Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,463
- 39,929
Kuna habari za kuaminika sana kuwa kuna kontena la futi 40 (karibu tani 30) na limeingie nchini kwa karibu wiki mbili sasa ambalo limejaa vitunguu saumu ambalo linajaribiwa kuingizwa nchini na kundi la Wachina. Sasa wakaguzi wa pale bandari wakagundua kuwa vitunguu vinaoneshwa (kwenye mifuko yake) kuwa vimeexpire tangu 2009. Sasa jana Wachina wetu walienda TFDA ili kupata kibali cha kuingiza vitunguu hivyo nchini. Lakini ilikuwa vikitoka hapo viende kutiwa moto - chanzo toka bandarini - kinadokeza kuwa hivyo vitunguu vimekomaa kiasi kwamba ukivipasua "unaweza kupata kizunguzungu au kupaliwa".
Sasa Wachina hawako tayari kuingia hasara. Nasikia wametembeza mlungula wa kitu kidogo kuanzia TFDA, Kilimo, TRA na kwa vile sijafuatilia leo tangu hili sakata lianze jana walikuwa waende na TBS. Sasa uwezekano wa vitunguu hivyo kuingizwa sokoni ni mkubwa hasa kama haitawezekana kuvirudisha China. Sasa hivi vimehifadhiwa katika mafriji ya bandari pale na jamaa hawataki ifanyike "manual" inspection wanataka "scanning". Jamaa wametembeza karibu dola 5000 ili kurahisisha utoaji wa vitunguu hivyo; kuanzia TFDA kwenyewe kilimo na TRA.
Sijui ni mazao gani yanalimwa huko Igunga (najaribu kukumbuka kama kuna maeneo ya Tabora wanalima Vitunguu saumu) lakini vyovyote vile ilivyo taifa lnapofikia kuagiza hata vigunguu saumu basi tuna hali mbaya sana. Ndio nimebakia kusema kuwa kuna kashfa nyingine ni za kijinga.
Sasa Wachina hawako tayari kuingia hasara. Nasikia wametembeza mlungula wa kitu kidogo kuanzia TFDA, Kilimo, TRA na kwa vile sijafuatilia leo tangu hili sakata lianze jana walikuwa waende na TBS. Sasa uwezekano wa vitunguu hivyo kuingizwa sokoni ni mkubwa hasa kama haitawezekana kuvirudisha China. Sasa hivi vimehifadhiwa katika mafriji ya bandari pale na jamaa hawataki ifanyike "manual" inspection wanataka "scanning". Jamaa wametembeza karibu dola 5000 ili kurahisisha utoaji wa vitunguu hivyo; kuanzia TFDA kwenyewe kilimo na TRA.
Sijui ni mazao gani yanalimwa huko Igunga (najaribu kukumbuka kama kuna maeneo ya Tabora wanalima Vitunguu saumu) lakini vyovyote vile ilivyo taifa lnapofikia kuagiza hata vigunguu saumu basi tuna hali mbaya sana. Ndio nimebakia kusema kuwa kuna kashfa nyingine ni za kijinga.