BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Kasi ya Watanzania kuzaliana inatisha
Imeandikwa na Anna Makange, Muheza; Tarehe: 11th July 2011
TANZANIA itakumbwa na ongezeko la watu maradufu katika kipindi cha miaka 25 ijayo, kutokana na kufikia kiwango cha asilimia 2.9 cha ukuaji wa idadi ya watu ambacho ni cha juu ikilinganishwa na kiwango cha asilimia 1.8 katika nchi zinazoendelea.
Ongezeko hilo linatokana na kiwango kikubwa cha uzazi ambapo kwa wastani mwanamke wa Kitanzania huzaa watoto sita ikilinganishwa na wastani wa watoto watatu kwa kila mwanamke duniani, kiashiria hicho kinachochewa na idadi ndogo ya Watanzania wanaotumia huduma za kisasa za uzazi wa mpango.
Hayo yamebainishwa jana wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Idadi ya Watu Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye viwanja vya Jitegemee wilayani Muheza katika Mkoa wa Tanga.
Ni asilimia 27 tu ya kinamama wa Kitanzania ndio wanatumia njia za kisasa za uzazi wa mpango ikilinganishwa na nchi nyingine zinazoendelea kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Kenya ambayo imepiga hatua kubwa kwa kufikia asilimia 46 kwa takwimu za 2009.
Akizungumza katika sherehe hizo, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Florence Mwanri alisema, ni ukweli ulio wazi kuwa rasilimali watu ndiyo nguzo muhimu katika maendeleo, lakini ni dhahiri kwamba idadi kubwa isiyoendana na ukuaji wa uchumi ni changamoto katika harakati za kufikia maendeleo.
"Makisio ya idadi ya watu inaonesha Tanzania ilikuwa na watu milioni 43 mwaka 2010 na inatarajiwa kufikia milioni 63.5 mwaka 2025 kutokana na kiwango cha sasa cha ukuaji wa idadi ya watu cha asilimia 2.9 kwa mwaka kuwa juu hasa ikilinganishwa na cha asilimia 1.8 kwenye nchi zinazoendelea na kwa kuzingatia kwamba asilimia 50 ya watu hao ni vijana ikilinganishwa asilimia 30 ya vijana kwenye nchi zinazoendelea.
"Hii inaonesha kuwa juhudi za makusudi zinahitajika ili kutumia rasilimaji ya vijana katika kukuza uzalishaji wenye tija na kuongeza pato," alisema Mwanri ambaye ofisi yake ndiyo inayoandaa sherehe hizo.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Kalembo aliwataka wananchi kushiriki kwa vitendo kuunga mkono juhudi za Serikali na wadau wengine wa maendeleo kutekeleza mikakati itakayosaidia kukabili changamoto zinazotokana na kasi ya ongezeko la idadi ya watu kwa kuchukua hatua ya kuanza kupanga uzazi na kupunguza idadi ya watoto.
"Kasi hii ya ongezeko la idadi ya watu mara mbili ni changamoto kubwa sio tu kwa Serikali ambayo inatakiwa kuwekeza zaidi kwenye huduma za elimu na afya ili kuharakisha maendeleo, bali pia kwa familia ambayo inayo wajibu wa kutumia nguvu na ujuzi wao katika kuongeza uzalishaji ili kukuza kipato kitakachowezesha kuondokana na umasikini.
Imeandikwa na Anna Makange, Muheza; Tarehe: 11th July 2011
TANZANIA itakumbwa na ongezeko la watu maradufu katika kipindi cha miaka 25 ijayo, kutokana na kufikia kiwango cha asilimia 2.9 cha ukuaji wa idadi ya watu ambacho ni cha juu ikilinganishwa na kiwango cha asilimia 1.8 katika nchi zinazoendelea.
Ongezeko hilo linatokana na kiwango kikubwa cha uzazi ambapo kwa wastani mwanamke wa Kitanzania huzaa watoto sita ikilinganishwa na wastani wa watoto watatu kwa kila mwanamke duniani, kiashiria hicho kinachochewa na idadi ndogo ya Watanzania wanaotumia huduma za kisasa za uzazi wa mpango.
Hayo yamebainishwa jana wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Idadi ya Watu Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye viwanja vya Jitegemee wilayani Muheza katika Mkoa wa Tanga.
Ni asilimia 27 tu ya kinamama wa Kitanzania ndio wanatumia njia za kisasa za uzazi wa mpango ikilinganishwa na nchi nyingine zinazoendelea kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Kenya ambayo imepiga hatua kubwa kwa kufikia asilimia 46 kwa takwimu za 2009.
Akizungumza katika sherehe hizo, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Florence Mwanri alisema, ni ukweli ulio wazi kuwa rasilimali watu ndiyo nguzo muhimu katika maendeleo, lakini ni dhahiri kwamba idadi kubwa isiyoendana na ukuaji wa uchumi ni changamoto katika harakati za kufikia maendeleo.
"Makisio ya idadi ya watu inaonesha Tanzania ilikuwa na watu milioni 43 mwaka 2010 na inatarajiwa kufikia milioni 63.5 mwaka 2025 kutokana na kiwango cha sasa cha ukuaji wa idadi ya watu cha asilimia 2.9 kwa mwaka kuwa juu hasa ikilinganishwa na cha asilimia 1.8 kwenye nchi zinazoendelea na kwa kuzingatia kwamba asilimia 50 ya watu hao ni vijana ikilinganishwa asilimia 30 ya vijana kwenye nchi zinazoendelea.
"Hii inaonesha kuwa juhudi za makusudi zinahitajika ili kutumia rasilimaji ya vijana katika kukuza uzalishaji wenye tija na kuongeza pato," alisema Mwanri ambaye ofisi yake ndiyo inayoandaa sherehe hizo.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Said Kalembo aliwataka wananchi kushiriki kwa vitendo kuunga mkono juhudi za Serikali na wadau wengine wa maendeleo kutekeleza mikakati itakayosaidia kukabili changamoto zinazotokana na kasi ya ongezeko la idadi ya watu kwa kuchukua hatua ya kuanza kupanga uzazi na kupunguza idadi ya watoto.
"Kasi hii ya ongezeko la idadi ya watu mara mbili ni changamoto kubwa sio tu kwa Serikali ambayo inatakiwa kuwekeza zaidi kwenye huduma za elimu na afya ili kuharakisha maendeleo, bali pia kwa familia ambayo inayo wajibu wa kutumia nguvu na ujuzi wao katika kuongeza uzalishaji ili kukuza kipato kitakachowezesha kuondokana na umasikini.