Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,005
- 9,872
Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi Mkoa wa Dar es Salaam, Adrew Majaliwa amezuia operesheni zote zinazofanywa na Bodi ya Nyama Tanzania kwa wafanyabiashara wa machinjio ya Vingunguti wanaouza nje ya machinjio pamoja na wasiokuwa na vifungashio maalumu vya kubebea.
Hatua hiyo imekuja baada ya wafanyabiashara hao kuilalamikia Bodi ya Nyama wakidai kuwa imechukua nyama zaidi ya kilo 600 na kuzipeleka katika kituo cha polisi cha Buguruni ambako pia wamedai polisi wa kituo hicho wamegawana nyama hizo.
Akizungumza hayo leo Jumatatu Machi 15 alipokuwa kwenye mkutano wa wafanyabiashara hao, Majaliwa amesema operesheni ya kuwakamata wafanyabiashara wanaouza nje ya machinjio hayo na wasiokuwa na vifungashio maalumu amesitisha hadi eneo lililotengwa kwa ajili ya wafanyabiashara hao litakapokamilika.
Majaliwa ameiagiza bodi ya nyama waende kwenye machinjio hayo kutoa elimu kwa wafanyabiashara hao jinsi ya kuhifadhi nyama hizo kwenye vifaa maalumu wanavyotakiwa kuwa navyo.
"Bodi ya nyama mnatakiwa kutoa elimu ili wafanyabiashara wajue vifaa gani vya kuhifadhia nyama hizo na vizimba 29 vya wauza nyama vinajengwa ambavyo vitakamilika baada ya miezi mitatu hivyo miezi hiyo ikiisha operesheni hivyo ifanyike,"amesema amajaliwa.
Hata hivyo, Mkuu wa Kituo cha Polisi Buguruni, Adamu Maro amekana polisi kugawana nyama hiyo, bali walichofanya ni operesheni baada ya kupewa taarifa kuwa kuna nyama ambazo ni kibudu zisiingizwa kwenye machinjio hayo
"Sisi tulifanya operesheni baada ya kupewa rasmi barua kuwa kuna nyama ya kibudu imeingizwa machinjioni haiwezekani polisi akachukua nyama ambayo haifai kuliwa,” amesema Maro
Naye Meya wa jiji la Dar es Salaam, Omary Kumbilamoto amesema mkurugenzi wa jiji, mkuu wa wilaya, mtendaji wa kata na mwenyekiti wa mtaa huo hawakupewa taarifa kama kuna operesheni ya kuwakamata wafanyabiashara wanaofanya biashara nje ya machinjio hayo pamoja na wasiokuwa na vifungashio vya kuhifadhia nyama hizo.
MWANANCHI
Hatua hiyo imekuja baada ya wafanyabiashara hao kuilalamikia Bodi ya Nyama wakidai kuwa imechukua nyama zaidi ya kilo 600 na kuzipeleka katika kituo cha polisi cha Buguruni ambako pia wamedai polisi wa kituo hicho wamegawana nyama hizo.
Akizungumza hayo leo Jumatatu Machi 15 alipokuwa kwenye mkutano wa wafanyabiashara hao, Majaliwa amesema operesheni ya kuwakamata wafanyabiashara wanaouza nje ya machinjio hayo na wasiokuwa na vifungashio maalumu amesitisha hadi eneo lililotengwa kwa ajili ya wafanyabiashara hao litakapokamilika.
Majaliwa ameiagiza bodi ya nyama waende kwenye machinjio hayo kutoa elimu kwa wafanyabiashara hao jinsi ya kuhifadhi nyama hizo kwenye vifaa maalumu wanavyotakiwa kuwa navyo.
"Bodi ya nyama mnatakiwa kutoa elimu ili wafanyabiashara wajue vifaa gani vya kuhifadhia nyama hizo na vizimba 29 vya wauza nyama vinajengwa ambavyo vitakamilika baada ya miezi mitatu hivyo miezi hiyo ikiisha operesheni hivyo ifanyike,"amesema amajaliwa.
Hata hivyo, Mkuu wa Kituo cha Polisi Buguruni, Adamu Maro amekana polisi kugawana nyama hiyo, bali walichofanya ni operesheni baada ya kupewa taarifa kuwa kuna nyama ambazo ni kibudu zisiingizwa kwenye machinjio hayo
"Sisi tulifanya operesheni baada ya kupewa rasmi barua kuwa kuna nyama ya kibudu imeingizwa machinjioni haiwezekani polisi akachukua nyama ambayo haifai kuliwa,” amesema Maro
Naye Meya wa jiji la Dar es Salaam, Omary Kumbilamoto amesema mkurugenzi wa jiji, mkuu wa wilaya, mtendaji wa kata na mwenyekiti wa mtaa huo hawakupewa taarifa kama kuna operesheni ya kuwakamata wafanyabiashara wanaofanya biashara nje ya machinjio hayo pamoja na wasiokuwa na vifungashio vya kuhifadhia nyama hizo.
MWANANCHI