KASHFA YA DOWANS: Takukuru kumhoji Dr. Idrissa Rashid?

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,172
Nimepata tetesi hivi punde kuwa Takukuru walikuwa na mjadala mrefu wa kumwajibisha Dr. Idrissa Rashid na vibosile wenzie waliokuwepo TANESCO na ambao ndiyo walioamua kuzuia mitambo ya DOWANS kinyume na sheria na isivyo halali na kulisababishia taifa maumivu ya Tshs 185 Billions...............

Pia Takukuru walikuwa wameagiza watumiwe muhutasari wa kikao kilichoamua mitambo ya DOWANS ikamatwe na kama Bodi nzima ya Tanesco ilishirikishwa kwenye uamuzi huo ambao sasa unaelekea kumweka JK hali mbaya kisiasa hasa ukizingatia Wikileaks wamemshutumu kwa kulea mafisadi....................

Tupo wengi tunaoamini ya kuwa uongozi wa Dr. Idrissa Rashid uliamua kushikilia hiyo mitambo ya DOWANS kama njia ya kulilazimisha Bunge la nchi hii ili liwaruhusu kuinunua mitambo hiyo michakavu kinyume na sheria ya manunuzi ambayo inakataza serikali kununua mitambo chakavu.........................

Ujanja huo uliposhindikana ilikuwa ni suala la wakati tu kabla ya nchi kuingizwa mkenge na wajanja wachache....................

Taarifa zaidi nitazimwaga hapa jamvini mara nitakapozinasa kwenye luninga yangu...................
 
Nimepata tetesi hivi punde kuwa Takukuru walikuwa na mjadala mrefu wa kumwajibisha Dr. Idrissa Rashid na vibosile wenzie waliokuwepo TANESCO na ambao ndiyo walioamua kuzuia mitambo ya DOWANS kinyume na sheria na isivyo halali na kulisababishia taifa maumivu ya Tshs 185 Billions...............

Pia Takukuru walikuwa wameagiza watumiwe muhutasari wa kikao kilichoamua mitambo ya DOWANS ikamatwe na kama Bodi nzima ya Tanesco ilishirikishwa kwenye uamuzi huo ambao sasa unaelekea kumweka JK hali mbaya kisiasa hasa ukizingatia Weekleaks wamemshutumu kwa kulea mafisadi....................

Makosa haya wanayoweza kutuhumiwa akina Dr. Idrissa Rashid na wenzake huitwa kwa jina la kitaalamu "criminal negligence".............
 
Kwanini suala la nani mmiliki wa Dowans halijibiwi? unamlipa mtu usiyemfahamu mara Capacity charge baaday fidia. Richmond walisema wamiliki wake ni hewa. Kwanini wa Dowans hamtuamibii? Kama kuwafahamu mmiliki mpaka tuende Brela kwanini kwenye malipo tunaambiwa kiasi? Ninavyofahmu kwa mujibu wa sheria ya Makampuni kila raia ana haki ya kupata taarifa za 'any public Company'. Hii Dowans ni kampuni ya aina gani?
 
Why are people evading the real issue and discuss issues which were in their jurisdiction(sp) to act, if TAKUKURU thought Dr Rashidi erred it could have filed all those stuff way back in 2008 when the heat was up...to do it now when there is money to pay is just a sham! Eng Nsiande
 
nafikiri TRA ndio walizuia mitambo isiondolewe kwa kuwa walikua wanaidai dowans kodi?tuulize aliyekatisha mkataba wa dowans kuiuzia umeme tanesco nani?
 
nafikiri TRA ndio walizuia mitambo isiondolewe kwa kuwa walikua wanaidai dowans kodi?tuulize aliyekatisha mkataba wa dowans kuiuzia umeme tanesco nani?
Dowans ndio walikatisha mkataba na kufungua kesi baada ya kupata letter of intent from TANESCO ya kutoa notice ya kusitisha mkataba, wameshinda kesi simply bcoz they claimed kuleta mitambo hiyo kuliwanufaisha public waliokuwa gizani and also kusitisha mkataba kwao was due to pressure from the govt na wakaonyesha kauli mbalimbali za defamation from wanasiasa na mass @ large na zote judge alizikubali!!!
 
Yote haya ni kujaribu kuteka nyoyo za watanzania ya kuwa serikali yao iko makini katika suala hili. Itakumbukwa mtu wa kwanza kuzungumzia uwezekano wa Dowans kulipwa alikuwa Pinda. Bila shaka yeye alikuwa amepewa kazi ya kuwatayarisha wananchi kisaikolojia kwa uamuzi ambao serikali ingelitangaza baadaye wa kuilipa Dowans. Sifa pekee iliyomfanya Pinda aonekane kuwa alikuwa anafaa kwa kazi hiyo nikutokuwa na uhusiano na kundi la mafisadi wanaotegemewa kufaidika na uamuzi huo. Ingawaje hapo awali kazi yakutangaza uamuzi huo alikuwa amepewa Ngereja lakini iliporipotiwa ya kuwa anao uhusiano wa karibu na kundi hilo, ndipo ilipo alipopewa kazi hiyo Werema. Haina budi ikumbukwe ya kuwa wadadisi wengi wa habari wanahusika kuteuliwa kwa Werema kuwa Mwanasheria mkuu wa serikali na kundi hilo la ufisadi.
 
Kwanini suala la nani mmiliki wa Dowans halijibiwi? unamlipa mtu usiyemfahamu mara Capacity charge baaday fidia. Richmond walisema wamiliki wake ni hewa. Kwanini wa Dowans hamtuamibii? Kama kuwafahamu mmiliki mpaka tuende Brela kwanini kwenye malipo tunaambiwa kiasi? Ninavyofahmu kwa mujibu wa sheria ya Makampuni kila raia ana haki ya kupata taarifa za 'any public Company'. Hii Dowans ni kampuni ya aina gani?

Hukumu ya DOWANS iko wazi.juu ya ni nani ni mmiliki wa DOWANS.....................................hili halina utata anafahamika..........
 
nafikiri TRA ndio walizuia mitambo isiondolewe kwa kuwa walikua wanaidai dowans kodi?tuulize aliyekatisha mkataba wa dowans kuiuzia umeme tanesco nani?

Suala hili halina cha kufikiri kwa sababu ushahidi upo wazi ni Tanesco ambao walienda Mahakama Kuu na wala siyo TRA ambao ndiyo walipaswa kwenda huko kudai kodi ambayo walikuwa hawajalipwa ya karibu ya jumla ya Tshs 9 Bilioni .....................hata yule Jaji aliyewakubalia Tanesco kuzuia mitambo ya kampuni ambayo hawana mgogoro nao anapaswa kuundiwa jopo na kuchunguzwa ya kuwa aliyafanya hayo maamuzi kwa kutumia sheria zipi?
 
Why are people evading the real issue and discuss issues which were in their jurisdiction(sp) to act, if TAKUKURU thought Dr Rashidi erred it could have filed all those stuff way back in 2008 when the heat was up...to do it now when there is money to pay is just a sham! Eng Nsiande

We all become wise afterwards..................Kama Tanesco wangelishinda hiyo rufani ya DOWANS leo tusingekuwa na huu mjadala..........
 
Udaku huu sisi tunataka katiba mpya tu sio hayo madudu

Madai ya katiba mpya ni mema lakini yasitumiwe kama mwanya wa kuruhusu ujambazi wa namna hii uendelee....kwa visingizio hatuna katiba mpya na ndiyo maana majambazi wanapata mwanya wa kutudhulumu haki yetu ya kimsingi.....................
 
Mwenye Dowans ni Rostam Aziz full stop

ila aliisaidia sana CCM 2010 - 2015 kwenye uchaguzi. So hawawezi kumtosa.. Ila ukweli uko wazi..

Sasa angalia Waziri Mkuu na Rais watakaa kimya tu.

Jamani nasema tena na tena Katiba mpya ndiyo mambo yote hata Tanzania kwa sasa..
 
Mwenye Dowans ni Rostam Aziz full stop

ila aliisaidia sana CCM 2010 - 2015 kwenye uchaguzi. So hawawezi kumtosa.. Ila ukweli uko wazi..

Sasa angalia Waziri Mkuu na Rais watakaa kimya tu.

Jamani nasema tena na tena Katiba mpya ndiyo mambo yote hata Tanzania kwa sasa..

Mawazo mazuri lakini hatuwezi kuwaachia wezi wale eti kwa kisingizio cha katiba mbovu..................tuyafanye yote mawili.....tutafuta katiba mpya na wakati huohuo wezi tulionao tuwashughulikie ipasavyo...........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom