Kata ya Azimio Wilaya ya Temeke mgombea Udiwani nafasi ya pili adai kuwasomea 'Halbadiri' wajumbe

PendoLyimo

JF-Expert Member
Sep 30, 2014
866
939
Ndugu wana jukwaa habari za muda huu?

Kwa ari ya kushangaza kidogo hi imetokea kwenye kata ya azimio wilaya ya temeke kwenye kipindi Cha uchaguzi wa kura za maoni kumpata muwakirishi wa nafasi ya Udiwani kwa chama Cha mapinduzi kwenye kata ya Azimio.

Mnyukano wa kifedha ulipamba Moto siku moja kabla ya kuingia kwenye kura za maoni tarehe 24/7/2020 Kati ya mshindi wa kwanza mbaye ni mwana mama aliye kuwa diwani viti maalumu miaka kumi nyuma na jamaa mmoja mwenye asili ya kipemba ambaye ameshika nafasi ya pili

Wawili hao waliwapitia wajumbe usiku kwa usiku na kuwaonga pesa na kuaidiwa kupigiwa kura

Sasa wajumbe walichokifanya ni kuangalia mwenye mzigo mkubwa ndio wamempa kura nyingi

Siku ya uchaguzi baada ya matokeo kutoka mwana mama akaongoza kwa kura nyingi sana,na yule jamaa akapata kura ndogo na kumfanya kushika nafasi ya pili.

Kilichofata hapo mshindi wa pili alirudi kwa wale wajumbe na kuomba arudishiwe pesa zake alizowapatia wajumbe na Kama hawata rudisha atawasomea halbadiri wajumbe wote waliokula pesa yake na kutompigia kura wamrudishie pesa zake haraka iwezekanavyo.
 
Albadir na siasa wapi na wapi
AZIMIO hiyo
Screenshot_2020-08-04-18-22-05.jpg
Screenshot_2020-08-04-18-21-39.jpg
 
Chama kinahitajika kushuka chini Tena hadhabu kali itakayo wapata hao wagombea wawili walio shindana kwa rushwa pia iwapate na wajumbe wa kamati ya siasa maana hao ndio wasababishaji wakubwa
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom