Susuviri
JF-Expert Member
- Oct 6, 2007
- 3,713
- 888
Lowasa alishasema anayehusika na Richmond ni mkuu wa kaya lakini mbona hawamwambii Rais Jk aseme ukweli badala yake Lowasa!
Lowasa hahusiki na ukweli ni huu:
Mambo yote ya mikataba na mengine makubwa yanapitishwa na baraza la mawaziri ambalo;
Mwenyekiti ni Rais wa JMT
Katibu ni katibu kiongozi wa serikali wakati huo akiwa P.Luhanjo
Waziri mkuu ni msimamizi yaani kiranja.
Jambo linaposhindikana hupigwa kura.
Lowasa alisema hahusiki na katika mfumo huo wa baraza la mawaziri mwenye kura ya VETO ni rais pekee kama jambo limeleta mvutano.
Pili mitambo iliyokuwa ya Richmond ndiyo sasa inaitwa SIMBION,sasa tujue mmiliki wa simbion ni nani? Huyo ndiyo atwambie alirithi mitambo hiyo kutoka kwa mmiliki gani ili tujue asili ya Richmond.
Pili hadi mwaka jana Richmond ilikuwa bado inalipwa! Je serikali ilikuwa inamlipa nani? Lowasa! Kama Lowasa ndiyo alikuwa analipwa ilikuwaje akiwa nje ya mfumo?
Naona makamba huko Tanga anadanganya umma.
Maneno mengi lakini labda ulikuwa mtoto bado Richmond ilipotokea.
Unajua nafasi aliyocheza Lowassa katika utoaji tenda? Unajua kuwa tenda ya Richmond ilitoka nje ya utaratibu na aliyeiamuru Richmond ipewe tenda ni nani?
Lowassa ameidanganya umma lakini kuna evidence inaonyesha kila kitu kilifanyika kwa maagizo yake. Kusema aliaambiwa na mkuu wake ni uongo kwani kwa maelezo yake hii aliambiwa na subordinate wake. Haiwezekani. Waziri Mkuu ni mtendaji mkuu wa serikali. Richmond, Dowans na hatimaye Symbion ni dili iliyofanywa na rafiki yake mpenzi Rostam kupitia kampuni yake ya Caspian.
Rostam ndiye business partner wake katika madili mengine pia mfano Vodacom Tanzania.
Taratibu kila kitu kitajulikana na hata waliomzunguka Lowassa akina Masha hawajui details na mzee akili yake si ile ya zamani!