu MKANGAFFU, naunga mkono hoja yako kwa 100%.
Mazingira ya ugumu wa maisha yakichanganyikana na njaa, yanatengeneza hatari kubwa sana mtaani. Hawa
wasaka tonge na watu wasio na uaminifu watatumia fursa yoyote ya zawadi za fedha kuwasingizia na kuwazushia majungu maadui zao wa kibiashara au kisiasa ili tu wapate hizo shilingi milioni kadhaa. Ndio maana nasisitiza sana kuwa taarifa lazima zithibitike kwa ushahidi thabiti badala ya kuendekeza propaganda za kisiasa na
kutafuta kiki za kijinga.
Kama mfano hai wa hili ninachokisema, hebu tuangalie kule Pakistan kwenye sheria yao ya
blasphemy. Kule watu wengi sana wamepoteza maisha, kushambuliwa, au hata kuhukumiwa kunyongwa mahakamani kwa ushahidi wa uongo wa maneno tu. Mtu anakutuhumu tu kwa visasi vyake binafsi au vya kibiashara, unakamatwa na kusulubiwa bila uchunguzi makini wa kisayansi.
Huu ndio uhalisia kwamba mifumo ikikosa umakini, inakuwa silaha ya kuangamiza wasio na hatia. Hawa mawaziri wetu wa kuokoteza wanaopenda
kupiga denda na sifa za kijinga za kisiasa lazima serikali ijiangalie sana nao. Wasikurupuke kuweka mifumo itakayowapa watu mwanya wa kulipiza visasi na kutengeneza majungu mtaani kwa sababu ya njaa zao. Lazima kuwepo na uchunguzi thabiti na huru (
vetting) kabla ya kuchukua hatua yoyote.
Mwisho kabisa,
bado nahoji sana umakini wa uchunguzi wao. Kama serikali hii hii tangu mwaka 2017
haijawapata waliompiga risasi Mhe. Tundu Lissu, na wale
wauaji wa Oktoba 29, ndiyo tuiamini leo kama
itafanya uchunguzi kwa uwazi? Ama mfumo huu utakuja kuwa
silaha tu ya kuwafunga wapinzani kisiasa kwa kuwatumia
machawa na
vikosi vya propaganda kutuhumu watu ovyo mtaani?