Cheap threat
Ni hivi, wachochezi kama maria sarungi, mange kimambi, sativa na wengine wengi hawaishi hapa na wala hawatakuwepo kwenye vurugu, watakuwa wanafantilia mnavyouuliwa kwenye insta na x huku wakiposti ili kuongeza likes na kujipatia hela wakiwa wameweka miguu juu
Heche na wenzake itakuwa kama 29, watajifungia ndani, hakuna hata mmjoa atatoka
Haya sasa akili kukichwa, ni nani atadhurika kama sio wewe na wenzako?
Na safari hii bodaboda na wamachinga wamejifunza, hawataki kusikia huu ujinga wa vurugu huku wakikosa hela
Hivi huwa tunafikiri kati ya watawala na watawaliwa ni nani mvunjanji wa Amani namba moja? Nchi nyingi zilizoingia kwenye vita sehemu kubwa visababishi ni walioko madarakani; na sababu ni kama kung'ang'ania kukaa madarakani kwa muda mrefu, matumizi mabaya ya raslimali za nchi ikiwa ni pamoja na kuingia kwenye mikataba ya wizi ktk Mali za umma kama madini, n.k., ubadhilifu, upindishaji/ kibakizaji wa kesi na upokaji was haki, rushwa, undugunisation ktk ugawaji kazi katikautumishi was umma, utoroshaji wa maliasili, na mengine mengi yanayopindisha Sheria; wizi wa kura; na mengine mengi yasiyo zingatia siasa safi na uongozi bora.
Viongozi wanapofika mahali wakaacha kusikiliza wananchi waliowengi husababisha kufanya kundi la waliowengi kujiona wametengwa na kuona kama mgawanyo wa keki ya taifa unaenda kwa wachache ambao ndiyo watawala.
Vile vile tunahiaji kuwa na matazamo chanya. Hii habari ya kuwafikiria wengine kama waleta vurugu nadhani siyo mtazamo sahihi. Tunatakiwa tuone kuwa kila mwananchi yuko sawa kwa kuwa havunji Sheria. Tunapotanguliza 'vurugu', na 'wapigwe' tu, hatujengi taifa Bali tunachochea uhasama baina yetu - raia kwa raia, raia kwa askari, na au askari kwa askari. Lakini pia, busara na Hekima inatakiwa itumike kwani hata hao askari wana ndugu mwiongoni mwao; kwani unapo mwaga damu au kuumiza Mtanzania mwenzako unapata faraja gani ya Moyo? Tukumbuke kwamba mwanadamu anaishi kwa kumtegemea mwenzake. Hivyo, kujaliana na kupendana, kuvumiliana, na kupendana ni nguzo muhimu kwa kila mmoja wetu. Si sawa mwingine kujiona yu juu ya Sheria au anahaki ya kutumia raslimali za nchi kuliko mwingine.
Tuhimize upendo, kujaliana, kuvumiliana, uzalendo kwa nchi yetu. Hatuna nchi nyingine mbadala. Tujenge nchi yetu kwa Moyo. Raslimali za nchi zimfaidishe kwa usawa kila Mtanzania, zisiwe kwa kwa kundi fulani tu la wachache kuepuka kuchochea hasira miongoni mwa wengi ambao mwisho wa siku wanajiona kudhurumiwa.
Viongozi na nyie wote wenye mamlaka, msiwaone wananchi kana kwamba muda wote ni waharifu. Ongozeni kwa HAKI; na AMANI ya kweli itapatikana.