KASHFA: Ni kweli Jeshi la Polisi "linaiba" simu kwa kigezo cha upelelezi?

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,434
7,055
Acha tuhoji sasa. Hii ni kansa ya kimya kimya na wahanga ni wengi japo hawasemi.

Madai yaliyopo ni kwamba mtuhumiwa ukikamatwa, halafu simu yako ikachukuliwa na polisi kwa ajili ya upelelezi, basi andika maumivu! Tena zinafanyiwa refurbishing kabisa!

Ni mara chache sana watuhumiwa hurudishiwa simu zao. Unaweza kuachiwa kwa dhamana lakini upelelezi ukachukua mwaka mzima na zaidi. Mpaka unakata tamaa.

Nataja simu kwa sababu ndio "zinapendwa" zaidi. Lakini kuna iPads na Laptops pia.

Nahoji hili kwa sababu maneno yanasemwa sana chini chini na naona yanalitia doa Jeshi letu tukufu linalofanya kazi ngumu ya kulinda raia na mali zao usiku na mchana.

Ni kweli wazee mna kamradi maalum ka kuziuza simu hizo kwenye "black market" na wadosi?

Hili lichunguzwe!
 
Mkuu, hizi mambo hujawahi kusikia? Ulizia hata mtaani kwako.

Nadhani iundwe tume maalum ichunguze hili suala. Isijekuwa kuna maofisa fulani walioaminiwa wanatajirika kupitia mradi huu!
 
Ukirudi kuifata unaweza ukawekwa ndina ko unaamua kuiacha huko waendelee tu kuitumia
Yaani hautamani kuirudia kabisa sema ndo ivo utasema wapi watekekeza sharia wameichukua
 
Mkuu, hizi mambo hujawahi kusikia? Ulizia hata mtaani kwako.

Nadhani iundwe tume maalum ichunguze hili suala. Isijekuwa kuna maofisa fulani walioaminiwa wanatajirika kupitia mradi huu!
Nitafanya uchunguzi juu ya hilo, kwa hii nchi kila kitu kinawezekana kwa hawa walinzi wetu hata siwezi kataa sana...
Natamani siku moja niandike Uzi jinsi walivoniibia hawa polisi Wa Tanzania....
 
Nitafanya uchunguzi juu ya hilo, kwa hii nchi kila kitu kinawezekana kwa hawa walinzi wetu hata siwezi kataa sana...
Natamani siku moja niandike Uzi jinsi walivoniibia hawa polisi Wa Tanzania....
Fanya uandike boss. Pengine kuna watu wachache wanataka kuharibu kazi kubwa inayofanywa na hawa jamaa.
 
Ukirudi kuifata unaweza ukawekwa ndina ko unaamua kuiacha huko waendelee tu kuitumia
Yaani hautamani kuirudia kabisa sema ndo ivo utasema wapi watekekeza sharia wameichukua
Na wengi wanahofia hii. Mazingira ya kudai haki yako kutoka kwa Polisi hapa Bongo ni suicide!

Mtu anaishia kusema aah, nitapata nyingine.

Wangapi sasa?
 
Hata wakikamata mtu kwa sababu yoyote hasa nyakati za usiku lazima wafanye kusachi kila kilichopo mfukoni...
 
Nilimuhurumia sana yule jamaa wa bureau de change ambaye hela zake zote zilizokutwa walizichukua kama 'kidhibiti'
 
Eti polisi mnafanyia je hizo Simu upelelezi na hamzirudishi.. kama kunapolisi humu jf tujuze basi
 
Nitafanya uchunguzi juu ya hilo, kwa hii nchi kila kitu kinawezekana kwa hawa walinzi wetu hata siwezi kataa sana...
Natamani siku moja niandike Uzi jinsi walivoniibia hawa polisi Wa Tanzania....
Andika mkuu tupate Cha kujifunza
 
Binafsi naweza sema nikweli hiyo kitu ipo,japo ni mara chache sana kutokea na mtu simu au kitu kingine chochote anaweza akakosa kam jinsi alivyosema mtoa mada.

Ila ni hiv hawa jamaa mara nyingine wanaangalia upepo wako ,ukionesha unyonge kwa meng wana weza kukuonea kutokana mtu hajui haki yake aidai vip.
Mfano hai ni Mimi mwenyew ilikua ni kituo cha police magenge20 kiburugwa nilipo fikishwa pale Kama kawaida yao ni kavua mkanda viatu simu na pesa elfu 12000 na mia mbili.
Wakat natoka ktk vitu nilivyo kua nimeandika pale miambili ilipelea Mimi nilidai na nilikaza kweli kweli na nilipewa.
Na tatizo kubwa ni kwamba police wetu ,ukifika pale unachukuliwa kam mtu flani ambae una uwenyeji na kila kitu kisheria
 
Back
Top Bottom