Kashfa ya kwanza Richard...

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,556
29,640
Siku ya jumatano, watanzania hasa wakazi wa dar es salaam kwa shauku kubwa walijazana kwa shauku kubwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu Kambarage (maksudi)kumlaki kipenzi chao Richard ambaye umaarufu wake umeongezeka hasa baada ya kujinyakulia kitita cha dola laki moja kutoka big braza.

Nikiwa naangalia mapokezi yake, nilistushwa kuona wanajamii waliowakilisha furaha zetu wakilalama utaratibu mbovu uliotumika kumtorosha Richard ili asionwe na watu. Niliangalia sura za simanzi za wabongo wale ambao walikwenda na maua na mashada yake kumpongeza kuitangaza Tanzania huko sauzi...

Inawezekana waandaaji wa mapokezi wanaugua akili au labda Richard mwenyewe kuamua kutojitokeza mbele ya halaiki. Lakini kwa nini multchoice-Tanzania waliwahamasisha wabongo kujazana uwanjani?? Inasemekana kwamba, kulikuwa kumeandaliwa hafla ya kumpongeza ktk ukumbi fulani, na kila atakayetaka kumwona shurti alipe kiingilio, sasa kinachogomba ktk ubongo wangu ni kwanini basi uwaambie watu wajitokeze kwa wingi uwanjani? Mbona hata kina Kofi Olomide wanalakiwa na watu wengi hata wengine kupiga nae picha ingawa inajulikana amekuja kwa show yenye kiingilio kikali?

Nadhani wababaishaji hawako katika siasa peke yake, hata katika sanaa kuna wababaishaji kinoma. Matajiri wa bongo wapo wachache hivyo kura zao zisingetosha kumpatia ushindi richard, watu walimtwangia kura na sanasana vijana ambao walikuwa wanahamasika kumpa tafu mwenzao. Hivyo kuwanyima fursa ya kumwona angalau hata kuwapungia mkono ni kuwapoka ushindi wao.

Natumaini macho ya JF yalikuwepo pia uwanjani, hivyo watatujuza kilichotokea na wenye kuwafahamu waandaaji wa mapokezi watawahiji ili tuletewe majibu hapa. KWA NINI WABONGO WADHALILISHWE????
 
Huu ni ushamba tu na ufinyu wa mawazo. Umaarufu wake wameshaona ni dili ya kuvunia hela. Akichuja wanamkimbia.
 
Watanzania pia tumezidi ujinga, hivi kwa mvua ilonyesha siku nzima jana hadi usiku na magari yalivyokuwa ya shida zaidi na foleni isiyoelezeka, watu walithubutu kujazana uwanjani eti kumpokea richard du, kweli watu hawana kazi za kufanya na huu moyo wa upendo na uzalendo sijui ndo huu au hii ni aina ingine ya kupoteza muda na kusahau shida zetu. pole zao maskini, poor them
 
Watanzania pia tumezidi ujinga, hivi kwa mvua ilonyesha siku nzima jana hadi usiku na magari yalivyokuwa ya shida zaidi na foleni isiyoelezeka, watu walithubutu kujazana uwanjani eti kumpokea richard du, kweli watu hawana kazi za kufanya na huu moyo wa upendo na uzalendo sijui ndo huu au hii ni aina ingine ya kupoteza muda na kusahau shida zetu. pole zao maskini, poor them

...Judy
unajua wabongo wameshadungwa sana ktk madini yao na kukosa maisha bora hivyo vijiishu kama hivi huwa vinapooza machungu na kusahaulisha kwa muda madhila ya kisiasa. Halafu ufahamu kuna watu wengine wanashabikia sana watu maarufu na hiyo ndiyo hobi yao. wape haki yao as funs of richard (ingawa i hate the guy kwa matendo yake) lakini utalii utaongezeka kwa kulitangaza jina la tanzania nje.

CCM wajitoe ktk hili maana ni aibu kusema kuwa malezi ya richard ni mojawapo ya sera ya ccm. kioja cha mwaka. Labda hao ccm wanashabikia kutokuwa mwaminifu ktk ndoa as they do in politic marriage....
 
Siku ya jumatano, watanzania hasa wakazi wa dar es salaam kwa shauku kubwa walijazana kwa shauku kubwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu Kambarage (maksudi)kumlaki kipenzi chao Richard ambaye umaarufu wake umeongezeka hasa baada ya kujinyakulia kitita cha dola laki moja kutoka big braza.

Mimi simo kabisa. Sishabikii kabisa huu ujinga na mfano mbaya wa malezi na hauendani kabisa na utamaduni wetu.

Hebu fikiri fate ya taifa lenye vijana wenye tabia za BBA.
Anayebisha na alee watoto wake ki-big brother na aone madudu yatakayoikumba familia na jamii inayomzunguka.

Tatizo watanzania tunashindwa kutafakari hali yetu ngumu tuliyonayo ambayo sehemu kubwa inatokana na aina ya uongozi ambao tumekuwa nao; tunalukia tu mambo ya ajabu ajabu.

Itakuwa siku ******* nao wataanzisha kombe lao na Mtanzania mmoja akajishindia Dola Milion moja (Dola laki moja x 10) alafu waheshimiwa wakasema ni matokeo ya sera bora za malezi ya vijana! Ili mradi tu fulani kajishindia Dola nyingi.

I am getting worried of the kind of people Tanzania will be composed of in the next 50 years.

Narudia, mimi simo.
 
Umoja wa Vijana wa CCM waliosema ndo waandalizi wa mapokezi walikuwa wapi?

Waliumbuka na vinguo vyao vya kijani? kwani nilimsikia Kibonde wa Clouds akitoa taarifa ya uwepo wa wana CCM katika mavazi yao rasmi pale Undege.

Kamanda wa vijana hebu tueleze ilivyokuwa!
 
Labda tuseme richard alikuwa anaikimbia ccm ambapo ni jambo zuri pia kwa upande wak
 
Hivi itakuwa imefikia shs ngapi kumuona yule mwakilishi wa BBA2 aliyepita .. Misho Mwampamba!?
 
BIG BROTHER AFRICA II RICHARD LEO AMEONGEA NA WAANDISHI WA HABARI KATIKA HOTELI YA HOLIDAY INN MILANGO YA SAA TANO ASUBUHI. IFUATAYO NI SEHEMU YA MKUTANO HUO KAMA NILIVYOAHIDI. MASWALI NA MAJIBU YALIKUWA KIBAO NAMI NIMECHAGUA MACHACHE AMBAYO NADHANI YATAKIDHI KIU YA WADAU KIASI...

Richard: Shikamooni… Kwanza nitaanza kwa kushukuru wananchi wa Tanzania kwa sapoti mliyonipa. Nawahaeshimu sana. Mmenionesha mapenzi ambayo sijawahi kupata. Na nitaendelea kutangaza nchi yangu popote pale nitapokuwa katika mambo yangu nitayokuwa nafanya. Na pia, jambo lililotokea jana, la vurugu kiasi cha kushindwa kusalimia wapenzi waliokuja kunilaki, naomba radhi. Naomba wananchi muelewe kwamba sio rahisi mimi kumsalimia kila mmoja wenu. Lilikuwa ni swala la usalama. Asanteni.

Lucy: Lilikuwa ni swala la usalama, lakini Richard bado yupo. Na wiki ijayo atakuwepo na tutatangaza utaratibu wa sehemu ya kwenda kumuona. Kwa kuanzia, kwa wananchi, sababu tunajua kwamba wote wanasubiria kutakuwa kuna party lakini Jumamosi saa sita mchana Richard atakuwepo ofisi za MultiChoice. Kwa wale watakaotaka kumuona, kwa ajili ya kusaini autographs na kila kitu ina maana watakuja pale na kupata opportunity ya kuongea naye na kupiga naye picha. Hii wiki yote tuta focus kwa wanahabari. Kesho Ijumaa atakuwa na ziara ya kutembelea vyombo vya habari vyote. Nyie hapa tunajua mnawakilisha lakini kesho atawafuata kule mnakofanyia kazi ili aweze kusalimia watu wote kwa pamoja. Baada ya hapo tutatangaza wapi wananchi wanaopenda kujirusha watakutana naye wapi. Kwa hiyo kwa sasa hivi tunaklaribisha maswali.
 
Mimi nawasifu sana Multi Choice kwa uamuzi wao wa kumtorosha Richard ila nasikitika tuu ya kuwa umewaletea adha wale waliokuja kwa mapenzi mema kumpokea kijana huyo.
Nasema hivyo kwa kuwa Jamaa wa Multi wamekereshwa sana na kitendo cha CCM kuvamia jambo baada ya kuona kuna ushindi ili wapandie kwenye migongo ya wenzao pasipo kutoa jasho,HAIWEZEKANI.
Walikuwa wapi ktk hiyo miezi mitatu ya mashindano hayo kutoa kauli yeyote? Leo wameona vijana wa kiTZ wamefurahi wanaleta longolongo eti hiyo ni juhudi na sera zao!
Dawa ilikuwa ni hiyo,kuwaacha nje na T~shirt zao za kijani wapigwe mvua basi. Pole sana wale wengine ambao hawakuja kwa mwamvuli wa UVCCM,lakini mumuunge mkono Dada Lucy kwa uamuzi wake huo kwani vinginevyo kesho yake wangetangaza "UVCCM WAFANYA MAPOKEZI YA KUFA MTU".
Na hii ndio dawa ya wanaopenda kudandia mambo kwa manufaa binafsi.
 
nasikia ameomba radhi kwa kitendi kile alichokifanya uwanja wa ndege.

le atawea kurudiana na mkewe au ndo nadharia ktk mapenzi itatumika?????
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom