nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Mwandishi Wetu
Serikali yavutana na Shirika la Fedha la Kimataifa
KUMEJITOKEZA mvutano kati ya Serikali na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kuhusu sekta ya madini nchini na hasa dhahabu, huku utafiti wa awali uliofanywa na Kampuni ya CRA-International, ukibainisha kuwa baadhi ya migodi ya dhahabu nchini, imekuwa ikijihusisha na ukwepaji kodi, Raia Mwema, imeelezwa.
Hali hiyo inajitokeza wakati ambao Serikali ikitarajia kukusanya takriban Sh bilioni 99.5 kutokana na utozaji mrabaha kwenye kampuni za uchimbaji katika miezi 12 kuanzia Juni, mwaka huu hadi Juni, mwaka 2012.
Hata hivyo, makusanyo hayo yanayotarajiwa ni kidogo mno, yakitajwa kufikia asilimia 4.5 tu ya mauzo ya dhahabu nje ya nchi, yanayofanywa na migodi ya dhahabu nchini.
Mvutano huo wa IMF na Serikali ambao umezua hali ya kutokukubaliana kwa pande hizo, umechangiwa na mapendekezo ya IMF kutaka mrabaha usiongezwe kinyume cha nia ya Serikali, ambayo imekuwa katika shinikizo la kupandisha mrabaha.
Kikao kilichoibua hali ya kutofautiana, ingawa mapendekezo mengine ya IMF yalikubaliwa na Serikali, kilifanyika Septemba 15, mwaka huu, Dar es Salaam.
Katika kikao hicho, IMF waliwasilisha mapendekezo yao yaliyotokana na ufuatiliaji waliofanya kuhusu sekta ya madini nchini.
Msimamo wa Wakala wa Kodi Norway
Kikao hicho kilishirikisha pia taasisi nyingine ambazo zilitoa mtazamo wao, ikiwamo Wakala wa Kodi wa Norway (NTA), ambapo mwakilishi wake alielezea mgongano wa mtazamo kati ya migodi nchini na serikali.
Wakala hiyo ilieleza kuwa migodi ya madini nchini imekuwa ikieleza kulipa kodi
ya kutosha serikalini lakini wakati huo huo, Serikali imekuwa ikilalamika kutopata kodi ya kutosha kutoka kwenye sekta ya madini.
"Ingawa kiwango cha mapato kutoka kwenye migodi kimekuwa kikiongezeka, lakini changamoto bado ipo kwamba je, taarifa za gharama za uendeshaji zinazowasilishwa na mgodi ni za ukweli kiasi gani?
"Ukweli ni kwamba, hapa vyombo vya Serikali ni muhimu kujijengea uwezo kujiridhisha na taarifa za migodi hasa ya dhahabu," anaeleza mwakilishi wa Wakala wa Kodi Norway (Norwegian Tax Agency-NTA).
Msimamo wa Serikali ya Tanzania
Katika maelezo ya mwakilishi wa Serikali ya Tanzania, ilielezwa kuwa misamaha ya kodi, ambayo wadau wengine walipendekeza ifutwe au kuangaliwa upya, misamaha hiyo ni ya lazima hasa kwa miradi ya ufadhili.
"Katika suala la kuvutia mitaji, kuweka vivutio kwenye mfumo wa kodi si la lazima na wala si kigezo pekee cha kuvutia wawekezaji nchini. Vipo vivutio vingine ambavyo tunaweza kufanya, kama kuboresha miundombinu na mazingira ya uendeshaji biashara.
"Kwa hiyo, msamaha wa kodi hauwezi kuendelea kuchukuliwa kama kigezo pekee cha kuvutia mitaji ya kigeni nchini.
"Kampuni nyingi kubwa za kimataifa zimejijengea tabia ya kutangaza kupata hasara katika shughuli zake katika nchi za Afrika lakini wanatangaza kupata faida kwenye nchi zao ambako ndiko makao makuu ya kampuni hizo. Kwa nini? Nadhani kuna hujuma hapa!" alieleza mwakilishi wa serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu.
Wakala wa Ukaguzi Madini nchini
Hapa ndipo mgongano ulipojitokeza, hasa baada ya IMF kupendekeza kutoongezwa utozaji mrabaha, na Serikali ilikataa.
Serikali kupitia Tanzania Mining Audit agency (TMAA) ilikataa mapendekezo hayo, ikisisitiza kuwa bei ya dhahabu imekuwa ikiongezeka duniani.
"Kuhusu hili suala la viwango vya utozaji mrabaha, Serikali inatambua viwango vinavyotozwa kwa sasa ni kidogo ikilinganishwa na nchi nyingine mfano Botswana na Ghana.
"Na kwa hiyo, Serikali inaendelea kufikiria kuongeza mrabaha na hali ya ushindani katika uwekezaji wa migodi ikaendelea kuwa bora.
Siri migodi ya North Mara na Geita
Katika hatua nyingine, uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwapo kwa Kampuni ya Kimataifa CRA-International, iliyofanya utafiti kuhusu migodi ya dhahabu ya North Mara na Geita.
Utafiti huo ambao ripoti yake inaweza kuwasilishwa serikalini na hususan Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), umefichua hujuma nzito zinazofanywa katika migodi hiyo ya dhahabu, ikihusisha mazingira ya utoaji taarifa za shaka kuhusu gharama za uendeshaji na hata mauzo ya dhahabu.
Taarifa za migodi hiyo ndiyo zinazotumiwa na Serikali kukokotoa hesabu zinazohusisha uendeshaji wa migodi hiyo ili kubaini kama inajiendesha kwa faida au hasara.
Raia Mwema limepata ripoti ya awali ya utafiti huo ambao umehusisha migodi miwili mikubwa ya dhahabu nchini, North Mara Gold Mine, ulioko Nyamongo, mkoani Mara na Geita Gold Mining Ltd, ulioko Geita, mkoani Mwanza.
Kati ya mambo yaliyofichuliwa kwenye ripoti hiyo ni pamoja na migodi hiyo kujipatia mitaji kwa njia ya mikopo ambayo mazingira yake pia ni tata.
Ni kwenye hiyo mikopo ambamo, faida inayotokana na uuzaji dhahabu haikatwi kodi na badala yake, hufidia katika ulipaji mkopo hasa pale, kampuni inapoamua kujitangaza haikupata faida kubwa. Hali hiyo huifanya Serikali kutoambulia chochote kwa maana ya kodi.
Hali kama hii iliwahi kuzungumzwa bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Kabwe Zitto, ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani.
Katika hotuba yake ya Bajeti Mbadala, Zitto ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Fedha, alisema: "Sehemu kubwa ya fedha zinazotokana na faida wanazopata (migodi mikubwa) kwenye mauzo ya dhahabu huishia kulipia madeni na riba na hivyo kukosesha Serikali mapato.
"Hii kwa wataalamu wa kodi, inaitwa ‘tax planning measures'. Muundo huu wa mitaji ya uwekezaji itapelekea makampuni haya kutangaza hasara kila mwaka," alisema Zitto, maelezo ambayo kwa kiasi kikubwa yamebainika katika utafiti huo uliofanywa na CRA-International.
Mwenendo wa sekta ya madini nchini si wa kuridhisha ingawa Rais Jakaya Kikwete, aliunda Kamati ya Kutafiti na Kupendekeza namna bora ya kufaidika na sekta hiyo, bila kudhulumu wawekezaji na Watanzania. Kamati hiyo iliongozwa na Jaji Mark Bomani na imekwishawasilisha ripoti yake kwa Rais.
Serikali yavutana na Shirika la Fedha la Kimataifa
KUMEJITOKEZA mvutano kati ya Serikali na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kuhusu sekta ya madini nchini na hasa dhahabu, huku utafiti wa awali uliofanywa na Kampuni ya CRA-International, ukibainisha kuwa baadhi ya migodi ya dhahabu nchini, imekuwa ikijihusisha na ukwepaji kodi, Raia Mwema, imeelezwa.
Hali hiyo inajitokeza wakati ambao Serikali ikitarajia kukusanya takriban Sh bilioni 99.5 kutokana na utozaji mrabaha kwenye kampuni za uchimbaji katika miezi 12 kuanzia Juni, mwaka huu hadi Juni, mwaka 2012.
Hata hivyo, makusanyo hayo yanayotarajiwa ni kidogo mno, yakitajwa kufikia asilimia 4.5 tu ya mauzo ya dhahabu nje ya nchi, yanayofanywa na migodi ya dhahabu nchini.
Mvutano huo wa IMF na Serikali ambao umezua hali ya kutokukubaliana kwa pande hizo, umechangiwa na mapendekezo ya IMF kutaka mrabaha usiongezwe kinyume cha nia ya Serikali, ambayo imekuwa katika shinikizo la kupandisha mrabaha.
Kikao kilichoibua hali ya kutofautiana, ingawa mapendekezo mengine ya IMF yalikubaliwa na Serikali, kilifanyika Septemba 15, mwaka huu, Dar es Salaam.
Katika kikao hicho, IMF waliwasilisha mapendekezo yao yaliyotokana na ufuatiliaji waliofanya kuhusu sekta ya madini nchini.
Msimamo wa Wakala wa Kodi Norway
Kikao hicho kilishirikisha pia taasisi nyingine ambazo zilitoa mtazamo wao, ikiwamo Wakala wa Kodi wa Norway (NTA), ambapo mwakilishi wake alielezea mgongano wa mtazamo kati ya migodi nchini na serikali.
Wakala hiyo ilieleza kuwa migodi ya madini nchini imekuwa ikieleza kulipa kodi
ya kutosha serikalini lakini wakati huo huo, Serikali imekuwa ikilalamika kutopata kodi ya kutosha kutoka kwenye sekta ya madini.
"Ingawa kiwango cha mapato kutoka kwenye migodi kimekuwa kikiongezeka, lakini changamoto bado ipo kwamba je, taarifa za gharama za uendeshaji zinazowasilishwa na mgodi ni za ukweli kiasi gani?
"Ukweli ni kwamba, hapa vyombo vya Serikali ni muhimu kujijengea uwezo kujiridhisha na taarifa za migodi hasa ya dhahabu," anaeleza mwakilishi wa Wakala wa Kodi Norway (Norwegian Tax Agency-NTA).
Msimamo wa Serikali ya Tanzania
Katika maelezo ya mwakilishi wa Serikali ya Tanzania, ilielezwa kuwa misamaha ya kodi, ambayo wadau wengine walipendekeza ifutwe au kuangaliwa upya, misamaha hiyo ni ya lazima hasa kwa miradi ya ufadhili.
"Katika suala la kuvutia mitaji, kuweka vivutio kwenye mfumo wa kodi si la lazima na wala si kigezo pekee cha kuvutia wawekezaji nchini. Vipo vivutio vingine ambavyo tunaweza kufanya, kama kuboresha miundombinu na mazingira ya uendeshaji biashara.
"Kwa hiyo, msamaha wa kodi hauwezi kuendelea kuchukuliwa kama kigezo pekee cha kuvutia mitaji ya kigeni nchini.
"Kampuni nyingi kubwa za kimataifa zimejijengea tabia ya kutangaza kupata hasara katika shughuli zake katika nchi za Afrika lakini wanatangaza kupata faida kwenye nchi zao ambako ndiko makao makuu ya kampuni hizo. Kwa nini? Nadhani kuna hujuma hapa!" alieleza mwakilishi wa serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu.
Wakala wa Ukaguzi Madini nchini
Hapa ndipo mgongano ulipojitokeza, hasa baada ya IMF kupendekeza kutoongezwa utozaji mrabaha, na Serikali ilikataa.
Serikali kupitia Tanzania Mining Audit agency (TMAA) ilikataa mapendekezo hayo, ikisisitiza kuwa bei ya dhahabu imekuwa ikiongezeka duniani.
"Kuhusu hili suala la viwango vya utozaji mrabaha, Serikali inatambua viwango vinavyotozwa kwa sasa ni kidogo ikilinganishwa na nchi nyingine mfano Botswana na Ghana.
"Na kwa hiyo, Serikali inaendelea kufikiria kuongeza mrabaha na hali ya ushindani katika uwekezaji wa migodi ikaendelea kuwa bora.
Siri migodi ya North Mara na Geita
Katika hatua nyingine, uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwapo kwa Kampuni ya Kimataifa CRA-International, iliyofanya utafiti kuhusu migodi ya dhahabu ya North Mara na Geita.
Utafiti huo ambao ripoti yake inaweza kuwasilishwa serikalini na hususan Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), umefichua hujuma nzito zinazofanywa katika migodi hiyo ya dhahabu, ikihusisha mazingira ya utoaji taarifa za shaka kuhusu gharama za uendeshaji na hata mauzo ya dhahabu.
Taarifa za migodi hiyo ndiyo zinazotumiwa na Serikali kukokotoa hesabu zinazohusisha uendeshaji wa migodi hiyo ili kubaini kama inajiendesha kwa faida au hasara.
Raia Mwema limepata ripoti ya awali ya utafiti huo ambao umehusisha migodi miwili mikubwa ya dhahabu nchini, North Mara Gold Mine, ulioko Nyamongo, mkoani Mara na Geita Gold Mining Ltd, ulioko Geita, mkoani Mwanza.
Kati ya mambo yaliyofichuliwa kwenye ripoti hiyo ni pamoja na migodi hiyo kujipatia mitaji kwa njia ya mikopo ambayo mazingira yake pia ni tata.
Ni kwenye hiyo mikopo ambamo, faida inayotokana na uuzaji dhahabu haikatwi kodi na badala yake, hufidia katika ulipaji mkopo hasa pale, kampuni inapoamua kujitangaza haikupata faida kubwa. Hali hiyo huifanya Serikali kutoambulia chochote kwa maana ya kodi.
Hali kama hii iliwahi kuzungumzwa bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Kabwe Zitto, ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani.
Katika hotuba yake ya Bajeti Mbadala, Zitto ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Fedha, alisema: "Sehemu kubwa ya fedha zinazotokana na faida wanazopata (migodi mikubwa) kwenye mauzo ya dhahabu huishia kulipia madeni na riba na hivyo kukosesha Serikali mapato.
"Hii kwa wataalamu wa kodi, inaitwa ‘tax planning measures'. Muundo huu wa mitaji ya uwekezaji itapelekea makampuni haya kutangaza hasara kila mwaka," alisema Zitto, maelezo ambayo kwa kiasi kikubwa yamebainika katika utafiti huo uliofanywa na CRA-International.
Mwenendo wa sekta ya madini nchini si wa kuridhisha ingawa Rais Jakaya Kikwete, aliunda Kamati ya Kutafiti na Kupendekeza namna bora ya kufaidika na sekta hiyo, bila kudhulumu wawekezaji na Watanzania. Kamati hiyo iliongozwa na Jaji Mark Bomani na imekwishawasilisha ripoti yake kwa Rais.