Kasoro katika ubalozi wa Tanzania Washington DC

shilanona

Member
Oct 31, 2010
55
22
Wana jamii,
Wale ambao hamjafika kwenye ofisi za ubalozi wa Bongo mjini Washington DC, mnaomba kupita hapo siku moja. Ukiingia ndani utaona floor imepigwa carpet la nguvu na kuta zinameremeta kama umeingia mbinguni. Nilikuwepo hapo wiki iliyopita.
HAYA, mbele yako utakaribishwa na bibi kizee mmoja wa Kihindi kama Receptionist. Ukimsalimia "habari gani" bibi huyu hajui kiswahili, anachojua ni Kiingereza cha kihindi na kihindi chenyewe.
Hivi kweli HAKUNA watanzania wanaoishi hapo Washington DC wanaoweza kufanya kazi hii mpaka bibi kizee wa Kihindi aletwe Toka India kuja kufanya kazi ya mapokezi? Au labda anafahamiana na Waziri wa Mambo ya nje wa Tanzania?
NADHANI HII HAIJAKAA VIZURI
 
Wonders shall mever. But what do you expect from such a government devoid of its citizens? I mean it is a government empowered by mafisadi.
 
Wana jamii,
Wale ambao hamjafika kwenye ofisi za ubalozi wa Bongo mjini Washington DC, mnaomba kupita hapo siku moja. Ukiingia ndani utaona floor imepigwa carpet la nguvu na kuta zinameremeta kama umeingia mbinguni. Nilikuwepo hapo wiki iliyopita.
HAYA, mbele yako utakaribishwa na bibi kizee mmoja wa Kihindi kama Receptionist. Ukimsalimia "habari gani" bibi huyu hajui kiswahili, anachojua ni Kiingereza cha kihindi na kihindi chenyewe.
Hivi kweli HAKUNA watanzania wanaoishi hapo Washington DC wanaoweza kufanya kazi hii mpaka bibi kizee wa Kihindi aletwe Toka India kuja kufanya kazi ya mapokezi? Au labda anafahamiana na Waziri wa Mambo ya nje wa Tanzania?
NADHANI HII HAIJAKAA VIZURI

Du tumekwisha jamani.
 
Kuna kazi ambazo waajiriwa wanatakiwa kuwa wakazi au raia wa Marekani. Hata ubalozi wa Marekani nchi Tanzania una wafanyakazi wengi ambao ni raia wa Tanzania. Je receptionist wa ubalozi wa Marekani nchi Tanzania ni mMarekani? Kuna vitu vingine tuvifanyie utafiti kabla ya kuvimwaga hapa jamvini. Hama sivyo tunaonekana ni wabishi wa kuchanjia tu.
 
Siyo lazima ajira kama hizi wawe ni raia wa Kimarekani. Kuna watanzania wangapi hapo DC ambao ni Permanent resident wa Marekani na ambao wanaongea Kiswahili na Kiingereza vizuri? Mbona Belinda alikaa kwenye hilo benchi la receptionist kwa miaka kadhaa kabla ya kuletewa mizengwe na vigogo wa ubalozi? Sasa, angalau huyo mhindi angekuwa anaweza kusema Kiswahili hilo lingekuwa jambo jingine. Hata hao unaowasema ni ma-reception pale ubalozi wa Marekani nchini Tanzania wanaelewa lugha ya Host country na ile ya kwao. Mkuu huu ni mchemsho, tunapomuona huyu mama hapo tunatamani kutapika.
 
Haija kaa vizuri lakani hainishangazi kwa huu utawala wetu. Huko nyumbani bongo ndio usiseme maana madirector wote ni watu kutoka nje
ya Tanzania. Serikali yetu haina sera ya kumlinda mtaanzania na umeuona mfano mwenyewe hapo ubalozini ..........:A S angry:
 
Siyo lazima ajira kama hizi wawe ni raia wa Kimarekani. Kuna watanzania wangapi hapo DC ambao ni Permanent resident wa Marekani na ambao wanaongea Kiswahili na Kiingereza vizuri? Mbona Belinda alikaa kwenye hilo benchi la receptionist kwa miaka kadhaa kabla ya kuletewa mizengwe na vigogo wa ubalozi? Sasa, angalau huyo mhindi angekuwa anaweza kusema Kiswahili hilo lingekuwa jambo jingine. Hata hao unaowasema ni ma-reception pale ubalozi wa Marekani nchini Tanzania wanaelewa lugha ya Host country na ile ya kwao. Mkuu huu ni mchemsho, tunapomuona huyu mama hapo tunatamani kutapika.

Acheni hayo mambo. Ni nani kakwambia kuwa kiSwahili ni kigezo cha kupata kazi zisizo za kibalozi katika ubalozi ulipo Marekani? Mtataka hata wanaosafisha vyoo na kuendesha magari walonge kwa kiswahili? Anyway English is our second official language. Hivyo kulalamika hakuna mpango.
 
Mamsapu wa Balozi? Balozi ni Mwanamke...
Tatizo la watanzania wengi waishio hapa hawana makaratasi ya kuishi hapa na hata kama wanayo -- kazi hiyo haiwezi kulipia gharama za maisha DC

Mama huyo malipo yake sio ghali kulinganisha na Mtanzania mwenye Makaratasi Marekani --- Kwahiyo Tulia Ndugu Yangu
 
Acheni hayo mambo. Ni nani kakwambia kuwa kiSwahili ni kigezo cha kupata kazi zisizo za kibalozi katika ubalozi ulipo Marekani? Mtataka hata wanaosafisha vyoo na kuendesha magari walonge kwa kiswahili? Anyway English is our second official language. Hivyo kulalamika hakuna mpango.

Mkuu
Wacha ulimbukeni kama unafanya kazi kwa Watanzania na hutaki kujifunza lugha yao kwa nini ufanye kazi huko? Ujinga wa mwafrika, ndio wale wale huku wataka na kule wataka chagua moja kusuka ama kunyoa.
 
Mkuu wacha ulimbukeni kama unafanya kazi kwa Watanzania na hutaki kujifunza lugha yao kwa nini ufanye kazi huko? Ujinga wa mwafrika, ndio wale wale huku wataka na kule wataka chagua moja kusuka ama kunyoa.


Mkuu wangu:

Tofautisha basi political incorrectness na ulimbukeni. Nakubali la kwanza lakini sio ulimbukeni.
 
Kama hizo ajira chache za ubalozi kama hiyo ya receptionist unataka kuwabagua wamarekani, unadhani itakuwa sahihi kwa wamerakani pia kubagua utoaji wa kazi on the basis of nationality? unadhani nani ataathirika zaidi.
Je ni watanzania wangapi wanaonufaika na marekani ukilinganisha na huyo bibi mmoja anayefanya kazi embassy?
Je una uhakika gani kuwa huyo bibi siyo mtanzania? au kila mtanzania lazima ajue kiswahili.
Ubaguzi haufai.
 
Mkuu wangu:

Tofautisha basi political incorrectness na ulimbukeni. Nakubali la kwanza lakini sio ulimbukeni.

Kama hufahamu maana ya ulimbukeni tafuta kamusi.


Kama hizo ajira chache za ubalozi kama hiyo ya receptionist unataka kuwabagua wamarekani, unadhani itakuwa sahihi kwa wamerakani pia kubagua utoaji wa kazi on the basis of nationality? unadhani nani ataathirika zaidi.
Je ni watanzania wangapi wanaonufaika na marekani ukilinganisha na huyo bibi mmoja anayefanya kazi embassy?
Je una uhakika gani kuwa huyo bibi siyo mtanzania? au kila mtanzania lazima ajue kiswahili. Ubaguzi haufai.

Sidhani kama ajira hiyo itawaathiri wabongo vile inavyofikiria, wanaonufaika ni Mafioso wa Chama Cha Majambazi na hakuna Mtanzania asiyejua kutoa salam kwa kiswahili ili hali anakaa na kufanya kazi kwa waswahili huu ni ujinga uliopita kiasi, hatuongelei ubaguzi tunaongelea principals ni sawa hata hivi sasa huwezi kwenda nchi yoyote ile duniani na kufanya kazi bila kibali huo nao utaita ubaguzi?
 
Kama hufahamu maana ya ulimbukeni tafuta kamusi.

Soma posti ZeMarcoPolo na uone kuwa it's not a big issue. Mpaka sasa sijatumia lugha ya matusi. Kumwita mtu mjinga au limbukeni ni kushindwa kutoa hoja.
 
Soma posti ZeMarcoPolo na uone kuwa it's not a big issue. Mpaka sasa sijatumia lugha ya matusi. Kumwita mtu mjinga au limbukeni ni kushindwa kutoa hoja.

Sio big issue kwa punguani, lakini hiyo ni very big issue ndio sababu tuna mizoga ya mahayawani kwenye serikali ya Chama Cha Majambazi.

Kumbe hata kiswahili fasaha nacho kinakupiga chenga.
 
Sio big issue kwa punguani, lakini hiyo ni very big issue ndio sababu tuna mizoga ya mahayawani kwenye serikali ya Chama Cha Majambazi.

Kumbe hata kiswahili fasaha nacho kinakupiga chenga.

I really enjoy your efforts, but don't forget to take your medicine regularly.
 
@Wacha1
Balozini kuna waajiriwa wa aina mbili. Diplomats and non diplomats. Waajiriwa diplomats huajiriwa kwa kuzingatia sheria za nchi zao, lakini waajiriwa non diplomats huajiriwa kwa kuzingatia sheria za nchi ulipo ubalozi.
Receptionist ni non-diplomat, kama walivyo madereva, walinzi etc. kwenye kuwaajiri hawa, ni lazima kipengele cha equal opportunity kizingatiwe.
Pili, naomba nisisitze kwa mara nyingine kuwa kuongea kiswahili sio kipimo cha utanzania. Kuna watanzania wengi tu hawaongei kiswahili.
 
@Wacha1
Balozini kuna waajiriwa wa aina mbili. Diplomats and non diplomats. Waajiriwa diplomats huajiriwa kwa kuzingatia sheria za nchi zao, lakini waajiriwa non diplomats huajiriwa kwa kuzingatia sheria za nchi ulipo ubalozi.
Receptionist ni non-diplomat, kama walivyo madereva, walinzi etc. kwenye kuwaajiri hawa, ni lazima kipengele cha equal opportunity kizingatiwe.
Pili, naomba nisisitze kwa mara nyingine kuwa kuongea kiswahili sio kipimo cha utanzania. Kuna watanzania wengi tu hawaongei kiswahili.

Mkuu hii hadithi unamwambia nani? Kuna watu ambao sio watanzania na hawashindwi kusalimia kwa kiswahili haiingii akilini mwako kwamba unapoweka non diplomat employee kuwa receptionist moja ya requirement ni lazima ufahamu angalao kusalimia Kiswahili Period unahitaji kuambiwa vipi tena?
 
Mkuu hii hadithi unamwambia nani? Kuna watu ambao sio watanzania na hawashindwi kusalimia kwa kiswahili haiingii akilini mwako kwamba unapoweka non diplomat employee kuwa receptionist moja ya requirement ni lazima ufahamu angalao kusalimia Kiswahili Period unahitaji kuambiwa vipi tena?

Kiongozi,
naona hapa unachanganya mambo. Tatizo ni nini? kutokuwa mtanzania? kuwa bibi mzee? kuwa mhindi? au kutokuongea kiswahili?
Swala la kiswahili sioni kama issue kwa sababu Tanzania ina official languages mbili: kiswahili na kiingereza. Kama receptionist anaongea any of those hakuna tatizo (tena for that matter kiingereza kinaweza kuhitajika zaidi ya kiswahili). Jiulize, wageni wangapi wanaoingia hapo ambao wanajua kiswahili tu?!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom