johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,840
- 141,765
Kasi ya Rais Magufuli katika kuwaletea wananchi maendeleo imewavuruga kabisa wafuasi wa Chadema kiasi cha kushindwa kumuona mbadala wa Mbowe katika nafasi ya Mwenyekiti.
Kwa sasa kila anayetamani kuchukua fomu anaonekana ana mahaba na CCM isipokuwa Freeman pekee ambaye yuko Chadema tokea mwaka 1992 wakati chama hicho kinaasisiwa. Kinachosahaulika hapa ni kuwa mzee Mbowe alikuwa mwanaccm kabla Chadema haijazaliwa.
Tatizo la Chadema siyo Mbowe bali ni tishio la chama hicho kumezwa na CCM na nafasi yake kama chama kikuu cha Upinzani kuchukuliwa na ACT wazalendo ambayo ina uhakika wa kupata wabunge kutoka Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa 2020.
Tayari Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru ameshasema ana barua lukuki kutoka kwa wabunge na madiwani wa Chadema wanaoomba kujiunga CCM.
Kiuhalisia kilichomkimbiza mzee Sumaye pale Ufipa siyo " kuonja sumu kwa kulamba " bali kaisoma kasi ya Magufuli na kugundua kuwa Chadema inaelekea kibra na wengi watamfuata Sumaye kabla ya Krismas na mwaka mpya.
Maendeleo hayana vyama!
Kwa sasa kila anayetamani kuchukua fomu anaonekana ana mahaba na CCM isipokuwa Freeman pekee ambaye yuko Chadema tokea mwaka 1992 wakati chama hicho kinaasisiwa. Kinachosahaulika hapa ni kuwa mzee Mbowe alikuwa mwanaccm kabla Chadema haijazaliwa.
Tatizo la Chadema siyo Mbowe bali ni tishio la chama hicho kumezwa na CCM na nafasi yake kama chama kikuu cha Upinzani kuchukuliwa na ACT wazalendo ambayo ina uhakika wa kupata wabunge kutoka Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa 2020.
Tayari Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru ameshasema ana barua lukuki kutoka kwa wabunge na madiwani wa Chadema wanaoomba kujiunga CCM.
Kiuhalisia kilichomkimbiza mzee Sumaye pale Ufipa siyo " kuonja sumu kwa kulamba " bali kaisoma kasi ya Magufuli na kugundua kuwa Chadema inaelekea kibra na wengi watamfuata Sumaye kabla ya Krismas na mwaka mpya.
Maendeleo hayana vyama!